Victor Emilian
Member
- Jul 19, 2022
- 11
- 33
Muhtasari:
Dhumuni la nakala hii ni kuelimisha jamii kuhusiana na kanuni za kuzingatia ili kuweza kutajirika kwa kuwekeza kwenye soko la hisa. Pia, kutoa hamasa kwa vijana na wajasiriamali mbalimbali kukuza mitaji na utajiri kwa kuwekeza kwenye soko la hisa la Dar es Salaam.
(Nembo ya Soko la Hisa la Dar es Salaam “Dar es Salaam Stock Exchange” pamoja na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana “Capital Market and Security Authority” (CMSA). Chanzo: https://www.cmsa.go.tz/ , https://dse.co.tz/)
Utangulizi:
Hisa ni nini? Hisa ni sehemu ndogo ya biashara inayowakilisha umiliki wa mtu/kampuni katika biashara hiyo. Soko la hisa ni taasisi ya serikali inayowawezesha wananchi wote pamoja na raia wa kigeni kununua na kumiliki kampuni kwa kununua hisa zake. Soko la Hisa la Dar es Salaam lilianzishwa mnamo tarehe 19, mwezi Septemba, mwaka 1996 chini ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).
Hisa za kampuni kadha wa kadha huuzwa na kununuliwa kwenye soko la hisa kila siku. Mfano wa kampuni ambazo hisa zake zinapatikana kwenye soko la hisa la Dar es Salaam ni; CRDB, Dar Es Salaam Stock Exchange (DSE), National MicroFinance Bank (NMB), Swissport (SWISS), Tanga Cement Company Limited (TCCL), na kadhalika.
(Picha ya nembo za baadhi ya makampuni yaliyosajiliwa kwenye soko la hisa. Chanzo: Hifadhi ya maktaba ya picha google)
Kanuni ambazo matajiri huzingatia kabla ya kufanya uamuzi wa kununua au kuuza hisa:
1. Uwiano kati ya bei ya hisa na thamani ya hisa (Price to Value Ratio).
Kuna tofauti kati ya thamani na bei ya hisa. Bei ni kile unacholipa ili kuwa mmiliki wa hisa. Bei ya hisa hutegemea ugavi na uhitaji wa hisa (supply and demand). Thamani ni kile unachopokea kama mwekezaji baada ya kununua hisa. Thamani ya hisa hutegemea ukubwa wa mali (assets) na madeni (liabilities) katika biashara. Lengo kubwa la mwekezaji makini ni kutafuta biashara zenye mali nyingi kuliko madeni. Thamani ya biashara hupimwa kwa kuchukua mali (assets) za biashara toa madeni (liabilities) ya biashara hiyo. Kinachobaki huitwa mali wavu (net worth). Ukigawanya mali wavu (net worth) ya kampuni kwa idadi ya hisa zilizouzwa na kampuni hiyo, utapata thamani ya kila hisa moja. Kama thamani ya hisa moja ni kubwa kuliko bei ya hisa moja, inashauriwa kununua. Kwanini? Kwa sababu ni sawa na kununua kiwanja chenye mgodi wa dhahabu ndani yake kwa bei nafuu. Thamani unayopokea ni kubwa kuliko bei unayolipia. Thamani ikiwa ndogo kuliko bei, maana yake utalipia fedha nyingi kupata kitu chenye thamani ndogo.
2. Uwiano kati ya bei ya hisa na mapato kwa kila hisa moja (Price to Earnings Ratio).
Mapato katika muktadha huu ni faida baada ya kulipa kodi na riba. Mapato kwa kila hisa moja hupatikana kwa kugawanya mapato baada ya kodi na riba kwa jumla ya hisa zilizouzwa. Jibu litakalopatikana (mapato ya hisa moja) litatumika kugawanya bei ya hisa moja. Jibu litakalopatikana likiwa dogo(chini ya tano) litaashiria kwamba bei ya hisa ni nafuu na mapato kwa kila hisa moja ni makubwa(fursa ya kununua). Jibu likiwa kubwa (zaidi ya kumi) litaashiria kwamba bei ya hisa ni kubwa sana na mapato kwa kila hisa ni madogo (fursa ya kuuza na kutengeneza faida).
