Earthmover
JF-Expert Member
- Sep 28, 2012
- 23,107
- 20,648
Jumuiya ya Maendeleo ya nchini za Kusini mwa Afrika (SADC), imetangaza kuwa vikosi vyake nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vitafanya mashambulizi, kwa ushirikiano na vikosi vya serikali, ili "kuwamaliza waasi wa M23 na kurejesha amani na usalama."
SADC ilitangaza hayo katika taarifa yake ikilaani shambulio la bomu dhidi ya kambi ya wakimbizi ya Mugunga nje kidogo ya mji wa Goma, ambalo inasema lilitekelezwa na M23, kusababisha vifo vya watu takriban watu 16 na kujeruhi wengine takriban 30.
M23 walikanusha vikali madai hayo. Gavana wa Jimbo la Kivu, Ruguru, alisema kuwa watu 14 walifariki na wengine zaidi ya 35 kujeruhiwa katika shambulio la kambi ya Mugunga.
Vikosi vya SADC vimekuwa Kivu Kaskazini tangu mwishoni mwa mwaka jana, tangu Januari (1) vimeshiriki katika makabiliano ya "moja kw amoja" dhidi ya M23 kwa kutumia "mizinga nzito, ndege za kivita, ndege zisizo na rubani, na vifaru" katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa M23, kama mkuu wa M23 alivyotangaza wakati huo
Maswali yamekuwa yakiulizwa ikiwa onyo hili jipya kutoka kwa vikosi vya SADC linamaanisha kwamba vikosi hivi, hasa kutoka Afrika Kusini, vitatumia nguvu za kijeshi za ajabu katika mzozo huo.
Mwezi uliopita, Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini akiwa nchini Rwanda, aliwaambia waandishi wa habari kwamba ana "nguvu mpya na azma" ya kutafuta "suluhisho la kisiasa" la mzozo wa DR Congo.
Taarifa ya SADC iliyotolewa siku ya Jumapili ilisema kwamba vikosi vyake lazima vifanye mashambulizi haya ili "kuwalinda raia na mali zao, wanaokabiliwa na tishio la kushambuliwa", "kufungua barabara ili kukidhi mahitaji", "na kulinda raia wanaokimbia kuua."
M23 inakanusha kmadai hayo, ikilaumu vikosi vya serikali na waasi wa watiifu kwa serikali ya Kinshasa, ikisema kuwa walitumia silaha nzito karibu na kambi za wakimbizi.
Kujibu madai hayo, serikali ya Rwanda iliikosoa Marekani kwa "kufikia uamuzi mara moja wa kuilaumu Rwanda bila uchunguzi wowote", ikisema kwamba uchunguzi wa kuaminika lazima kwanza ukamilike ili kufichua kilichotokea.
Watu wengine 30 walijeruhiwa wakati makombora yalipopiga kambi za wakimbizi karibu na mji wa Goma mashariki mwa Congo siku ya Ijumaa iliyopita.
Katika taarifa yake, serikali ya Rwanda iliikosoa Marekani kwa "kufikia uamuzi mara moja wa kuilaumu Rwanda bila uchunguzi wowote" ikisisitiza kwamba uchunguzi wa kuaminika lazima kwanza ukamilike ili kufichua ni nini hasa kilitokea.
kwa mjibu wa tangazo lilitolewa na msemaji wa serikali ya Rwanda Yolande Makolo ,Rwanda haitabeba jukumu la shambulio hilo la makombora katika kambi za Mugunga na Lac Vert karibu na mji wa Goma, au kushindwa kwa utawala wa Congo kurejesha usalama mashariki mwa Congo.
Source : BBC news swahi
Nzambe bubariki Bakongomani bosee na majirani zetu kutoka MuTanzania na Afika ya Kusini kumupiga huyu adui ya kwetu huko kumapori busambaratishwe na Congo yetu kuwa sehemu salama ya kuishi
SADC ilitangaza hayo katika taarifa yake ikilaani shambulio la bomu dhidi ya kambi ya wakimbizi ya Mugunga nje kidogo ya mji wa Goma, ambalo inasema lilitekelezwa na M23, kusababisha vifo vya watu takriban watu 16 na kujeruhi wengine takriban 30.
M23 walikanusha vikali madai hayo. Gavana wa Jimbo la Kivu, Ruguru, alisema kuwa watu 14 walifariki na wengine zaidi ya 35 kujeruhiwa katika shambulio la kambi ya Mugunga.
Vikosi vya SADC vimekuwa Kivu Kaskazini tangu mwishoni mwa mwaka jana, tangu Januari (1) vimeshiriki katika makabiliano ya "moja kw amoja" dhidi ya M23 kwa kutumia "mizinga nzito, ndege za kivita, ndege zisizo na rubani, na vifaru" katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa M23, kama mkuu wa M23 alivyotangaza wakati huo
Maswali yamekuwa yakiulizwa ikiwa onyo hili jipya kutoka kwa vikosi vya SADC linamaanisha kwamba vikosi hivi, hasa kutoka Afrika Kusini, vitatumia nguvu za kijeshi za ajabu katika mzozo huo.
Mwezi uliopita, Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini akiwa nchini Rwanda, aliwaambia waandishi wa habari kwamba ana "nguvu mpya na azma" ya kutafuta "suluhisho la kisiasa" la mzozo wa DR Congo.
Taarifa ya SADC iliyotolewa siku ya Jumapili ilisema kwamba vikosi vyake lazima vifanye mashambulizi haya ili "kuwalinda raia na mali zao, wanaokabiliwa na tishio la kushambuliwa", "kufungua barabara ili kukidhi mahitaji", "na kulinda raia wanaokimbia kuua."
Ni nani aliyeshambulia kambi ya wakimbizi Mugunga?
Serikali za Marekani na DR Congo zilithibitisha kwamba shambulio hilo lilifanywa na waasi wa M23 kwa msaada wa Rwanda. SADC pia ilithibitisha kwamba ilifanywa na M23.M23 inakanusha kmadai hayo, ikilaumu vikosi vya serikali na waasi wa watiifu kwa serikali ya Kinshasa, ikisema kuwa walitumia silaha nzito karibu na kambi za wakimbizi.
Kujibu madai hayo, serikali ya Rwanda iliikosoa Marekani kwa "kufikia uamuzi mara moja wa kuilaumu Rwanda bila uchunguzi wowote", ikisema kwamba uchunguzi wa kuaminika lazima kwanza ukamilike ili kufichua kilichotokea.
Watu wengine 30 walijeruhiwa wakati makombora yalipopiga kambi za wakimbizi karibu na mji wa Goma mashariki mwa Congo siku ya Ijumaa iliyopita.
Katika taarifa yake, serikali ya Rwanda iliikosoa Marekani kwa "kufikia uamuzi mara moja wa kuilaumu Rwanda bila uchunguzi wowote" ikisisitiza kwamba uchunguzi wa kuaminika lazima kwanza ukamilike ili kufichua ni nini hasa kilitokea.
kwa mjibu wa tangazo lilitolewa na msemaji wa serikali ya Rwanda Yolande Makolo ,Rwanda haitabeba jukumu la shambulio hilo la makombora katika kambi za Mugunga na Lac Vert karibu na mji wa Goma, au kushindwa kwa utawala wa Congo kurejesha usalama mashariki mwa Congo.
Source : BBC news swahi
Nzambe bubariki Bakongomani bosee na majirani zetu kutoka MuTanzania na Afika ya Kusini kumupiga huyu adui ya kwetu huko kumapori busambaratishwe na Congo yetu kuwa sehemu salama ya kuishi