Akilihuru
JF-Expert Member
- May 20, 2022
- 1,447
- 2,838
Ndugu nawasalim kwa jina la yule alieumba mbingu, ardhi na vyote vilivyomo ndan yake.
Ndugu zangu nakumbuka marehem babu yangu aliwahi kuniambia kwamba, kama mwanamuziki mkongwe nchini Tanzania hayati Marijani Rajabu aka Jabali la muziki angejaaliwa elimu katika maisha yake ya dunia, basi angekuwa msaada mkubwa sana kwa taifa letu. Marijani Rajabu alikuwa mwanamuziki mwenye maono na upeo wa hali ya juu ktk tasnia ya muziki wetu, hali iliyopelekea nyimbo zake nyingi kupendwa na watu wa rika mbali mbali wakiwemo wazee, vijana na hata watoto pia ukiwapigia jojina leo watakatika mauno mpaka mwisho wa wimbo.
Ni Marijani Rajabu pekee ndio mara nyingi huchukuliwa kama nembo ya muziki wa dansi nchini. Mfano unaweza kumsikia mzazi anamwambia mtoto wake "wewe unaimba nini bwana mbona mziki wenyewe haueleweki, watu tumewaona kina Marijani Rajabu na tukacheza mziki haswa, sasa wewe sijui unaimba nini hapa". Au utasikia mtu anasema "eti na wewe nae msanii, unataka kuwa kama Marijani Rajabu nini".
Pia Marijani ni kati wa wasanii ambao ndimbo zake zimekuwa zikirudiwa na wasanii mbali mbali wenye majina makubwa mfano Lady J dee aliirudia - Siwema, mkongwe Mr Paul aliirudia -Zuwena, wengine wamerudia Jojina nk. Wenye kumjua jabali huyu wanasema kwamba 80% ya nyimbo zake ni visa vya kweli vilivyomtokea yeye, rafiki zake au ndugu zake. Mfano kuna mdogo wake alitoka Marekani kufika bongo akawa anajifanya yeye matawi ya juu basi jabali hakumchelewesha akamtungia nyimbo fasta fasta, dogo alipogundua hilo kwa aibu akaomba msamaha kwa familia yao kwa yote aliyokuwa akiyafanya baada ya kutoka ughaibuni.
Pia Siwema, Sadiki, masudi, Zuwena, Mwanameka, Jojina na nyingine nyingi ni visa vya kweli vilivyotokea ktk jamii afu mwamba huyo akavitolea nyimbo ili kunyoosha mambo.
Nyimbo ya mwanamkiwa nayo inasemekana ni kisa cha kweli kilichotokea katika familia ya jirani yake ambae alifiwa na mkewe na kuowa mke mungine, mwanamke yule akaanza kumtesa mtoto, ndo Jabali kuona vile akamtolea jirani huyo nyimbo kumuonya juu ya kumtesa mtoto yatima.
Marijani Rajabu nyimbo zake zimekuwa ni elimu tosha kwa wazee na vijana mbali mbali. Kila sehemu aliyogusa aliacha ujumbe unaoeleweka. Akiimba mapenzi utafaidika na ujumbe uliopo ndan ya mapenzi, akiimba usia utafaidika usia huo, akiimba maisha utafaidika na alichoimba, kifupi hakuwa kushindwa katika kufikisha ujumbe wake katika jamii.
Babu yang aliwahi niambia kwamba kama huyu mwamba angesomea uchumi na kufikia kuitwa dokta au profesa wa uchumi basi angetoa mchango mkubwa wa uchumi kwa watanzania kupitia taalum yake aliyojifunza maana alikuwa mtu wa watu na kwa bahati nzuri alijaaliwa utu. Kwa wasiomjua 👇
Marijani alizaliwa tar 3 March 1955, Kariakoo, wilaya ya Ilala, jijini Dar. Na alifariki tar 23 March 1995 jijini Dar es salaam.
Marijani ameacha alama kubwa ktk tasnia ya mziki nchini Tanzania. Pichani ni baadhi ya vibao vyake vilivyotamba miaka hiyo.
Mwaka 2016 aliwahi kupewa tuzo ya mwanamuziki bora wa muda wote na aliekuwa raisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania mh Jakaya M. Kikwete katika kutambua mchango wake wa tasnia ya muziki hapa Tanzania, maana nyimbo zake zilitumika mpaka kufundishia shule na nyingine kuelekezwa katika maswali ya mitihani ya shule.
