Mikoa inayotumia grid ya Taifa ya umeme yakosa umeme, grid ya taifa imesumbua Kidogo

TANESCO

Official Account
Jul 12, 2014
4,584
2,104
TANESCO
Tunaomba radhi wateja wetu
Imetokea hitilafu gridi ya taifa na kusababisha umeme eneo lote la Dar es Salaam na baadhi ya mikoa kukosa umeme.

Tatizo hili linashughulikiwa na umeme utarudi baada ya muda mfupi

=======

SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA YA KUTOKEA KWA HITILAFU KATIKA GRIDI YA TAIFA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake waliounganishwa katika Mikoa iliyo katika Gridi ya Taifa kuwa majira ya Saa 12:30 imetokea hitilafu kwenye Gridi ya Taifa na kusababisha Mikoa hiyo kukosa umeme.

Jitihada zimefanyika ili kurejesha umeme na baadhi ya Mikoa imeshaanza kupata huduma ya umeme

Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi.

TANESCO inaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza.

Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.

Toa taarifa kupitia namba za simu zifuatazo

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu 0222194400 na 0768 985100

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya Kijamii
www.facebook/twitter.com/tanescoyetu

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu

25/10/2017

=======
UPDATE: Oktoba 26, 2017

Tunapenda kuwataarifu Wateja wetu waliounganishwa katika Mikoa iliyo katika Gridi ya Taifa kuwa leo Alhamisi Oktoba 26, 2017 majira ya Saa 12:03 Asubuhi imetokea hitilafu tena kwenye Gridi ya Taifa na kusabisha Mikoa hiyo kukosa umeme.

Mafundi wanafanya jitihada usiku na mchana ili kuhakikisha hali hii haijirudii na umeme unarejea katika hali ya kawaida kwa haraka

Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi...

TANESCO
 
Ikitoka Grid jamani mikoa yote iliyomo kwenye Grid lazima umeme ukate. Kuweni tu wavumilivu maana kama ni Grid kidogo shughuli ipo
 
Back
Top Bottom