Group la WhatsApp latumika kuchangisha mifuko 300 ya saruji ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya Nachingwea Boys

Peter Madukwa

JF-Expert Member
Sep 20, 2012
3,137
2,478
Baadhi ya wananchi wa Nachingwea ambao wapo ktk kundi sogozi la WhatsApp la NACHINGWEA YETU, wamekabidhi mifuko 300 ya saruji kuunga mkono ujenzi wa mradi mpya wa Nachingwea boys high school inayojengwa kwa kutumia mapato ya ndani ya halmashauri ya wilaya ya Nachingwea iliyopo mkoa wa Lindi

Shule hiyo inatarajiwa kukamilika kwake kuchukua wanafunzi 1600 kuanzia kidato Cha Kwanza Hadi Cha sita.

Aidha shule hiyo mpya ya wavulana inatarajiwa kuwa na jumla ya majengo 54 ikiwemo madarasa, mabweni, nyumba za walimu, duka, zahanati na sehemu ya kula chakula.

Shule hiyo inajengwa nje kidogo ya mji wa Nachingwea katika kijiji Cha chiumbati kata ya chiumbati tarafa ya Naipanga

Akizungumza wakati wa kupokea mchango huo, aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo ambaye kwa sasa Ni katibu tawala mkoa wa DSM Bwn Hassan Abasi Rugwa, amewashukuru wadau hao wa Nachingwea Yetu Whatsapp group kwa mchango wao na kuwasisitiza wananchi wa Nachingwea kuendelea kushikamana kwa pamoja ili kufanya Mambo makubwa zaidi.

Wanafamilia hao wa Nachingwea Yetu WhatsApp group wamesema kuwa lengo la kuchangishana mchango huo Ni pamoja na

1. kushiriki kama wadau ktk ujenzi wa mradi huo
2. Kuwatia moyo watendaji wa halmashauri ya Nachingwea ktk jitihada za kutatua changamoto za elimu
3. Kutoka hamasa kwa wananchi kushiriki ktk ujenzi miradi ya maendeleo hasa miradi ya wananchi
4. Kujenga umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi Kama silaha ya kutatua changamoto mbalimbali za wilaya ya Nachingwea

Serikali imeonesha Nia ya kuunga mkono ujenzi wa shule hiyo baada ya kuona jitihada za dhati zinazofanywa na wakazi wa Nachingwea


IMG_20210605_155846_330.jpg


IMG_20210605_160505_068.jpg
 
Hongera kijana ndio utu huo. Sio kuishia kuchangia matukio ya kianasa tu huko Zurich, Y2K na NR . Vitu hivi ni adimu sana kwa Kusini huku
 
Baadhi ya wananchi wa Nachingwea ambao wapo ktk kundi sogozi la WhatsApp la NACHINGWEA YETU, wamekabidhi mifuko 300 ya saruji kuunga mkono ujenzi wa mradi mpya wa Nachingwea boys high school inayojengwa kwa kutumia mapato ya ndani ya halmashauri ya wilaya ya Nachingwea iliyopo mkoa wa Lindi

Shule hiyo inatarajiwa kukamilika kwake kuchukua wanafunzi 1600 kuanzia kidato Cha Kwanza Hadi Cha sita.

Aidha shule hiyo mpya ya wavulana inatarajiwa kuwa na jumla ya majengo 54 ikiwemo madarasa, mabweni, nyumba za walimu, duka, zahanati na sehemu ya kula chakula.

Shule hiyo inajengwa nje kidogo ya mji wa Nachingwea katika kijiji Cha chiumbati kata ya chiumbati tarafa ya Naipanga

Akizungumza wakati wa kupokea mchango huo, aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo ambaye kwa sasa Ni katibu tawala mkoa wa DSM Bwn Hassan Abasi Rugwa, amewashukuru wadau hao wa Nachingwea Yetu Whatsapp group kwa mchango wao na kuwasisitiza wananchi wa Nachingwea kuendelea kushikamana kwa pamoja ili kufanya Mambo makubwa zaidi.

Serikali imeonesha Nia ya kuunga mkono ujenzi wa shule hiyo baada ya kuona jitihada za dhati zinazofanywa na wananchi

View attachment 1809113

View attachment 1809115
Kitambo sana nachingwea.

Nawaona class met wangu hapo wamekuwa wazee wengine wamekuwa wamama kabisa kumbe watoto wa 90 tu hahhahhhha.

Hongereni wana nachingwea wasalimieni sana hapo nachingwea days,nambambo days shule ambazo zinashindana katika ufaulu hapo mjini.

Nakumbuka enzi za miaka ya 2011 wkuna vijana walituwakilisha vizuri sana kaka wenye majina ya kufanana mmoja akitoka nambambo mwingine akitoka nachingwea.

Ila nachingwea mnaacha kuchanga kufanya vitu vya maana mnajenga shule kwa wakati huu,hamko siriaz.

Hapo nachingwe wananchi wanashida nyingi tu achilia mbali na elimu.

Yani kama bado wana nachingwea mnawaza kuwa elimu iko chini kwa sababu ya majengo basi poleni sana sana sana sana sana sana
 
Kitambo sana nachingwea.

Nawaona class met wangu hapo wamekuwa wazee wengine wamekuwa wamama kabisa kumbe watoto wa 90 tu hahhahhhha.

Hongereni wana nachingwea wasalimieni sana hapo nachingwea days,nambambo days shule ambazo zinashindana katika ufaulu hapo mjini.

Nakumbuka enzi za miaka ya 2011 wkuna vijana walituwakilisha vizuri sana kaka wenye majina ya kufanana mmoja akitoka nambambo mwingine akitoka nachingwea.

