Witch hunter
JF-Expert Member
- Nov 21, 2018
- 1,437
- 3,320
Ndugu zangu niliona uzi humu ukikataza kuwa na urafiki na askari polisi, ila mimi nakazia zaidi hata hawa mgambo ni wa hovyoo tu.
Kuna mgambo alikuja kwangu kunipa taarifa kwamba nahitajika kituo cha polisi akanipa na sababu ya wito, basi sikuwa na hiyana nikamwambia twende. Kwa kuwa nafahamika hapa mtaani hakuona haja ya kunifunga pingu kama wahalifu wengine hivyo tulitembea mdogo mdogo kuelekea kituoni huku tukipiga story mbili tatu maana ni mtu tunayejuana.
Cha ajabu tulipokaribia kufika kituoni, na baada ya kuona askari pale kituoni, mgambo yule alinigeukia na kuniuliza kwa ukali “unataka kugoma? Unataka kugoma? Hata wale askari walimsikia. Kabla sijamjibu akashika suruali yangu kwa nyuma akaniinua nikaanza kutembelea vidole, kisha akaanza kunipiga huku tukielekea kuingia kabisa kituoni tena mbele ya askari.
Sikutaka kufanya fujo maana askari wa Bongo nawajua, ila nimemtunza tu huyu mgambo. Ipo siku mtamsikia kwenye vyombo vya khabari. I SWEAR ON MY LIFE.
Kuna mgambo alikuja kwangu kunipa taarifa kwamba nahitajika kituo cha polisi akanipa na sababu ya wito, basi sikuwa na hiyana nikamwambia twende. Kwa kuwa nafahamika hapa mtaani hakuona haja ya kunifunga pingu kama wahalifu wengine hivyo tulitembea mdogo mdogo kuelekea kituoni huku tukipiga story mbili tatu maana ni mtu tunayejuana.
Cha ajabu tulipokaribia kufika kituoni, na baada ya kuona askari pale kituoni, mgambo yule alinigeukia na kuniuliza kwa ukali “unataka kugoma? Unataka kugoma? Hata wale askari walimsikia. Kabla sijamjibu akashika suruali yangu kwa nyuma akaniinua nikaanza kutembelea vidole, kisha akaanza kunipiga huku tukielekea kuingia kabisa kituoni tena mbele ya askari.
Sikutaka kufanya fujo maana askari wa Bongo nawajua, ila nimemtunza tu huyu mgambo. Ipo siku mtamsikia kwenye vyombo vya khabari. I SWEAR ON MY LIFE.