Walker Water
JF-Expert Member
- Aug 23, 2022
- 799
- 3,001
Nianze na salamu za mwaka huu wa 2024 kwa wanajukwaa wote,nilibanwa kidogo na shughuli nyingi mwaka huu ila sasa nimerudi tena jukwaani.
Tunaanza; Tambua kuwa nafsi ndiyo sehemu ya mtu iliyobeba hatma yake yote awapo hapa duniani. Kazi ya roho ni kutia nguvu tu vilivyopo kwenye nafsi ili mtu aweze kuishi katika kiwango chake cha maisha.
Sasa, ili uweze kufanikiwa katika haya maisha na watu wote ambao tayari wameshafanikiwa, ni lazima uwe na uwezo mkubwa wa ku control (kuendesha) nafsi za wengine ili zikutumikie kwa vipawa vilivyopo ndani yake ndipo ufanikiwe.
Namaanisha kuwa unaweza kuishi hapa duniani na ukawa unatumikia watu wengine maisha yako yote kwa nafsi yako kukamatwa na kuendeshwa na watu hao.
Hapa tunazungumzia masuala ya kiroho. Katika ulimwengu wa kiroho upande wa nuru na upande wa giza,wote huvuta watu,kuwafunga na kuwaendesha kwa namna watakavyo wao ili wao waweze kufikia hatma zao.
Tuangalie mifano kidogo, wafanyabiashara; ili bidhaa zao ziuzike lazima wavute na ku control nafsi za watu, usije ukaona unapendelea kununua bidhaa zako sehemu fulani ukafikiri ni kawaida tu!,nafsi imekamatwa hapo. Watu wengine ni wanasiasa, kwenye mipira,kwenye uongozi, kwenye kuvuta wateja kwenye taasisi na mashirika mbalimbali hususani sekta binafsi na wahubiri wakubwa.
Wote hawa wakikosa nguvu za kuvuta na ku control nafsi za watu ili ziwatumikie,kamwe hawataweza kufanikiwa!. Sasa kazi itaanzia hapa kwa kujifunza vitu wanavyotumia kuvuta na ku control nafsi za watu katika pande zote za nuru na za giza. Vitu vinavyotumika ni;
1. Kiapo (maneno yenye ahadi kamili).
2. Sadaka (fedha au chochote kwa lengo maalumu).
3. Maneno/Maombi (yenye roho ndani yake).
4. Kiwakilishi chako chochote (mfano nguo au picha).
Nitakuwa nachambua kimoja kimoja kadri muda utakavyokuwa unapatikana na ninaimani watu wengi sana watajikomboa kutoka kutumikishwa na watu wengine na watajua mengi sana na siri nyingi sana na kuwa huru kuendesha maisha yao.
NB; Hakuna nafsi yoyote ya mwanadamu isiyokuwa na thamani,kama unataka kuamini we nenda kwa Mungu au kwa shetani ukiwa hali yoyote uone kama atakukataa!,na ukifuata masharti yao kikamilifu utakuwa milionea pasipo kujali ulikuwa katika hali gani ya nafsi yako.
Tunaanza; Tambua kuwa nafsi ndiyo sehemu ya mtu iliyobeba hatma yake yote awapo hapa duniani. Kazi ya roho ni kutia nguvu tu vilivyopo kwenye nafsi ili mtu aweze kuishi katika kiwango chake cha maisha.
Sasa, ili uweze kufanikiwa katika haya maisha na watu wote ambao tayari wameshafanikiwa, ni lazima uwe na uwezo mkubwa wa ku control (kuendesha) nafsi za wengine ili zikutumikie kwa vipawa vilivyopo ndani yake ndipo ufanikiwe.
Namaanisha kuwa unaweza kuishi hapa duniani na ukawa unatumikia watu wengine maisha yako yote kwa nafsi yako kukamatwa na kuendeshwa na watu hao.
Hapa tunazungumzia masuala ya kiroho. Katika ulimwengu wa kiroho upande wa nuru na upande wa giza,wote huvuta watu,kuwafunga na kuwaendesha kwa namna watakavyo wao ili wao waweze kufikia hatma zao.
Tuangalie mifano kidogo, wafanyabiashara; ili bidhaa zao ziuzike lazima wavute na ku control nafsi za watu, usije ukaona unapendelea kununua bidhaa zako sehemu fulani ukafikiri ni kawaida tu!,nafsi imekamatwa hapo. Watu wengine ni wanasiasa, kwenye mipira,kwenye uongozi, kwenye kuvuta wateja kwenye taasisi na mashirika mbalimbali hususani sekta binafsi na wahubiri wakubwa.
Wote hawa wakikosa nguvu za kuvuta na ku control nafsi za watu ili ziwatumikie,kamwe hawataweza kufanikiwa!. Sasa kazi itaanzia hapa kwa kujifunza vitu wanavyotumia kuvuta na ku control nafsi za watu katika pande zote za nuru na za giza. Vitu vinavyotumika ni;
1. Kiapo (maneno yenye ahadi kamili).
2. Sadaka (fedha au chochote kwa lengo maalumu).
3. Maneno/Maombi (yenye roho ndani yake).
4. Kiwakilishi chako chochote (mfano nguo au picha).
Nitakuwa nachambua kimoja kimoja kadri muda utakavyokuwa unapatikana na ninaimani watu wengi sana watajikomboa kutoka kutumikishwa na watu wengine na watajua mengi sana na siri nyingi sana na kuwa huru kuendesha maisha yao.
NB; Hakuna nafsi yoyote ya mwanadamu isiyokuwa na thamani,kama unataka kuamini we nenda kwa Mungu au kwa shetani ukiwa hali yoyote uone kama atakukataa!,na ukifuata masharti yao kikamilifu utakuwa milionea pasipo kujali ulikuwa katika hali gani ya nafsi yako.