Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,328
Wakuu.
Leo mwenyekiti wa chama Taifa kamanda Freeman Mbowe yuko makao makuu ya kanda ya Magharibi inayoundwa na mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi kwenye kikao cha baraza la uongozi wa kanda kinachofanyika hapa makao makuu ya kanda mjini Tabora.
Kikao cha leo ni muendelezo wa vikao vya maboresho ya kanda ambavyo tayari vimeshafanyika kwenye kanda nyingine tangu mwanzoni mwa mwezi wa pili. Mpaka sasa hii ni kanda ya saba kutembelea katika mfumo wa kanda nane za kichama chini ya mfumo chama kwa Tanganyika. Kanda zilizokwisha tembelewa ni Pwani, kati, juu Kusini, kaskazini, Ziwa Victoria na ziwa Serengeti.
Kanda hii ina ukubwa wa eneo za kilometa za mraba zipatazo 177,647 na ina jumla ya watu 4,984,157. Kikao cha leo kitafuatiwa na mkutano wa hadhara na Kesho mwenyekiti Taifa anakutana na wadau wa kanda ya Magharibi kutoka kwenye nyanja na taaluma mbalimbali ambao ni wapenzi na wanachama wa CHADEMA
Leo mwenyekiti wa chama Taifa kamanda Freeman Mbowe yuko makao makuu ya kanda ya Magharibi inayoundwa na mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi kwenye kikao cha baraza la uongozi wa kanda kinachofanyika hapa makao makuu ya kanda mjini Tabora.
Kikao cha leo ni muendelezo wa vikao vya maboresho ya kanda ambavyo tayari vimeshafanyika kwenye kanda nyingine tangu mwanzoni mwa mwezi wa pili. Mpaka sasa hii ni kanda ya saba kutembelea katika mfumo wa kanda nane za kichama chini ya mfumo chama kwa Tanganyika. Kanda zilizokwisha tembelewa ni Pwani, kati, juu Kusini, kaskazini, Ziwa Victoria na ziwa Serengeti.
Kanda hii ina ukubwa wa eneo za kilometa za mraba zipatazo 177,647 na ina jumla ya watu 4,984,157. Kikao cha leo kitafuatiwa na mkutano wa hadhara na Kesho mwenyekiti Taifa anakutana na wadau wa kanda ya Magharibi kutoka kwenye nyanja na taaluma mbalimbali ambao ni wapenzi na wanachama wa CHADEMA