Care Giver
Member
- Apr 2, 2024
- 51
- 177
Habari, kwanza kabisa nitoe salam zangu za pole kwa majirani zetu Kenya kwa msiba wa CDF na wafuasi wake katika ajali ya ndege ya kivita iliyotokea tarehe 19/04/2024 wakiwa katika ziara za kikazi.
Baada ya kifo cha Mkuu wa Majeshi wao (CDF) nimetokea kuvutiwa sana na utaratibu wa majirani zetu baada ya uteuzi wa CDF mpya kuteuliwa kutoka kamandi ya majini (Navy).
Swala hili likanivutia sana nikaamua kuwafuatilia kidogo, nikagundua kumbe wao wana utaratibu wa kupokezana kwa kila kamandi kutoa CDF.
Swali langu, Je mbona huku kwetu asilimia kubwa kama si zote tunatoa Mkuu wa majeshi (CDF) kutoka Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi (MMJ) pekee?
Ina maana hizi Kamandi nyingine kama Kamandi ya Nchi Kavu, Kamandi ya Anga, Kamandi ya Majini, Kamandi ya JKT na Kamandi ya Mgambo Mkuu wa Majeshi hawezi kutokea huko?
Naomba kuwasilisha.
Baada ya kifo cha Mkuu wa Majeshi wao (CDF) nimetokea kuvutiwa sana na utaratibu wa majirani zetu baada ya uteuzi wa CDF mpya kuteuliwa kutoka kamandi ya majini (Navy).
Swala hili likanivutia sana nikaamua kuwafuatilia kidogo, nikagundua kumbe wao wana utaratibu wa kupokezana kwa kila kamandi kutoa CDF.
Swali langu, Je mbona huku kwetu asilimia kubwa kama si zote tunatoa Mkuu wa majeshi (CDF) kutoka Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi (MMJ) pekee?
Ina maana hizi Kamandi nyingine kama Kamandi ya Nchi Kavu, Kamandi ya Anga, Kamandi ya Majini, Kamandi ya JKT na Kamandi ya Mgambo Mkuu wa Majeshi hawezi kutokea huko?
Naomba kuwasilisha.