Kwanini Mashariki ya Kati ni eneo korofi lisilopata utulivu watu wanaishi ngumi mkononi?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,972
46,738
Eneo la Mashariki ya kati ni kama eneo lenye laana fulani hivi ya vurugu. Tangu nimeanza kupata akili za kufuatilia habari sijawahi kusikiliza taarifa ya habari katika redio au TV bila kusikia kuna watu Mashariki ya wakati wamezinguana.

Yani huwa hakuna kutulia, ukiachilia mbali mgogoro wa Israel na Palestina wa kudumu utasikia Iran anazinguana na Saudia, Qatar wanataka kuzichapa na Saudia, Kuna magaidi wamelipua Iraq, Maandamano ya kuwaondoa watawala, Qatar kapigwa blocked, watu wanapora meli baharini n.k
Kila pande ukigeuka ni michakato na dili za amani!

Vita vya Urusi na Ukraine vitaisha na amani ikapatikana huku Mashariki ya kati watu bado wakiwa wanashikana mashati tu, Africa japo haina amani ila vita ambavyo mara nyingi na vya ndani ya nchi huwa vinapiganwa vinaisha amani inapatikana kama ni nchi kugawanyika zinagawanyika maisha yanaendela ila sio huko Mashariki ya kati.

Ni kwa nini Mashariki ya kati hilo eneo siku zote liko kishari, kwenye tension na watu wanaishi ngumi mkononi?
 
Hata East Asia & South East Asia ilikuwa hivyo hivyo wakati na baada ya vita vya pili vya dunia hasa kipindi cha vita baridi kati ya marekani na usoviet na China.

Palichafuka kule balaah sema wametulia nowadays wamefocus na uchumi.

Na future ya dunia ni East Asia & South East Asia huko ndipo dunia inaelekea.

Nao Middle east watatulia tu muda ukifika
 
Hujiulizi hata Congo imezungukwa na nchi zipo stable kiasi lakini yenyewe haikai kwa kutulia??...

Mkuu tembo huponzwa na mkonga wake, kwa hiyo rasilimali ndio laana yenyewe maana inavutia uchumaji wa njia yoyote ile
 
Eneo la Mashariki ya kati ni kama eneo lenye laana fulani hivi ya vurugu. Tangu nimeanza kupata akili za kufuatilia habari sijawahi kusikiliza taarifa ya habari katika redio au TV bila kusikia kuna watu Mashariki ya wakati wamezinguana.

Yani huwa hakuna kutulia, ukiachilia mbali mgogoro wa Israel na Palestina wa kudumu utasikia Iran anazinguana na Saudia, Qatar wanataka kuzichapa na Saudia, Kuna magaidi wamelipua Iraq, Maandamano ya kuwaondoa watawala, Qatar kapigwa blocked, watu wanapora meli baharini n.k
Kila pande ukigeuka ni michakato na dili za amani!

Vita vya Urusi na Ukraine vitaisha na amani ikapatikana huku Mashariki ya kati watu bado wakiwa wanashikana mashati tu, Africa japo haina amani ila vita ambavyo mara nyingi na vya ndani ya nchi huwa vinapiganwa vinaisha amani inapatikana kama ni nchi kugawanyika zinagawanyika maisha yanaendela ila sio huko Mashariki ya kati.

Ni kwa nini Mashariki ya kati hilo eneo siku zote liko kishari, kwenye tension na watu wanaishi ngumi mkononi?
Hilo eneo kutulia labda hadi Abraham arudi tena......
Awaite watoto wake wawili kati ya wale nane wajadiliane halafu watupe muongozo!!
 
Westerners hawawezi kuondoka leo wala kesho kwa sababu kuna mataifa hapo wanawahitaji sana hadi wamewapa maeneo waweke base zao za kijeshi.
Wanawahitaji au marekani ndo anawahitaji ili awatumie kufanikisha malengo yake maovu na kunyonya resources zao
 
Back
Top Bottom