mdukuzi
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 16,303
- 36,738
Huenda hili likakushangaza lakini ukweli ndio huu, zaidi ya nusu ya watu wa jimboni kwake hawakumpenda.
Ila wale waliompenda walimpenda sana tena sana.
Visa vyote ninavyoandika kumuhusu Hayati Magufuli ni vya kweli sababu nilikuwa nae karibu kwa kazi fulani ambayo sitaitaja humu,nimeishi jimboni kwake Chato nikifanya kazi hiyo,nimeingia Ikulu bila appointment nikifanya kazi hiyo.haikuwa kazi ya serikali bali nikiwa kibarua kwenye mradi fulani wilayani Chato,mradi wake binafsi
Naifahamu Chato kama ninavyoifahamu Dar na Dodoma
Kwa wasiofahamu jimbo hili ngoja niwape muhtasari kidogo,nimezunguka Tanzania hii sijawahi kuona jimbo lina makabila mengi kama jimbo la Chato,huwezi kujua kabila kipi ni dominant na lipi predominant,
Chato kuna
Wahangaza,wanyambo,watutsi,
warundi,waha,wazinza,wasubi,wahaya,wazinza,wasumbwa,wasukuma,na kila mmoja hujiona hapo ni kwao kwa asili.watu wa huko hufahamu lugha hizo zote,hata hayati JPM alijua hizo lugha zote japo kihistoria baba yake alihamia.
Miaka ya nyuma Chato ilikuwa tarafa ndani ya wilaya ya Biharamulo mkoa wa Kagera ,Sasa mwaka 1990 hayati JPM akagombea ubunge na mzee Phares Kabuye,alishindwa vibaya sana kura za maoni unajua kwa nini?
Jpm alikuwa akienda vijiji vyenye wasukuma anajifanya msukuma na kuwaponda wasubi kuwa ni wakulima wa migomba mbunge wao hawezi kuwasaidia wao wakulima wa pamba,hivyo wamchague yeye.
Meanwhile akienda Biharamulo anajifanya ni Msubi na kuongea Kisubi na anawaambia yeye ni ukoo wa Wayango wazilankende,ukoo ambao hauko usukumani bali kigoma ,butundi,rwanda,uganda na makabila yanayosikilizana na wahaya.hapo atajifanya msubi orijino na kuwaponda wasukuma kuwa ni wanyamahanga yaani wavamizi wa mkoa wa Kagera,
Akienda maeneo yenye waha wengi atajifanya muha na kuongea kiha na kirundi,siasa za ukabila zikamponza akadondokea pua.
Mizimu ya kwao ikamsaidia jimbo likagawanywa mashariki na magharibi 1995 akagombea mashariki ilipo kata ya Chato akajibatiza usukuma ila kuna wakati alikuwa akijisahau na kurudia kusema yeye ni myango ukoo ambao hauko usukumani,
Akagombea kwa style ileile ya kutumia vernacular languages kulingana na audience.
Akajikuta anachukiwa na makabila mengine jimboni kwake isipokuwa wasukuma.
Uwekezaji alioufanya jimboni kwake baada ya kuwa Rais ilikuwa ni kutafuta huruma na kufuta makovu ya makabila mengine na alifanikiwa maana makabila yote yalifaidi uwekezaji ule.
Lakini watu wa Biharamulo magharibi hawatamsahau kwa maana barabara ya lami oliyotakiwa kupita mjini kwao kuelekea Bukoba ilipofika kata ya Bwanga akaichepusha kuelekea Chato,Muleba kama adhabu ya kumnyima kura 1990.
Barabara hiyo ilikuja kuwekwa lami baadae baadae sana.
Utajiuliza mbona alikuwa anashinda ubunge kila mara
kama hakuwa anapendwa?
Ni kwamba ulitumika umafia na hadaa kwa washindani wake,wengine wakitishwa au kutekwa au kuahidiwa vyeo na pesa ili wajitoe kugombea nae
Hitimisho;
Ukabila upo na Hayati JPM alichukiwa jimboni kwake sababu ya mbegu ya ukabila iliyopandwa na........
