KERO Mashirika ya kigeni yanayojiita Humanitarian au International NGO's na kasumba za ubaguzi kwa waajiriwa wazawa!

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Ndivyo yalivyo hayo Mashirika,lipo lingine linajiita GOOD NEIGHBORS ni la Kikorea,nalo ni Shirika la kihuni linajifanya linahamasisha miradi ya maendeleo vijijini lakini kiuhalisia linahamisha USHOGA. Wananchi hupewa sharti kwamba wajaze fomu wakikiri kwamba ni washiriki wa mapenzi ya jinsia moja ili waletewe misaada kama zana za kilimo nk.

Ukitaka udumu kwenye hilo Shirika ni ujipendekeze sana kwa kimama fulani ki-Country Director(Kikorea)na kidada fulani ki-Head of HR kinaitwa Helena. Yaani ni Umbea na Majungu tu kwenye hili Shirika,wao kufuata Sheria za Nchi ni kwa kinyumenyume.

Na hawakomi,miaka minne iliyopita aliyewahi kuwa Mkuu wao hapa Tanzania alifukuzwa nchini na Serikali kwa makosa mbalinbali ya kunyanyasa wazawa lakini hata aliyekuja mambo ni yaleyale na Serikali inashindwa kuchukua hatua.

Nilifanya kazi mwaka mmoja na hili Shirika, kazi ya kuhamasisha USHOGA ilinishinda nikaamua kuacha kazi
Kwendeni huko wabongo ni watu wavivu sana halafu tunataka kula kwa ulaini tu. Kazi kulalamika muda wote. Mkiambiwa CCM ni janga unganeni itoke mnajifanya hamsikii.
 
Mleta mada umeongea mengi lakini kukujibu

1 Mashirika yote ya kigeni huwa wana idadi ya watu wanaoruhusiwa kuwaleta watakaoamua wenyewe Kumbuka hizo pesa za misaada au mitaji wanatoka nayo kwao kwa hiyo. Lazima wawe na watu wao wa kusimamia hizo shughuli na pesa zao.Uhamiaji wanaruhudu watu sita .Wao wenyewe wenye hela zao ndio huamua wamlete nani kwa nafasi ipi mara nyingi vyeo vya juu na vya fedha,na usimamizi vitengo mara nyingi hushika wao wenyewe iwe NGO ya kimataifa au kampuni ya kimataifa ya uwekezaji .Hivyo mwajiriwa mzawa kushika vyeo hivyo vikubwa vya juu huwa sio rahisi japo wengine huachia lakini hawalazimiki

2.Mishahara huwa kuna utofauti wao wa nje hulipwa mishahara yao kule kwao makao makuu kwa dola wakati sheria zetu xinataka mwajiriwa mzawa alipwe kwa viwango vya dani ya nchi kwa pesa ya ndani alipoajiriwa na NGO iliposajiliwa.Ikisajiliwa Tanzania kama tawi utalipwa kwa sheria na viwango vya Tanzania sio vya nje.Wao wenye shirika watalipwa kwa viwango vya kwao nchini kwao na sheria za kwao

Sheria za nchi zinakubana wewe mzawa.Ukitaka kufaidika upate uhamisho wa shirika hilo hilo utoke Tanzania uhamishiwe hata kenya hapo.Mshahara utabadilika utalipwa kwa viwango vya kimataifa vya kwao sio vya kenya au Tanzania sababu sasa unakuwa mfanyakazi wa head office

Ushauri vuta subira chapa kazi kuna siku waweza kuona kama uko vizuri wakakupeleka branch zingine nchi zingine
wewe unaijua idadi ya watu wa kigeni waliopo MSF sasa hvi? au unaongea tu? ni zaidi ya sita kwa project ya Nduta na nasikia kwa project ya liwale wako 10 na zaidi, na ndio mana nikasema wametumia sheria zetu kutubana wazawa kawasababu wameona loop hole kwenye sheria na hata sheria za uhamiaji.
wanapewa business visa lakini mtu anafanya kazi anatakiwa kupewa work permit. kwahiyo ndio mana wale wanaozidi sita hawakai muda mrefu anakaa less than six months alaf anakuja mwingine wanasema amekuja kutembea kumbe anafanya kazi without work permit.
Alaf wanakuja watu ni wabaguzi sana yani acha tu.
 
