kidonto
JF-Expert Member
- Jan 5, 2014
- 1,946
- 2,839
Mzazi alikutamkia Maneno ambayo ukiwa mtoto ulichukulia kawaida...! Bila elimu ya kiroho bila kujua namna ya kuzuia Uhai wa hayo maneno mabaya kama unavyofundisha hapa...!4B; MANENO KAMA SILAHA YA KIROHO KATIKA UPANDE WA UFALME WA NURU. Kama tulivyoona silaha hii katika ufalme wa giza, hivyohivyo na katika ufalme huu wa nuru silaha hii inakuwa na nguvu zaidi ikiambatana na silaha ya Kiti. Maneno mtu anayozungumza yanakuwa na uhusiano mkubwa sana na kiti alichokalia, pia unapaswa kujua kila mtu ana kiti cha maisha yake (unatawala maisha yako), hivyo unapaswa kuwa makini na maneno unayojitamkia na unayotamkia wengine. Namna ya kupata ushindi na silaha hii; Kwanza unapaswa kujinenea/ kujitamkia maneno mzuri na kusikiliza kwa umakini maneno unayotamkiwa na watu wengine, kama wanakutamkia maneno mazuri unapaswa kuyatia uhai (maneno ni roho) kuulinda uhai huo hadi maneno hayo yatimie kwako kwa kuyapiga muhuri kwenye kiti cha ufalme wa nuru. Kama umetamkiwa maneno mabaya ya kukukwamisha unapaswa kuyatoa uhai kwa haraka kabla maneno hayo hayajaleta matokeo kwako, unayatoa uhai kwa kuyakataa na kuyafuta kabla hayajafika kwenye kiti cha ufalme wa nuru. Jifunze muundo huu ukusaidie; katika ulimwengu wa kiroho kuna kiti cha Mwenyenzi Mungu (Mungu Mkuu) na chini yake kuna kiti cha wazazi wako, chini yake kuna kiti cha maisha yako na mwisho ndipo vinafuata viti vyote (nafasi zote za mamlaka/ uongozi). Kwakupitia muundo huu unaweza kukalia viti vyote ila kamwe hutaweza kukalia au kuwa juu ya kiti cha wazazi wako!. Na hapa ndipo tunapata neno "laana ya wazazi". Laana ya wazazi inatokana na matumizi mabaya ya maneno anayoyatoa mzazi dhidi yako akiwa amekalia hiki kiti chake mbele ya kiti kikuu cha Mwenyenzi Mungu. Maneno hayo ya mzazi yanakuwa na nguvu sana kuliko maneno yanayotolewa na mtu mwingine yeyote au na kiti chochote. Hivyo chunga sana maneno unayotamkiwa na wazazi wako au unayomtamkia mtoto wako. Baraka ya wazazi ni matumizi mazuri ya kiti anachotumia mzazi / wazazi kukunenea maneno mazuri mbele ya kiti cha Mwenyenzi Mungu na akaweza kuulinda uhai wa maneno hayo. Kwakusikiliza maneno ya mtu kunakusaidia kujua malengo yake, makusudi yake, kiti alichokalia, roho iliyopo ndani yake na kusudi la yeye kuishi. Hivyo silaha hii ni muhimu sana kuijua vizuri. Mwisho kwa leo, unapaswa kujua kuwa kila kitu katika dunia hii kama wanyama, ndege, mawe, miti, upepo nk vyote vina maneno (sauti) na vinauwezo wa kukunenea maneno mazuri au mabaya ni wewe tu kutumia hekima yako kutafsiri na kujua chakufanya na chakutokufanya ili vikunenee maneno mazuri mbele ya kiti. Nb; sauti ni tafsiri ya maneno. Na usiogope sana maneno ya mtu bali ugopa zaidi kiti anachokalia anapotamka maneno hayo, maana maneno ya mtu ni tofauti na maneno ya kiti lakini yote yanapitia kwenye kinywa cha aliyekalia hicho kiti.
Sasa nimekuwa nimekutana na Uzi wako nimerudi nyuma utotoni kukumbuka maneno ambayo Mzazi aliwahi kutamka....!
Naweza kuyafuta....!?
Nayafutaje...!?
Naweza kuyabadirisha yakaleta Maana..!?
Nayabadirishaje....!?