Kwanini CCM pamoja na kujilimbikizia mali lakini bado wanapora Mali za Umma?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,546
34,438
Tanzania yote kuanzia kwa wenyeviti wa vitongoji, wenyeviti wa vijiji/Mitaa, madiwani, wabunge na Rais, kwa asilimia tisini na tisa nukta tisa tisa (99.99) wanatokana na Chama cha Mapinduzi.

Kwa ivo unaposikia CAG anaposema fedha zinaibiwa kwenye taasisi za umma ujue hapo anamaanisha wanaosimamia taasisi hizo ndiyo wanaoiba fedha hizo ama wanashirikiana na wezi hao wa fedha na mali za Umma.

Kwa kuwa serikali za mitaa na serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania zinasimamiwa na CCM, kwa maana nyingine wanaoiba mali za umma ama ni CCM ama CCM inashirikiana na wezi hao au CCM inafaidika na wizi huo, ama CCM haina uwezo wa kupambana na wizi huo wa mali za Umma.

Lakini mtu unaweza kujiuliza ni kwa nini wana CCM na CCM yao ambayo imejilimbikizia mali za umma BADO wanakwiba mali za umma!?

Kila wizi mkubwa unaohusisha fedha nyingi za umma huwezi kosa wana CCM ndani mwake na hukuti mwana CHADEMA hata mmoja. Sote tunakumbuka zile fedha za Tegeta Escrow zilivyochotwa na nani waliohusika kama si wana CCM?

Mpaka leo hatujaambiwa ni kina nani walibeba hela toka kwenye Benki ya Stanbic zikiwa kwenye mifuko ya sandarusi (Visalfeti). Kama wabebaji wa zile fedha wasingekuwa ni wana CCM leo hii wangekuwa washatajwa kitambo sana.

CCM ridhikeni basi kwa mlichotupora kwa kuzionea huruma mali za Umma.
 
Nenda ukaibe uone cha mtema kuni . Chini ya serikali ya CCM na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan ukigusa pesa ya umma ni lazima unate kama ulimbo.na kukiona cha moto.ndio maana waliogusa pesa za umma wengine walishapotea kazi zao,wengine kutenguliwa nafasi zao,wengine kufikishwa mahakamani,wengine kuendelea kuhojiwa na kuchubguzwa zaidi na zaidi kubaini mitandao yao ya wizi.

Ndio maana wananchi wanaendelea kuwa na imani kubwa sana na CCM na Serikali yake.
 
Nenda ukaibe uone cha mtema kuni . Chini ya serikali ya CCM na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan ukigusa pesa ya umma ni lazima unate kama ulimbo.na kukiona cha moto.ndio maana waliogusa pesa za umma wengine walishapotea kazi zao,wengine kutenguliwa nafasi zao,wengine kufikishwa mahakamani,wengine kuendelea kuhojiwa na kuchubguzwa zaidi na zaidi kubaini mitandao yao ya wizi.

Ndio maana wananchi wanaendelea kuwa na imani kubwa sana na CCM na Serikali yake.
Wewe nawe ni kama maiti inayotembea tu.
 
Ndio maana wananchi wanaendelea kuwa na imani kubwa sana na CCM na Serikali yake.
Kuna watu watahisi wewe ni msukule uliyefufuka kwenye makaburi ya nchi nyingine na CCM unayoitaja siyo hii inayoongoza Tanzania!!

Wananchi kama wana imani na CCM vitisho vya kuua wengine vinatokana na kitu gani!!??

CCM inayopendwa na watazania ndiyo kila siku inavuruga chaguzi ili sauti halisi za watanzania zisisikike!!??
 
Wizi ni tabia! Tabia haifi inaweza kupotea kwa muda lakini inarudi.
Ukishakula nyama ya mtu huwezi kuacha utaendelea tu-by the late Nyerere.
 
Nenda ukaibe uone cha mtema kuni . Chini ya serikali ya CCM na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hasssan ukigusa pesa ya umma ni lazima unate kama ulimbo.na kukiona cha moto.ndio maana waliogusa pesa za umma wengine walishapotea kazi zao,wengine kutenguliwa nafasi zao,wengine kufikishwa mahakamani,wengine kuendelea kuhojiwa na kuchubguzwa zaidi na zaidi kubaini mitandao yao ya wizi.

Ndio maana wananchi wanaendelea kuwa na imani kubwa sana na CCM na Serikali yake.
Akili yako huwa Iko sawa muda wote au kuna muda inafyatuka?
 
Kuna watu watahisi wewe ni msukule uliyefufuka kwenye makaburi ya nchi nyingine na CCM unayoitaja siyo hii inayoongoza Tanzania!!

Wananchi kama wana imani na CCM vitisho vya kuua wengine vinatokana na kitu gani!!??

CCM inayopendwa na watazania ndiyo kila siku inavuruga chaguzi ili sauti halisi za watanzania zisisikike!!??
CCM inaungwa mkono na kuendelea kuaminika sana mioyoni mwa watanzania,kutokana na kuwa na ajenda na sera zinazogusa maisha ya watu pamoja na kukidhi matarajio ya watanzania.
 
Halafu hawatosheki
Kuna wale wenyewe wenye chama chao wanawaita "Mazombie" kama wale wateka watu kule Zanzibar. Kanzu imejaa viraka lakini yupo vichochoroni kuvizia wanaoipinga CCM wakati wenzao wako Kizimkazi wanakula supu ya Pweza.
 
Lucas mara nyingi haileweki kama uandishi wako huwa unajali ama unazingatia majibu ya hoja iliyopo mezani, ama unakurupuka tu ili kuonyesha uchawa na mahaba yako kwa CCM. Sijui kwa nini huwa unajitoa ufahamu hata kwa mambo ambayo yapo bayana.

Wewe tunatambua bado u kijana. Watu wenye kujielewa tulitegemea kuwa ungekuwa ukihoji mambo ya msingi hasa yahusuyo fursa, vikwazo, pamoja na changamoto mbalimbali za vijana ambazo zinatokana na madudu yanayofanywa na watawala. Lakini wewe kutwa kuchwa kazi yako ni kusifia tu hata vile visivyostahili kusifiwa.

Shauri zako dogo, Muda ni mwalimu mzuri sana, na majuto ni mjukuu, kwa kuwa sikio lisikilizalo vyema kamwe haliwezi kutenganishwa na kichwa.
 
Back
Top Bottom