Kero ya wananchi mbele ya Mkuu wa Mkoa Arusha ndugu Makonda

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
497
921
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa.

Mimi naona wananchi wengi wanapoteza muda wao na hawatasaidiwa chochote na Mkuu wa Mkoa ni vema wakafuata taratibu za kisheria. Hata yule Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha alioagiza ahamishwe, mimi naona siyo utawala bora kusema mbele ya watu kuwa ahamishwe.

Usitafute popularity ambayo haisaidii. Najua wananchi wana kero nyingi na wanaonewa lakini ni hakuna budi sheria zifuatwe kutatua kero hizo.
 
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa...
Aisee nashangaa Arusha ghafla nao wamegeuka wamekuwa kama watu wa kule Katavi na Tandahimba kulialia wakati wanaelewa sheria na utaratibu wa kupata haki,wanahangaika na mtu wakuwapotosha tu na kisha kuwaacha kwenye mataa ya mianzini
 
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa...
Sheria ipi unaizungumzia. Kuna mwanamama alishinda na kukabidhiwa shamba lake na dalali wa mahakama kule Karatu 2015, lakini mpk leo walioshindwa kesi wamekataa kuondoka badala yake wanalindwa na OCD wa Karatu kwa kula rushwa. Ulitegemea nani amsaidie. Kuna maeneo anasaidia
 
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa.

Mimi naona wananchi wengi wanapoteza muda wao na hawatasaidiwa chochote na Mkuu wa Mkoa ni vema wakafuata taratibu za kisheria. Hata yule Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha alioagiza ahamishwe, mimi naona siyo utawala bora kusema mbele ya watu kuwa ahamishwe.

Usitafute popularity ambayo haisaidii. Najua wananchi wana kero nyingi na wanaonewa lakini ni budi sheria zifuatwe kutatua kero hizo.
Huu ushauri wako ungekuwa mzuri zaidi kama na wewe ungekuwa unaenda kuutoa kwa wananchi pindi ambapo makonda anaongea nao na wewe unashauri hivi,utasaidia zaidi. Kuliko kukaa nyuma ya keyboard unaongea pumba ambazo hazionyeshi kuwasaidia hao wananchi
 
Kweli umemsikiliza vizuri namna anavyosikiliza kero hizo na namna anavyozitanzua, au mmejipanga tu kutafuta huruma ya umma kwa kuleta mada za namna hii humu?

Kwa jinsi kero za watu wengi wanavyozisema wazi mahakama kutumika kudhulumu haki zao, ama haki zinazotolewa mahakamani kutokupatikana kwa kushindikana utekelezaji wake, ninamuunga mkono sana Rc Makonda, angalau kuonesha kupoza machungu ya raia.

Hakuna popote Makonda alipoingilia Mahakama, bali anasikiliza kero zote zikiwemo dhuluma za kisheria na wanasheria na kuelekeza kufuatilia kuziba tobo ulipoanzia uharibifu.

Serikali ina utatu wake: Serikali kuu, Bunge na Mahakama.

Vyombo vyote hivyo vimewekwa kusaidia watu , hakuna kilicho juu ya sheria kutokuchunguzwa kikitenda kinyume na maadili ya umma.

Huyo mwanasheria wako wa Halmashauri ni mtumishi wa umma mzembe na mbinafsi sana, ni mfano wa uozo wa watumishi wa umma iliotamalaki nchini.

Hakutakiwa hata kupewa upendeleo wa uhamisho kwa namna uzembe wa wazi ulivyojidhihirisha katika eneo lake kiuwajibikaji.

Tungelikuwa na maRc wengine kama Makonda huko kwingine, Serikali hii isingelichukiwa na kutukanwa kama ilivyo sasa na sababu kubwa za wazi watu kuichukia Serikali yao ni kuwa Serikali yote imelala usingizi wa pono, hakuna anayeweza kumuamsha mwingine kutoka usingizini.

Makonda kaonesha njia ya namna kiongozi mwajibikaji anatakiwa awe.

