kwa wapenzi wa Ulanzi WANYALUKOLO

Ulanzi
Ulanzi ni kinywaji kinachotokana na mmea ambao huota kwa wingi sehemu moja na hukua sana kwenda juu. Mimea hii ikiwa bado michanga hukatwa juu na ikishakatwa hutoa maji na kitu mithili ya povu hujaa juu ya pale palipokatwa. Maji hayo yanayotoka hukingwa kwenye kitu kiitwacho
“mbeta”: halina kiswahili sahihi. Maji hayo yanayotoka ni matamu sana na tena yana uwezo wa kulewesha.Historia yake.
Inasemekana ulanzi uligunduliwa na mnyama mdogo aitwaye panya ambaye kwa mara ya kwanza waling’ata ule mmea mchanga wa ulanzi na maji yakaanza kutoka. Kila siku panya walionekana kupenda kulamba ile sehemu walioing’ata. Binadamu, baada ya kugundua hilo, walifuatilia na wakajaribu kulamba na wao, ndipo walipogundua kuwa yale maji yaliyotoka ni matamu.
Basi wakakata ile mimea michanga ya mianzi na kuona maji mengi yakitoka na kitu mithili ya povu juu yake.
Baadaye wakatumia mianzi iliyokomaa kwa kutengenezea kitu cha kukingia yale maji yanayotoka. Zinaitwa “mbeta”Maelezo
Ulanzi ni kinywaji cha asili kinachopendwa sana na watu wa mikoa ya Iringa, Mbeya na Songea, Kanda za Juu ya nchi ya Tanzania.
Ni kinywaji cha asili ambacho hakitengenezwi bali kinatokana na mti unaoitwa mwanzi.
Ulanzi unagemwa mara tatu kwa siku:
¨ Asubuhi: hugema na kutoa ulanzi kutoka kwenye vile vyombo vya kukingia (mbeta). Ulanzi huu wa asubuhi daima ni mtamu na togwa sana.
¨ Mchana huenda kugema kusudi kuweza kutoa sehemu iliyokauka ili ulanzi uendelee kutoka.
¨ Jioni: hugemwa tena na kutoa ulanzi uliomo kwenye vyombo vya kukingia. Ulanzi huu wa jioni ni mkali kidogo kwa sababu unakuwa umewakiwa na jua.
Ili kupata ulanzi ulio mzuri, wagemaji huchanganya ulanzi wa asubuhi na wa jioni ili uwe bora zaidi na kwa hiyo upendwe na wengi zaidi.
Utomvu:
Ni kitu kama uji unaotuama juu ya ile sehemu iliyokatwa kwenye kitindi kichanga kwa ajili ya kutoa ulanzi.
Kitindi
Ni mti ule unaotoa ulanzi. Kitindi ni umoja, vikiwa vingi huitwa vitindi na daima huwa vingi ili kupata vitindi vichanga vingi. Kitindi kikiwa kimoja huwezi kugema ulanzi kwa sababu kitindi kichanga hakiwezi kupatikana.
Hugemwa lini?
Ulanzi huu hugemwa kwa kipindi, kwa sehemu zilizo nyingi hasa kipindi cha kifuku (masika) ulanzi huwa mwingi sana na unazidi kupungua kadiri kipindi cha masika kinavyoisha. Lakini kuna baadhi ya sehemu ambazo zina baridi sana na hali ya ubichi kwa mwaka mzima, kwa mfano katika mbuga ya Kitulo, wilaya ya Makete (Tanzania).
Hunyweka kwa siku ngapi?
Ulanzi hunyweka kwa siku moja kimsingi hapo huwa mtamu wa ladha safi. Lakini ukishalala, ulanzi hupoteza ubora wake na hivi hauwi mtamu sana. Lakini ukichanganya na uliogemwa siku hiyo, hurudi katika hali njema tena, ingawa siyo safi sana.
Kiswahili ni lugha ya kutengenezwa na binadamu, tatizo la BAKITA wapo tu kupokea mshahra mwisho wa mwezi, nadhani wameamini hata lugha zetu za ASILI ni 'USHENZI!'. Neno hilo lingeingizwa katika kiswahili 'badala ya kiingereza au kiarabu' lugha hii ingekuwa ya KIBANTU zaidi.
 