Ila wale waliompenda walimpenda sana tena sana.
Visa vyote ninavyoandika kumuhusu Hayati Magufuli ni vya kweli sababu nilikuwa nae karibu kwa kazi fulani ambayo sitaitaja humu,nimeishi jimboni kwake Chato nikifanya kazi hiyo,nimeingia Ikulu bila appointment nikifanya kazi hiyo.haikuwa kazi ya serikali bali nikiwa kibarua kwenye mradi fulani wilayani Chato,mradi wake binafsi
Naifahamu Chato kama ninavyoifahamu Dar na Dodoma
Kwa wasiofahamu jimbo hili ngoja niwape muhtasari kidogo,nimezunguka Tanzania hii sijawahi kuona jimbo lina makabila mengi kama jimbo la Chato,huwezi kujua kabila kipi ni dominant na lipi predominant,
Chato kuna
Wahangaza,wanyambo,watutsi,
warundi,waha,wazinza,wasubi,wahaya,wazinza,wasumbwa,wasukuma,na kila mmoja hujiona hapo ni kwao kwa asili.watu wa huko hufahamu lugha hizo zote,hata hayati JPM alijua hizo lugha zote japo kihistoria baba yake alihamia.
Miaka ya nyuma Chato ilikuwa tarafa ndani ya wilaya ya Biharamulo mkoa wa Kagera ,Sasa mwaka 1990 hayati JPM akagombea ubunge na mzee Phares Kabuye,alishindwa vibaya sana kura za maoni unajua kwa nini?
Jpm alikuwa akienda vijiji vyenye wasukuma anajifanya msukuma na kuwaponda wasubi kuwa ni wakulima wa migomba mbunge wao hawezi kuwasaidia wao wakulima wa pamba,hivyo wamchague yeye.
Meanwhile akienda Biharamulo anajifanya ni Msubi na kuongea Kisubi na anawaambia yeye ni ukoo wa Wayango wazilankende,ukoo ambao hauko usukumani bali kigoma ,butundi,rwanda,uganda na makabila yanayosikilizana na wahaya.hapo atajifanya msubi orijino na kuwaponda wasukuma kuwa ni wanyamahanga yaani wavamizi wa mkoa wa Kagera,
Akienda maeneo yenye waha wengi atajifanya muha na kuongea kiha na kirundi,siasa za ukabila zikamponza akadondokea pua.
Mizimu ya kwao ikamsaidia jimbo likagawanywa mashariki na magharibi 1995 akagombea mashariki ilipo kata ya Chato akajibatiza usukuma ila kuna wakati alikuwa akijisahau na kurudia kusema yeye ni myango ukoo ambao hauko usukumani,
Akagombea kwa style ileile ya kutumia vernacular languages kulingana na audience.
Akajikuta anachukiwa na makabila mengine jimboni kwake isipokuwa wasukuma.
Uwekezaji alioufanya jimboni kwake baada ya kuwa Rais ilikuwa ni kutafuta huruma na kufuta makovu ya makabila mengine na alifanikiwa maana makabila yote yalifaidi uwekezaji ule.
Lakini watu wa Biharamulo magharibi hawatamsahau kwa maana barabara ya lami oliyotakiwa kupita mjini kwao kuelekea Bukoba ilipofika kata ya Bwanga akaichepusha kuelekea Chato,Muleba kama adhabu ya kumnyima kura 1990.
Barabara hiyo ilikuja kuwekwa lami baadae baadae sana.
Utajiuliza mbona alikuwa anashinda ubunge kila mara
kama hakuwa anapendwa?
Ni kwamba ulitumika umafia na hadaa kwa washindani wake,wengine wakitishwa au kutekwa au kuahidiwa vyeo na pesa ili wajitoe kugombea nae
Hitimisho;
Ukabila upo na Hayati JPM alichukiwa jimboni kwake sababu ya mbegu ya ukabila iliyopandwa na........