Kwako Mzee Wangu Mohammed Said

passion_amo1

JF-Expert Member
Dec 3, 2023
1,650
3,344
Wakuu Heshima mbele.

Mimi binafsi kwanza niseme ni mtu ambaye napenda sana kusoma historia tofauti tofauti. Nimekuwa nikivutiwa na mzee wangu Mohamed Said katika maandiko yake mengi, mzee Mohamed saidi ni mtu ambaye mara nyingi ameweza kuielezea historia Ya Tanganyika tangu harakati za uhuru zinapoanza mwanzoni kabisa, mzee Mohamed ameweza kuelezea ni kwa namna gani wazee Wa mwanzoni kabisa wa TANU ambao wengi wakiwa ni waislamu na wakaweza kumpokea mwalimu kwa upendo wote.

Mzee Mohamed Said mimi ni mtu ambaye napenda sana unachoandika. Lakini mbali na hilo watu wengi wamekuwa wakimshutumu mbali na kipaji na talanta kubwa aliyonayo ya kuandika, historia zake mara nyingi huwa zinaambatana na udini ( ZEALOTISM).

Mfano; katika moja ya komenti zake nitamnukuu hapa chini

Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:

Mawaziri na Manaibu: 30.

Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.

Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.

Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.

Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.

Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.

Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.

Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.

Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.

Wakurugenzi mbalimbali: 249.

Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.

Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.

Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.

Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.

Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33

Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.

Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.

Jumla Kuu ya Uteuzi:

Waislamu asilimia 20%.

Wakristo asilimia 80%.

Hio ni moja ya komenti aliyoiandika mzee wangu Mohamed kuhusu uwiano kati ya waislamu Na wakristo. Na akaendelea chini kwa kusema kwamba:

Uteuzi huo umekuwa kama Sera kwa teuzi zinazoendelea ndani ya miaka yote mitano. Vilevile kama Mwongozo kwa wateule wenye mamlaka ya kuteuwa. Mwelekeo huo unakinzana na Katiba ya nchi ibara ya 13(4)(5), inayokataza ubaguzi wa aina zote. Kwa hakika Taifa halihitaji kiongozi wa nchi akiwa Muislamu basi ateuwe idadi kubwa ya Waislamu wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi au akiwa Mkristo atumie uongozi wake kuteua idadi kubwa ya Wakristo wenzake katika uongozi nchini. Au akiwa Mzanaki ateuwe idadi kubwa ya Wazanaki wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi na mfano wa hayo.

Kama takwimu hizi ni za kweli mzee wangu Mohamed Said unafikiri ni nini kinasababisha kuendelea kuwepo kwa Mizani kutoku-balance?

Katika kitabu cha Kwa heri ukoloni kwa heri uhuru. Umetuonyesha ni jinsi gani makubaliano Baina ya waziri mkuu wa Kenya Ndg. Jommo kenyata na waziri mkuu wa Zanzibar Ndg. Mohamed shamte hayakufanikiwa na kupelekea kunyanga’nywa Kwa waislamu Taasisi ya (MIOME) mombasa institute of muslims education.

Mzee wangu Mohamed si mtu mwenye nia mbaya akijaribu kueleza kwa namna gani historia ya TANU haikuwa sawa kwa kiasi fulani, hivyo anajaribu kutufumbua macho zaidi. Lakini ni kama vile waislamu bado ni watu ambao kwa maandishi yake hakuna uwiano sawa na wakristo.

Mzee wangu Mohamed Said mimi naomba kufahamu kutoka kwako mbali na yote , ni kipi kifanyike ili kutengeneza uwiano sawa baina ya waislamu na wakristo katika Ngazi zote za nchi yetu? Haswa katika kipindi hichi tulichonacho elimu inatolewa kwa usawa bila kujali dini zetu.

NB. This is not intended to divisive or inflammatory only for learning purpose.
 
