Kuna kinyama kinaning'inia sehemu ya haja kubwa, naombeni msaada

kalanga1

JF-Expert Member
Apr 10, 2017
318
424
Habarini wapendwa, naombeni msaada wenu, kipindi cha nyuma mimi niliwahi kusumbuliwa na tatizo la umeng'enyaji chakula, nilikuwa najisaidia choo kigumu sana, nikaambiwa na doctor kuwa nina tatizo kwenye mfumo wa umeng'enyaji chakula, chakula hakimeng'enywi inavyotakiwa, nikapewa dawa tatizo hilo likaisha.

Lakini sasa kuna siku najisaidia nikapata choo kigumu sana nikachanika sehemu ya haja kubwa halafu kuna linyama likaning'inia chini, nikaanza kuuguza kidonda pale nilipochanika, kidonda kikapona lakini lile linyama bado lipo.

Nilienda hospital nikapewa anisol niwe napaka, nimepaka tube 2 bado hakijatoka, nikaanza kupaka mafuta ya mnyonyo bdo hiyo nyama ipo tu, nikaanza mafuta ya mzaituni bdo hiyo nyama ipo tu. Je nifanyaje?

Naombeni msaada wenu, na kuna kipindi nikiigusa hiyo nyama nahisi maumivu. Ahsanteni
 
Duuhh! Pole sana hiyo ni BAWASIRI na mara nyingi hupona Kwa tiba asili! Pia nakushauri ubadili namna ya kula, kama unatumia ugali wa sembe ACHA tumia Dona, matunda Kwa wingi. Itakusaidia kutopata choo laini.
 
Iyo ni hicho ulichotajiwa na wakuu hapo juu. Hapo tumia tiba za asili na kubadili mfumo wa kula pia kama unafanya kazi umekaa muda mrefu badili huo utaratibu.

kitu siwezi kushauri ni kufanyiwa operesheni ndogo iyo achana nayo kabisa Mkuu, itakupa matokeo ya chapu ila itarudi upya.
 
Iyo ni hicho ulichotajiwa na wakuu hapo juu. Hapo tumia tiba za asili na kubadili mfumo wa kula pia kama unafanya kazi umekaa muda mrefu badili huo utaratibu.

kitu siwezi kushauri ni kufanyiwa operesheni ndogo iyo achana nayo kabisa Mkuu, itakupa matokeo ya chapu ila itarudi upya.
Dawa zipi za asili?
 
Iyo ni hicho ulichotajiwa na wakuu hapo juu. Hapo tumia tiba za asili na kubadili mfumo wa kula pia kama unafanya kazi umekaa muda mrefu badili huo utaratibu.

kitu siwezi kushauri ni kufanyiwa operesheni ndogo iyo achana nayo kabisa Mkuu, itakupa matokeo ya chapu ila itarudi upya.
Dawa zip ss
 
Kila mtu anasema ni bawasiri, ingawa wewe unadai ilichanika.

Je inaning'inia kama nyama imeshuka au inanging'inia kama nguo imechanika?

Bila picha ni ngumu kueleza. Finally hospital muone daktari kwa msaada zaidi. Hata ukiandika mtandaoni jibu litakuja tu, fika umuone daktari ili kinyama kikatwe.
 
Dawa zipi za asili?
Kuna ya kuchemsha maji na kuyawekea chumvi kisha anayaweka kwenye ndoo alafu anaikalia apigwe na ule mvuke yaani anakuwa kama anajifukiza hivi.

Atafanya ilo zoezi kwa muda atapona au kupata nafuu kubwa. Huku akila matunda na kunywa maji yakutosha na kupunguza kukaa. Pia akifanya mazoezi mepesi ya skwati itachochea kupona kwake

Pia dawa za sunna zipo ni kwenda kuwaona wauzaji ukawaeleza tatizo.

Ila mimi sio daktari Wakuu.
kalanga1
 
Habarini wapendwa, naombeni msaada wenu, kipindi cha nyuma mimi niliwahi kusumbuliwa na tatizo la umeng'enyaji chakula, nilikuwa najisaidia choo kigumu sana, nikaambiwa na doctor kuwa nina tatizo kwenye mfumo wa umeng'enyaji chakula, chakula hakimeng'enywi inavyotakiwa, nikapewa dawa tatizo hilo likaisha.

Lakini sasa kuna siku najisaidia nikapata choo kigumu sana nikachanika sehemu ya haja kubwa halafu kuna linyama likaning'inia chini, nikaanza kuuguza kidonda pale nilipochanika, kidonda kikapona lakini lile linyama bado lipo.

Nilienda hospital nikapewa anisol niwe napaka, nimepaka tube 2 bado hakijatoka, nikaanza kupaka mafuta ya mnyonyo bdo hiyo nyama ipo tu, nikaanza mafuta ya mzaituni bdo hiyo nyama ipo tu. Je nifanyaje?

Naombeni msaada wenu, na kuna kipindi nikiigusa hiyo nyama nahisi maumivu. Ahsanteni
DR Mambo Jambo ...

Bawasiri hiyo...wahi tiba mapema
 
Hiyo ni bawasiri, niliwahi kuugua ila namshukuru MUNGU ilipona baada ya kubadilisha mtindo wa maisha

  • Kula chakula kilaini (hasahasa ugali usile liugali ligumu kama jiwe)
  • Kunywa maji mengi
  • Epuka kuinua vitu vizito (mfano: mizigo,
  • kula mbogamboga kwa wingi (kama una uwezo kama huna pia sio issue)

Tiba ( sio 100% sure)
  • Kata tawi la aloe vera paka ule utomvu wake hapo asubuhi na jioni)
  • ukienda haja kubwa usimalize madakika huko 😃, kata gogo ukimaliza shenena chap afu usepe

Kyala akutule nkamu, kilabhu....
 
Habarini wapendwa, naombeni msaada wenu, kipindi cha nyuma mimi niliwahi kusumbuliwa na tatizo la umeng'enyaji chakula, nilikuwa najisaidia choo kigumu sana, nikaambiwa na doctor kuwa nina tatizo kwenye mfumo wa umeng'enyaji chakula, chakula hakimeng'enywi inavyotakiwa, nikapewa dawa tatizo hilo likaisha.

Lakini sasa kuna siku najisaidia nikapata choo kigumu sana nikachanika sehemu ya haja kubwa halafu kuna linyama likaning'inia chini, nikaanza kuuguza kidonda pale nilipochanika, kidonda kikapona lakini lile linyama bado lipo.

Nilienda hospital nikapewa anisol niwe napaka, nimepaka tube 2 bado hakijatoka, nikaanza kupaka mafuta ya mnyonyo bdo hiyo nyama ipo tu, nikaanza mafuta ya mzaituni bdo hiyo nyama ipo tu. Je nifanyaje?

Naombeni msaada wenu, na kuna kipindi nikiigusa hiyo nyama nahisi maumivu. Ahsanteni

1. Hiyo kitaalamu waita "haemorrhoid" achana hadithi za "bawasili" na uswahili uswahili wake na tiba zake za kinyungu nyungu.

2. Nenda hospitali ukatibiwe kibeberu.

3. Kasikilize ushauri wa daktari hata kama ni ka minor surgery.
 
Back
Top Bottom