Anakugharimu nini?Anatugharimu hivyo tunajitahidi kumuweka sawa na pengine inawezakana mwenzetu Wewe upeo wako wa ' Kufikiri ' unaishia tu Chooni kwa kujua Kunya na Kujitawaza na huku Kwingine ambako kunahitaji matumizi makubwa ya akili zilizotukuka hupawezi hivyo ndiyo maana huoni ' tija ' ya sisi kumlaumu kama siyo kumshangaa.
Anakugharimu nini?
Tunadharaulika na nani?Tunadharaulika mno na kuonekana wa ' hovyo hovyo ' kama vile ulivyo Wewe Mkuu.
Akazinguaa hataree
Ni heri kuuchuna tu,maana hata wasaidizi wakaribu yake wamemshindwa.Roho katili itaonaje kosa?ingekuwa kuna kuzindua terrible teens angepanga na vijembe vya kuongea na kutaka fent fod zote awe yeye na bashite.
Mheshimiwa Rais wangu Dkt. Magufuli kusema ukweli na wala hili nisikufiche kama wengine wanavyokuchekea kukuambia ukweli kuwa hata kama unatonyesha jitahada zako na kwakweli nyingi tu tunaanza kuziona na tunakushukuru kwa hilo ILA unatupa Kazi ngumu na kubwa mno ya ' kukutea ' humu mitaani na hata mitandaoni juu ya hii tabia yako ambayo sasa naanza kujiuliza ni ya Wasukuma kweli hawa hawa ninaowajua au labda mwenzetu Wewe ni Mwana Diaspora wa Taifa jingine ambalo halina utu huu wa Kitanzania uliozoeleka?
Katika utamaduni wa Kiafrika ni SIFA mbaya sana tena kwa Kiongozi kabisa wa nchi ( HEAD OF STATE / PRESIDENT ) kukacha kabisa kwenda kuhudhuria ' Misiba ' ambayo yawezekana hata hao waliokufa 99% walikupigia Kura au pengine hata Wazazi wao walihakikisha leo Wewe uwe hapo ulipo.
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli Mimi GENTAMYCINE itabidi tu univumilie kwani huwa sina tabia ya kumficha Mtu hata kama ni Rafiki yangu au ni Kipenzi changu na hivi ndivyo Mwenyezi Mungu alivyoniumba na sitokuja kubadilika hadi naingia Kaburini na nitasema ukweli pale panapostahili na nitakosoa mara moja kama hivi pale ninapoona pana tatizo kwani sikuumbwa kuwa ' Mnafiki ' kama wengi wanaokuzunguka.
Mheshimiwa Rais wangu Dkt. Magufuli hivi una ' matatizo ' gani na Misiba au Maiti? Mbona Mimi nimeishi miaka mitatu ( 3 ) na ' Wananzengo ' wa Kisukuma kule Nyegezi, Luchelele, Nsumba, Malimbe, Mkolani na Buhongwa lakini tulikuwa ' tunajumuika ' nao sana Misibani na hata Mazishini? Hii picha unayotuonyesha Watanzania sasa unataka tukueleweje Mheshimiwa?
Hukwenda Kagera Watu tukajipinda humu kukutetea labda kwa kuhisi kuwa ungejishtukia na kubadilika ikawa vile vile tukasema ' poa ' mara tena ' Wapiganaji ' wako Askari wa Police waliuwawa ' Kinyama ' mno kule Kibiti kama kawaida hukwenda na kama jadi yetu Wanaume tukaja humu tena ' kutiririka ' kwa kukutetea lakini mioyo yetu inatusuta ila tumeshazoea kujikaza ' kisabuni ' kwa kujua labda moyo wako ungajawa na ' aibu ' na ungabadilika kumbe ndiyo kama vile tulikuwa tunapaka ' Upepo ' rangi.
Sasa kali katika yote Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli hili la juzi tu ' masikini ya Mungu ' Taifa limepoteza Wapendwa wetu kabisa tena wakiwa bado wadogo na wana Ndoto za kuja kuwa Watu fulani wa muhimu katika Taifa hili huku kuna wengine pia huwezi jua walikuwa wanataka kuja kuwa ' watiririkaji ' kama GENTAMYCINE lakini safari yao ikafikia tamati katika Mlima wa Rhotie Marera kwa kufariki dunia pamoja na Walimu wao na Dereva wa lile Basi.
Huku ' watetezi ' wako ' tukisikilizia ' kwa mbali kuona labda safari hii ' mshipa ' wako wa ' aibu ' utakunjuka kwa ' kutukuka ' na utahudhuria Msiba ghafla tunaona Press Release kutoka IKULU ya kutoa rambirambi zako na baadae tena tunatangaziwa kuwa Wewe hutokwenda ila utawakilishwa na Makamu wako wa Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassan.