Mimi nafikiri chaguzi hizo zinafanyika random tu bila kuaangalia udini , ukianza kufanya chaguzi kwa kubalance mambo ya udini apo ndipo tatzo litakapo anzia .serikali haina dini mkuu.

hapo ndipo kwenye tatizo, ikitokea raisi muislamu wagalatia munalalamika Udini kila kukicha, bila ya hata hoja za msingi, ila munayofanya nyinyi huwa muna hoja nyingi za kujitetea.
 
Kwa takwimu hizo naona kuna tatizo mahala,,,tusizungumze kwa hisia hapa bali tuzungumze kama watu wakomavu wa mambo

Huwezi sema kwa takwimu hizo eti uteuzi ulifanyika bila mpangalio,,hapana ila kuna lengo nyuma yake na kama ungekuwepi uteuzi bila mpango maalumu basi kada fulani ingejikuta ina waislamu wengi pia.

Ni nini cha kufanya,,,wenye mamlaka na uteuzi ebu jaribuni kuondoa hii tabia ya kupendeleana kwa misingi ya kidini,,sikatai haiwezi mizani ikawa sawa lkn kusiwepo na tofauti kiasi kwamba mtu anajiuliza hii imekuwaje?

Kwa takwimu hizo kwa mtu mwenye uelewa wa kawaida na ambaye hajamezwa na hisia au mapenzi kwa dini yake ataona hakuna haki hapo

Ni hayo tu
 
Mimi nafikiri chaguzi hizo zinafanyika random tu bila kuaangalia udini , ukianza kufanya chaguzi kwa kubalance mambo ya udini apo ndipo tatzo litakapo anzia .serikali haina dini mkuu.
Mkuu Min,

Hoja si serikali haina dini, hoja ya mzee Mohamed ni Kwanini uwiano uwe na tofauti kubwa? Anafikiri kuna mahala hakupo sawa kwa mamlaka katika chaguzi katika ngazi tofauti tofauti za uongozi.

Unafikiri nini kinasababisha mbali na kuwepo Raisi muislamu, waziri Mkuu muislamu lakini bado hapana mlinganyiko unaokaribiana?
 
Mkuu Min,

Hoja si serikali haina dini, hoja ya mzee Mohamed ni Kwanini uwiano uwe na tofauti kubwa? Anafikiri kuna mahala hakupo sawa kwa mamlaka katika chaguzi katika ngazi tofauti tofauti za uongozi.

Unafikiri nini kinasababisha mbali na kuwepo Raisi muislamu, waziri Mkuu muislamu lakini bado hapana mlinganyiko unaokaribiana?
Mimi nafikiri taasisi mbalimbali za katholic na Lutheran hutoa wasomi mahiri katika nyanja mbalimbali , kuliko taasisi za kiislamu na madhehebu mengine hasa ya kilokole , ndio maana wakiitajika watu mahiri kwenye ngazi mbalimbali za kiutawala asilimia kubwa hukuta ni watu wa dini hizo , wala sifikiri kama kuna ubaguzi wowote .
 
Mimi nafikiri taasisi mbalimbali za katholic na Lutheran hutoa wasomi mahiri katika nyanja mbalimbali , kuliko taasisi za kiislamu na madhehebu mengine hasa ya kilokole , ndio maana wakiitajika watu mahiri kwenye ngazi mbalimbali za kiutawa asilimia kuwa hukuta ni watu wa dini hizo , wala sifikiri kama kuna ubaguzi wowote .
Chief

Kwanza nashukuru kwa maoni yako,,,na nimependezwa na mjadala huu mpaka sasa haujaingiliwa na wapuuzi wa mihemko

Hivi mpaka karne hii ni kweli hakuna waislamu wasomi? Au ndio mambo yale yale kuwa waislamu walikazania madrasa tu?

Unashawishika na hilo?
 
Kwa takwimu hizo naona kuna tatizo mahala,,,tusizungumze kwa hisia hapa bali tuzungumze kama watu wakomavu wa mambo

Huwezi sema kwa takwimu hizo eti uteuzi ulifanyika bila mpangalio,,hapana ila kuna lengo nyuma yake na kama ungekuwepi uteuzi bila mpango maalumu basi kada fulani ingejikuta ina waislamu wengi pia.