3. Mavuno ya gawio (Dividend yield) .
Gawio ni faida inayoingia mfukoni mwa mwekezaji. Mavuno ya gawio hupatikana kwa kuchukua gawio kwa hisa, gawanya kwa bei ya kununulia hisa mara asilimia mia. Jibu (asilimia) likiwa kubwa huashiria kwamba, kampuni inatengeneza faida kubwa na bei ya kununua hisa ni nafuu sana(fursa ya kununua). Jibu (asilimia) dogo huashiria kwamba, faida katika biashara hio ni ndogo au bei ya hisa ni kubwa sana (fursa ya kuuza).
4. Utendaji na mwenendo wa biashara pamoja na mazingira ya biashara
Mwenendo wa biashara huweza kupimwa kwa kuangalia vigezo vifuatavyo; Je? bidhaa inayouzwa inamatumizi makubwa kwenye jamii?, bidhaa itaendelea kutumika majira ya mbeleni?, je ni biashara halali?,ina ubunifu wa kutosha kuzidi biashara shindani?, inajali maslahi ya wateja,wafanyakazi pamoja na wadau wengine katika biashara hio?, je kuna uongozi bora? na kadhalika.
🤑💰💸 HADITHI YA MWANAFUNZI ANAYELIPWA HUKU AKISOMA SHULE 🤑💰💸
Kijana huyu anafahamika kwa jina la nadharia “Ukwasi". Ukwasi alitamani sana kukuza mtaji wake kwa kuwekeza kwenye biashara zenye kutengeneza faida na ambazo hazitagharimu muda wake wa masomo. Ukwasi akaanza kufuatilia jinsi ya kukuza mtaji kupitia soko la hisa na kujifunza kwa MABILIONEA waliotajirika kwa kuwekeza kwenye soko la hisa kama Charlie Munger, Benjamin Graham na Philip Fisher. Baada ya kuweka akiba kwa zaidi ya mwaka mmoja, Ukwasi akanunua hisa za benki ya CRDB kwa Tzs 100 mwaka 2019, hisa za Tanga cement kwa Tzs 1,100 mwaka 2021 na hisa za Swissport mwaka 2022 kwa Tzs 1,120. Hivi sasa yupo chuo akifaidi matunda ya jasho lake huku mtaji aliowekeza CRDB ukiwa umekua kwa 390%, mtaji aliowekeza Swissport umekua kwa 82% na mtaji aliowekeza Tanga Cement umekua kwa 35%. Licha ya hapo kila biashara hizo zikitengeneza faida anapata gawio kila mwaka. Anasoma kwa raha mustarehee!!!
(Picha za katuni zinazoashiria ukuaji wa fedha za Ukwasi kutokana na jitihada zake katika uwekezaji kwenye soko la hisa. Chanzo: https://www.vectorstock.com/royalty-free-vector/cartoon-savings-value-growth-money-profit-vector-27455969 , Rich Businessman Sleeping On Money Bags Cartoon Clipart Vector - FriendlyStock)
Tulipomuuliza siri ya mafanikio yake alitaja kanuni zilizoongelewa kwenye nakala hii hapo awali. Pia aligusia tabia ambazo zimemsaidia kufikia mafanikio hayo. Hizi ni pamoja na kuweka akiba, kujifunza kuhusu uwekezaji kwa kusoma nakala kuhusu biashara na uwekezaji na kusikiliza matajiri waliofanikiwa kwa kununua hisa. Cha mwisho na muhimu zaidi, alizungumzia kuhusu umuhimu wa kumuomba Mungu na uthubutu wa kuchukua hatua. Ukwasi anaamini kwamba kanuni pamoja na tabia hizi zitaweza kuisaidia jamii kuweza kuwa matajiri kwa kuwekeza kwenye soko la hisa.