hahaaa watu wa tosa, malangali, njoss na wengineo wanamiss sana hii kitu.
aisee nimekumbuka idete kwenye mapera na ulanzi,lupalama B, na ipamba kwa manesi...those time are gone now....ulanzi uliwafanya wazungu wasahau wine wahamie kwenye ulanzi...kwa waliokuwepo tosa wanamkumbuka Mr. Simon na Mr. Jonathan? (kama sijakosea) hawa jamaa walikuwa wakiwa zamu tu then wakakukamata na kosa wanaomba jiti kwa ajili ya ulanzi kama adhabu.
 
aisee nimekumbuka idete kwenye mapera na ulanzi,lupalama B, na ipamba kwa manesi...those time are gone now....ulanzi uliwafanya wazungu wasahau wine wahamie kwenye ulanzi...kwa waliokuwepo tosa wanamkumbuka Mr. Simon na Mr. Jonathan? (kama sijakosea) hawa jamaa walikuwa wakiwa zamu tu then wakakukamata na kosa wanaomba jiti kwa ajili ya ulanzi kama adhabu.

vipi unakumbuka kina -niangushage mwenyewe! hizi zitakuwa dhambi zako mwenyewe

maisha yalikuwa ni matamu iringa tanangozi na basili la milango miwili na nyota basi servise jioni linatoka tanangozi linaingia mjini na wanywaji kibao. hii ya leo ni inside iringa kama mtu wa iringa hakuyaona haya alikosa vitu vikali sana bado hujapita nyumba ya mtu ukasikia amepiga mziki wa kidamali yaani miziki ya jaluo
 
Mnazi unanuka balaa mkuu
mkuu kilimasera nashukuru kwa kunikumbusha ulanzi...nshazoea mnazi xaxa....but naomba nikusahihishe kidogo. mimea ya mianzi, vitindi huwa havikui sana kwenda juu....hurefuka yapata mita tano hivi then inapinda kwenda down, na pia mbeta hazitokani na mianzi (vitindi) vya ulanzi but hutokana na mianzi mingine ambayo haitoi ulanzi bali hutumiak kwa kutengenezea mbeta na bidhaa zingine kama vitanda, nyungo, vikapu nk.
ulanzi uliokomaa sana unaitwa kilama, huu ulanzi ni full spirit kwani ukimwagia kwenye majani yanaungua,na ukiunywa bila kuchanganya na togwa afya yako ni hatihati.
 
Hapo huyu Mama anafanya kitu kinaitwa "KUPYATILA" ni mchana yapata saa Saba ambapo unagema bila kujaza contena zako badala yake utajaza pombe hiyo jioni. Mbeta moja ameishikilia mkononi na nyingine inaning'inia katika muanzi wa nyuma yake.


Wakati anagema huimba wimbo laini sana kama vile "Semwagala aivemba lukwika X2.."



