Mbinu za kupata Mishangazi ya JF

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Aug 6, 2020
3,735
7,074
Hizi mbinu ninazo wapa haimaanishi kwamba mimi binafsi nimezitumia au nilishawahi kuzitumia ila hii inatokana na uzoefu wangu mdogo humu jamvini

Kwakuwa wanawake wanapenda mambo mazuri basi hupenda kuwa na wanaume ambao walau wako njema hata kama hawana pesa mingi kivile ili mradi wapate uhakika wa kutimiziwa mahitaji yao na kutatuliwa shida zao ndogo ndogo.

Kwanza mwamba ingia jukwaa la ujenzi kule halafu ulizia gharama mbali mbali za vifaa vya ujenzi, na ikikupendeza waeza kuulizia sehemu ambayo unaweza kupata viwanja kwa ajili ya makazi, hapo mwamba utakuwa umeanza safari yako ya kuwakaribia mashangazi

Nenda jukwaa la gereji kule kwa wataalamu wa magari, ima jifanye unataka kujua aina nzuri ya gari na upatikanaji wa vipuli kwa bei rahisi,,au kutaka kujua gari gani ndio ziko hot kwasasa, trust me hapo mishangazi itakuwa inakukodolea mimacho kazi kwako

Hakikisha unapoleta mastory katika uzi au unapo comment, tengeneza matukio ambayo yataonyesha kuwa unamiliki gari, kwa mfano "nilipofika pale nikapaki gari yangu kisha nikaenda sehemu fulani au ofisi fulani, mwamba hapo unablow their mind

Ikikupendeza zaidi onyesha unajali sana kuhusu wanawake na uwe mkali kwa kila member ambaye kwa namna moja au nyingine anadharau madam zetu, hapo utakuwa umejipa hadhi ya juu kabisa kuhusu hawa viumbe

Linapokuja swala la kutoka out wikiend onyesha unapendelea kutembelea sehemu ambazo zina hadhi hapo mjini ambazo watu wenye hadhi zao hupendelea maeneo hayo, hii inanikumbusha madam mmoja ambaye alikuwa best yangu alikuwa anawasiliana na mwamba mmoja katika mitandao ya kijamii

Huyo mwamba alikuwa anaswaga si za nchi hii, kila anapoenda basi anamwambia yule madam, kwamba katoka sehemu fulani now anaenda sehemu fulani, mara katoka supermarket fulani na sasa anaelekea kiwanja fulani, na sehumu zote hizo ni zenye hadhi yake mjini, basi yule madam akawa ana hamu kweli ya kuonana na yule mwamba, hao ndio madam zetu.

Anyways turudi katika mada yetu sasa, baada ya hatua hizo now ni hatua za utekelezaji, usiingie pm ghafla kama mvamizi bali tengeneza ukaribu na mshangazi uliye mpoint.

Hakikisha una get their attention kwa kulike comment zao hata kama za kipuuzi, lengo ni kuwa familiar kwake kwahiyo hata ukiingia pm unakuwa sio mgeni kwake

Angalizo, tumieni mbinu zozote mnazo weza lakini msizitumie kwa madam mmoja huku jf huwa napenda kumwita "my" siku hizi, mwenyewe anajijua hahaha! It does'nt matter whether am serious or just joking but i do like her anyway

Mbinu nyingine nitawapa mara baada ya mwanasheria wangu kupatikana hewani naona yupo sehemu ambayo network haipatikani vizuri

Utakuja kunipa medali zangu baadae ukizifuata mbinu hizi

Ni hayo tu!
 
FB_IMG_1712649996673.jpg
 
Back
Top Bottom