Dhumuni la nakala hii ni kuelimisha jamii kuhusiana na kanuni za kuzingatia ili kuweza kutajirika kwa kuwekeza kwenye soko la hisa. Pia, kutoa hamasa kwa vijana na wajasiriamali mbalimbali kukuza mitaji na utajiri kwa kuwekeza kwenye soko la hisa la Dar es Salaam.
(Nembo ya Soko la Hisa la Dar es Salaam “Dar es Salaam Stock Exchange” pamoja na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana “Capital Market and Security Authority” (CMSA). Chanzo: https://www.cmsa.go.tz/ , https://dse.co.tz/)
Utangulizi:
Hisa ni nini? Hisa ni sehemu ndogo ya biashara inayowakilisha umiliki wa mtu/kampuni katika biashara hiyo. Soko la hisa ni taasisi ya serikali inayowawezesha wananchi wote pamoja na raia wa kigeni kununua na kumiliki kampuni kwa kununua hisa zake. Soko la Hisa la Dar es Salaam lilianzishwa mnamo tarehe 19, mwezi Septemba, mwaka 1996 chini ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).
Hisa za kampuni kadha wa kadha huuzwa na kununuliwa kwenye soko la hisa kila siku. Mfano wa kampuni ambazo hisa zake zinapatikana kwenye soko la hisa la Dar es Salaam ni; CRDB, Dar Es Salaam Stock Exchange (DSE), National MicroFinance Bank (NMB), Swissport (SWISS), Tanga Cement Company Limited (TCCL), na kadhalika.
(Picha ya nembo za baadhi ya makampuni yaliyosajiliwa kwenye soko la hisa. Chanzo: Hifadhi ya maktaba ya picha google)
Kanuni ambazo matajiri huzingatia kabla ya kufanya uamuzi wa kununua au kuuza hisa:
1. Uwiano kati ya bei ya hisa na thamani ya hisa (Price to Value Ratio).
Kuna tofauti kati ya thamani na bei ya hisa. Bei ni kile unacholipa ili kuwa mmiliki wa hisa. Bei ya hisa hutegemea ugavi na uhitaji wa hisa (supply and demand). Thamani ni kile unachopokea kama mwekezaji baada ya kununua hisa. Thamani ya hisa hutegemea ukubwa wa mali (assets) na madeni (liabilities) katika biashara. Lengo kubwa la mwekezaji makini ni kutafuta biashara zenye mali nyingi kuliko madeni. Thamani ya biashara hupimwa kwa kuchukua mali (assets) za biashara toa madeni (liabilities) ya biashara hiyo. Kinachobaki huitwa mali wavu (net worth). Ukigawanya mali wavu (net worth) ya kampuni kwa idadi ya hisa zilizouzwa na kampuni hiyo, utapata thamani ya kila hisa moja. Kama thamani ya hisa moja ni kubwa kuliko bei ya hisa moja, inashauriwa kununua. Kwanini? Kwa sababu ni sawa na kununua kiwanja chenye mgodi wa dhahabu ndani yake kwa bei nafuu. Thamani unayopokea ni kubwa kuliko bei unayolipia. Thamani ikiwa ndogo kuliko bei, maana yake utalipia fedha nyingi kupata kitu chenye thamani ndogo.
2. Uwiano kati ya bei ya hisa na mapato kwa kila hisa moja (Price to Earnings Ratio).
Mapato katika muktadha huu ni faida baada ya kulipa kodi na riba. Mapato kwa kila hisa moja hupatikana kwa kugawanya mapato baada ya kodi na riba kwa jumla ya hisa zilizouzwa. Jibu litakalopatikana (mapato ya hisa moja) litatumika kugawanya bei ya hisa moja. Jibu litakalopatikana likiwa dogo(chini ya tano) litaashiria kwamba bei ya hisa ni nafuu na mapato kwa kila hisa moja ni makubwa(fursa ya kununua). Jibu likiwa kubwa (zaidi ya kumi) litaashiria kwamba bei ya hisa ni kubwa sana na mapato kwa kila hisa ni madogo (fursa ya kuuza na kutengeneza faida).
