Je, Wajua Bunge linaweza kutoa azimio batili? CAG yuko kikatiba. Je, Bunge lina uwezo kutopokea ripoti ya CAG?

Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali na alama za kuuliza nimeziweka, maana watu tusije itwa mahali kuhojiwa kuwa tumelidhalilisha Bunge.

Swali lenyewe ni hili,
Jee Wajua Bunge Linaweza Kutoa Azimio Batili?. CAG yuko Kikatiba, Jee Bunge Lina Uwezo Kutopokea Ripoti ya CAG?.

Tuliisha zungumza sana kuhusu kuhusu kitu kinachoitwa "The Principle of Separation of Powers, Checks and Balances" tukasema kanuni hii hutumika na mihimili hii mitatu ya dola kwa lengo kila mhimili kuwa a watchdogs wa mihimili mingine isijiinue kupita mamlaka yake.

Jee Azimio hili la Bunge kuamua halitafanya kazi na CAG ni Azimio Batili?, kwa sababu Ofisi ya CAG ipo kwa mujibu wa katiba, na Ripoti ya CAG inawasilishwa Bungeni kwa mujibu wa katiba, Jee Bunge lina uwezo huo wa kuamua kutofanya kazi na CAG, wakati Bunge sio Mamlaka ya nidhamu ya CAG, kama CAG amelikosea Bunge, then Bunge ama limshitaki CAG mahakamani au limshitaki CAG kwa mamlaka yake ya nidhamu, hiyo mamlaka ndio iamue kumchukulia CAG hatua za kinidhamu tena kwa mujibu wa Katiba lakini sio kwa Bunge kutoa Azimio Batili la altimatum kuilazimisha serikali kumuondoa CAG.

Bunge ni tukufu haliwezi kukosea, lakini linaongozwa na watu hivyo watu hawa wanaweza kukosea na ndio maana wakikosea, wanaweza kuondolewa.

Serikali inaongozwa na rais na pale Ikulu ni mahali patakatifu hivyo rais wetu anapaswa kuwa Mtakatifu ambaye hawezi kukosea na ndio maana rais hawezi kushitakiwa, ana kinga ya kutokushitakiwa kutokana na utakatifu huu, lakini rais pia ni binaadamu anaweza kufanya makosa ya kibinaadamu na anaweza asiwe Mtakatifu, ndio maana akikosea anaweza kushitakiwa na Bunge na akikutwa na hatia anaondolewa.

Ofisi ya CAG ni vivyo hivyo, ipo pale kwa mujibu wa katiba na CAG yupo kikatiba, Bunge haliwezi kujiamulia kuwa halifanyi kazi na CAG, bali kwa vile ofisi ya CAG nayo inaongozwa na mtu anayeitwa CAG, mtu huyu anaweza kukosea, akikosea anashitakiwa na akithibitishwa amekosea, anaondolewa.

Rais anapokea ripoti ya CAG kwa mujibu wa katiba, na baada ya rais kupokea ripoti hiyo bado inakuwa ni closed document.

CAG anatakiwa kuiwasilisha ripoti hiyo Bungeni within 7 days za mwanzo za kikao cha Bunge, baada ya rais kupokea ripoti hiyo.

Ripoti hiyo ikiisha wasilishwa tuu Bungeni, from that moment, Ripoti hiyo ni Public document, CAG anakuwa amemaliza kazi yake .

Sasa Bunge lijadili au lisijadili, it's up to Bunge na hapa ndipo kwenye udhaifu wenyewe wa Bunge letu.

Bunge halina mamlaka kukataa ripoti ya CAG bali lina uhuru lisiijadili.

Hivyo kama CAG, ana makosa dawa sio kwa Bunge kuamua kutofanya kazi na CAG, kwa kutoa Azimio batili, bali kumshitaki, GAG aondolewe, maisha yaendelee.

Naomba msaada kwa wabobezi wa sheria, taratibu na kanuni, watufafanulie jee Bunge letu tukufu, lina uwezo huo?.

Paskali
Kwanza rekebisha.
Bunge si takatifu.
Ikulu si patakatifu.

Mungu alipatamka mahali hapa ni patakatifu shehemu moja tu dunia enzi za nabii Mussa.
Hayo maeneo mengine tunajitengenezea utakatifu sisi wenyewe kitu ambacho siyo sahihi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bunge haliwezi kukataa kupokea ripoti ya CAG ila hawatataka ushirikiano nae.

