Hii misafara ya viongozi imekuwa kero sasa

xox

JF-Expert Member
Sep 23, 2018
1,427
6,600
Kuna haja serikali itafute njia mbadala ya kusafirisha viongozi maana ishakuwa adhabu kwa raia wengine hasa kwa Dar.

Leo kwa watumiaji wa Pugu Road kuanzia Vingunguti mpaka Airport watakuwa mashuhuda wa hili.

Barabara za Vingunguti kwenda kwa Mnyamani na ya Majumba Sita kwenda Kinyerezi zote zimefungwa sababu ya ujenzi. Mbadala pekee ni mchepuko wa mataa ya Airport.

Sasa leo bila taarifa maalum traffic wamejazana kwenye mataa ya Airport na kwa ubabe kabisa wanaforce watu waende moja kwa moja wasiingie barabara inayokwenda kulia kuelekea majumba sita.

Baada ya takriban lisaa limoja ndio misafara inaanza kutoka Airport. Sasa kwa starehe ya viongozi wachache nusu ya mji ulisimama ama kutaabisha watu kwenda masafa marefu kufika makwao. Kuna baadhi ya watu makazi yao yapo mita chache tu toka petrol station ya Airport lakini walilazimishwa kwenda mpaka mataa ya majumba sita ambapo napo kumefungwa kulazimisha kugeuza tena na kurudi nyuma.

Na hao matraffic waliokuwepo hapo walikuwa wakorofi na kuwa na lugha mbovu walipoulizwa sababu za kuzuia magari. Kuna polisi mmoja bonge alikuwa na uniform za khaki alidiriki hata kutishia kupiga baadhi ya madereva.

Nadhani ni wakati sasa serikali ijitathmini upya katika swala zima la kuratibu misafara ya viongozi. Maana hii ishakuwa kero kubwa hasa mida ya asubuhi na jioni njia ya Airport.

Kuna wakati hata ndege hazijatua magari yanasimamishwa, mpaka itue na hao viongozi wajivute kutoka wakati huo wengine wamenasa kwenye foleni tu.
 
Sitahasau ile foleni nimetoka kariakoo saa 12 nikafika chanika saa 4 usiku foleni ilikua mataa ya airport near barabara ya kwenda kinyerezi na majumba sita
 
Ila hii nchi kuna kuendekezana sana. Juzi gari zilisimamishwa kuanzia airport saa zima kisa kuna bwenyenye moja na ving'ora vyake anawahishwa kwenda vacation.

Kipindi gari zinasimamishwa yeye ndio anajisaidia haja kubwa nyumbani kwake.
 
  • Thanks
Reactions: xox
Sitahasau ile foleni nimetoka kariakoo saa 12 nikafika chanika saa 4 usiku foleni ilikua mataa ya airport near barabara ya kwenda kinyerezi na majumba sita
Imekuwa jambo la kawaida siku hizi kukaa masaa mpaka matatu kwenye foleni sababu kiongozi mmoja anarudi/anakwenda safari.
 
Kulalamika kisa njia a imefungwa kwaajili ya ujenzi na mbadala wake ikawa ndio njia watakayotumia viongozi ulipendekeza iweje..?
Kama hicho ndicho ulichoelewa mimi ni nani nikupinge ama kuhoji uwezo wako wa kuelewa ikizingatiwa umetumia bundle lako na simu yako.
Tufanye upo sahihi teacher. Usiku mwema.
 
Masikini amekuwa kiongozi * sasa anapita na msafara anatutemea raia makohozi.
Aahh John Kipilato acha mambo yako * tunakoga vumbi kwa ajili yako.
Kura yangu imekufikisha hapo ulipo * sasa unatutesa foleni ya magari kutoka ulipo mpaka uendapo.
John kipilato huu muda wako * acha kututesa wana wa wenzako punguza kiburi chako.
 
  • Thanks
Reactions: xox
Wenzetu FM Radio zao huwa zinawajulisha Motorist kwenye maeneo yenye msongamano na jinsi ya kuchepuka au kama sehemu kuna ajali hizi za kwetu Mungu ndie ajuae.
 
Wenzetu FM Radio zao huwa zinawajulisha Motorist kwenye maeneo yenye msongamano na jinsi ya kuchepuka au kama sehemu kuna ajali hizi za kwetu Mungu ndie ajuae.
Za kwetu zinachezesha kamari 24/7. Na ukikutana na wanaopaswa kutoa msaada barabarani (traffic) wao wanawaza kupiga hela tu.
 
Za kwetu zinachezesha kamari 24/7. Na ukikutana na wanaopaswa kutoa msaada barabarani (traffic) wao wanawaza kupiga hela tu.
Hicho huwa ni Kipindi kabisa ambacho hupata wafadhili Motorist wengi husikiliza FM Radios kuliko Pedestrians.
 