RIP Majirani Rajabu aka jabali la mziki.
Ndugu zangu nakumbuka marehem babu yangu aliwahi kuniambia kwamba, kama mwanamuziki mkongwe nchini Tanzania hayati Marijani Rajabu aka Jabali la muziki angejaaliwa elimu katika maisha yake ya dunia, basi angekuwa msaada mkubwa sana kwa taifa letu. Marijani Rajabu alikuwa mwanamuziki mwenye maono na upeo wa hali ya juu ktk tasnia ya muziki wetu, hali iliyopelekea nyimbo zake nyingi kupendwa na watu wa rika mbali mbali wakiwemo wazee, vijana na hata watoto pia ukiwapigia jojina leo watakatika mauno mpaka mwisho wa wimbo.
Ni Marijani Rajabu pekee ndio mara nyingi huchukuliwa kama nembo ya muziki wa dansi nchini. Mfano unaweza kumsikia mzazi anamwambia mtoto wake "wewe unaimba nini bwana mbona mziki wenyewe haueleweki, watu tumewaona kina Marijani Rajabu na tukacheza mziki haswa, sasa wewe sijui unaimba nini hapa". Au utasikia mtu anasema "eti na wewe nae msanii, unataka kuwa kama Marijani Rajabu nini".
Pia Marijani ni kati wa wasanii ambao ndimbo zake zimekuwa zikirudiwa na wasanii mbali mbali wenye majina makubwa mfano Lady J dee aliirudia - Siwema, mkongwe Mr Paul aliirudia -Zuwena, wengine wamerudia Jojina nk. Wenye kumjua jabali huyu wanasema kwamba 80% ya nyimbo zake ni visa vya kweli vilivyomtokea yeye, rafiki zake au ndugu zake. Mfano kuna mdogo wake alitoka Marekani kufika bongo akawa anajifanya yeye matawi ya juu basi jabali hakumchelewesha akamtungia nyimbo fasta fasta, dogo alipogundua hilo kwa aibu akaomba msamaha kwa familia yao kwa yote aliyokuwa akiyafanya baada ya kutoka ughaibuni.
Pia Siwema, Sadiki, masudi, Zuwena, Mwanameka, Jojina na nyingine nyingi ni visa vya kweli vilivyotokea ktk jamii afu mwamba huyo akavitolea nyimbo ili kunyoosha mambo.
Nyimbo ya mwanamkiwa nayo inasemekana ni kisa cha kweli kilichotokea katika familia ya jirani yake ambae alifiwa na mkewe na kuowa mke mungine, mwanamke yule akaanza kumtesa mtoto, ndo Jabali kuona vile akamtolea jirani huyo nyimbo kumuonya juu ya kumtesa mtoto yatima.
Marijani Rajabu nyimbo zake zimekuwa ni elimu tosha kwa wazee na vijana mbali mbali. Kila sehemu aliyogusa aliacha ujumbe unaoeleweka. Akiimba mapenzi utafaidika na ujumbe uliopo ndan ya mapenzi, akiimba usia utafaidika usia huo, akiimba maisha utafaidika na alichoimba, kifupi hakuwa kushindwa katika kufikisha ujumbe wake katika jamii.
Babu yang aliwahi niambia kwamba kama huyu mwamba angesomea uchumi na kufikia kuitwa dokta au profesa wa uchumi basi angetoa mchango mkubwa wa uchumi kwa watanzania kupitia taalum yake aliyojifunza maana alikuwa mtu wa watu na kwa bahati nzuri alijaaliwa utu. Kwa wasiomjua 👇
Marijani alizaliwa tar 3 March 1955, Kariakoo, wilaya ya Ilala, jijini Dar. Na alifariki tar 23 March 1995 jijini Dar es salaam.
Marijani ameacha alama kubwa ktk tasnia ya mziki nchini Tanzania. Pichani ni baadhi ya vibao vyake vilivyotamba miaka hiyo.
Mwaka 2016 aliwahi kupewa tuzo ya mwanamuziki bora wa muda wote na aliekuwa raisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania mh Jakaya M. Kikwete katika kutambua mchango wake wa tasnia ya muziki hapa Tanzania, maana nyimbo zake zilitumika mpaka kufundishia shule na nyingine kuelekezwa katika maswali ya mitihani ya shule.
RIP Majirani Rajabu aka jabali la mziki.