Jinsi mitumba inavyotuunganisha na watu tusiowapenda!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,518
34,322
Asubuhi ya leo wakati navua raba nilipotoka mazoezini, ghafla lilinijia wazo la ni nani alikuwa anaivaa raba hiyo kabla haijaletwa Tanzania kama mtumba?

Nikaanza kuangalia jinsi mitumba ilivyotawala maisha ya Watanzania kwa kiasi kikubwa Sana. Lakini huwa tunajiuliza hiyo mitumba ilikotoka ilikuwa inatumiwa na nani?

Kwa mfano magari ingawa hatupendi sana kuyaita mitumba, badala yake tunayaita "Used" lakini ukweli wa mambo na yenyewe pia ni mitumba.

Unaweza kuwa unachukia watu wenye tabia ya ushoga, lakini una hakika mitumba unayotumia hakuna ambao ulikuwa unatumiwa na shoga kabla ya wewe kuununua?

Ipo mitumba toka kwa wezi, majambazi, makahaba, watu wa dini tofauti na sisi, wabaguzi, wauwaji, wafungwa, wabakaji, matapeli na lundo jingine kubwa sana la watu tusiowapenda.

Unapotumia mtumba jua kuwa inawezekana kabisa kabla ya kuletwa Tanzania huko ulikotoka ulikuwa unatumiwa na mtu/watu usiowapenda kabisa.
 
Asubuhi ya leo wakati navua raba nilipotoka mazoezini, ghafla lilinijia wazo la ni nani alikuwa anaivaa raba hiyo kabla haijaletwa Tanzania kama mtumba!!??

Nikaanza kuangalia jinsi mitumba ilivyotawala maisha ya watanzania kwa kiasi kikubwa Sana. Lakini huwa tunajiuliza hiyo mitumba ilikotoka ilikuwa inatumiwa na nani!?

Kwa mfano magari ingawa hatupendi sana kuyaita mitumba, badala yake tunayaita "Used" lakini ukweli wa mambo na yenyewe pia ni mitumba.

Unaweza kuwa unachukia watu wenye tabia ya ushoga, lakini una hakika mitumba unayotumia hakuna ambao ulikuwa unatumiwa na shoga kabla ya wewe kuununua!??

Ipo mitumba toka kwa wezi, majambazi, makahaba, watu wa dini tofauti na sisi, wabaguzi, wauwaji, wafungwa, wabakaji, matapeli na lundo jingine kubwa sana la watu tusiowapenda.

Unapotumia mtumba jua kuwa inawezekana kabisa kabla ya kuletwa Tanzania huko ulikotoka ulikuwa unatumiwa na mtu/watu usiowapenda kabisa.
Nikipata nafasi ya kuwaamulia, mitumba ya mavazi ya ndani lazima ipotee sokoni haraka kadiri itakavyowezekana.........Ni dharau iliyoje?
 
Mtoa mada sijui akili zako zipoje,umekuja kutangaza ushoga ama? Kwani ukienda mgahawani huwezi kula chakula kilichopikwa na Shoga? Hiyo suti mpya unayovaa je haijashonwa na Shoga? Chumba ulichopanga hajawahi kupanga kahaba kabla yako? au mwizi? au yeyote yule usiyempenda? Usihukumu usije ukahukumiwa.
 
Hiyo mitumba unajua kuwa huwa inatolewa bure Ila MTU mweusi akiikusanya analeta anauza
Sikubaliani na kauli hii 👆 👆 👆 . Ukweli ni kwamba mitumba:
1. Mitumba esp. nguo, hutolewa na watu waliokuwa wanazimiliki nguo hizo kwa sababu mbalimbali e.g. Haziwatoshei tena(zimekuwa ndogo), zimepitwa na wakati i.e sio fashion tena, mtu ana nguo nyingi na hazitumii, nguo zimepata dosari e.g. madoa yasiyo toka n.k. Nguo hizo huwekwa kwenye mapipa kama ili zikatupwe (sio takataka) na wapo wanaolipwa kwa kazi ya kuzichambua.Kuzifua, kuzitakatisha kwa kuweka Formalinhalafu kuziweka katika mabelo. Hapo kuna gharama kufanikisha mchakato wote huo. Inakuwa tayari ni biashara.Watu wanaozihitaji ni watu wa aina zote -weupe kwa weusi. Kwa mafano huko Denmark yapo maduka ya mitumba almaarufu kama Genbrok na utawakuta Wazungu na Wengineo wakifukua-fukua kuchagua mitumba hiyo.
Wale wafanyabiashara wakubwa ndo huweza kufanya miamala na wafanya biashara waTz.
Zamani mitumba hiyo ilikuwa iunanunuliwa na makanisa kwa fedha ya sadaka na kuletwa huku kwetu na kugawiwa kwa wahitaji bure lakini kwa kigezo cha uwe ni muumini wao au kama limetokea janga.
2. Mitumba ipo hata magari, Tv, vyombo vya music n.k.
 
Gharama sio kubwa Sana ukilonganisha na bei wanayotumia kuuza hiyo mitumba
Ni kweli ila kwa wabongo tunaangalia pia na uimara wa kudumu tofauti na hizi za madukani unanunua leo kesho imechanika au kufumuka i.e. hazidumu kama za mitumba.
 
Sikubaliani na kauli hii 👆 👆 👆 . Ukweli ni kwamba mitumba:
1. Mitumba esp. nguo, hutolewa na watu waliokuwa wanazimiliki nguo hizo kwa sababu mbalimbali e.g. Haziwatoshei tena(zimekuwa ndogo), zimepitwa na wakati i.e sio fashion tena, mtu ana nguo nyingi na hazitumii, nguo zimepata dosari e.g. madoa yasiyo toka n.k. Nguo hizo huwekwa kwenye mapipa kama ili zikatupwe (sio takataka) na wapo wanaolipwa kwa kazi ya kuzichambua.Kuzifua, kuzitakatisha kwa kuweka Formalinhalafu kuziweka katika mabelo. Hapo kuna gharama kufanikisha mchakato wote huo. Inakuwa tayari ni biashara.Watu wanaozihitaji ni watu wa aina zote -weupe kwa weusi. Kwa mafano huko Denmark yapo maduka ya mitumba almaarufu kama Genbrok na utawakuta Wazungu na Wengineo wakifukua-fukua kuchagua mitumba hiyo.
Wale wafanyabiashara wakubwa ndo huweza kufanya miamala na wafanya biashara waTz.
Zamani mitumba hiyo ilikuwa iunanunuliwa na makanisa kwa fedha ya sadaka na kuletwa huku kwetu na kugawiwa kwa wahitaji bure lakini kwa kigezo cha uwe ni muumini wao au kama limetokea janga.
2. Mitumba ipo hata magari, Tv, vyombo vya music n.k.



Mitumba upande wa nguo zinazoletwa Africa kwanza mitumba imechoka , imechakaa michafu

Ndo tunaleta ili tuvae ni umasikini tu.

Kukuta nguo ya mtumba ya maana ni Nada Sana.

Tukubali kuwa sisi ni dark country
 
Back
Top Bottom