Hatukatai kuwa uwepo wa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan pale Sheikh Amri Abeid Kaluta ni jambo jema ila nadhani uwepo wake pale ' ungenoga ' kama si ' kupendeza ' mno endapo Wewe Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ungekuwa haupo nchini Tanzania ila kumbe umemtuma Yeye ( Makamu wa Rais ) halafu Wewe ' umeunyuti ' zako tu hapo IKULU ya Magogoni na ratiba zako za hapa na pale.
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli leo kwa mara ya Kwanza kabisa naungana na maneno yako unayopenda kuyasema kila mara kuwa nakunukuu " Watanzani mniombee " na yawezekana kumbe sisi Watanzania tukawa hatujui huwa unamaanisha nini ila GENTAMYCINE leo nimegundua kuwa yawezekana unaposema tukuombee labda unataka Watanzania tumwambie Mwenyezi Mungu aweze kuukunjua huo moyo wako mgumu, akujaze upendo uliotukuka na pengine aweze kukuondolea Kisirani chako au Chuki zako au Pepo la ukatili ukatili ambalo labda mwenzetu ' umeshalichungulia ' mahala na ukaona kuwa linakuijia na si ajabu tayari limeshaweka makazi ya kudumu katika roho yako kama siyo moyo wako.
Nimalizie tu kwa kusema kuwa Mheshimiwa Rais wangu Dkt. Magufuli unatupa wakati mgumu sana wa ' kukutetea ' kwa matendo ya ajabu kama pia si ya kustaajabisha unayoyafanya. Hivi kabisa huna hata ' uchungu ' na hawa Watoto? Je ukiachillia mbali Wewe kuwa Rais wetu lakini na Wewe si ni Mzazi pia au? Basi hata ' ungetuzuga ' tu Watanzania kwa kumtuma pia Mkeo Mama yetu Janet Magufuli aandamane na Makamu wa Rais kwenda Arusha lakini hata Yeye pia hajaenda.
Hivi kwa mtindo huu hizi kauli ambazo sasa zinaanza ' kutiririka ' kuwa yawezekana haya matukio labda mwenzetu huwa unayajua kupitia ' African Traditional Science / Ndumbaism ' wakisema kuwa huenda mwenzetu unatoa ' sadaka ' unadhani zitakuwa na mashaka? Hivi na Wewe ungekuwa ' unajichanganya ' Misibani ' umbea ' huu wa sisi ' Waswahili ' kuwa unafanya ' shiriki ' ungeanza kushika kasi na hata kuanza kuaminika na wengi?
Nakuruhusu unichukie kama utapenda au kujisikia kufanya hivyo ILA nakuomba tu haya ambayo huwa nakuandikia uwe unayachukua na kuyafanyia Kazi kwani kwa ' Zawadi ' ya Kipekee kabisa ambayo nimepewa na Mwenyezi Mungu yawezekana Mimi pamoja na Wana JamiiForums wote humu tukawa ni ' Tochi ' yako nzuri ya kukusaidia utuongoze vyema ila bahati mbaya sana mwenzetu hii ' Tochi ' unaichukia na unaidharau sana.
Nawapeni pole zangu za dhati sana Wafiwa wote, Uongozi mzima wa Shule ya Lucky Vicent na Walimu wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, wana Arusha wote na Watanzania kwa ujumla kwa Msiba huu mkubwa na mzito sana na kikubwa sote tuungane na tuwaombee maziko na makazi mema huko katika Nyumba zao za Milele hawa Wapendwa wetu. Tuliwapenda ila Mwenyezi Mungu kawapenda zaidi na Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe Amen.
Alivyoshangiliwa lowassa alitamani kuzima TVRais ametumia busara kudelegate msiba kwa mkuu wa mkoa na viongozi wengine.
Hivi Rais akianza kuhudhuria kila msiba ili awaridhishe watu na kuonyesha 'utu' wake, kila siku atajikuta yupo msibani. Kweli ni msiba wa watoto wetu, inauma sana kupoteza vijana wetu wadogo, hazina ya Taifa. Je na wale waliofariki kwenye ajali iliyofuatia kutokea Tanga Jumapili nao si ni Watanzania, wazazi, walezi na watoto pengine. Nao ufanywe msiba wa Taifa, bendera iwe nusu mlingoti na Rais ahudhurie msibani kuwapa pole wafiwa.
Whats next kwa vifo vingine ? Ndio maana hata kule Bukoba baada ya tetemeko hakukimbilia kwenda. Angekwenda leo angekua kwenye lawama kubwa kulaumiwa ubaguzi wa misiba.
hivi kwa akili yako unadhani kuwa wewe ndiye mwenye akiliu peke yako hapa duniani. na hata kutoa vioja vyako hapa kwa lugha ya kujilinda linda ili eti usijibiwe wewe ni naniNilishaacha ' kujibizana ' na ' Hopeless Creatures ' zamani sana.