Ni nini cha kufanya,,,wenye mamlaka na uteuzi ebu jaribuni kuondoa hii tabia ya kupendeleana kwa misingi ya kidini,,sikatai haiwezi mizani ikawa sawa lkn kusiwepo na tofauti kiasi kwamba mtu anajiuliza hii imekuwaje?

Kwa takwimu hizo kwa mtu mwenye uelewa wa kawaida na ambaye hajamezwa na hisia au mapenzi kwa dini yake ataona hakuna haki hapo

Ni hayo tu
Thread 'Hatusambazi propaganda za udini kwa wanasiasa,tunalipenda taifa letu na tunakemea vikali' Hatusambazi propaganda za udini kwa wanasiasa,tunalipenda taifa letu na tunakemea vikali

Copy & pasted
 
Mkuu Etugrul Bey

Mzee Mohamed anasema chaguzi hizi zinakinzana na katiba ibara ya 13 (4) (5)
Ambacho kinasema kuhusu ubaguzi wa aina yoyote ile.

Katika maneno yake mzee Mohamed inaonyesha dini ya kikristo inapendelewa zidi ya dini ya kiislamu.

Swali ni kwamba kulingana na kifungu hicho cha katiba serikali inatazama ufanisi na elimu ya mtu katika teuzi au inatazama Dini pasi na sababu hizo zingine kuwepo?

Lakini pia Mkuu;

Mbali na kuwepo kwa Raisi muislamu na waziri mkuu, mbali na kuwepo kwa usawa wa kupata elimu unafikiri ni Kwanini tatizo hili bado lipo?
 
Chief

Kwanza nashukuru kwa maoni yako,,,na nimependezwa na mjadala huu mpaka sasa haujaingiliwa na wapuuzi wa mihemko

Hivi mpaka karne hii ni kweli hakuna waislamu wasomi? Au ndio mambo yale yale kuwa waislamu walikazania madrasa tu?

Unashawishika na hilo?
Waislam wasomi wapo kwa kiasi chake tena ni wabobezi kwenye fani zao nawasio penda kuyumbishwa , sema tatzo la Tanzania mikoa mingi yenye jamii za Waislam wengi walikua nyuma kidgo kwenye mambo ya kielimu, apo tatizo sio dini tatizo ni vipaumbele vya jamii husika .

Mfano kwenye jamii ya wachaga hasa wamachame kuna jamii kubwa tu ya waislamu ila ni waislamu wabobezi kwenye nyanja ya elimu na mahiri sna kwenye biashara na maendeleo binafsi tofauti na jamii ya wazaramo au warangi ambapo pia kundi kubwa ni Waislam , unaona apo tatzo sio dini tatzo ni kipaumbele cha jamii husika.
 
Wakuu Heshima mbele.

Mimi binafsi kwanza niseme ni mtu ambaye napenda sana kusoma historia tofauti tofauti. Nimekuwa nikivutiwa na mzee wangu Mohamed Said katika maandiko yake mengi, mzee Mohamed saidi ni mtu ambaye mara nyingi ameweza kuielezea historia Ya Tanganyika tangu harakati za uhuru zinapoanza mwanzoni kabisa, mzee Mohamed ameweza kuelezea ni kwa namna gani wazee Wa mwanzoni kabisa wa TANU ambao wengi wakiwa ni waislamu na wakaweza kumpokea mwalimu kwa upendo wote.

Mzee Mohamed Said mimi ni mtu ambaye napenda sana unachoandika. Lakini mbali na hilo watu wengi wamekuwa wakimshutumu mbali na kipaji na talanta kubwa aliyonayo ya kuandika, historia zake mara nyingi huwa zinaambatana na udini ( ZEALOTISM).

Mfano; katika moja ya komenti zake nitamnukuu hapa chini

Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:

Mawaziri na Manaibu: 30.

Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.

Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.

Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.

Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.

Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.

Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.

Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.

Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.

Wakurugenzi mbalimbali: 249.

Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.

Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.

Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.

Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.

Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33

Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.

Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.

Jumla Kuu ya Uteuzi:

Waislamu asilimia 20%.