Mara nyingi pale taarifa ya CAG inapopelekwa bungeni, baada ya kusomwa na kujadiliwa na wabunge, hua wataalam wa CAG wanaitwa mara kwa mara kwenda kuwafafanulia wabunge baadhi ya vitu wasivyo vielewa na mambo kama hayo. Hivyo kwa sasa ripoti ikisomwa bunge litatafta watu wengine wa kuja kuwasaidia kufana nao kazi na sio CAG.

Pure hilarity.
Maamuzi hayo ni ya utoto wa kiutuuzima.Hivi wasomi wetu wamekumbwa na jinamizi gani? Mbona hawatendi kadiri ya viwango Vya elimu waliyo nayo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Hasira za mkizi furaha kwa mvuvi" Mimi niwaombe tu mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi na watendaji wengine huu ndo mda wenu wa kupiga hela, bunge limewapa shavu pigeni madili ya maana kwa sababu mtakaguliwa ila hamtajadiliwa popote huu ndo wakati wenu msipoteze nafasi aadhim hii.
 
Kumbuka bunge linaweza kuweka azimio la kutokuwa na imani na rais na kupiga kura kumkataa, wakati huohuo rais ana mamlaka ya kulivunja bunge na uchaguzi ukarudiwa.hivyo kila mmoja ana mamlaka kikatiba juu ya mwenzake inategemea nani kamuwahi mwenzake.
Hili swala la ASSAD liko zaidi ya tunavyofikiri, alitafutwa ili aondolewe toka wakati alipokiuka agizo la rais na kusafiri kwenda nairobi kenya bila kibali, pia huko nssf alikuwa na conflict of interest na pia kutoa siri za wizi wa 1.5t hakungemuacha salama.
Muda mwingine ni bora wasomi kuwaachia Nchi hao wanaodhani ni werevu zaidi ya wengine na kwenda kufanya kazi nje ya nchi,ili kuondokana na haya mambo ya kulazimishana ufanye kile usicho kiamini.
 
Adhabu hii kwa Mdhibiti na Mkaguzi wa mahesabu ya serikali imeangukia upande wa wananchi (umma), kwa adhabu hii bunge imeadhibu umma na kutoa mwanya kwa wabadhirifu walio kwenye ripoti 2017/2018 kuula. Ninaamini kwamba ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali haiwezi kukosa kasoro. Kwa kukataa kufanya kazi na Mkaguzi tunawapa ushindi mafisadi. Ukweli ni kwamba, ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali inafanya kazi ya wananchi kwa manufaa ya taifa, kitendo cha kususia kufanya naye kazi ni kususia wananchi, Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) ndiye jicho pekee la umma, ndio mlinzi wa mfuko wa fedha za umma, amewekwa kikatiba kwa misingi ya kuongeza uwajibikaji katika matumizi fedha za umma. Kwa nini bunge litoe adhabu kwa umma kwa kukataa kufanya kazi na mtu muhimu kiasi hiki?!

Ni muhimu Bunge likazingatia haki ya umma kuhusu ukaguzi wa hesabu za serikali na mashirika yake. Hakuna kosa kubwa kama bajeti ya matrilioni ya shillingi kupita bila kukaguliwa na ripoti kuwekwa wazi kwa mujibu wa katiba, Bunge lipo kutokana na katiba na Mkaguzi mkuu wa hesabu za umma yupo kikatiba, tofauti ya bunge na mkaguzi zisilete gharama hii kubwa kwa nchi kiuchumi, kidemokrasia, uwajibikaji na utawala bora.Kama Bunge litashikilia msimamo wake litakuwa limeondoa hadhi na heshima ya ripoti zinazotoka katika ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali kwa siku za usoni.
 
Bunge halijakataa kufanya Kazi na CAG limekataa kufanya kazi na prof Asad aliyelidharau bunge.
cha mhimu labda tuanze mchakato wa kumpata CAG mwingine
 
Kwanza rekebisha.
Bunge si takatifu.
Ikulu si patakatifu.

Mungu alipatamka mahali hapa ni patakatifu shehemu moja tu dunia enzi za nabii Mussa.
Hayo maeneo mengine tunajitengenezea utakatifu sisi wenyewe kitu ambacho siyo sahihi

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijasema Bunge takatifu nimesema Bunge Tukufu, kwa sababu linafanya kazi iliyotukuka.
Ikulu ni kweli ni mahali patakatifu hivyo mpangaji wetu wa mahali pale lazima awe mtakatifu.
Aliyepaita Ikulu ni mahali patakatifu sio mimi, ni Baba mwenyewe wa Taifa Mwalimu Nyerere.
P
 
Nakumbuka kipindi cha JK kulikuwa na operation TOKOMEZA ambayo ililenga kuwaondoa majangili. Baada ya malalamiko zoezi lile lilisitishwa na mawaziri watatu akina Nahodha, Kagasheki na Nchimbi wakajiuzulu. Wakati wa kuhitimisha Kagasheki pamoja na kuomba radhi kwa mapungufu yaliyojitokeza, aliliambia Bunge kuwa MSHINDI KWENYE AZIMIO LILE LA BUNGE NI MAJANGILI na kweli hali iliendelea kuwa mbaya mpaka JPM alipoingia madarakani na kufanya reforms nyingine.
Nikilinganisha na kinachotokea kwa CAG na Azimio hili nauona UMMA WA TANZANIA ulivyogalagazwa chali.
 