What facts do you want????Mtazamo mzuri. Ila sio fact
hivi kwa akili yako unadhani kuwa wewe ndiye mwenye akiliu peke yako hapa duniani. na hata kutoa vioja vyako hapa kwa lugha ya kujilinda linda ili eti usijibiwe wewe ni nani
Ndiyo hivyo sasa ' ulijipendekeza ' na nikakupa ' dozi ' yako ' mujarab ' kabisa na sasa naona unaanza kuweweseka nami.
Hakuna cha dozi hapo nimekumbia ukweli na ndiyo maaana wewe ndiye unaweweseka .Ndiyo hivyo sasa ' ulijipendekeza ' na nikakupa ' dozi ' yako ' mujarab ' kabisa na sasa naona unaanza kuweweseka nami.
Ni heri kuuchuna tu,maana hata wasaidizi wakaribu yake wamemshindwa.
Lakini si uliona alilia? ile inatosha asije akaenda kwenye misiba kutimiliza ndoto ya Godbles Lema.Mheshimiwa Rais wangu Dkt. Magufuli kusema ukweli na wala hili nisikufiche kama wengine wanavyokuchekea kukuambia ukweli kuwa hata kama unatonyesha jitahada zako na kwakweli nyingi tu tunaanza kuziona na tunakushukuru kwa hilo ILA unatupa Kazi ngumu na kubwa mno ya ' kukutea ' humu mitaani na hata mitandaoni juu ya hii tabia yako ambayo sasa naanza kujiuliza ni ya Wasukuma kweli hawa hawa ninaowajua au labda mwenzetu Wewe ni Mwana Diaspora wa Taifa jingine ambalo halina utu huu wa Kitanzania uliozoeleka?
Katika utamaduni wa Kiafrika ni SIFA mbaya sana tena kwa Kiongozi kabisa wa nchi ( HEAD OF STATE / PRESIDENT ) kukacha kabisa kwenda kuhudhuria ' Misiba ' ambayo yawezekana hata hao waliokufa 99% walikupigia Kura au pengine hata Wazazi wao walihakikisha leo Wewe uwe hapo ulipo.
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli Mimi GENTAMYCINE itabidi tu univumilie kwani huwa sina tabia ya kumficha Mtu hata kama ni Rafiki yangu au ni Kipenzi changu na hivi ndivyo Mwenyezi Mungu alivyoniumba na sitokuja kubadilika hadi naingia Kaburini na nitasema ukweli pale panapostahili na nitakosoa mara moja kama hivi pale ninapoona pana tatizo kwani sikuumbwa kuwa ' Mnafiki ' kama wengi wanaokuzunguka.
Mheshimiwa Rais wangu Dkt. Magufuli hivi una ' matatizo ' gani na Misiba au Maiti? Mbona Mimi nimeishi miaka mitatu ( 3 ) na ' Wananzengo ' wa Kisukuma kule Nyegezi, Luchelele, Nsumba, Malimbe, Mkolani na Buhongwa lakini tulikuwa ' tunajumuika ' nao sana Misibani na hata Mazishini? Hii picha unayotuonyesha Watanzania sasa unataka tukueleweje Mheshimiwa?
Hukwenda Kagera Watu tukajipinda humu kukutetea labda kwa kuhisi kuwa ungejishtukia na kubadilika ikawa vile vile tukasema ' poa ' mara tena ' Wapiganaji ' wako Askari wa Police waliuwawa ' Kinyama ' mno kule Kibiti kama kawaida hukwenda na kama jadi yetu Wanaume tukaja humu tena ' kutiririka ' kwa kukutetea lakini mioyo yetu inatusuta ila tumeshazoea kujikaza ' kisabuni ' kwa kujua labda moyo wako ungajawa na ' aibu ' na ungabadilika kumbe ndiyo kama vile tulikuwa tunapaka ' Upepo ' rangi.
Sasa kali katika yote Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli hili la juzi tu ' masikini ya Mungu ' Taifa limepoteza Wapendwa wetu kabisa tena wakiwa bado wadogo na wana Ndoto za kuja kuwa Watu fulani wa muhimu katika Taifa hili huku kuna wengine pia huwezi jua walikuwa wanataka kuja kuwa ' watiririkaji ' kama GENTAMYCINE lakini safari yao ikafikia tamati katika Mlima wa Rhotie Marera kwa kufariki dunia pamoja na Walimu wao na Dereva wa lile Basi.
Huku ' watetezi ' wako ' tukisikilizia ' kwa mbali kuona labda safari hii ' mshipa ' wako wa ' aibu ' utakunjuka kwa ' kutukuka ' na utahudhuria Msiba ghafla tunaona Press Release kutoka IKULU ya kutoa rambirambi zako na baadae tena tunatangaziwa kuwa Wewe hutokwenda ila utawakilishwa na Makamu wako wa Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassan.
