Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 1,669
- 4,921
Siku ya leo Kanisa Katoliki kupitia idara ya habari ya Vatican limetoa waraka mpya unaoitwa "Dignitas Infinita" Miongoni mwa mambo yanayozungumziwa kwenye waraka huo Uliosainiwa na Papa ni pamoja na Msimamo wa Kanisa katoliki katika Kupinga Utoaji Mimba, Kubadilisha Jinsia na Upandikizaji wa Mimba.
Katika waraka huo wenye Point 66, umevavaduliwa kama ifuatavyo
USHOGA NA KUBADILI JINSIA
Point ya 60 katika Waraka huu inapinga hali ya ushoga au kubadili jinsi. Kanisa likisisitiza mtu kuheshimu jinsi alivyoumbwa tangu anazaliwa, hivyo kuheshimu mpangilio wa asili wa mwili wa binadamu tangu anazaliwa. Kanisa linapinga kitendo chochote cha ubadilishaji jinsia kinyume na asili ya mwanadamu ukiachilia mbali wale waliozaliwa wakiwa na shida ya maumbile ambapo Daktari atathibitisha hilo.
KUTOA MIMBA
Point ya 47 inasisitiza kanisa linakataa utoaji mimba, na kwamba ni kinyume cha mapenzi ya MUNGU, na kwa sababu mtoto yeye hana makosa na hawezi kujitetea. Utoaji mimba ni kosa katika miiko ya kanisa
KUPANDIKIZA MIMBA (SURROGACY)
Point ya 48, 49, na 50 Kanisa linakemea kitendo cha kubeba mwanamke kubeba mimba kwa niaba ya mwanamke mwingine au kupandikiza mimba, likisisitiza Mtoto anatakiwa kubebwa katika mfuko wa uzazi wa mama yake na si mtu mwingine.
VITA
Point ya 38 na 39 kanisa linahimiza kuepuka vita, na kupinga vikali vitendo vyote vinavyochochea vita au ubaguzi kwa namna yeyote.
WAHAMIAJI HARAMU (IMMIGRANTS)
Point ya 40 kanisa linasisitiza wahamiaji haramu wasitengwe au kufanyiwa uvunjifu wa utu wao, Kanisa linataka wahamiaji haramu watendewe mema kama watu wengine kwa sababu hawakutaka kuwa katika hali hiyo, hivyo jamii ziwapokee, ziwasaidie na si kuwabagua.
USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU (HUMAN TRAFFICKING)
Point ya 41 na 42 kanisa linasema litaendelea kupambana na vitendo vya kusafirisha binadamu kwa ajili ya kuuza viungo vyao vya mwili, kwa ajili ya kazi za kitumwa, kwa ajili ta kazi za umalaya, kwa ajili ya kuwatumikisha kingono mabinti na vijana wadogo, kwa ajili ya vitendo vya kigaidi na kazi zote za namna hiyo.
UKATILI WA KIJINSIA
Point ya 43 kanisa linapinga ukatili wa aina yoyote wa kijinsia
UKATILI WA WANAWAKE
Point ya 44, 45 na 46 Kanisa linapinga ukatili wa wanawake ikiwemo rushwa ya ngono, kitendo cha kuwatumia wanawake kama chombo cha starehe kuwafurahisha wanaume, vipigo, kuwashurutisha kutoa mimba, bila kusahau kuwafanyia ndoa za mitaala (wake wengi), vitendo hivyo vyote vinapingwa na kanisa
KUSITISHA MAISHA YA MGONJWA, AU KUSAIDIA MTU KUJITOA UHAI
Point ya 51 na 52 kanisa linakataza kitendo cha kukatisha maisha ya mgonjwa kwa namna yoyote au kumsaidia mtu kujitoa uhai. Kanisa linaimiza hata kama mtu ni mahututi kiasi gani au hawezi kupona basi ni vyema tumfariji mpaka pale umauti wake utakapomfika na si kutoa uhai wake kwa namna yoyote hata kama ni kwa ridhaa yake.
UBAGUZI WA WALEMAVU
Point ya 53 na 54 Kanisa linapinga vitendo vya ubaguzi na kuwatenga walemavu.
VURUGU MITANDAONI YA KIDIGITALI
Point ya 61 na 62 kanisa linakumbusha kutumia mitandao katika njia nzuri, na sio kutumia kuumiza wengine. Kanisa linasema kazi ya Teknolojia ya kidigitali ni kumsaidia binadamu na si kumdhuru.
