Huyu ndio gwiji, jabali na Mfalme wa muziki nchini Tanzania

Akilihuru

JF-Expert Member
May 20, 2022
1,447
2,838
Ndugu nawasalim kwa jina la yule alieumba mbingu, ardhi na vyote vilivyomo ndan yake.

Ndugu zangu nakumbuka marehem babu yangu aliwahi kuniambia kwamba, kama mwanamuziki mkongwe nchini Tanzania hayati Marijani Rajabu aka Jabali la muziki angejaaliwa elimu katika maisha yake ya dunia, basi angekuwa msaada mkubwa sana kwa taifa letu. Marijani Rajabu alikuwa mwanamuziki mwenye maono na upeo wa hali ya juu ktk tasnia ya muziki wetu, hali iliyopelekea nyimbo zake nyingi kupendwa na watu wa rika mbali mbali wakiwemo wazee, vijana na hata watoto pia ukiwapigia jojina leo watakatika mauno mpaka mwisho wa wimbo.

Ni Marijani Rajabu pekee ndio mara nyingi huchukuliwa kama nembo ya muziki wa dansi nchini. Mfano unaweza kumsikia mzazi anamwambia mtoto wake "wewe unaimba nini bwana mbona mziki wenyewe haueleweki, watu tumewaona kina Marijani Rajabu na tukacheza mziki haswa, sasa wewe sijui unaimba nini hapa". Au utasikia mtu anasema "eti na wewe nae msanii, unataka kuwa kama Marijani Rajabu nini".

Pia Marijani ni kati wa wasanii ambao ndimbo zake zimekuwa zikirudiwa na wasanii mbali mbali wenye majina makubwa mfano Lady J dee aliirudia - Siwema, mkongwe Mr Paul aliirudia -Zuwena, wengine wamerudia Jojina nk. Wenye kumjua jabali huyu wanasema kwamba 80% ya nyimbo zake ni visa vya kweli vilivyomtokea yeye, rafiki zake au ndugu zake. Mfano kuna mdogo wake alitoka Marekani kufika bongo akawa anajifanya yeye matawi ya juu basi jabali hakumchelewesha akamtungia nyimbo fasta fasta, dogo alipogundua hilo kwa aibu akaomba msamaha kwa familia yao kwa yote aliyokuwa akiyafanya baada ya kutoka ughaibuni.

Pia Siwema, Sadiki, masudi, Zuwena, Mwanameka, Jojina na nyingine nyingi ni visa vya kweli vilivyotokea ktk jamii afu mwamba huyo akavitolea nyimbo ili kunyoosha mambo.

Nyimbo ya mwanamkiwa nayo inasemekana ni kisa cha kweli kilichotokea katika familia ya jirani yake ambae alifiwa na mkewe na kuowa mke mungine, mwanamke yule akaanza kumtesa mtoto, ndo Jabali kuona vile akamtolea jirani huyo nyimbo kumuonya juu ya kumtesa mtoto yatima.

Marijani Rajabu nyimbo zake zimekuwa ni elimu tosha kwa wazee na vijana mbali mbali. Kila sehemu aliyogusa aliacha ujumbe unaoeleweka. Akiimba mapenzi utafaidika na ujumbe uliopo ndan ya mapenzi, akiimba usia utafaidika usia huo, akiimba maisha utafaidika na alichoimba, kifupi hakuwa kushindwa katika kufikisha ujumbe wake katika jamii.

Babu yang aliwahi niambia kwamba kama huyu mwamba angesomea uchumi na kufikia kuitwa dokta au profesa wa uchumi basi angetoa mchango mkubwa wa uchumi kwa watanzania kupitia taalum yake aliyojifunza maana alikuwa mtu wa watu na kwa bahati nzuri alijaaliwa utu. Kwa wasiomjua 👇

Marijani alizaliwa tar 3 March 1955, Kariakoo, wilaya ya Ilala, jijini Dar. Na alifariki tar 23 March 1995 jijini Dar es salaam.
Marijani ameacha alama kubwa ktk tasnia ya mziki nchini Tanzania. Pichani ni baadhi ya vibao vyake vilivyotamba miaka hiyo.