Hatukatai kuwa uwepo wa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan pale Sheikh Amri Abeid Kaluta ni jambo jema ila nadhani uwepo wake pale ' ungenoga ' kama si ' kupendeza ' mno endapo Wewe Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ungekuwa haupo nchini Tanzania ila kumbe umemtuma Yeye ( Makamu wa Rais ) halafu Wewe ' umeunyuti ' zako tu hapo IKULU ya Magogoni na ratiba zako za hapa na pale.
Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli leo kwa mara ya Kwanza kabisa naungana na maneno yako unayopenda kuyasema kila mara kuwa nakunukuu " Watanzani mniombee " na yawezekana kumbe sisi Watanzania tukawa hatujui huwa unamaanisha nini ila GENTAMYCINE leo nimegundua kuwa yawezekana unaposema tukuombee labda unataka Watanzania tumwambie Mwenyezi Mungu aweze kuukunjua huo moyo wako mgumu, akujaze upendo uliotukuka na pengine aweze kukuondolea Kisirani chako au Chuki zako au Pepo la ukatili ukatili ambalo labda mwenzetu ' umeshalichungulia ' mahala na ukaona kuwa linakuijia na si ajabu tayari limeshaweka makazi ya kudumu katika roho yako kama siyo moyo wako.
Nimalizie tu kwa kusema kuwa Mheshimiwa Rais wangu Dkt. Magufuli unatupa wakati mgumu sana wa ' kukutetea ' kwa matendo ya ajabu kama pia si ya kustaajabisha unayoyafanya. Hivi kabisa huna hata ' uchungu ' na hawa Watoto? Je ukiachillia mbali Wewe kuwa Rais wetu lakini na Wewe si ni Mzazi pia au? Basi hata ' ungetuzuga ' tu Watanzania kwa kumtuma pia Mkeo Mama yetu Janet Magufuli aandamane na Makamu wa Rais kwenda Arusha lakini hata Yeye pia hajaenda.
Hivi kwa mtindo huu hizi kauli ambazo sasa zinaanza ' kutiririka ' kuwa yawezekana haya matukio labda mwenzetu huwa unayajua kupitia ' African Traditional Science / Ndumbaism ' wakisema kuwa huenda mwenzetu unatoa ' sadaka ' unadhani zitakuwa na mashaka? Hivi na Wewe ungekuwa ' unajichanganya ' Misibani ' umbea ' huu wa sisi ' Waswahili ' kuwa unafanya ' shiriki ' ungeanza kushika kasi na hata kuanza kuaminika na wengi?
Nakuruhusu unichukie kama utapenda au kujisikia kufanya hivyo ILA nakuomba tu haya ambayo huwa nakuandikia uwe unayachukua na kuyafanyia Kazi kwani kwa ' Zawadi ' ya Kipekee kabisa ambayo nimepewa na Mwenyezi Mungu yawezekana Mimi pamoja na Wana JamiiForums wote humu tukawa ni ' Tochi ' yako nzuri ya kukusaidia utuongoze vyema ila bahati mbaya sana mwenzetu hii ' Tochi ' unaichukia na unaidharau sana.
Nawapeni pole zangu za dhati sana Wafiwa wote, Uongozi mzima wa Shule ya Lucky Vicent na Walimu wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, wana Arusha wote na Watanzania kwa ujumla kwa Msiba huu mkubwa na mzito sana na kikubwa sote tuungane na tuwaombee maziko na makazi mema huko katika Nyumba zao za Milele hawa Wapendwa wetu. Tuliwapenda ila Mwenyezi Mungu kawapenda zaidi na Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe Amen.
Kusalimia kukejeli?mwacheni huwezi jua amepatwa na nini? ni mtu mzima yule anajua anachokifanya mbona kagera alienda baadaye kusalimia labda ana moyo mwepesi analia zake ndani, kumuona rais analia nje aibu nayo...mwacheni akipata nguvu atakuja kutoa pole.
May b,It was in DSMSi huwa anaenda mingine jamani!! Kama nakumbuka vizuri alienda kwenye msiba wa Dr. Didas masaburi.
Kukaa IKULU na kuangalia ' mubashara ' uagwaji wa Marehemu na ' kutwiti ' mtandaoni kuwa nae amelia ndiyo hayo ' Maendeleo ' yako unayosema anayafanya? Mkuu tafadhali sitaki ' nikudharau ' halafu ukajiona Mtu usiye na thamani tena hapa duniani. Kajifunze kujenga ' Hoja ' na ukishakomaa kisawasawa urudi tena humu ili tukupime kama ' umekwiva ' au bado sawa?