Jukumu la Bunge kushirikiana na CAG sio jambo la iari. Nais kuna seem haipo sawa.
Dalili znaonesha ktk kikao Mzee hakuungama badala yake alipiga lecture matata wajumbe wote walijuta kumuita. Sasa busara imekosekana ndo matamko ya ajabu yanaibuka km kumkomoa Simba (Assad).
Cha msingi Bunge lisipitishe ilo azimio na maisha yasonge mbele.
 
Jukumu la Bunge kushirikiana na CAG sio jambo la iari. Nais kuna seem haipo sawa.
Dalili znaonesha ktk kikao Mzee hakuungama badala yake alipiga lecture matata wajumbe wote walijuta kumuita. Sasa busara imekosekana ndo matamko ya ajabu yanaibuka km kumkomoa Simba (Assad).
Cha msingi Bunge lisipitishe ilo azimio na maisha yasonge mbele.
Ndio maana ameomba hansadi iwekwe wazi ila hawa wanafiki hawawezi. Wao ndio walalamikaji, wao ndio wachunguzi na wao ndio watoa maamuzi kama sio maigizo ni nini??
 
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali na alama za kuuliza nimeziweka, maana watu tusije itwa mahali kuhojiwa kuwa tumelidhalilisha Bunge.

Swali lenyewe ni hili,
Jee Wajua Bunge Linaweza Kutoa Azimio Batili?. CAG yuko Kikatiba, Jee Bunge Lina Uwezo Kutofanyakazi na CAG?. au kutopokea Ripoti ya CAG?.

Hawa wabunge waliopitisha azimio hilo, wanakijua kitu kinachoitwa CAG "The Constitutional mandates of the Controller and Auditor-General"?. Yaani mandate ya CAG iwekwe kwenye katiba yetu halafu wahe watu walioapa kulinda katiba, wazuie jambo lililoelekezwa kikatiba?.
Constitutional Mandates
The Constitutional mandates of the Controller and Auditor-General shall be to- (a) authorize the use of money to be paid out of the Consolidated Fund upon being satisfied that Article 136 of the Constitution has been or shall be complied with; (b) ensure the money authorized to be charged on the Consolidated Fund or the money the use of which is authorized by law, have been spent for purposes connected and incurred in accordance with authorization; and (c) audit and report on the accounts, financial statements and financial management of –
(i) the Government of the United Republic, that is to say, Ministries, Independent Departments, Executive Agencies, Public Authorities and Other Bodies and Donor Funded Projects;
(ii) the local government authorities;
(iii) the Judiciary; and
(iv) the National Assembly.

Huu ulevi wa madaraka utatufikisha wapi?, walidhani nafasi ya CAG ni kama House Boy, House Girl or Shamba Boy, akija bosi mwingine hakupendi, unaambiwa fungasha ondoka.

Jee Waheshimiwa wabunge wetu walipokuwa wanapitisha azimio hilo, hivi wanazijua Powers of Controller and Auditor-General?. Ni kweli Serikali, Bunge na Mahakama, zote zina powers zake na independencis zake, but when it comes to public funds na ukaguzi, all the powera lies with CAG, kusema hufanyi kazi na CAG ni kumzuia CAG asitimize wahibu wake, Bunge linao uwezo huo?.

(1)In the performance of his functions and responsibilities, the Controller and Auditor-General may
(a) call upon any public officer for any explanation and information which the Controller and Auditor-General may require in order to enable him to perform those functions and responsibilities;
(b) summon and examine under oath any person as he may determine in connection with the receipt or expenditure of public monies or the receipt or issue of any public property affected by the provisions of this Act and in connection with any matter necessary for the proper performance of his functions;
(c) authorize any person eligible to be appointed as an auditor as the requirements of the Accountants and Auditors (Registration) Act, to conduct an inquiry, examination or audit on his behalf and that person or officer shall report to him;
(d) without payment of any fee, cause search to be made in and extracts to be taken from any book, document or record in any public office;
(e) seek the professional opinion or advice of the Attorney-General or any other qualified person on matters of a legal nature or of any qualified person on any accounting, auditing or other matter;
(f) accept as correct without further examination, or rely upon a certificate of any other person as hi thinks fit, on the accounts of any other person entrusted with the collection, receipt, custody, control or payment of public monies or public property or with the issue, sale, transfer or delivery of public property;
(g)from time to time acquire the services of any person as provided for under section 16 of this Act.

