Kwa hali inayoendelea sasa nchini wananchi wanaenda kwenye mikutano ya kisiasa kusikiliza sera au kuangalia Wasanii?

Cute Wife

Senior Member
Nov 17, 2023
153
390
Habari zenu Wakuu,

IMG_20240419_002741_754.PNG

Kwa hizi siasa zinavyoendelea nchini sidhani kama raia wanaojaa kwenye mikutano ya kiasiasa wanakuwa wanaenda kweli kusikiliza sera, hasa wale wanaojaza wasanii kibao utafikiri wanafanya tamasha.

Kila mtu sasa hivi ni chawa, viongozi ni chawa ili kubakia kwenye nafasi zao na wananchi wanakuwa chawa kwa kufanya lolote ili kupata nafasi ya kula sehemu ya mema ya nchi.

Ndio tumefikia huku? Kiongozi unaona sifa kusifiwa, unajifanya hupendi na kukemea lakini unaacha viendelee, wanaosifia ndio wanapata nafasi wakati wanaokukosoa wanakula joto ya jiwe au hawapati nafasi za kuongoza huku kila mtu akiona uwezo wao mkubwa wa kufanya maamuzi!

Ina maana viongozi wameishiwa sera na mipango ya kuiuza kwa wananchi ili wawakubali? Kuna uwezekano wa viongozi hao kutoboa bila kutumia ushawishi wa wasanii wanaombatana nao?

Mna maoni gani kweny hili wakuu?

CC johnthebaptist Lucas Mwashambwa Mshana Jr Erythrocyte
 
Ndugu yangu na hata hao wanaoenda kwa mvuto wa wasanii ni wale tunaowaita kwa lugha isiyo nzuri wajinga.
 
Ndugu yangu na hata hao wanaoenda kwa mvuto wa wasanii ni wale tunaowaita kwa lugha isiyo nzuri wajinga.
Wenye akili hawana muda wa kwenda huko sababu wanaona mambo hayabadiliki au kuna sababu nyingine Mkuu?
 
Wenye akili hawana muda wa kwenda huko sababu wanaona mambo hayabadiliki au kuna sababu nyingine Mkuu?
Ppamoja na kukosa muda lakini sidhani kama kuna mtu hata mmoja anayetarajia kurudi na kitu cha maana kutoka kwenye mikutano ya siasa, hii ni kwa vyama vyote!
Bora hata Vyama vingine ila hiki kinacho tuongoza sana utarudi nyumbani na frustration za kutosha.
 
Ppamoja na kukosa muda lakini sidhani kama kuna mtu hata mmoja anayetarajia kurudi na kitu cha maana kutoka kwenye mikutano ya siasa, hii ni kwa vyama vyote!
Bora hata Vyama vingine ila hiki kinacho tuongoza sana utarudi nyumbani na frustration za kutosha.
Hawana chochote to brag about
 
Ni kipindi (msimu) wa mavuno kwa wasanii wa Tanzania - hela ya CCM (Taifa) ni nje nje - usipojenga sasa hujengi tena.
 
CCM Ndio Tumaini la watanzania ndio maana inaungwa mkono na mamilioni ya watanzania kutokana na kuwa na sera na ajenda zinazogusa maisha ya watu. CCM Ndio chama pekee chenye uwezo wa kuiongoza Tanzania na kumfanya kila mtu kutimiza ndoto na malengo yake. Ndio chama chenye uchungu na maisha ya watanzania.tofauti na vyama kama CHADEMA ambavyo vipo vipo tu kama madalali wa kisiasa kwa ajili ya kuneemesha matumbo yao
 
Wanaenda kuangalia wasanii akuna cha msingi kinacho zungumziwa kwa sababu matatizo ya kila siku kama afya elimu miundombinu wamefanya kama kichaka cha kujikosha mwisho wa siku matatizo haya awajatatui bali wanaacha ili mwisho wa siku wa rudi tena kutukumbusha matatizo waliyo shindwa kujatatua ni bola kwenda kuona wasanii huenda asilimia kubwa wanainch wanafalijika
 
Voters behavior.
Sisi watanzania tunashawishika kirahisi na vitu vya kijinga.

Ndo maana hata kwenye misiba au maharusi,usijeona kumejaa ukajua wote Nia Yao moja. Wengine wanaenda kupiga tathimini ya bei ya jeneza au marehemu kavishwaje.

Wengine kula tu,wakimaliza waleeeee
 
CCM Ndio Tumaini la watanzania ndio maana inaungwa mkono na mamilioni ya watanzania kutokana na kuwa na sera na ajenda zinazogusa maisha ya watu. CCM Ndio chama pekee chenye uwezo wa kuiongoza Tanzania na kumfanya kila mtu kutimiza ndoto na malengo yake. Ndio chama chenye uchungu na maisha ya watanzania.tofauti na vyama kama CHADEMA ambavyo vipo vipo tu kama madalali wa kisiasa kwa ajili ya kuneemesha matumbo yao
Ilikuwa ni zamani, ambapo viongozi walikuw wazalendo,sio zama hizi !. Unajua kwa nn nyerere alipiga marufuku matajiri wasigombee nafasi za uongozi au kupewa uongozi. Think twice Mr ✍️🧠
 
Back
Top Bottom