Je, ni sahihi kwa mwanaume kuhubiri ama kusali akiwa amefunika kichwa chake?

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,716
29,947
Ndugu zangu. Hata sasa tumeshuhudia anguko la mwanadamu katika nyakati hizi za Neema ya Mungu ya Wokovu kupitia damu ya Thamani ya Yesu Kristo...

Manabii wa uongo walikuwepo tangu nyakati za Torati
Yeremia 14
4. Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake.
14. Ndipo BWANA akaniambia, Hao manabii wanatabiri uongo kwa jina langu mimi; mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao; wanawapeni unabii wa maono ya uongo, na uaguzi, na neno la ubatili, na hadaa ya mioyo yao.
15. Basi, kwa hiyo BWANA asema hivi, Kwa habari za manabii wanaotabiri kwa jina langu, wala mimi sikuwatuma, lakini husema, Upanga na njaa havitaingia katika nchi hii; Kwa upanga na njaa manabii hao wataangamizwa
.

Swali ninaweka hapa, je yampasa mwanaume anaposimama kuhubiri ama kusali hali amefunika kichwa chake? Mtume Paulo ametuasa katika
1 Wakorintho 11
4. Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake.

papal-history.jpeg


bishop.jpeg
.
pastor.jpeg
pastor2.jpeg


Hapo awali makuhani wa Wayahudi walikuwa wanafunika vichwa vyao, lakini tangu Bwana Yesu aliposema IMEKWISHA na pazia la Hekalu kupasuka katikati (linalotenganisha Patakatifu pa Patakatifu), ameleta kwetu Agano Jipya ambalo ndiyo kanuni za kuishi kwa Imani na Kumtumainia Mungu. Hivyo Maandiko ya Agano Jipya yamebeba hatima ya Imani yetu kwa Mungu na si vinginevyo.

Tunashuhudia makaasisi wa makanisa mengi wakisimama madhabahuni wakideliver Neno na kuongoza Ibada wakiwa wamefunika vichwa vyao. Je hayo ni makufuru dhidi ya Mungu au ni taratibu halali?

Tuelimishane bila kudhalilisha imani na dini za watu.
 
Nukuu ya maandiko kutoka katika Agano Jipya pia hutufundisha kama vile ifuatavyo,

1 WAKORINTHO 11

2 Ninawasifu kwa sababu mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kuwa mnashika mafundisho niliyowakabidhi.

3 Lakini napenda muelewe kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, kama vile mume alivyo kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.

4 Kwa hiyo mwanamume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anaaib isha kichwa chake.

5 Na mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anaaibisha kichwa chake, ni sawa kama amenyoa nywele zote kichwani.

6 Kama mwanamke hataki kufunika kichwa chake, nywele zake zinyolewe; na kama ni aibu kwa mwanamke kunyoa kichwa chake, au kukata nywele zake, basi afunike kichwa chake.

7 Mwanamume asifunike kichwa chake kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.

8 Kwa maana mwanamume hakuumbwa kutoka kwa mwanamke, bali mwanamke ame toka kwa mwanamume.

9 Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.

10 Hii ndio sababu inampasa mwanamke afunike kichwa chake na kwa ajili ya malaika.

11 Lakini katika Bwana mwanamke hawezi kufanya lo lote pasipo mwanamume, wala mwanamume hawezi kufanya lo lote pasipo mwanamke.


Mkuu katika hoja yako umechokoza kitu cha msingi mno ili kipate kueleweka na kujadiliwa kwa hekima hapa jukwaani. Mafundisho mengi waliokabidhiwa mitume na manabii yamechakachuliwa sana katika nyakati za sasa za kanisa. Madhehebu mengi ya Kikristo yanahubiri injili bandia na iliyoghoshiwa. Injili ambayo ni kinyume kabisa na ile ambayo walikabidhiwa mitume wa Bwana Yesu Kristo.
 
Nukuu ya maandiko kutoka katika Agano Jipya pia hutufundisha kama vile ifuatavyo,

1 WAKORINTHO 11

2 Ninawasifu kwa sababu mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kuwa mnashika mafundisho niliyowakabidhi.

3 Lakini napenda muelewe kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, kama vile mume alivyo kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.

4 Kwa hiyo mwanamume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anaaib isha kichwa chake.

5 Na mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anaaibisha kichwa chake, ni sawa kama amenyoa nywele zote kichwani.

6 Kama mwanamke hataki kufunika kichwa chake, nywele zake zinyolewe; na kama ni aibu kwa mwanamke kunyoa kichwa chake, au kukata nywele zake, basi afunike kichwa chake.

7 Mwanamume asifunike kichwa chake kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.

8 Kwa maana mwanamume hakuumbwa kutoka kwa mwanamke, bali mwanamke ame toka kwa mwanamume.

9 Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.

10 Hii ndio sababu inampasa mwanamke afunike kichwa chake na kwa ajili ya malaika.

11 Lakini katika Bwana mwanamke hawezi kufanya lo lote pasipo mwanamume, wala mwanamume hawezi kufanya lo lote pasipo mwanamke.


Mkuu katika hoja yako umechokoza kitu cha msingi mno ili kipate kueleweka na kujadiliwa kwa hekima hapa jukwaani. Mafundisho mengi waliokabidhiwa mitume na manabii yamechakachuliwa sana katika nyakati za sasa za kanisa. Madhehebu mengi ya Kikristo yanahubiri injili bandia na iliyoghoshiwa. Injili ambayo ni kinyume kabisa na ile ambayo walikabidhiwa mitume wa Bwana Yesu Kristo.
Hakika hakika
Alisema Yesu Kristo katika Mathayo 24
15. Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu
),

Mpaka sasa sehemu kubwa ya Madhabahu ya Kweli ya Neno la Mungu inasimamiwa na chukizo la uharibifu...
 
Back
Top Bottom