Hivi wabunge walipopitisha azimio hilo, jee walizingatia Ibara ya 143 ya Katiba inasema nini kuhusu The independence and status of the Office of the Controller and Auditor-General shall be as provided for under Article 143 of the Constitution?.
Tukisema azimio hili ni batili tutakuwa tumelionea Bunge?. Au Ubatili nao ni udhalilishaji?.

Tuliisha zungumza sana kuhusu kuhusu kitu kinachoitwa "The Principle of Separation of Powers, Checks and Balances" tukasema kanuni hii hutumika na mihimili hii mitatu ya dola kwa lengo kila mhimili kuwa a watchdogs wa mihimili mingine isijiinue kupita mamlaka yake.

Jee Azimio hili la Bunge kuamua halitafanya kazi na CAG ni Azimio Batili?, kwa sababu Ofisi ya CAG ipo kwa mujibu wa katiba, na Ripoti ya CAG inawasilishwa Bungeni kwa mujibu wa katiba, Jee Bunge lina uwezo huo wa kuamua kutofanya kazi na CAG, wakati Bunge sio Mamlaka ya nidhamu ya CAG, kama CAG amelikosea Bunge, then Bunge ama limshitaki CAG mahakamani au limshitaki CAG kwa mamlaka yake ya nidhamu, hiyo mamlaka ndio iamue kumchukulia CAG hatua za kinidhamu tena kwa mujibu wa Katiba lakini sio kwa Bunge kutoa Azimio Batili la altimatum kuilazimisha serikali kumuondoa CAG.

Bunge ni tukufu haliwezi kukosea, lakini linaongozwa na watu hivyo watu hawa wanaweza kukosea na ndio maana wakikosea, wanaweza kuondolewa.

Serikali inaongozwa na rais na pale Ikulu ni mahali patakatifu hivyo rais wetu anapaswa kuwa Mtakatifu ambaye hawezi kukosea na ndio maana rais hawezi kushitakiwa, ana kinga ya kutokushitakiwa kutokana na utakatifu huu, lakini rais pia ni binaadamu anaweza kufanya makosa ya kibinaadamu na anaweza asiwe Mtakatifu, ndio maana akikosea anaweza kushitakiwa na Bunge na akikutwa na hatia anaondolewa.

Ofisi ya CAG ni vivyo hivyo, ipo pale kwa mujibu wa katiba na CAG yupo kikatiba, Bunge haliwezi kujiamulia kuwa halifanyi kazi na CAG, bali kwa vile ofisi ya CAG nayo inaongozwa na mtu anayeitwa CAG, mtu huyu anaweza kukosea, akikosea anashitakiwa na akithibitishwa amekosea, anaondolewa.

Rais anapokea ripoti ya CAG kwa mujibu wa katiba, na baada ya rais kupokea ripoti hiyo bado inakuwa ni closed document.

CAG anatakiwa kuiwasilisha ripoti hiyo Bungeni within 7 days za mwanzo za kikao cha Bunge, baada ya rais kupokea ripoti hiyo.

Ripoti hiyo ikiisha wasilishwa tuu Bungeni, from that moment, Ripoti hiyo ni Public document, CAG anakuwa amemaliza kazi yake .

Sasa Bunge lijadili au lisijadili, it's up to Bunge na hapa ndipo kwenye udhaifu wenyewe wa Bunge letu.

Bunge halina mamlaka kukataa ripoti ya CAG bali lina uhuru lisiijadili.

Hivyo kama CAG, ana makosa dawa sio kwa Bunge kuamua kutofanya kazi na CAG, kwa kutoa Azimio batili, bali kumshitaki, GAG aondolewe, maisha yaendelee.

Naomba msaada kwa wabobezi wa sheria, taratibu na kanuni, watufafanulie jee Bunge letu tukufu, lina uwezo huo?.

Paskali
Asante sana mzalendo paskal mm wasiwasi wangu bunge kuitwa tukufu ni kufuru ndio maana Leo hawafanyi mambo matakatifu,.
Tukiyaacha haya yaendelee IPO siku bunge litaazimia kutokufanya kazi na rais !

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom