Mipango yangu ya kutafuta TSH milioni 2+ ndani ya miezi 18

LA7

JF-Expert Member
Aug 26, 2019
462
1,767
Habari za humu ndugu zangu, mm ni yule yule ndugu yenu wa kuishia LA7,

Leo nimekuja na plani ya kuisaka milioni zaidi ya 2 ndani ya miezi 18

Ukweli mimi toka nizaliwe pesa yangu cash niliyoishika na umri wangu huh wa zaidi ya miaka 25 ilikuwa ni laki nne na sabini ambayo niliikusanya kwa kuweka kidogo kidogo ndani ya sabufa kwa miezi kadhaa.

Sasa toka huu mwaka uingie nataka kuboresha ofisi yangu yenye thamani isiyopungua m1 na kuiboresha,

Kipato change kwa mwezi kisicho rasmi ni zaidi ya laki tatu kama umeme hautasumbua, hivo kuanzia mwezi wa pili nilipata wazo la kuweza kukusanya pesa kidogo kidogo hadi nifikishe hicho kiwango

Nimeanza kukusanya ndoo kubwa tupu za mafuta ya kula

Nimepanga kila mwezi nitakusanya ndoo zisiopungua ishirini kwa miezi 18,

Ampapo kama mipango itaenda sawa mpaka tamati nitakuwa na ndoo 300+

Je, Soko la ndoo linapatikana wapi?

Sijajua soko la uhakika lakini nimepanga kwenda kuuza mm mwenyewe kijijini kwetu singida, kwasababu mwaka juzi wakati nikiwa huko nilishudia ndoo kubwa ikiuzwa 8000-10000 na ndoo ndogo 6000

Pia nakusanya ndoo ndogo japo sio kwa kiwango kikubwa,

Naamini nitatoboa kwani ndani ya miezi miwili nimekusanya ndoo 40

Nimeweka kiwango cha 20 kwa mwezi sababu pia majukumu ya kifamilia, ndoo maja nauziwa kuanzia 3000 hadi 4000.

FB_IMG_17120087319363345.jpg


Naamini nitatoboa kikubwa uzima tu, ntaleta mrejesho hapa hapa.
 
Ili ufanikiwe fanya yafuatayo....utanishukuru

KATAA NDOA NI UTAPELI
KATAA NDOA NI UTAPELI
KATAA NDOA NI UTAPELI
KATAA NDOA NI UTAPELI
KATAA NDOA NI UTAPELI
Ili ufanikiwe fanya yafuatayo....utanishukuru

KATAA NDOA NI UTAPELI
KATAA NDOA NI UTAPELI
KATAA NDOA NI UTAPELI
KATAA NDOA NI UTAPELI
KATAA NDOA NI UTAPELI
Nina mke na watoto wawili pia bado nimepanga😡
 
Habari za humu ndugu zangu, mm ni yule yule ndugu yenu wa kuishia LA7,


Leo nimekuja na plani ya kuisaka milioni zaidi ya 2 ndani ya miezi 18


Ukweli mm toka nizaliwe pesa yangu cash niliyoishika na umri wangu huh wa zaidi ya miaka 25 ilikuwa ni laki nne na sabini ambayo niliikusanya kwa kuweka kidogo kidogo ndani ya sabufa kwa miezi kazaa,


Sasa toka huu mwaka uingie nataka kuboresha ofisi yangu yenye thamani isiyopungua m1 na kuiboresha,


Kipato change kwa mwezi kisicho rasmi ni zaidi ya laki tatu kama umeme hautasumbua, hivo kuanzia mwezi wa pili nilipata wazo la kuweza kukusanya pesa kidogo kidogo hadi nifikishe hicho kiwango


Nimeanza kukusanya ndoo kubwa tupu za mafuta ya kula


Nimepanga kila mwezi nitakusanya ndoo zisiopungua ishirini kwa miezi 18,


Ampapo kama mipango itaenda sawa mpaka tamati nitakuwa na ndoo 300+


Je? Soko la ndoo linapatikana wapi?


Sijajua soko la uhakika lakini nimepanga kwenda kuuza mm mwenyewe kijijini kwetu singida, kwasababu mwaka juzi wakati nikiwa huko nilishudia ndoo kubwa ikiuzwa 8000-10000 na ndoo ndogo 6000


Pia nakusanya ndoo ndogo japo sio kwa kiwango kikubwa,


Naamini nitatoboa kwani ndani ya miezi miwili nimekusanya ndoo 40


Nimeweka kiwango cha 20 kwa mwezi sababu pia majukumu ya kifamilia, ndoo maja nauziwa kuanzia 3000 hadi 4000
View attachment 2951180

Naamini nitatoboa kikubwa uzima tu, ntaleta mrejesho hapa hapa.
Nakutia moyo
Pia kusanya madumu ya lita 20 ya njano...yana soko kubwa ukanda huo...minadani mpaka Mboka.
 
Back
Top Bottom