Kama lengo la chama cha siasa ni kushika madaraka, kwa sasa CCM ndiyo chama chenye mafanikio zaidi Afrika?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,369
12,970
Nimesikia mara nyingi sana viongozi, hasa viongozi wa vyama vya upinzani wakisema kuwa lengo kuu la chama cha siasa ni kushika madaraka. Maana yake chama kikishika madaraka kinakuwa kimetimiza lengo lake kuu. Na kikiyashika kwa muda mrefu zaidi ndivyo kinavyokuwa kimetimiza lengo lake kuu kwa mafanikio zaidi.

Sasa kwa vyama vilivyopo madarakani Afrika Nzima, CCM ndicho chama kilichokaa madarakani kwa muda mrefu zaidi. Na katika historia nzima ya Afrika ni chama cha pili kwa kutawala muda mrefu. Hilo haliifanyi CCM kuwa chama chenye mafanikio zaidi Afrika? Kitu gani kimefanya CCM ifikie mafanikio hayo? Vyama vingi vya aina yake vimeishapotea siasani. Tena vingine vikiwa na nguvu kubwa sana ya dola nyuma yake lakini vimeanguka. Nini siri ya mafanikio haya makubwa ya CCM?
 
๐๐š ๐ฆ๐š๐Ÿ๐š๐ง๐ข๐ค๐ข๐จ ๐ฒ๐ž๐ง๐ฒ๐ž๐ฐ๐ž ๐ง๐ข ๐ค๐ฎ๐ญ๐ฎ๐ฆ๐ข๐š ๐ง๐ ๐ฎ๐ฏ๐ฎ ๐ฒ๐š ๐ฏ๐ฒ๐จ๐ฆ๐›๐จ ๐ฏ๐ฒ๐š ๐ฎ๐ฌ๐š๐ฅ๐š๐ฆ๐š ๐ค๐ฎ๐ฌ๐ก๐ข๐ง๐๐ข ๐ค๐ข๐ฅ๐š ๐œ๐ก๐š๐ ๐ฎ๐ณ๐ข .
 
Uongozi bora siasa na umoja ndani ya chama kubwa makofii tafadhali pwah pwah pwah.......
 
Back
Top Bottom