Mrejesho wa yale niliyosema kuhusu kijana wa hovyo Majaliwa aliyeidanganya nchi na wasomi wake

yash_ed

Senior Member
Jan 9, 2020
146
391
INASIKITISHA SANA TENA SANA 😭

WALIOOKOLEWA WAKANA KUSAIDIWA NA MAJALIWA, WADAI WALITUMIA JUHUDI ZAO KUJIOKOA.

Furaha ya Majaliwa Shujaa aliyeokoa watu kwe ajali ya ndege ya Precision Air iliyotokea Bukoba mkoani Kagera huenda ikageuka huzuni baada ya abiria waliookolewa kwenye ajali hiyo kudai walitumia juhudi zao wenyewe kufungua mlango na kisha kutoka.

Akizungumza mmoja wa abiria hao amesema yeye ndiye angeweza kuwa kinara wa tukio hilo kwani baada ya ndege kutua kwenye maji, yeye na muhudumu mmoja wa ndege hiyo waling'ang'ana kufanya jitihada za kufungua mlango wakati huo mitambo ya umeme ilikuwa imezima na mlango ulikuwa umejilock.

"Baada ya ndege kutua kwenye maji nilianza kutapatapa kutafuta mlango wa kutokea, haikuwa rahisi lakini kwakuwa mimi nilikuwa viti vya nyuma nilijitahidi kutafuta namna ya kutokea, tulikuwa tunaenda kufa, nikawambia wenzangu "kwahiyo tunakufa huku tunajiona" hapo maji yalikuwa yamejaa, lakini baadae niliona mlango unajifungua kidogo baada ya muhudumu wa ndege kuuchokonoa kwa chini ndipo nilipotumia upenyo ule kuusukuma mlango nikatoka nje"

Abiria huyo ameongeza kwa kusema "baada ya mimi kutoka nilianza kuwaokoa wenzangu, na kila aliyekuwa anatoka alikuwa anakaa juu ya ndege maana maboti ya wavuvi yalikuwa bado kufika, nilijawa na ujasiri mkubwa ingawa hali yangu ilikuwa mbaya, nikawa nawavuta watu kuwatoa nje akiwemo mama mmoja na mwanae ambao pia niliwaokoa mimi nikisaidiana na mchina, baadae watu waliisha kwenye ndege nikajua wote wametoka ndipo wavuvi walipoanza kuja kutuchukua kutupeleka hospitali";- ameeleza mmoja wa waliookolewa.
 
INASIKITISHA SANA TENA SANA 😭

WALIOOKOLEWA WAKANA KUSAIDIWA NA MAJALIWA, WADAI WALITUMIA JUHUDI ZAO KUJIOKOA.

Furaha ya Majaliwa Shujaa aliyeokoa watu kwe ajali ya ndege ya Precision Air iliyotokea Bukoba mkoani Kagera huenda ikageuka huzuni baada ya abiria waliookolewa kwenye ajali hiyo kudai walitumia juhudi zao wenyewe kufungua mlango na kisha kutoka.

Akizungumza mmoja wa abiria hao amesema yeye ndiye angeweza kuwa kinara wa tukio hilo kwani baada ya ndege kutua kwenye maji, yeye na muhudumu mmoja wa ndege hiyo waling'ang'ana kufanya jitihada za kufungua mlango wakati huo mitambo ya umeme ilikuwa imezima na mlango ulikuwa umejilock.

"Baada ya ndege kutua kwenye maji nilianza kutapatapa kutafuta mlango wa kutokea, haikuwa rahisi lakini kwakuwa mimi nilikuwa viti vya nyuma nilijitahidi kutafuta namna ya kutokea, tulikuwa tunaenda kufa, nikawambia wenzangu "kwahiyo tunakufa huku tunajiona" hapo maji yalikuwa yamejaa, lakini baadae niliona mlango unajifungua kidogo baada ya muhudumu wa ndege kuuchokonoa kwa chini ndipo nilipotumia upenyo ule kuusukuma mlango nikatoka nje"