SOMA WARAKA WOTE HAPA CHINI: Declaration of the Dicastery for the Doctrine of the Faith “Dignitas Infinita” on Human Dignity
Katika waraka huo wenye Point 66, umevavaduliwa kama ifuatavyo
USHOGA NA KUBADILI JINSIA
Point ya 60 katika Waraka huu inapinga hali ya ushoga au kubadili jinsi. Kanisa likisisitiza mtu kuheshimu jinsi alivyoumbwa tangu anazaliwa, hivyo kuheshimu mpangilio wa asili wa mwili wa binadamu tangu anazaliwa. Kanisa linapinga kitendo chochote cha ubadilishaji jinsia kinyume na asili ya mwanadamu ukiachilia mbali wale waliozaliwa wakiwa na shida ya maumbile ambapo Daktari atathibitisha hilo.
KUTOA MIMBA
Point ya 47 inasisitiza kanisa linakataa utoaji mimba, na kwamba ni kinyume cha mapenzi ya MUNGU, na kwa sababu mtoto yeye hana makosa na hawezi kujitetea. Utoaji mimba ni kosa katika miiko ya kanisa
KUPANDIKIZA MIMBA (SURROGACY)
Point ya 48, 49, na 50 Kanisa linakemea kitendo cha kubeba mwanamke kubeba mimba kwa niaba ya mwanamke mwingine au kupandikiza mimba, likisisitiza Mtoto anatakiwa kubebwa katika mfuko wa uzazi wa mama yake na si mtu mwingine.
VITA
Point ya 38 na 39 kanisa linahimiza kuepuka vita, na kupinga vikali vitendo vyote vinavyochochea vita au ubaguzi kwa namna yeyote.
WAHAMIAJI HARAMU (IMMIGRANTS)
Point ya 40 kanisa linasisitiza wahamiaji haramu wasitengwe au kufanyiwa uvunjifu wa utu wao, Kanisa linataka wahamiaji haramu watendewe mema kama watu wengine kwa sababu hawakutaka kuwa katika hali hiyo, hivyo jamii ziwapokee, ziwasaidie na si kuwabagua.
USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU (HUMAN TRAFFICKING)
Point ya 41 na 42 kanisa linasema litaendelea kupambana na vitendo vya kusafirisha binadamu kwa ajili ya kuuza viungo vyao vya mwili, kwa ajili ya kazi za kitumwa, kwa ajili ta kazi za umalaya, kwa ajili ya kuwatumikisha kingono mabinti na vijana wadogo, kwa ajili ya vitendo vya kigaidi na kazi zote za namna hiyo.
UKATILI WA KIJINSIA
Point ya 43 kanisa linapinga ukatili wa aina yoyote wa kijinsia
UKATILI WA WANAWAKE
Point ya 44, 45 na 46 Kanisa linapinga ukatili wa wanawake ikiwemo rushwa ya ngono, kitendo cha kuwatumia wanawake kama chombo cha starehe kuwafurahisha wanaume, vipigo, kuwashurutisha kutoa mimba, bila kusahau kuwafanyia ndoa za mitaala (wake wengi), vitendo hivyo vyote vinapingwa na kanisa
KUSITISHA MAISHA YA MGONJWA, AU KUSAIDIA MTU KUJITOA UHAI
Point ya 51 na 52 kanisa linakataza kitendo cha kukatisha maisha ya mgonjwa kwa namna yoyote au kumsaidia mtu kujitoa uhai. Kanisa linaimiza hata kama mtu ni mahututi kiasi gani au hawezi kupona basi ni vyema tumfariji mpaka pale umauti wake utakapomfika na si kutoa uhai wake kwa namna yoyote hata kama ni kwa ridhaa yake.
UBAGUZI WA WALEMAVU
Point ya 53 na 54 Kanisa linapinga vitendo vya ubaguzi na kuwatenga walemavu.
VURUGU MITANDAONI YA KIDIGITALI
Point ya 61 na 62 kanisa linakumbusha kutumia mitandao katika njia nzuri, na sio kutumia kuumiza wengine. Kanisa linasema kazi ya Teknolojia ya kidigitali ni kumsaidia binadamu na si kumdhuru.
SOMA WARAKA WOTE HAPA CHINI: Declaration of the Dicastery for the Doctrine of the Faith “Dignitas Infinita” on Human Dignity