Kanisa Katoliki latoa waraka mpya unaiotwa 'Dignitas Infinita' likipinga Utoaji Mimba, Kubadilisha Jinsia na Upandikizaji wa Mimba

Andiko gani linasema wapenzi wa jinsia moja wabarikiwe kanisani?

Nakubali hakuna mwenye dhambi anapaswa kufungiwa mlango, na natambua Yesu alikuja kwa ajili ya wenye dhambi.

1.Lakini kuna tofauti hapo, Yesu alimfata Zakayo mtoza ushuru (alikuwa mwenye dhambi maana aliwadhurumu watu mali zao), akampa injili hatimae Zakayo akaacha dhambi (akaacha kudhurumu na akarudisha mali za aliowadhurumu mara 4 zaidi)

2.Yesu alipoletewa mwanamke aliefumaniwa akifanya uzinzi (dhambi), alimsamehe na kumwagiza asitende dhambi tena.

Swali langu kwako, Papa aliposema wapenzi wa jinsia moja wabarikiwe je kuwabariki kungewafanya waache dhambi zao (kufanya mapenzi ya jinsia moja) au wakibarikiwa maana yake aendelee kufanya dhambi (kuendeleza mapenzi ya jinsia moja)?

Kama walipata uongozi wa Mungu kubariki wapenzi wa jinsia moja
1. Kwanini watu wa sodoma na gomora walichomwa?
2. Kwa nini kauli imebadilika sasa, je Mungu amegundua alikosea kuruhusu jambo alilolikataza mwenyewe?
Papa hakusema ushoga wao ubarikiwe, bali mashoga wabarikiwe.
Kuna ushoga hapo na mashoga.
Ushoga wao kanisa haliukubali, ila linapinga kuwatenga mashoga.
 
Ukisoma vitabu vyote 72 kwenye biblia yako, hakuna sehemu Mungu wala nabii wala mtume kasema WAPENZI WA JINSIA MOJA WABARIKIWE.
Ulivyosema tamko lipo kibiblia ulidanganya.

Unataka darasa kuhusu nini?
Kuwa specific
Mathayo 5:45 BHN
ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaangazia jua lake watu wabaya na wema, na kuwanyeshea mvua watu wanyofu na waovu.
 
Hawawezi kuacha
2015-01-06T101900Z_445121593_GM1EB161EBK01_RTRMADP_3_USA-FLORIDA-GAYMARRIAGE.jpg
 
Ukisoma vitabu vyote 72 kwenye biblia yako, hakuna sehemu Mungu wala nabii wala mtume kasema WAPENZI WA JINSIA MOJA WABARIKIWE.
Ulivyosema tamko lipo kibiblia ulidanganya.

Unataka darasa kuhusu nini?
Kuwa specific
Righteous mmefura, wenyewe mmejivika utakatifu.
Aliyeziumba mbingu na kutenga nyakati mnamuona si mkamilifu, mnataka mhariri nyendo zake.

Ah, si Yeye aliyesema"acha Magugu na Ngano vikue pamoja?".
Righteous mmeona anachelewa, mnataka mchukue Mundu mtenge Magugu na Ngano hata kabla ya wakati haujafika!.
😅
 
Papa hakusema ushoga wao ubarikiwe, bali mashoga wabarikiwe.
Kuna ushoga hapo na mashoga.
Ushoga wao kanisa haliukubali, ila linapinga kuwatenga mashoga.
Kwahiyo kanisa halitaki ushoga ila linapinga kuwatenga mashoga !!
WAGALATI 3:1 Ninyi wagalatia mmekua wajinga kweli! Ni nani aliewaroga?
 
Umemaanisha huo mstari unasema WAPENZI WA JINSIA MOJA WABARIKIWE?
Hoja ni kwamba, mbona wazinzi wanabarikiwa?.
Mbona wala rushwa wanabarikiwa?.
Huwezi kuwa selective swala linapokuja kwenye dhambi.
Mla rushwa kanunua gari lake na kulipeleka kwa Padri kubarikiwa, Padri analibariki.
Ila Shoga Akiwa na jogoo wake akitaka Padri ambariki, Padri anakataa kisa ni Shoga.
Uoni kuwa ni double standard
 
Righteous mmefura, wenyewe mmejivika utakatifu.
Aliyeziumba mbingu na kutenga nyakati mnamuona si mkamilifu, mnataka mhariri nyendo zake.

Ah, si Yeye aliyesema"acha Magugu na Ngano vikue pamoja?".
Righteous mmeona anachelewa, mnataka mchukue Mundu mtenge Magugu na Ngano hata kabla ya wakati haujafika!.
😅
Kejeri hazikufanyi uonekane una akiri sana.
Nikiemuuliza swali alidai tamko liko Biblia, nikataka aniambie ni sehemu gani akashindwa.
Umeni quote na andiko la matayo, nikakuuliza ndilo linasema kuhusu kubariki mashoga unakuja na kejeri.

