ubarinolutu
JF-Expert Member
- Oct 22, 2012
- 1,978
- 3,917
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya linamshikilia Joseph Mbilinyi (SUGU) kwa tuhuma za kuratibu maandamano kinyume cha Sheria, tukio hilo limetokea leo alipokuwa anachukua fomu ya kuwania tiketi ya Ubunge jimbo la Mbeya Mjini kupitia tiketi ya chama chake cha Chadema.
Sugu amekamatwa pamoja na wanachama wa Wengine wa CHADEMA. Baadhi ya Waliokamatwa ni Stive Mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa, Katibu wa mbunge, Kasambala.
Hii imetokeaa bila kujulikana sababu, angalia.
=====
UPDATES;
======
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya, limeiambia JamiiForums kwamba Lissu walimpeleka kituoni kumuelekeza utaratibu unaotakiwa kifuatwa wakati wa Mkusanyiko. Amesema kulikuwa na maandamano Makubwa na Polisi hawakua na taarifa. Hivyo ikabidi aelekezwe Umuhimu wa Ushirikiano kati ya vyama vya siasa na Polisi. Amesema Mbilinyi hajaingizwa Mahabusu wala kuandikishwa maelezo.
Walimuelekeza madhara ya maandamano yasiyokuwa ba utaratibu ikiwemo kuzuia shughuli za maendeleo.
Baada ya maongezi hayo walimuachia yeye na watu wengine waendelee na shughuli zao za kisiasa.
Sugu amekamatwa pamoja na wanachama wa Wengine wa CHADEMA. Baadhi ya Waliokamatwa ni Stive Mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa, Katibu wa mbunge, Kasambala.
Hii imetokeaa bila kujulikana sababu, angalia.
=====
UPDATES;
======
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya, limeiambia JamiiForums kwamba Lissu walimpeleka kituoni kumuelekeza utaratibu unaotakiwa kifuatwa wakati wa Mkusanyiko. Amesema kulikuwa na maandamano Makubwa na Polisi hawakua na taarifa. Hivyo ikabidi aelekezwe Umuhimu wa Ushirikiano kati ya vyama vya siasa na Polisi. Amesema Mbilinyi hajaingizwa Mahabusu wala kuandikishwa maelezo.
Walimuelekeza madhara ya maandamano yasiyokuwa ba utaratibu ikiwemo kuzuia shughuli za maendeleo.
Baada ya maongezi hayo walimuachia yeye na watu wengine waendelee na shughuli zao za kisiasa.