  • Thanks
Reactions: xox
Wenzetu FM Radio zao huwa zinawajulisha Motorist kwenye maeneo yenye msongamano na jinsi ya kuchepuka au kama sehemu kuna ajali hizi za kwetu Mungu ndie ajuae.
Hapa nimekupata vilivyo imhotep na hizi radio station za hapa kwetu sasa zimegubikwa na matangazo za kupiga hela (Bahati nasibu) wamesahau kabisa kutupa habari zilizopo na dondoo juu ya hali ya barabarani(traffic jams) Dah! Hii inchi imekua ya hovyo sana sio kwa Uongozi na viongozi wake tu hata sisi wananchi pia.
 
Hapa nimekupata vilivyo imhotep na hizi radio station za hapa kwetu sasa zimegubikwa na matangazo za kupiga hela (Bahati nasibu) wamesahau kabisa kutupa habari zilizopo na dondoo juu ya hali ya barabarani(traffic jams) Dah! Hii inchi imekua ya hovyo sana sio kwa Uongozi na viongozi wake tu hata sisi wananchi pia.
Hii nchi inaendeshwa kama mali binafsi ya watu wachache. Sisi wengine ni wasindikizaji tu.
 
Hapa nimekupata vilivyo imhotep na hizi radio station za hapa kwetu sasa zimegubikwa na matangazo za kupiga hela (Bahati nasibu) wamesahau kabisa kutupa habari zilizopo na dondoo juu ya hali ya barabarani(traffic jams) Dah! Hii inchi imekua ya hovyo sana sio kwa Uongozi na viongozi wake tu hata sisi wananchi pia.
Mimi nimeshakata tamaa,hebu ninyi Motorist wenzangu wapigieni simu Trafffic jam zimezidi na ujenzi ni mwingi (which is good thing) lakini kuna michepuko.

Mimi ninaendesha Petrol Tanker kuna kipindi natumia masaa manne hadi Ubungo mara kuna Ajali hujui wakati kama Radio zetu zingekuwa zinatuambia kwa mfano kuna ajalii Tabata Dampo unatafuta Petrol Station iliyo karibu unatulia salama salimini.
 
Mimi nimeshakata tamaa,hebu ninyi Motorist wenzangu wapigieni simu Trafffic jam zimezidi na ujenzi ni mwingi (which is good thing) lakini kuna michepuko.

Mimi ninaendesha Petrol Tanker kuna kipindi natumia masaa manne hadi Ubungo mara kuna Ajali hujui wakati kama Radio zetu zingekuwa zinatuambia kwa mfano kuna ajalii Tabata Dampo unatafuta Petrol Station iliyo karibu unatulia sakama salimini.
Shida ipo hapa nowadays huwa respond yao imekua ndogo sana wanasingizia wingi wa comments hivyo wanashindwa kuzisoma kwa wakati..
 
  • Thanks
Reactions: xox
Za kwetu zinachezesha kamari 24/7. Na ukikutana na wanaopaswa kutoa msaada barabarani (traffic) wao wanawaza kupiga hela tu.
Iko siku nimepigwa Tiket pale Chamwino nimekuta kuna Gari zimesimama kama gari 5 na mbele yangu kulikuwa na Gari la Rwanda hakukuwa na Traffic police wa kutuzuia kwamba kuna msafara kwakweli iliniuma sana ile hela basi tu kosa langu naambiwa nimeuingilia msafara wa kiongozi fulani.

Tuliwekwa pale saa nzima na,nilikuwa naelekea Bukavu.
 
Iko siku nimepigwa Tiket pale Chamwino nimekuta kuna Gari zimesimama kama gari 5 na mbele yangu kulikuwa na Gari la Rwanda hakukuwa na Traffic police wa kutuzuia kwamba kuna msafara kwakweli iliniuma sana ile hela basi tu kosa langu naambiwa nimeuingilia msafara wa kiongozi fulani.

Tuliwekwa pale saa nzima na,nilikuwa naelekea Bukavu.
Haya yote yanatokea sababu tushaaminishwa kuwa hatupaswi kuhoji wenye mamlaka. Mtu anaamua kukufanyq atakavyo kwa kujua tu huna utakapokwenda ama huna cha kumfanya.

Kwa itikadi hii tuliyojengewa ya kuwa mwenye madaraka daima yupo sahihi imepelekea kutoweza kutofautisha kati ya haki zetu na msaada. Imefikia wakati traffic kutokukuandikia ticket sababu kiuhalisia huna kosa basi inakuwa ni msaada na si haki yako.

Japo sheria inasema fine si lazima kulipwa hapo hapo, baadhi ya traffic wanashurtisha kulipwa hapo hapo ili tu kutengeneza mazingira ya rushwa. Na sisi kwa kupuuza haki zetu tunaona tumefanyiwa msaada kulipishwa 5000 badala ya 30,000 isiyo ya halali.
 
Back
Top Bottom