Aliesema acha magugu na ngano vikue pamoja, ndie aliteketeza kwa moto sodoma na gomora.

Kama Mungu alimwagiza papa kutoa lile tamko, kwa nini anabadilisha sasa?
 
Ukisoma vitabu vyote 72 kwenye biblia yako, hakuna sehemu Mungu wala nabii wala mtume kasema WAPENZI WA JINSIA MOJA WABARIKIWE.
Ulivyosema tamko lipo kibiblia ulidanganya.

Unataka darasa kuhusu nini?
Kuwa specific
Ningekuwa na muda rafiki kwangu ningeelea na huu mjadala kwa kina lengo haswa kufahamu na kuongeza ufahamu.

Kifungu katika Bilbia kwamba wapenzi wa jinsia moja wabarikiwe hamna.
Ila Yesu alisema tabibu hawezi kujiponya, hakuja kwa ajili ya wenye haki,na ndio maana alitoa ule mfano wa mfarisayo ma mtoza ushuru walioenda kusali .

Alitoa pia mfano sa kondoo aliyepotea na kupatika, ilikuwa furahaa kwa kondoo mmoja kupatika wakati alipokua amepotea kuliko furaha ya kondoo 99 ambao hawakuwa wamepotea.

Ni katika muktadha wa kujifunza zaidi, je mtu alie shoga, alibadili jinsia, aliye jambazi alie muuaji au alie mbaya kwa namna yoyote tunayoweza kutafsiri akifunguliwa mlango na kanisa, akaingia na kukutana na neema ya Mungu katika hali ya ubaya wake huo nakutafuta kutubu na kumrejea Mungu na kuacha ubaya wake , kanisa lilaumiwe kwa kufungulia mlango?
 
Hoja ni kwamba, mbona wazinzi wanabarikiwa?.
Mbona wala rushwa wanabarikiwa?.
Huwezi kuwa selective swala linapokuja kwenye dhambi.
Mla rushwa kanunua gari lake na kulipeleka kwa Padri kubarikiwa, Padri analibariki.
Ila Shoga Akiwa na jogoo wake akitaka Padri ambariki, Padri anakataa kisa ni Shoga.
Uoni kuwa ni double standard
Hayo yote si yanfanyika huko lilikotoka tamko.
 
Kejeri hazikufanyi uonekane una akiri sana.
Nikiemuuliza swali alidai tamko liko Biblia, nikataka aniambie ni sehemu gani akashindwa.
Umeni quote na andiko la matayo, nikakuuliza ndilo linasema kuhusu kubariki mashoga unakuja na kejeri.

Aliesema acha magugu na ngano vikue pamoja, ndie aliteketeza kwa moto sodoma na gomora.

Kama Mungu alimwagiza papa kutoa lile tamko, kwa nini anabadilisha sasa?
Umeninukuu vibaya Chief, tukomee hapa.
 
Kifungu katika Bilbia kwamba wapenzi wa jinsia moja wabarikiwe hamna.
Ila Yesu alisema tabibu hawezi kujiponya, hakuja kwa ajili ya wenye haki,na ndio maana alitoa ule mfano wa mfarisayo ma mtoza ushuru walioenda kusali .

Alitoa pia mfano sa kondoo aliyepotea na kupatika, ilikuwa furahaa kwa kondoo mmoja kupatika wakati alipokua amepotea kuliko furaha ya kondoo 99 ambao hawakuwa wamepotea.
You're honest bro, I like that.

Yesu ni kweli alisema hayo. Lengo lake ni kumfanya mwenye dhambi aache dhambi zake, atubu na kupokea msamaha. Kwa kufata huo mfano ilitakiwa papa aseme, mashoga wanaotubu na kuacha ushoga wabarikiwe hakungekuwa na shida maana wameacha dhambi yao na kutubu hivyo wanapaswa kupokelewa.

Ndio maana biblia inasema maombi ya mwenye dhambi yanayosikiwa na Mungu ni ya toba pekee.

Ni katika muktadha wa kujifunza zaidi, je mtu alie shoga, alibadili jinsia, aliye jambazi alie muuaji au alie mbaya kwa namna yoyote tunayoweza kutafsiri akifunguliwa mlango na kanisa, akaingia na kukutana na neema ya Mungu katika hali ya ubaya wake huo nakutafuta kutubu na kumrejea Mungu na kuacha ubaya wake , kanisa lilaumiwe kwa kufungulia mlango?
Mwenye dhambi anakaribishwa kanisani ili atubu na kuacha dhambi sio aje kanisani na kuendelea na dhambi yake. Kubariki jambazi ambae bado anaiba sio sawa, ila akitubu na kuacha ana haki kubarikiwa.
 
Back
Top Bottom