Ulanzi.jpg
 
Ulanzi
Ulanzi ni kinywaji kinachotokana na mmea ambao huota kwa wingi sehemu moja na hukua sana kwenda juu. Mimea hii ikiwa bado michanga hukatwa juu na ikishakatwa hutoa maji na kitu mithili ya povu hujaa juu ya pale palipokatwa. Maji hayo yanayotoka hukingwa kwenye kitu kiitwacho mbeta: halina kiswahili sahihi. Maji hayo yanayotoka ni matamu sana na tena yana uwezo wa kulewesha.Historia yake.
Inasemekana ulanzi uligunduliwa na mnyama mdogo aitwaye panya ambaye kwa mara ya kwanza walingata ule mmea mchanga wa ulanzi na maji yakaanza kutoka. Kila siku panya walionekana kupenda kulamba ile sehemu walioingata. Binadamu, baada ya kugundua hilo, walifuatilia na wakajaribu kulamba na wao, ndipo walipogundua kuwa yale maji yaliyotoka ni matamu.
Basi wakakata ile mimea michanga ya mianzi na kuona maji mengi yakitoka na kitu mithili ya povu juu yake.
Baadaye wakatumia mianzi iliyokomaa kwa kutengenezea kitu cha kukingia yale maji yanayotoka. Zinaitwa mbetaMaelezo
Ulanzi ni kinywaji cha asili kinachopendwa sana na watu wa mikoa ya Iringa, Mbeya na Songea, Kanda za Juu ya nchi ya Tanzania.
Ni kinywaji cha asili ambacho hakitengenezwi bali kinatokana na mti unaoitwa mwanzi.
Ulanzi unagemwa mara tatu kwa siku:
¨ Asubuhi: hugema na kutoa ulanzi kutoka kwenye vile vyombo vya kukingia (mbeta). Ulanzi huu wa asubuhi daima ni mtamu na togwa sana.
¨ Mchana huenda kugema kusudi kuweza kutoa sehemu iliyokauka ili ulanzi uendelee kutoka.
¨ Jioni: hugemwa tena na kutoa ulanzi uliomo kwenye vyombo vya kukingia. Ulanzi huu wa jioni ni mkali kidogo kwa sababu unakuwa umewakiwa na jua.
Ili kupata ulanzi ulio mzuri, wagemaji huchanganya ulanzi wa asubuhi na wa jioni ili uwe bora zaidi na kwa hiyo upendwe na wengi zaidi.
Utomvu:
Ni kitu kama uji unaotuama juu ya ile sehemu iliyokatwa kwenye kitindi kichanga kwa ajili ya kutoa ulanzi.
Kitindi
Ni mti ule unaotoa ulanzi. Kitindi ni umoja, vikiwa vingi huitwa vitindi na daima huwa vingi ili kupata vitindi vichanga vingi. Kitindi kikiwa kimoja huwezi kugema ulanzi kwa sababu kitindi kichanga hakiwezi kupatikana.
Hugemwa lini?
Ulanzi huu hugemwa kwa kipindi, kwa sehemu zilizo nyingi hasa kipindi cha kifuku (masika) ulanzi huwa mwingi sana na unazidi kupungua kadiri kipindi cha masika kinavyoisha. Lakini kuna baadhi ya sehemu ambazo zina baridi sana na hali ya ubichi kwa mwaka mzima, kwa mfano katika mbuga ya Kitulo, wilaya ya Makete (Tanzania).
Hunyweka kwa siku ngapi?
Ulanzi hunyweka kwa siku moja kimsingi hapo huwa mtamu wa ladha safi. Lakini ukishalala, ulanzi hupoteza ubora wake na hivi hauwi mtamu sana. Lakini ukichanganya na uliogemwa siku hiyo, hurudi katika hali njema tena, ingawa siyo safi sana.


Nyongeza:

Hapo kwenye kugema ulitakiwa kutaja neno "hupyatila" kama ulivyotaja mbeta kama taping tool na muanzi unaotumika kutengeneza mbeta unaitwa "libeta"

Hujataja aina zote za ulanzi, kuna ulanzi mtogwa, mkangafu na mdindifu, subiri kidogo waje wanywaji watakupa tofauti zao.

Pia kuna ndege aina ya ngaluniongo wao wana rangi nyingi sana nzuri na wanavutia sana, beak ya ndege huyo ni ndefu sana na imejikunja kuelekea chini, moja ya sifa yao kubwa ni kutumia sana kinywaji hicho nyakati zote.

Kadhalika kuna wanyama waitwao komba au (ki) vipwege, wao wanafanana sana na ngedere ila ni wadogo kwa umbo, wanyama hao pia wanakunywa sana ulanzi huko viungani, katika baadhi ya maeneo wanatoa mbeta wanakunywa na kuirudishia kwenye sehemu yake ili iendelee kujaa.

Ulanzi una sifa ya kuunguza au kukausha kabisa majani ukiyamwagia, ukiumwaga ulanzi kwenye majani, sehemu hiyo itabakia haina majani kwa muda fulani nadhani ni kutokana na acidity.
 
Back
Top Bottom