Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,504
- 30,202
Naangalia matangazo mubashara ya mazishi ya shujaa wa kupambana na utawala wa ubaguzi wa rangiu, mtu aliyetumia Maisha yake yote kupigania haki za wananchi wake, Askofu Desmond Tutu, unaoonyeshwa kwenye vituo mbalimbali vya kimataifa vya TV, kama vile SABC, CNN, BBC, Sky News na Al Jazeera.
Kitu kimoja nimekiona kwenye matangazo hayo ya moja kwa moja, ni hilo jeneza ambalo anazikwa nalo Askofu Tutu, ambalo ni la kawaida Sana na kwa maelezo ya watangazaji hao wa TV, ni kuwa huo ndiyo ulikuwa wosia wake yeye mwenyewe Desmond Tutu, kuwa atakapokufa azikwe kwenye jeneza lisilo na gharama kubwa.
Kwa hiyo waandaaji wa mazishi yake imebidi wafuate wosia wake, wa kuzikwa kwenye jeneza la "plywood" kwa kuwa kwa umaarufu wa Askofu Desmond Tutu, angeweza kuzikwa na jeneza la gharama kubwa Sana, kama walivyo "celebrities" walio wengi.
Mazishi haya ya Askofu Desmond Tutu, yachukuliwe kama somo kwa watu wengine kuwa ufahari kwenye mazishi haina maana hata kidogo kwa kuwa akishakufa mtu, hata ukizikwa na jeneza la mamilioni ya shilingi, bado uhai wako hauwezi kurudi
Kitu kimoja nimekiona kwenye matangazo hayo ya moja kwa moja, ni hilo jeneza ambalo anazikwa nalo Askofu Tutu, ambalo ni la kawaida Sana na kwa maelezo ya watangazaji hao wa TV, ni kuwa huo ndiyo ulikuwa wosia wake yeye mwenyewe Desmond Tutu, kuwa atakapokufa azikwe kwenye jeneza lisilo na gharama kubwa.
Kwa hiyo waandaaji wa mazishi yake imebidi wafuate wosia wake, wa kuzikwa kwenye jeneza la "plywood" kwa kuwa kwa umaarufu wa Askofu Desmond Tutu, angeweza kuzikwa na jeneza la gharama kubwa Sana, kama walivyo "celebrities" walio wengi.
Mazishi haya ya Askofu Desmond Tutu, yachukuliwe kama somo kwa watu wengine kuwa ufahari kwenye mazishi haina maana hata kidogo kwa kuwa akishakufa mtu, hata ukizikwa na jeneza la mamilioni ya shilingi, bado uhai wako hauwezi kurudi