Kama Bulembo anaweza kumdhaliisha Polepole, upi usalama wa waliounga juhudi mkono wakateuliwa nafasi mbalimbali?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Bulembo anapodiriki kusema Katibu Mkuu wa chama hakua mwana CCM anatuma salama Kwa akina Nassary, Mashinji, Mdee na wengine kwamba Muda wao wakufaidi keki ya Taifa umeisha wajiandae kukabidhi V8 vinginevyo waombe sana mwenyekiti wa CCM awakingie kifua.

Hawa wazee wana roho za kikatili na wanapenda sana maendeleo ya watoto wao SI Watanzania. JPM alifikia akawateua yeye na mtoto wake lakini Leo adharani anamdhaliisha kwa sababu TU hayupo hai. Hii inatoa picha kwa viongozi wengine kwamba Tanzania hakuna upendo kwa wanasiasa wanachofanya nikuangalia maslahi.

Upo uwezekano Mwenyekiti wa CCM akadhani amezungukwa na watu kumbe amezungukwa na mbwa mwitu. Upo wakati anaweza akafumbua macho uonevu wa wale wasio wanaccm akidhani wanaccm wapo naye kumbe Bora hata wsio wanaccm maana wanamweleza ukweli.

Huyu Mzee Leo ametufumbua macho hasa alipohoji kama polepole anapesa? Baada tu yakuhoji hivyo tunashuhudia chumba kimoja cha polepole huko Dodoma kikiwa na kila kitu. Means mzee anajua uwezo wa kiuchumi wa Polepole. Kwa mtizamo Wangu Bora polepole anayeishi kwenye chumba kimoja na hana pesa kuliko viongozi wenye pesa walizoiba Kwa wananachi na wanatumia Fedha hizo kudhalilisha wananchi.

Mwisho, Huyu Mzee anaposema alikuwa anabadilishana nguo na JPM kwenye kampeni ni dharau kubwa sana,lakini kibaya Zaid hawa ndio waliokuwa washauri wa JPM na watu wa aina hii ndio wenyeviti wa vyama mikoa na will na intelijensia ya chama haikuona dhamira zao. Je, wanaoutafsiri negatively uongoz wa chama uliopo ni wangapi? Wanavyoendleza hizi harakati ndani ya mfumo ambao chama ndiyo serikali tunadhani tutapata maendeleo? Kwamba uichukie awamu ya Tano na uishauri ipate maendeleo No. Tujitathimini
 
Alianza mzeevWasira akasema baada ya jiwe kutwaliwa sasa watanzania wanapumua

Akafuata mzee Diallo akasema jiwe alipaswa kuwa Milembe.

Sasa amekuja Bulembo anasema sasa watu Wana Uhuru wa kusema na diplomasia iliyoharibiwa na jiwe mama anaijenga upya.

Nani atafuata?
 
tofautisha kudhalilisha mtu, na kumpa ukweli mtu
Niliujua unafiki wa Bulembo alipo kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji wa FAT au TFF siku hizi. Huyu yeye anacho angalia maishani make ni FEDHA tu basi. Ni halali au ni haramu hilo utajua wewe.

Wakati ule alikuwa CHAWA wa Ndolanga na ndio alikuwa anamwambia kwa jinsi wajumbe wanavyo mpenda atadumu pale FAT milele.

Siku zile wajumbe wa mkutano mkuu walikuwa 62 tu, sasa yeye Bulembo , Marehemu Makanjira na Mwingine kutoka Rukwa nimemsahau jina, walikuwa wanamshauri Ndolanga awahonge wajumbe 37 tu ili hawa wakimpa kura zao tayari anakuwa mshindi na anakuwa Mwenyekiti wa FAT siku hizi TFF. Kwahiyo walipewa rushwa kubwa kupitia huyu Bulembo na Makanjira aliye kuwa mjumbe wa kamati kuu akitokea Iringa.

Serikali ilipo ona kuwa kumtoa Ndolanga kwa kura isingewezekana , walicho fanya kupitia BMT wakaongeza idadi ya wapiga kura mpaka kufikia 120. Katika uchaguzi ulio fuata serikali walikuwa upande wa LEODIGA CHILLA TENGA , na kumwaga TAKUKURU kila kona kuhakikisha Ndolanga na hawa akina Bulembo hawapati fursa ya kuwa rubuni wajumbe kwa RUSHWA. Ndolanga akashindwa katika uchaguzi ule.

Baada ya hapo huyu Bulembo aka akahamia kwenye siasa na kamwe hakuacha kuwa CHAWA. Ni mtu anaye angalia tumbo lake.

Nilicho jifunza katika maisha CHAWA ni wabaya kuliko SHETANI. Shetani ana huruma kwasababu akijua wewe unampambania Mungu , anakuacha uendelee na Mungu anakubali kushindwa. CHAWA huwa hawakubali kushindwa, ni wabaya.

Hapo alipo fikishwa Polepole ni lazima akubali kushindwa. Hawa darasa la saba akina Bulembo watammaliza siyo tu kisiasa lakini anaweza akajikuta amepoteza vingi including life.

ATAKWENDA POLISI, ATASHANGAA, HAWATA MSIKILIZA KWASABABU WATAKUWA WANASOMA UPEPO WAJUE WALIO MFANYIA HAYO NI CCM AU CHAWA WA TAIFA??

Polepole akubali kuwa Magufuli is No More, na huo ndio mwisho wao popote walipo, iwe bandarini, Dodoma au kwenye Siasa ndio mwisho wa ENZI.

Huyu CHAWA mbobevu amejua hilo, amesha jua ahamie shati lipi. Kwasasa yupo na Samia , kabla alikuwa kwa Kikwete. Huyo ndio Bulembo ninaye mjua mimi.
 
In my opinion mwendazake aliweka watu ambao sio CCM by origin kwa kuwa CCM was rotten to the core (Kinana etc) sasa wenye chama (rudia twitter post ya Nape) are back in full force.
 
Yawezekana huyu ni mmoja wa wale vifutu waliokuwa wamejimilikisha mali za chama. Hakuna namna mtu wa aina hiyo angeweza kumpenda mtu (Bashiru) aliyewatemesha kitumbua!
 
Very sad.
1639354650275.jpeg
 
Baada ya nyumba ya Polepole kuvunjwa na kuibiwa polisi walitakiwa wamkamate Bulembo na kumhoji kwani kauli zake zimeendana na yaliyomkuta Poleploe
 
Back
Top Bottom