Abiria huyo ameongeza kwa kusema "baada ya mimi kutoka nilianza kuwaokoa wenzangu, na kila aliyekuwa anatoka alikuwa anakaa juu ya ndege maana maboti ya wavuvi yalikuwa bado kufika, nilijawa na ujasiri mkubwa ingawa hali yangu ilikuwa mbaya, nikawa nawavuta watu kuwatoa nje akiwemo mama mmoja na mwanae ambao pia niliwaokoa mimi nikisaidiana na mchina, baadae watu waliisha kwenye ndege nikajua wote wametoka ndipo wavuvi walipoanza kuja kutuchukua kutupeleka hospitali";- ameeleza mmoja wa waliookolewa.
Huyu ni Eng. Victor?
Eng. Victor anasemaje?
Air hostess anasemaje?
Majaliwa huko uliko unalizungumziaje hili?
 
Hili swala wenye akili hawataki kutumia akili zao, na wanaojua ukweli hawataki kuongea au huenda wanaongea Ila hawasikiki.

1. Ni Nani aliekuwa anaongoza Ile ndege itue pale bukoba?

2. Baada ya kuona kuwa Kuna shida angani alijiandaa vipi endapo ndege ingeleta/kupata shida pale uwanjani na maeneo ya jirani?

3. Vikosi vya ulinzi na uokozi vilikuwa wapi ndani ya mpaka zaidi ya nusu saa Hadi masaa bila kutokea au kutoa msaada kwa wahanga?

4. Ni nini jukumu hasa la Rubani na muongoza ndege pale uwanjani baada ya kujua kuwa uwezekano wa kutua salama ulikuwa chini zaidi ya unavyotarajiwa?

5. Air hostesses wanawajibika vp kwa abiria Kama ndege ikipata tatizo?

6. Kwenye ndege hakukuwa na vifaa vya kujiokoa au kujikinga na maji.(boya)

7. Tatizo lipo kwa muongoza ndege au Rubani waliokuwa wanarusha ndege kwa labda kutokusikiliza vizuri au kutumia mazoea ya kazi/fani.

8. Precision Anawajibika kulipa fidia na gharama kwenye hyo ajali kwa kushindwa kuwahakikishia abiria wake usalama mpaka mwisho wa safari.

9. Kila mtu ana bahati yake katika maisha hujui iko wapi na utaipata lini na kivipi huyo Majaliwa tayari alishabahatika hvyo chuki, roho mbaya havisaidii, pambaneni na wataalamu walioshindwa kunusuru ajali isitokee.
 
Stories nyiiiiingi. Mwingine anasema yeye afungua mlango akakutana na kijana mdogo akamwomba aingie kwenye ndege akusanye mabegi, mwingine anasema alipitia bawa lilipokatikia. Kama umeme ulikata na lock inategemea umeme na Majaliwa anasema aligonga kwa kasia kuondoa lock na mwandishi anasema mhudumu alichokonoa mlango ukafunguka na kuna abiria anasema kuna kijana nilimwomba aingie ndani kuokoa mabegi, na majaliwa anasema nikaita wenzangu wakanipatia kamba niende kuifunga sehemu ili tuvute ndege na kwamba kuna waokoaji walipoteza uhai wakijaribu kufanya uokoaji. Kwa nini tunapenda kupoteza hii picha ya Majaliwa na wenzake waliozama hadi ndani hadi mmoja wapo akapoteza maisha?
 
Kwahiyo nani alimtengeneza majaliwa?
Ina maana umati wote ule ulidanganywa?
Wale wajeda waliofunikwa miavuli nao walijiunga na majaliwa kudanganya?
Nani alimpa nafasi hiyo ya kudanganya na hata umati mkubwa ule ukubali?
 
Ujinga tu. Majaliwa alikuwa sehemu sahihi wakati sahihi haya mengine ni kulazimisha ujinga ujinga. Kwann usishupalie uzembe wa maafisa uokoaji? Uzembe wa kutokuwa na vifaa? Uzembe wa administration ya airport? Ujinga mtupu. Kwani Majaliwa alijaza fomu ya kuomba kuitwa shujaa? UJINGA.
 
Back
Top Bottom