wewe unaijua idadi ya watu wa kigeni waliopo MSF sasa hvi? au unaongea tu? ni zaidi ya sita kwa project ya Nduta na nasikia kwa project ya liwale wako 10 na zaidi, na ndio mana nikasema wametumia sheria zetu kutubana wazawa kawasababu wameona loop hole kwenye sheria na hata sheria za uhamiaji.
wanapewa business visa lakini mtu anafanya kazi anatakiwa kupewa work permit. kwahiyo ndio mana wale wanaozidi sita hawakai muda mrefu anakaa less than six months alaf anakuja mwingine wanasema amekuja kutembea kumbe anafanya kazi without work permit.
Alaf wanakuja watu ni wabaguzi sana yani acha tu.
Mkuu tour guider Zanzibar analaza mpka laki 2 net. Mashirika haya kama Kuna Kaz nyibgine unafanya tu.. mm nataka nikasomee Italia na German niingie rasmi kwenye utalii.
 
wewe unaijua idadi ya watu wa kigeni waliopo MSF sasa hvi? au unaongea tu? ni zaidi ya sita kwa project ya Nduta na nasikia kwa project ya liwale wako 10 na zaidi, na ndio mana nikasema wametumia sheria zetu kutubana wazawa kawasababu wameona loop hole kwenye sheria na hata sheria za uhamiaji.
wanapewa business visa lakini mtu anafanya kazi anatakiwa kupewa work permit. kwahiyo ndio mana wale wanaozidi sita hawakai muda mrefu anakaa less than six months alaf anakuja mwingine wanasema amekuja kutembea kumbe anafanya kazi without work permit.
Alaf wanakuja watu ni wabaguzi sana yani acha tu.
Tena watakubana sana. Kuandika kwenyewe kiswahili hujui halafu unalilia mshahara mkubwa! Eti wabaguzi! Unabaguliwaje ukiwa kwenye nchi yako kama wewe siyo nanga!
 
Habari za Asubui wana JF,

Naomba kuleta mada kwenu kuhusu haya mashirika ya kigeni yanayojiita ya kusaidia binadamu (humanitarian) au kujiita mashirika ya kimataifa yasiokuwa ya kiserikali (INGO). kwa mfano; Medecins sans frontieres, Medecins du monde na mengine mengi.

Kwanza kabisa mimi ni mwajiriwa wa moja ya haya mashirika na kilichonileta huku ilikuwa sio mshahara au maslahi mazuri bali ukosefu wa ajira wa muda mrefu na kukaa sana mtaani bila kazi maalum.

Nilipata shavu kwenye hizi shirika za kigeni humanitarian, lakini nilichokutana nacho huku nafikiri sijawahi kutana nacho toka nimeanza kufanya kazi kwenye mashirika binafsi.

Kwanza kabisa ogopa shirika lenye chimbuko au kutokea uswisi au ufaransa, hawa jamaa ni wabaguzi sijawai kuona. Pili, viwango vyao vya mishahara ni vibovu sana na hata mazingira ya kazi kwa wazawa ni magumu sana. Kuna muda unajikuta upo kama mtumwa ndani ya nchi yako kwa sababu tu hauwezi kuacha kazi mana mtaani ni pagumu sana na kazi hakuna. na haya mashirika wanatumia kigezo hiko kama fimbo ya kuchapia wazawa.

Pia, wanatumia sana loop holes za sheria zetu za tanzania ili kutukandamiza, kwa mfano, kuna kitu kinaitwa internal regulations, hzi ni sheria za kikandamizi ambazo zimetungwa kulingana na sheria ya ajira ya Tanzania lakini wametumia mianya ya sheria hiyo ili kuwabana national staff.

Tukirudi kwenye mishahara, mtu anaitwa officer mshahara unaanzia laki 8 take home na hata kama ulitoka sehemu unalipwa zaidi watakuambia wao salary grid yao ipo fixed na hakuna makubaliano yoyote au negotiations zozote.

Hata ufanye kazi kama punda siku saba za wiki hakuna promotions au bonus yoyote, na hata ikitokea kuna nafasi zimetangazwa ambazo ni za level ya juu yako, itakubidi uiombe kama mtu alie nje ya shirika na ufanye interview na asilimia kubwa wanazikosa hizo nafasi.

Mwisho wa siku unajikuta unaletewa supervisor na utamfunindisha kazi. na lengo kuu ya wao kufanya hivi ni kwasababu wanataka watu wapya kutoka nje ya shirika wasiojua mienendo ya shirika. na mara nyingi wale wasiokuwa na uvumilivu huwa wanaacha kazi baada ya muda mfupi wa kuajiriwa.

Serikali yetu imelala wakati vijana wao wananyanyaswa kwenye nchi yao na wageni. mashirika haya pia ya sheria au policy inayosema mzawa au national staff kwenye field level hawezi kufika level ya manager bali ataishia level ya supervisor kushuka chini.

Mpaka muda huu toka nimeanza kazi, kuna watu kama nane wameacha kazi au kufukuzwa kwa makosa ya kipumbavu.

Sasa naendelea kujiuliza kwanini nafasi za juu za mashirika haya bado zimeshikiliwa na wazungu ambao hata sheria za tanzania hawazijui? hauwezi ukaleta HR manager kutoka vietnam au mexico au kenya ambae hajui sheria za nchi au project coordinator kutoka kenya, pakistan au nigeria wakati wapo watanzania wenye sifa na vigezo zaidi ya hao wanaokuja kushika hizo nafasi.

Kwa mfano, wana tabia ya kutangaza nafasi lakini lengo kuu ni kucheza na sheria za nchi wakati wanajua kabisa wazawa watakaoomba hizo nafasi hakuna atakaepewa kwasababu wanataka kutengeneza hoja kuwa hakuna mwenye vigezo ili walete watu wao wabaguzi kuja kushika hizo nafasi.

Kama kuna mhusika yoyote wa uhamiaji, wizara ya afya au serikali kuu ambae yumo hum tafadhali sana tunaomba muyachunguze haya masharika kabla ya kuyaruhusu kufanya kazi ndani ya nchi yetu nzuri.

Vijana wa kitanzania wanateseka na kunyanyasika ndani ya nchi yao kwa kigezo tu cha kutokuwa na ajira.

Naomba kuwasilisha!

Mkerekewa Mzawa anaefanya kazi MSF

Kazi mkipewa hamfanyi. Mkikosa mnalalamika.
 
Nipo Nduta, Nyarugusu palishafungwa. na sasa hivi baadhi yetu washapewa notice ya kufukuzwa kazi mana mradi unaelekea ukingoni!
Kama mdau hapo juu alivyodokeza, fanya mkakati wakuhamishie Uganda au Goma DRC, ukifanikiwa hapo ujue utahitajika mahali pengi Duniani. Usijifungie humu ndani! Sijui umri wako lakini naiona hiyo kama fursa ya kwenda kimataifa zaidi.
Nduta inafungwa? Kile kijiji matumizi ni yapi siku za usoni na wakimbizi watawapeleka wapi?... Sidhani kama MSF na mashirika yote ya kimataifa yaliyojichimbia hapo Kibondo watakuwa tayari kuwaruhusu wakimbizi waondoke, maana na wao kibarua kitaota mbawa!. Hakikisha shirika likiondoka Nduta na wewe usikose kwenye orodha. Kila la kheri mkuu.
 
wewe unaijua idadi ya watu wa kigeni waliopo MSF sasa hvi? au unaongea tu? ni zaidi ya sita kwa project ya Nduta na nasikia kwa project ya liwale wako 10 na zaidi, na ndio mana nikasema wametumia sheria zetu kutubana wazawa kawasababu wameona loop hole kwenye sheria na hata sheria za uhamiaji.
wanapewa business visa lakini mtu anafanya kazi anatakiwa kupewa work permit. kwahiyo ndio mana wale wanaozidi sita hawakai muda mrefu anakaa less than six months alaf anakuja mwingine wanasema amekuja kutembea kumbe anafanya kazi without work permit.
Alaf wanakuja watu ni wabaguzi sana yani acha tu.
Hamia Jhpiego au Amref

Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
 
Habari za Asubui wana JF,

Naomba kuleta mada kwenu kuhusu haya mashirika ya kigeni yanayojiita ya kusaidia binadamu (humanitarian) au kujiita mashirika ya kimataifa yasiokuwa ya kiserikali (INGO). kwa mfano; Medecins sans frontieres, Medecins du monde na mengine mengi.

Kwanza kabisa mimi ni mwajiriwa wa moja ya haya mashirika na kilichonileta huku ilikuwa sio mshahara au maslahi mazuri bali ukosefu wa ajira wa muda mrefu na kukaa sana mtaani bila kazi maalum.

Nilipata shavu kwenye hizi shirika za kigeni humanitarian, lakini nilichokutana nacho huku nafikiri sijawahi kutana nacho toka nimeanza kufanya kazi kwenye mashirika binafsi.

Kwanza kabisa ogopa shirika lenye chimbuko au kutokea uswisi au ufaransa, hawa jamaa ni wabaguzi sijawai kuona. Pili, viwango vyao vya mishahara ni vibovu sana na hata mazingira ya kazi kwa wazawa ni magumu sana. Kuna muda unajikuta upo kama mtumwa ndani ya nchi yako kwa sababu tu hauwezi kuacha kazi mana mtaani ni pagumu sana na kazi hakuna. na haya mashirika wanatumia kigezo hiko kama fimbo ya kuchapia wazawa.

Pia, wanatumia sana loop holes za sheria zetu za tanzania ili kutukandamiza, kwa mfano, kuna kitu kinaitwa internal regulations, hzi ni sheria za kikandamizi ambazo zimetungwa kulingana na sheria ya ajira ya Tanzania lakini wametumia mianya ya sheria hiyo ili kuwabana national staff.

Tukirudi kwenye mishahara, mtu anaitwa officer mshahara unaanzia laki 8 take home na hata kama ulitoka sehemu unalipwa zaidi watakuambia wao salary grid yao ipo fixed na hakuna makubaliano yoyote au negotiations zozote.

Hata ufanye kazi kama punda siku saba za wiki hakuna promotions au bonus yoyote, na hata ikitokea kuna nafasi zimetangazwa ambazo ni za level ya juu yako, itakubidi uiombe kama mtu alie nje ya shirika na ufanye interview na asilimia kubwa wanazikosa hizo nafasi.

Mwisho wa siku unajikuta unaletewa supervisor na utamfunindisha kazi. na lengo kuu ya wao kufanya hivi ni kwasababu wanataka watu wapya kutoka nje ya shirika wasiojua mienendo ya shirika. na mara nyingi wale wasiokuwa na uvumilivu huwa wanaacha kazi baada ya muda mfupi wa kuajiriwa.

Serikali yetu imelala wakati vijana wao wananyanyaswa kwenye nchi yao na wageni. mashirika haya pia ya sheria au policy inayosema mzawa au national staff kwenye field level hawezi kufika level ya manager bali ataishia level ya supervisor kushuka chini.

Mpaka muda huu toka nimeanza kazi, kuna watu kama nane wameacha kazi au kufukuzwa kwa makosa ya kipumbavu.

Sasa naendelea kujiuliza kwanini nafasi za juu za mashirika haya bado zimeshikiliwa na wazungu ambao hata sheria za tanzania hawazijui? hauwezi ukaleta HR manager kutoka vietnam au mexico au kenya ambae hajui sheria za nchi au project coordinator kutoka kenya, pakistan au nigeria wakati wapo watanzania wenye sifa na vigezo zaidi ya hao wanaokuja kushika hizo nafasi.

Kwa mfano, wana tabia ya kutangaza nafasi lakini lengo kuu ni kucheza na sheria za nchi wakati wanajua kabisa wazawa watakaoomba hizo nafasi hakuna atakaepewa kwasababu wanataka kutengeneza hoja kuwa hakuna mwenye vigezo ili walete watu wao wabaguzi kuja kushika hizo nafasi.

Kama kuna mhusika yoyote wa uhamiaji, wizara ya afya au serikali kuu ambae yumo hum tafadhali sana tunaomba muyachunguze haya masharika kabla ya kuyaruhusu kufanya kazi ndani ya nchi yetu nzuri.

Vijana wa kitanzania wanateseka na kunyanyasika ndani ya nchi yao kwa kigezo tu cha kutokuwa na ajira.

Naomba kuwasilisha!

Mkerekewa Mzawa anaefanya kazi MSF
Hauna qualifications wewe, acha kulialia
 
Pia sio mashirika yote ni ya hovyo
Tuko tunakula bata Chuga huku kiroho safi na International NGOs
Habar KIONGOZ,mi dereva ila sjawah fanya kazi international NGO yeyote,lkin nataman nifanye Kaz mashirika au hizo taasisi, Please km Kuna chance nisaidie hapo nijitose.
 
Back
Top Bottom