KERO Mamlaka ya Maji Morogoro (MORUWASA) itoe tamko sababu ya maji ya bomba kutoka machafu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Huduma ya Majisafi Manispaa ya Morogoro ni kitendawili kilichoshindikana kuteguliwa, mara nyingi maji yanatoka yakiwa machafu

Huduma ya Majisafi katika Manispaa ya Morogoro chini ya Mamlaka ya Moruwasa ni changamoto, mara kwa mara maji yamekuwa yakitoka yakiwa machafu jambo ambalo linatupa mashaka na hofu wakati tukiwa tunayatumia.
photo_2024-04-30_08-13-52.jpg
Jambo hili limekuwa kero ya muda sasa maana watumiaji tupo kwenye hatari ya kupata magonjwa yanayoweza kuepukika, suala hili limekuwa likisemwa kwa muda mrefu lakini mabadiliko ni kiduchi bado kero hiyo inaendelea kujitokeza mara kwa mara.

Kuna mdau amewahi kuleta hii kero hapa jukwaani lakini hatuoni mabadiliko yenye tija - MORUWASA hivi haya ndio maji safi mnayosambaza manispaa ya Morogoro?

Tunaomba Moruwasa watoke hadharani watueleze changamoto hii inasababishwa nanini na wawajibike kwa uharaka kuchukua hatua maana maji yamebeba usalama wetu kwa asilimia kubwa.

Hatuna taarifa zenye uthibitisho wa moja kwa moja lakini kuna watu wamekuwa wakiumwa matumbo ghafla jambo ambalo upelekea kuhusishwa na changamoto ya maji machafu yanayotoka baadhi ya nyakati kwenye mabomba ya Moruwasa.
 
Hii ishu ni ya muda mrefu sana Toka nimekuja Morogoro mwaka karibu 20 na kitu hii ishu ipo na haswa kipindi Cha mvua
 
Hayo maji yanatokea kwenye vyanzo ambavyo watu wanajisaidia huko milimani, mengine yanatoka Mindu ambayo yanatokea Mzinga jeshini na Mzumbe kwenywe mabwawa ya maji taka. Ni hatari tupu kwa afya.
 
Hayo maji yanatokea kwenye vyanzo ambavyo watu wanajisaidia huko milimani, mengine yanatoka Mindu ambayo yanatokea Mzinga jeshini na Mzumbe kwenywe mabwawa ya maji taka. Ni hatari tupu kwa afya.
Kama ni hivi Typhoid na magonjwa mengine yanayosababishwa na maji machafu itakuwa ni kawaida tu. Poleni wakazi wa Mji Kasoro Bahari!

Screenshot_20240510_133046.jpg
 
Back
Top Bottom