Mapishi ya Aina Mbalimbali, Matango ya Baharini na Pilipili Hoho

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,357
33,200
Mapishi ya kuku aliyekaangwa



Mahitaji
xinsrc_090504101553283165724.jpg

kuku mmoja, chumvi gramu 3, sukari gramu 15, mchuzi wa sosi gramu 10, mvinyo wa kupikia gramu 15, pilipili manga gramu 2, vitunguu maji gramu 15, tangawizi gramu 15, chembechembe za kukoleza ladha gramu 1, mafuta ya ufuta gramu 10.
Njia
1.Kataa kichwa, miguu ya kuku, halafu weka kwenye maji moto, chemsha kwa dakika 5 halafu apakue.
2.Changanya chumvi, sukari, mchuzi wa sosi, mvinyo wa kupikia, pilipili manga halafu paka kwenye kuku, halafu weka tangawizi na vitunguu maji kwenye tumbo la kuku, halafu weka kwenye sahani, chemsha maji, endelea kuchemsha maji kwa mvuke. Halafu pakua, na kupaka sukari na ondoa vitunguu maji, tangawizi na pilipili manga.
3.Washa moto mimina mafuta kwenye sufuria, weka kuku kwenye sufuria kasha mkaange, mpaka ngozi yake iwe rangi ya hudhurungi, ipakue. Uikate iwe vipande.
4.Koroga chembechembe za kukoleza ladha, sukari na mafuta ya ufuta pamoja na sosi ya kuchemshia kuku, halafu mimina kwenye kuku. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

Mapishi ya vipande vya mzizi wa yungiyungi



20080106_561a7c4cbadc2eb85135jfE2YcF6OQ44.jpg
Mahitaji Mzizi mmoja wa yungiyungi, pilipili hoho gramu 10, vitunguu saumu gramu 5, chumvi kijiko kimoja, sukari kijiko kimoja, siki vijiko viwili, mchuzi wa sosi nusu kijiko
Njia:
1. kata mzizi wa yungiyungi uwe vipande, halafu weka vipande kwenye maji, kasha katakata pilipili hoho iwe vipande.
2. washa moto, tia mafuta kwenye sufuria, halafu tia vipande vya pilipili hoho, vitunguu swaumu, korogakoroga, halafu tia vipande vya mzizi wa yungiyungi, korogakoroga, tia chumvi, mchuzi wa sosi, siki na sukari, korogakoroga, halafu ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

print.gif
tj.gif
mail.gif

Mapishi ya matango ya baharini na pilipili hoho


Mahitaji
2007110615281938955.jpg

Matango kumi ya baharini, pilipili hoho gramu 10, vipande vya vitunguu maji, mvinyo wa kupikia kijiko kimoja, sukari nusu ya kijiko, mchuzi wa sosi kijiko kimoja, maji ya wanga vijiko viwili, chumvi vijiko viwili.
Njia
1. osha matango ya baharini, halafu chemsha maji, tia matango ya baharini kwenye maji, halafu yapakue na uyakate yawe vipande.
2. washa moto, tia mafuta kwenye sufuria, tia vipande vya vitunguu maji, halafu tia matango ya baharini, korogakoroga, mimina mvinyo wa kupikia, tia sukari, mchuzi wa sosi, mimina maji ya wanga, baada ya kuchemka, tia pilipili hoho korogakoroga, tia chumvi korogakoroga, ipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.