3. Mavuno ya gawio (Dividend yield) .
Gawio ni faida inayoingia mfukoni mwa mwekezaji. Mavuno ya gawio hupatikana kwa kuchukua gawio kwa hisa, gawanya kwa bei ya kununulia hisa mara asilimia mia. Jibu (asilimia) likiwa kubwa huashiria kwamba, kampuni inatengeneza faida kubwa na bei ya kununua hisa ni nafuu sana(fursa ya kununua). Jibu (asilimia) dogo huashiria kwamba, faida katika biashara hio ni ndogo au bei ya hisa ni kubwa sana (fursa ya kuuza).
4. Utendaji na mwenendo wa biashara pamoja na mazingira ya biashara
Mwenendo wa biashara huweza kupimwa kwa kuangalia vigezo vifuatavyo; Je? bidhaa inayouzwa inamatumizi makubwa kwenye jamii?, bidhaa itaendelea kutumika majira ya mbeleni?, je ni biashara halali?,ina ubunifu wa kutosha kuzidi biashara shindani?, inajali maslahi ya wateja,wafanyakazi pamoja na wadau wengine katika biashara hio?, je kuna uongozi bora? na kadhalika.
🤑💰💸 HADITHI YA MWANAFUNZI ANAYELIPWA HUKU AKISOMA SHULE 🤑💰💸
Kijana huyu anafahamika kwa jina la nadharia “Ukwasi". Ukwasi alitamani sana kukuza mtaji wake kwa kuwekeza kwenye biashara zenye kutengeneza faida na ambazo hazitagharimu muda wake wa masomo. Ukwasi akaanza kufuatilia jinsi ya kukuza mtaji kupitia soko la hisa na kujifunza kwa MABILIONEA waliotajirika kwa kuwekeza kwenye soko la hisa kama Charlie Munger, Benjamin Graham na Philip Fisher. Baada ya kuweka akiba kwa zaidi ya mwaka mmoja, Ukwasi akanunua hisa za benki ya CRDB kwa Tzs 100 mwaka 2019, hisa za Tanga cement kwa Tzs 1,100 mwaka 2021 na hisa za Swissport mwaka 2022 kwa Tzs 1,120. Hivi sasa yupo chuo akifaidi matunda ya jasho lake huku mtaji aliowekeza CRDB ukiwa umekua kwa 390%, mtaji aliowekeza Swissport umekua kwa 82% na mtaji aliowekeza Tanga Cement umekua kwa 35%. Licha ya hapo kila biashara hizo zikitengeneza faida anapata gawio kila mwaka. Anasoma kwa raha mustarehee!!!
(Picha za katuni zinazoashiria ukuaji wa fedha za Ukwasi kutokana na jitihada zake katika uwekezaji kwenye soko la hisa. Chanzo: https://www.vectorstock.com/royalty-free-vector/cartoon-savings-value-growth-money-profit-vector-27455969 , Rich Businessman Sleeping On Money Bags Cartoon Clipart Vector - FriendlyStock)
Tulipomuuliza siri ya mafanikio yake alitaja kanuni zilizoongelewa kwenye nakala hii hapo awali. Pia aligusia tabia ambazo zimemsaidia kufikia mafanikio hayo. Hizi ni pamoja na kuweka akiba, kujifunza kuhusu uwekezaji kwa kusoma nakala kuhusu biashara na uwekezaji na kusikiliza matajiri waliofanikiwa kwa kununua hisa. Cha mwisho na muhimu zaidi, alizungumzia kuhusu umuhimu wa kumuomba Mungu na uthubutu wa kuchukua hatua. Ukwasi anaamini kwamba kanuni pamoja na tabia hizi zitaweza kuisaidia jamii kuweza kuwa matajiri kwa kuwekeza kwenye soko la hisa.