Tumpeni moyo na shime kwa kumuunga mkono.
 
Watu wengi tu wamesaidiwa kwenye matatizo mbalimbali waliyoleta.

Kuna waliosaidiwa msaada wa kisheria, kukaza hukumu, kurudishiwa viwanja vilivyotapeliwa kwa kuuzwa mara mbili, waliotekeleza familia zao kuingia makubaliano ya kulipa child support.

Msaada wa matibabu, migogoro mingi ya ardhi imepatiwa ufumbuzi kwa msaada wa Tanganyika Law Society.

Ukiona mtu anapinga wananchi kusaidiwa basi ana chuki binafsi au anafaidika na mtandao wa dhuluma au ndio matapeli wenyewe na mawakala wao.

Huwezi kupinga haki na kuunga mkono dhuluma kama una akili timamu.
 
Hata kama hajatatua tatizo kusikilizwa na kiongozi ni relief kubwa sana kwa mwananchi anayedhulumiwa. Kama yule Mwl Beatrice yule jamaa wa ofisi ya Halmashauri ya jiji anavyompiga danadana na figisu...wacha Makonda awanyooshe hawa wafanyakazi wa ofisi za Umma Arusha ambao wamejimilikisha hizo ofisi.
 
Mlianza kua Makonda anaigiza na hao wenye kero ni maigizo ikapita Kwa sasa ni Makonda hafuati sheria mnabadili kauli kila siku ili kukwamisha juhudi nzuri za kiongozi dhidi ya wanyonge wenye shida mbalimbali, kweli ninyi ni watu wa ajabu sana
 
Usanii tu, Nabii Lema atakuja kutatua kero kwa kufuata sheria na taratibu bila kuingilia vyombo.
 
Nimekuwa nikifuatilia wananchi wa Mkoa wa Arusha wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Makonda. Kwa asilimia kubwa lazima sheria zifuatwe na Mkuu wa Mkoa hayuko juu ya sheria. Inawezekana kero nyingi zilizotolewa tayari aidha ziko Mahakamani au uamuzi wa kisheria ulikwishapitiwa.

Mimi naona wananchi wengi wanapoteza muda wao na hawatasaidiwa chochote na Mkuu wa Mkoa ni vema wakafuata taratibu za kisheria. Hata yule Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha alioagiza ahamishwe, mimi naona siyo utawala bora kusema mbele ya watu kuwa ahamishwe.

Usitafute popularity ambayo haisaidii. Najua wananchi wana kero nyingi na wanaonewa lakini ni budi sheria zifuatwe kutatua kero hizo.

Sheria gani hizo unazo sema mbona hawakusaidiwa kabla kama sheria zipo, au unadhani hayo matatizo raia wanayo sema kwamba wameyapata Makonda alivo enda kule?

Watu mnapenda kutumia siasa kwenye maisha ya watu, watu wananyanyasika, wanateseka kwenye ardhi zao wengine wanauawa wakiwa wanatetea haki zao haya yote Makonda ndiye ameibua si kwamba hayakuwepo haya yalikuwepo na wanasheria wote wapo, ila leo mnataka kutoa kauli za hovyo tu kumchafua Makonda, *siasa ziwepo lakini na utu pia uwepo *
 
aisee nashangaa arusha ghafla nao wamegeuka wamekuwa kama watu wa kule katavi na tandahimba kulialia wakati wanaelewa sheria na utaratibu wa kupata haki,wanahangaika na mtu wakuwapotosha tu na kisha kuwaacha kwenye mataa ya mianzini

Je hizo sheria zinawasaidia watu?? Mambo madogo haya haya hitaji hata nguvu kubwa kuelewa,, acheni siasa nadhani unasema hivo sababu hujawahi kukumbana na changamoto yoyote ambayo ulijaribu kufata sheria lakini hukusikilizwa laiti ungepitia hivo ungetambua msaada wa Makonda
 
Back
Top Bottom