Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 943
- 4,458
Mwita Waitara akiwa mbele ya Komredi Kinana ameeleza wananchi na wanachama wa CCM kwamba uchaguzi wa serikali za mtaa na uchaguzi mkuu hautakuwa na demokrasia katika jimbo lake. Wakati akiyasema hayo viongozi wa CCM wa kitaifa wameonekana kufurahia kauli hiyo na kumuunga mkono.
Katika hali isiyo tegemewa amesema sheria za nchi zinaishia katika daraja la Mto Kirumi ambalo ni mpaka wa wilaya hiyo. Kwa mtizamo wangu na kuzingatia presha iliyopo kwa sasa naamini huu ndio msimamo wa CCM na Makamu mwenyekiti Kinana ameunga mkono hoja hii kwanza kwa kushangilia bila kuonyesha kukerwa, pili kwa kukaa kimya kwenye majumuisho na tatu kwa kumruhusu Mbunge huyu kuendelea kuhubiri chuki na uvunjaji wa sheria.
Lakini pia mbunge naposema hakutakuwa na sheria za uchaguzi na tume ikakaa kimya maana yake hii ni agenda ambayo imebarikiwa na watwala.
=======
Katika hali isiyo tegemewa amesema sheria za nchi zinaishia katika daraja la Mto Kirumi ambalo ni mpaka wa wilaya hiyo. Kwa mtizamo wangu na kuzingatia presha iliyopo kwa sasa naamini huu ndio msimamo wa CCM na Makamu mwenyekiti Kinana ameunga mkono hoja hii kwanza kwa kushangilia bila kuonyesha kukerwa, pili kwa kukaa kimya kwenye majumuisho na tatu kwa kumruhusu Mbunge huyu kuendelea kuhubiri chuki na uvunjaji wa sheria.
Lakini pia mbunge naposema hakutakuwa na sheria za uchaguzi na tume ikakaa kimya maana yake hii ni agenda ambayo imebarikiwa na watwala.
=======