Je, nawezaje kufanya mitihani ya science ya form IV & VI kama PC Candidate?

Mtafiti Pro

Member
May 5, 2018
12
6
Habari wana taaluma.Mimi nilihitimu kidato cha 4 mwaka 2010 masomo ya biashara.

Masomo yote nilipata D isipokuwa Book-keeping 'A' , Mathematics 'B' na History 'C'.
Niliendelea advance masomo ya biashara pia (ECA) na kuhitimu mwaka 2013.

Matokeo hayakuwa mazuri, sababu zilikuwa nyingi lakini nisingependa kuzifanya kuwa kikwazo cha kuto-move on maana muda haurudi nyuma na naamini ilikuwa ni mitihani tu ya kimaisha ambayo imenisukuma kuelekea katika dira mpya hadi kufikia hapa nilipo.

Haikuwa pendekezo langu kuchukua masomo ya biashara ila kwa wakati huo mazingira ya shule za kata walimu wa science ilikuwa issue sana.

Hivyo ilinilazimu nisome masomo haya ya biashara kwa sababu ya woga wa kufeli maana walimu wa science ilikuwa wanaonekana kipindi cha mitihani tu ila vipindi vya darasani ni mara chache sana.

Kusudio langu hasa ni kusoma masomo ya science (PCM au PGM) na kuyafanyia mitihani kwa level zote mbili kwa muda wa miaka miwili ili niwe na msingi imara utakaoniwezesha kuendelea na elimu ya juu hasa upande wa natural sciences au Engineering kutokana na fursa ambazo nakutana nazo.

Kwa sasa naishi DAR na ni mfanya biashara ila nashukuru nina muda mwingi wa kusoma.

Je, endapo nitaamua kuanza kuelekea kwenye dira hii mpya nitawezaje kufanya mitihani ya science kwa level zote mbili kama PC CANDIDATE?

Natanguliza shukrani kwa watakaonionesha njia.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Kwenye mitihani ya practical kwa level zote utatafuta mwalimu wako akufundishe, siku ya mtihani unafanya bila shida.

Pia kwa olevel unaweza opt kufanya alternative to practical.
 
Inawezekana Ndani ya mwaka Nipe 1M nikukatie phy,chem na Mathematics biology inaeleweka nitakupa notes zimenyooka kama rula.....advance tutapiga advanced mathematics pekee.
 
Kivipi ndugu yangu, naomba nipe njia.
Nenda kwenye shule yenye kituo cha watahiniwa binafsi, kisha omba kusajiliwa (mwaka huu umechelewa ingawa unaweza jiandikisha ila kuna penalt) kufanya mitahani yako.

Kwenye masomo ya sayansi olevel utachagua kufanya mitihani ya paper two either practical au alternative to practical.

Kwa advance vivyo hivyo tafuta shule ya advance yenye kituo cha watahiniwa binafsi muda ukifika ujiandikishe, ila utafanya practical.
Hivyo kama uko tayari chukua hatua haujachelewa.
 
Inawezekana Ndani ya mwaka Nipe 1M nikukatie phy,chem na Mathematics biology inaeleweka nitakupa notes zimenyooka kama rula.....advance tutapiga advanced mathematics pekee.
Hautaweza kumudu kumaliza mada zote za masomo matatu kwa 1M.

Contents za Physics, Chemistry na Advanced maths zinahitaji muda mwingi kumfundisha mtu.

Labda sijajua zama hizi huenda mtaala umebadilika, ila zama zetu huko nyuma ilikuwa shughuli pevu.

Mechanics tu ilihitaji miezi, ukija adv maths application za vectors au calculus tu unatabika nazo siku za kutosha, hapo hatujagusia chemistry n.k n.k
 
Hautaweza kumudu kumaliza mada zote za masomo matatu kwa 1M.

Contents za Physics, Chemistry na Advanced maths zinahitaji muda mwingi kumfundisha mtu.

Labda sijajua zama hizi huenda mtaala umebadilika, ila zama zetu huko nyuma ilikuwa shughuli pevu.
Mechanics tu ilihitaji miezi, ukija adv maths application za vectors au calculus tu unatabika nazo siku za kutosha, hapo hatujagusia chemistry n.k n.k
Hapo nazungumiza ni o level peke yake.....si umeona advancce nimesema tutasoma adv mathe pekee.....after all Muda wa kumaliza inategemeq na kichwa chake ila kama alimaliza 2010 imekuwa kitambo sana asee.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Hapo nazungumiza ni o level peke yake.....si umeona advancce nimesema tutasoma adv mathe pekee.....after all Muda wa kumaliza inategemeq na kichwa chake ila kama alimaliza 2010 imekuwa kitambo sana asee.
Nimekuelewa kiongozi
 
Hautaweza kumudu kumaliza mada zote za masomo matatu kwa 1M.

Contents za Physics, Chemistry na Advanced maths zinahitaji muda mwingi kumfundisha mtu.

Labda sijajua zama hizi huenda mtaala umebadilika, ila zama zetu huko nyuma ilikuwa shughuli pevu.
Mechanics tu ilihitaji miezi, ukija adv maths application za vectors au calculus tu unatabika nazo siku za kutosha, hapo hatujagusia chemistry n.k n.k
Bora umemuambia ukweli kabisaa,
 
Hongera sana mkuu.Hiyo PC ulisajili ituo gani na tuitions ulipitia wapi mkuu?
Inawezekana Kama Mimi form 4 nilisoma government science, advance nimesoma pc mwaka mmoja pcm nikagonga two ya 10 nipo zangu automobile engineering kikubwa ni kukaza sana tena sana mzee
 
Back
Top Bottom