Mwaka 2016 aliwahi kupewa tuzo ya mwanamuziki bora wa muda wote na aliekuwa raisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania mh Jakaya M. Kikwete katika kutambua mchango wake wa tasnia ya muziki hapa Tanzania, maana nyimbo zake zilitumika mpaka kufundishia shule na nyingine kuelekezwa katika maswali ya mitihani ya shule.
RIP Majirani Rajabu aka jabali la mziki.
images (42).jpeg
images (40).jpeg
Screenshot_20220902-112754.jpg
 
Ipo siku huko mbeleni kina Diamond na Ali Kiba watakuja kuandikwa kama hivi. SIjui kipindi hicho watakuwa wanasikiliza muziki wa aina gani.
Labda wakumbukwe kwa style yao ya kuzunguka zunguka stejini huku wameshika maeneo ya mbele ya zipu kama mtu aliebanwa na mkojo.
Lkn hawana miziki ya maana ambayo inaweza kuifunza jamii vizazi na vizazi kama ilivyo kwa wenzao waliopita.
 
Safi sana mkuu kwa Kuja na mada hii ili watanzania wasisahau watanzania wenzetu ambao kwa kutumia talent zao wakituelimisha,walituburudisha na mwisho mwa yote Wali make sure kuwa mila na desturi zetu zinainziwa duniani, miaka hiyo wimbo ukipigwa radioni hujiulizi ,moja kwa moja unajua hiyo ni TZ music ,sasa hawa kenge wa sasa wametuvuruga mno ,wameharibu muziki wetu kila wakati ni kushika mapumbu yao
Ndugu nawasalim kwa jina la yule alieumba mbingu, ardhi na vyote vilivyomo ndan yake.

Ndugu zangu nakumbuka marehem babu yangu aliwahi kuniambia kwamba, kama mwanamuziki mkongwe nchini Tanzania hayati Marijani Rajabu aka Jabali la muziki angejaaliwa elimu katika maisha yake ya dunia, basi angekuwa msaada mkubwa sana kwa taifa letu. Marijani Rajabu alikuwa mwanamuziki mwenye maono na upeo wa hali ya juu ktk tasnia ya muziki wetu, hali iliyopelekea nyimbo zake nyingi kupendwa na watu wa rika mbali mbali wakiwemo wazee, vijana na hata watoto pia ukiwapigia jojina leo watakatika mauno mpaka mwisho wa wimbo.

Ni Marijani Rajabu pekee ndio mara nyingi huchukuliwa kama nembo ya muziki wa dansi nchini. Mfano unaweza kumsikia mzazi anamwambia mtoto wake "wewe unaimba nini bwana mbona mziki wenyewe haueleweki, watu tumewaona kina Marijani Rajabu na tukacheza mziki haswa, sasa wewe sijui unaimba nini hapa". Au utasikia mtu anasema "eti na wewe nae msanii, unataka kuwa kama Marijani Rajabu nini".

Pia Marijani ni kati wa wasanii ambao ndimbo zake zimekuwa zikirudiwa na wasanii mbali mbali wenye majina makubwa mfano Lady J dee aliirudia - Siwema, mkongwe Mr Paul aliirudia -Zuwena, wengine wamerudia Jojina nk. Wenye kumjua jabali huyu wanasema kwamba 80% ya nyimbo zake ni visa vya kweli vilivyomtokea yeye, rafiki zake au ndugu zake. Mfano kuna mdogo wake alitoka Marekani kufika bongo akawa anajifanya yeye matawi ya juu basi jabali hakumchelewesha akamtungia nyimbo fasta fasta, dogo alipogundua hilo kwa aibu akaomba msamaha kwa familia yao kwa yote aliyokuwa akiyafanya baada ya kutoka ughaibuni.

Pia Siwema, Sadiki, masudi, Zuwena, Mwanameka, Jojina na nyingine nyingi ni visa vya kweli vilivyotokea ktk jamii afu mwamba huyo akavitolea nyimbo ili kunyoosha mambo.
Nyimbo ya mwanamkiwa nayo inasemekana ni kisa cha kweli kilichotokea katika familia ya jirani yake ambae alifiwa na mkewe na kuowa mke mungine, mwanamke yule akaanza kumtesa mtoto, ndo Jabali kuona vile akamtolea jirani huyo nyimbo kumuonya juu ya kumtesa mtoto yatima.
Marijani Rajabu nyimbo zake zimekuwa ni elimu tosha kwa wazee na vijana mbali mbali. Kila sehemu aliyogusa aliacha ujumbe unaoeleweka. Akiimba mapenzi utafaidika na ujumbe uliopo ndan ya mapenzi, akiimba usia utafaidika usia huo, akiimba maisha utafaidika na alichoimba, kifupi hakuwa kushindwa katika kufikisha ujumbe wake ktk jamii. Babu yang aliwahi niambia kwamba kama huyu mwamba angesomea uchumi na kufikia kuitwa dokta au profesa wa uchumi basi angetoa mchango mkubwa wa uchumi kwa watanzania kupitia taalum yake aliyojifunza maana alikuwa mtu wa watu na kwa bahati nzuri alijaaliwa utu. Kwa wasiomjua 👇

Marijani alizaliwa tar 3 March 1955, Kariakoo, wilaya ya Ilala, jijini Dar. Na alifariki tar 23 March 1995 jijini Dar es salaam.
Marijani ameacha alama kubwa ktk tasnia ya mziki nchini Tanzania. Pichani ni baadhi ya vibao vyake vilivyotamba miaka hiyo.

Mwaka 2016 aliwahi kupewa tuzo ya mwanamuziki bora wa muda wote na aliekuwa raisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania mh Jakaya M. Kikwete katika kutambua mchango wake wa tasnia ya muziki hapa Tanzania, maana nyimbo zake zilitumika mpaka kufundishia shule na nyingine kuelekezwa katika maswali ya mitihani ya shule.
RIP Majirani Rajabu aka jabali la mziki.

1. Marijani Radjab
2. Bitchuka
3. Maneti
4. Shaban Dede
5. Muhidin Gulumo
6. Tx Moshi
7. Mbaraka Mwinshehe
Shem Karenga, wema Abdallah, Joseph Mulenga.....nchi hii tumepoteza kabisa vocalists na soloist
 
Safi sana mkuu kwa Kuja na mada hii ili watanzania wasisahau watanzania wenzetu ambao kwa kutumia talent zao wakituelimisha,walituburudisha na mwisho mwa yote Wali make sure kuwa mila na desturi zetu zinainziwa duniani, miaka hiyo wimbo ukipigwa radioni hujiulizi ,moja kwa moja unajua hiyo ni TZ music ,sasa hawa kenge wa sasa wametuvuruga mno ,wameharibu muziki wetu kila wakati ni kushika mapumbu yao



Shem Karenga, wema Abdallah, Joseph Mulenga.....nchi hii tumepoteza kabisa vocalists na soloist
Kweli ndugu yangu, kwa kuwa serikali haikuweka utaratibu wa kuwaenzi wanamuziki hawa. Ngoja sisi wenyewe tuliotambua au tunaotambua mchango wao katika tasnia ya muziki wa mtanzania tuwaenzi kwa namna ya kuwandikia makala mbali mbali ili wale ambao hawakupata nafasi ya kuwajua waweze kuwajua.

Wasanii wa sasa wengi ni weupe, ukimpa gitaa hajui kupiga, ukimpa kinanda hajui kupiga, ukimwambia aimbe live bila play back pumzi hamna na mbaya zaidi hiyo style ya kushika mapumpu utafikiri mtu amebanwa na mkojo stejini.
Nampongeza sana mleta mada kwa kutambua mchango wa hawa magwiji wa muziki wetu wa muziki nchini.
 
Safi sana mkuu kwa Kuja na mada hii ili watanzania wasisahau watanzania wenzetu ambao kwa kutumia talent zao wakituelimisha,walituburudisha na mwisho mwa yote Wali make sure kuwa mila na desturi zetu zinainziwa duniani, miaka hiyo wimbo ukipigwa radioni hujiulizi ,moja kwa moja unajua hiyo ni TZ music ,sasa hawa kenge wa sasa wametuvuruga mno ,wameharibu muziki wetu kila wakati ni kushika mapumbu yao



Shem Karenga, wema Abdallah, Joseph Mulenga.....nchi hii tumepoteza kabisa vocalists na soloist
Asante sana mkuu kwa maelezo yako yaliojitosheleza. Hakika ww ni mmoja wa watu muhimu sana hapa JF.
 
Back
Top Bottom