Mapishi ya kupika samaki kwa mvuke



20071008114701203.jpg
Mahitaji: Samaki mmoja, nyama ya nguruwe gramu 100, karoti gramu 50, mvinyo wa kupikia vijiko vitatu, mchuzi wa sosi vijiko vitatu, sukari kijiko kimoja, siki kijiko kimoja, chumvi nusu kijiko, chembechembe za kukoleza ladha nusu kijiko, mafuta ya pilipili manga kijiko kimoja, sosi iliyotengenezwa na maharagwe, kiasi kidogo cha wanga, vitunguu maji na tangawizi.
Njia:
1. ondoa vitu vilivyo ndani ya tumbo la samaki, halafu osha samaki na umkate awe vipande, paka sosi iliyotengenezwa na maharagwe kwenye samaki. Washa moto mimina maji kwenye sufuria, weka vipande vya samaki kwenye sufuria vikaange, halafu vipakue.
2. washa moto tena, tia mafuta kwenye sufuria, tia vipande vya vitunguu maji na tangawizi, korogakoroga, tia vipande vya nyama ya nguruwe, vipande vya karoti korogakoroga, mimina mvinyo wa kupikia, siki, mchuzi wa sosi, sukari na chumvi baada ya kuchemka, tia vipande vya samaki, halafu punguza moto na funika kwa mfuniko pika kwa mvuke, baada ya sosi kukauka imekausha, ondoa vitunguu maji na tangawizi, tia chembechembe za kukoleza ladha, mimina maji ya wanga, korogakoroga, mimina mafuta ya pilipili manga. Pakua. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.



Mapishi ya ngisi na liki



debcca4997866d1bcdaed6b9b6cc9e2a.jpg
Mahitaji:

Liki gramu 20, pilipili mboga gramu 20, pilipili hoho gramu 20, ngisi gramu 50, chumvi kijiko kimoja, sosi ya chaza vijiko viwili, sosi ya mchuzi kijiko kimoja, vipande vya tangawizi na vitunguu saumu
Njia:
1. washa moto, halafu chemsha maji weka vipande vya ngisi kwenye maji korogakoroga, na vipakue.
2. kata liki iwe vipande, kata pilipili mboga na pilipili hoho ziwe vipande.
3.washa moto tena, mimina mafuta kwenye sufuria, tia vipande vya tangawizi na vitunguu saumu korogakoroga, tia vipande vya pilipili mboga na pilipili hoho korogakoroga, tia vipande vya liki korogakoroga, mimina sosi ya chaza, sosi ya mchuzi, chumvi, korogakoroga halafu tia vipande vya ngisi korogakoroga kwa
haraka, halafu kuipakue. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.





Mapishi ya supu ya mwani na nyama ya mbavu za nguruwe


Mahitaji
1190319558.jpg

Nyama ya mbavu za nguruwe gramu 200, mwani gramu 50, vipande vya tangawizi gramu 5, chumvi vijiko viwili, mvinyo wa kupikira kijiko kimoja, mafuta ya ufuta kijiko kimoja
Njia
1. osha mwani , halafu weka kwenye sufuria yenye maji, chemsha kwa mvuke kwa nusu saa, halafu osha tena, na weka kwenye maji kwa saa nne halafu uikate iwe vipande.
2. mimina maji kwenye sufuria, tia mbavu za nyama ya nguruwe, vipande vya tangawizi, vitunguu maji, mvinyo wa kupikia, chemsha kwa dakika 20, halafu punguza moto, tia vipande vya mwani, endelea kuchemsha kwa nusu saa, ondoa vipande vya tangawizi, vitunguu maji, tia chumvi, mimina mafuta ya ufuta, korogakoroga. Ipakue. Mpaka hapo supu hiyo iko tayari kuliwa.



Mapishi ya nyama ya ng'ombe na maharagwe



Mahitaji
file_16_18_1358764649.jpg

Maharagwe gramu 350, nyama ya ng'ombe gramu 150, chumvi gramu 5, chembechembe za kukoleza ladha gramu 8, sukari gramu 5, pilipili hoho gramu 5, vipande vya vitunguu maji gramu 3, mchuzi wa sosi gramu 3.
Njia
1. kata nyama iwe vipande, koroga nyama pamoja na wanga.
2. washa moto, mimina maji kwenye sufuria, baada ya kuchemka, tia maharagwe kwenye maji, korogakoroga, yapakue. Tia mafuta kwenye sufuria, halafu tia vipande vya nyama kwenye sufuria, korogakoroga vipakue.
3. washa moto tena, tia pilipili hoho korogakoroga, halafu tia maharagwe korogakoroga, halafu tia vipande vya nyama, tia chumvi, chembechembe za kukoleza ladha, mchuzi wa sosi, korogakoroga, tia sukari korogakoroga, halafu mimina maji ya wanga korogakoroga, ipakue, mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.




 

Similar Discussions

Back
Top Bottom