Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 11,208
- 19,001
Mkuu Gentamycine ngoja nikujibu, without fear or favor;
1. Nachukia Mtu ambaye haendi na muda na anajifanyia tu Mambo yake Kienyeji Kienyeji.
Inakuhusu nini kama mambo anayojifanyia hayakuathiri wewe binafsi?
2. Nachukia Mtu ambaye hajui Kujipanga Kiratiba na yupo yupo kama Zombie fulani hivi duniani
Inakuhusu nini kama hajui kujipangia ratiba na ratiba yake haikuathiri wewe binafsi?
3. Nachukia Mtu ambaye akiamka asubuhi hajui hata atafanya nini Siku nzima
Inakuhusu nini kama mambo atakayofanya siku nzima hayakuhusu wewe binafsi?
4. Nachukia Mtu ambaye hayuko Up to date kwa Taarifa za Ndani na Nje ya nchi
Inakuhusu nini kama kutokuwa kwake up to date na taarifa za ndani na nje haikuathiri wewe binafsi?
5. Nachukia Mtu ambaye najua kuwa Yeye ni Mpumbavu halafu Yeye anaona yuko sahihi kwa alifanyalo
Acha kubishana au kuongea na mtu huyo, hutakuwa na haja ya kuchukia
6. Nachukia Mtu ambaye hajui Kujichanganya na Watu wa kila rika
Acha kujichanganya nae, hutakuwa na haja ya kuchukia
7. Nachukia Mtu ambaye hapendi kuwa Mdadisi Mdadisi na Mpenda Kujisomea Magazeti na Vitabu
Inakuhusu nini kama mtu huyu kutojisomea magazeti na vitabu haiakuathiri wewe binafsi?
Sasa Mkuu, unaona hapa mwenye tatizo ni wewe, sio hao watu unaowachukia. Labda ni bora kafuta msaada psychiatrists kabla mambo hayajaharibika zaidi