Wakristo asilimia 80%.

Hio ni moja ya komenti aliyoiandika mzee wangu Mohamed kuhusu uwiano kati ya waislamu Na wakristo. Na akaendelea chini kwa kusema kwamba:

Uteuzi huo umekuwa kama Sera kwa teuzi zinazoendelea ndani ya miaka yote mitano. Vilevile kama Mwongozo kwa wateule wenye mamlaka ya kuteuwa. Mwelekeo huo unakinzana na Katiba ya nchi ibara ya 13(4)(5), inayokataza ubaguzi wa aina zote. Kwa hakika Taifa halihitaji kiongozi wa nchi akiwa Muislamu basi ateuwe idadi kubwa ya Waislamu wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi au akiwa Mkristo atumie uongozi wake kuteua idadi kubwa ya Wakristo wenzake katika uongozi nchini. Au akiwa Mzanaki ateuwe idadi kubwa ya Wazanaki wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi na mfano wa hayo.

Kama takwimu hizi ni za kweli mzee wangu Mohamed Said unafikiri ni nini kinasababisha kuendelea kuwepo kwa Mizani kutoku-balance?

Katika kitabu cha Kwa heri ukoloni kwa heri uhuru. Umetuonyesha ni jinsi gani makubaliano Baina ya waziri mkuu wa Kenya Ndg. Jommo kenyata na waziri mkuu wa Zanzibar Ndg. Mohamed shamte hayakufanikiwa na kupelekea kunyanga’nywa Kwa waislamu Taasisi ya (MIOME) mombasa institute of muslims education.

Mzee wangu Mohamed si mtu mwenye nia mbaya akijaribu kueleza kwa namna gani historia ya TANU haikuwa sawa kwa kiasi fulani, hivyo anajaribu kutufumbua macho zaidi. Lakini ni kama vile waislamu bado ni watu ambao kwa maandishi yake hakuna uwiano sawa na wakristo.

Mzee wangu Mohamed Said mimi naomba kufahamu kutoka kwako mbali na yote , ni kipi kifanyike ili kutengeneza uwiano sawa baina ya waislamu na wakristo katika Ngazi zote za nchi yetu? Haswa katika kipindi hichi tulichonacho elimu inatolewa kwa usawa bila kujali dini zetu.

NB. This is not intended to divisive or inflammatory only for learning purpose.
Hali ikoje kwa sasa? Kuna utofauti? Kwa nini?
 
Sasa kama jamii zingine hazikuwapokea wamisionari walioleta elimu wakakumbatia dini basi walipumbazika na dini wakaacha kusoma matokeo yake wakaishia kuwa maamuma. Watateuliwa vipi na elimu hawana? Wakasome
 
Wakuu Heshima mbele.

Mimi binafsi kwanza niseme ni mtu ambaye napenda sana kusoma historia tofauti tofauti. Nimekuwa nikivutiwa na mzee wangu Mohamed Said katika maandiko yake mengi, mzee Mohamed saidi ni mtu ambaye mara nyingi ameweza kuielezea historia Ya Tanganyika tangu harakati za uhuru zinapoanza mwanzoni kabisa, mzee Mohamed ameweza kuelezea ni kwa namna gani wazee Wa mwanzoni kabisa wa TANU ambao wengi wakiwa ni waislamu na wakaweza kumpokea mwalimu kwa upendo wote.

Mzee Mohamed Said mimi ni mtu ambaye napenda sana unachoandika. Lakini mbali na hilo watu wengi wamekuwa wakimshutumu mbali na kipaji na talanta kubwa aliyonayo ya kuandika, historia zake mara nyingi huwa zinaambatana na udini ( ZEALOTISM).

Mfano; katika moja ya komenti zake nitamnukuu hapa chini

Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:

Mawaziri na Manaibu: 30.

Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.

Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.

Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.

Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.

Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.

Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.

Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.

Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.

Wakurugenzi mbalimbali: 249.

Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.

Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.

Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.

Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.

Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33

Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.

Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.

Jumla Kuu ya Uteuzi:

Waislamu asilimia 20%.

Wakristo asilimia 80%.

Hio ni moja ya komenti aliyoiandika mzee wangu Mohamed kuhusu uwiano kati ya waislamu Na wakristo. Na akaendelea chini kwa kusema kwamba:

Uteuzi huo umekuwa kama Sera kwa teuzi zinazoendelea ndani ya miaka yote mitano. Vilevile kama Mwongozo kwa wateule wenye mamlaka ya kuteuwa. Mwelekeo huo unakinzana na Katiba ya nchi ibara ya 13(4)(5), inayokataza ubaguzi wa aina zote. Kwa hakika Taifa halihitaji kiongozi wa nchi akiwa Muislamu basi ateuwe idadi kubwa ya Waislamu wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi au akiwa Mkristo atumie uongozi wake kuteua idadi kubwa ya Wakristo wenzake katika uongozi nchini. Au akiwa Mzanaki ateuwe idadi kubwa ya Wazanaki wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi na mfano wa hayo.

Kama takwimu hizi ni za kweli mzee wangu Mohamed Said unafikiri ni nini kinasababisha kuendelea kuwepo kwa Mizani kutoku-balance?

Katika kitabu cha Kwa heri ukoloni kwa heri uhuru. Umetuonyesha ni jinsi gani makubaliano Baina ya waziri mkuu wa Kenya Ndg. Jommo kenyata na waziri mkuu wa Zanzibar Ndg. Mohamed shamte hayakufanikiwa na kupelekea kunyanga’nywa Kwa waislamu Taasisi ya (MIOME) mombasa institute of muslims education.

Mzee wangu Mohamed si mtu mwenye nia mbaya akijaribu kueleza kwa namna gani historia ya TANU haikuwa sawa kwa kiasi fulani, hivyo anajaribu kutufumbua macho zaidi. Lakini ni kama vile waislamu bado ni watu ambao kwa maandishi yake hakuna uwiano sawa na wakristo.

Mzee wangu Mohamed Said mimi naomba kufahamu kutoka kwako mbali na yote , ni kipi kifanyike ili kutengeneza uwiano sawa baina ya waislamu na wakristo katika Ngazi zote za nchi yetu? Haswa katika kipindi hichi tulichonacho elimu inatolewa kwa usawa bila kujali dini zetu.

NB. This is not intended to divisive or inflammatory only for learning purpose.
Achana na huyo mzee, hoja yake ni mfu kwa 100%.
Mimi nitakusaidia kukujibu na kumkosoa vikali mzee Mohamed Said.

1. Nchi yetu haina dini, hivyo huwezi kutumia kigezo cha dini katika kuajili na kuteua nafasi mbali mbali za utumishi wa umma.

2. Dini ni suala la moyoni na sio jambo la lazima kubakia moyoni mwa mtu siku zote (inawezekana wakati nateuliwa nilikuwa Mkristo, wakati naapa nikawa Muislamu na wakati natumbuliwa nilikuwa mpagani), huwezi kujua dini halisi ya mtu mpaka uingie moyoni mwake. Kutazama majina ya mtu, haitoshi kujua imani yake halisi ya kidini.

3. Jamii imegawanyika katika mambo mbalimbali yakiwemo Imani, Kabila, Jinsia, Kipato, Taaluma, Makazi. Kama serikali itaamua kuteua watu kwa misingi yao ya kijamii basi uwiano wa kidini pekee hautoshi kuwawakilisha hao watu.

4. Rais atateua watu kutoka katika bwawa (pool) la watu wenye sifa stahiki kwake, hakuna mtu anajua hilo bwawa analotumia Rais kuchagua watu wake lina uwiano gani kidini. Unaweza kukuta ndani yake lina waislamu wachache sana, hivyo litaishia kuteua waislamu wachache.

5. Mamlaka ya uteuzi iko ndani ya utashi na uhuru wa Rais aliyepo madarakani, anawajibika kwake mwenyewe, hivyo huwezi kujenga hoja ya kuwepo uwiano wa kidini katika kuteuliwa.
 
Back
Top Bottom