Ila nachingwea mnaacha kuchanga kufanya vitu vya maana mnajenga shule kwa wakati huu,hamko siriaz.

Hapo nachingwe wananchi wanashida nyingi tu achilia mbali na elimu.

Yani kama bado wana nachingwea mnawaza kuwa elimu iko chini kwa sababu ya majengo basi poleni sana sana sana sana sana sana
Hebu shauri nini kifanyike na kipi ndio kipewe kipaumbele kwa sasa
 
Hebu shauri nini kifanyike na kipi ndio kipewe kipaumbele kwa sasa
Sijui kwa sasa kuna changamoto gani ila nina uhakika nachingwea hakuna changamoto ya majengo ya shule bali changamoto ni kwa watoto wetu.

Hatujawekeza kwa watoto tunawekeza kwwnye majengo tu wakati watakaokuja kuyatumia majengo hayo bado hawajaamka wamelala fofofo.

Acheni mambo ya kujenga mashule angalieni mnatatua vipi changamoto za maji,na changamoto zingine za maisha na sio kupoteza kwenye majengo ya shule tu.

Mnaweza kujichanga mkaanzisha mradi wowote ule wa maendeleo ya wana nachingwea kama suala la maji nadhani bado ni changamoto kubwa watu hamuwazi mtarahisisha vipi watu wasiende tena kule kwa Mungu hataki badala yake waende kuchota maji safi na salama kwenye mradi fulani ulioanzishwa na michango ya wananchi wenyewe.

Bahat nzuri naskia munae mkuu wa wilaya msikivu na mstaarabu,tumieni.

Achaneni na majengo ya shule angalieni mtarahisisha vipi changamoto zenu za maisha.

Kwenye korosho mnashindwa kuangalia kuna fursa gani.
Kwenye vilimo vingi tunashindwa kuangalia kuna fursa gani.

Nyie mnadhani kwa sasa elimu itatukomboa.

Sisi ndo runatakiwa tuikomboe hii elimu.

Na kuikomboa elimu sio kujenga majengo,nini mnakomboa majengo badala ya kuikomboa elimu.

Kaeni na huyo mkuu wa wilaya mtulize vichwa muachache na majengo ya shule ambayo watoto hawajajua umuhimu wake
 
Wewe umepitwa na wakati, elimu ni bora usiwakatishe tama wenzako. Hongereni wana watsap

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Hahaha sawa mkuu.

Sasa hivi bora uanzishhe mradi wa maji unakuwa umewasaidia wana nachingwea kuliko haya majengo ambayo yako mfanowe mengi tu lakini matokeo ni madogo.

Shule zipo lakini walimu hakuna,alafu mtu anakuja anaongeza majengo mengine ili waalimu wazidi kuwa wachache.
 
Sijui kwa sasa kuna changamoto gani ila nina uhakika nachingwea hakuna changamoto ya majengo ya shule bali changamoto ni kwa watoto wetu.

Hatujawekeza kwa watoto tunawekeza kwwnye majengo tu wakati watakaokuja kuyatumia majengo hayo bado hawajaamka wamelala fofofo.

Acheni mambo ya kujenga mashule angalieni mnatatua vipi changamoto za maji,na changamoto zingine za maisha na sio kupoteza kwenye majengo ya shule tu.

Mnaweza kujichanga mkaanzisha mradi wowote ule wa maendeleo ya wana nachingwea kama suala la maji nadhani bado ni changamoto kubwa watu hamuwazi mtarahisisha vipi watu wasiende tena kule kwa Mungu hataki badala yake waende kuchota maji safi na salama kwenye mradi fulani ulioanzishwa na michango ya wananchi wenyewe.

Bahat nzuri naskia munae mkuu wa wilaya msikivu na mstaarabu,tumieni.

Achaneni na majengo ya shule angalieni mtarahisisha vipi changamoto zenu za maisha.

Kwenye korosho mnashindwa kuangalia kuna fursa gani.
Kwenye vilimo vingi tunashindwa kuangalia kuna fursa gani.

Nyie mnadhani kwa sasa elimu itatukomboa.

Sisi ndo runatakiwa tuikomboe hii elimu.

Na kuikomboa elimu sio kujenga majengo,nini mnakomboa majengo badala ya kuikomboa elimu.

Kaeni na huyo mkuu wa wilaya mtulize vichwa muachache na majengo ya shule ambayo watoto hawajajua umuhimu wake
NACHINGWEA unaijua vizur ila kuna kitu hakiko sawa kwenye maamuzi / maono yako Peter Madukwa Peter Madukwa njoo uongezee nyama kwa hili ila kwa mimi binafsi yangu naona hili ni sahihi kabisa
 
Hapo nachingwea kuna shule ngapi za highschool, Ni chache sana. Hivyo hiyo ni hatua njema ya kujenga majengo. Kikwete alijenga maabara shule za sekondari,aliyefuatilia aliweka tools and lab equipments

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
NACHINGWEA unaijua vizur ila kuna kitu hakiko sawa kwenye maamuzi / maono yako Peter Madukwa Peter Madukwa njoo uongezee nyama kwa hili ila kwa mimi binafsi yangu naona hili ni sahihi kabisa
Sawa mkuu mimi nimetoa maoni tu lakini huko nimezaliwa.

Najua idadi ya wanafunzi wanaofaulu kwenda sekondari.

Najua idadi ya wanaopasi kutoka sekondari kwenda A level.

Kiukweli idadi hairidhishi kabisa kulinganisha na kanda zingine.

Bado wana nachingwea hawajaamka na kuona kuwa tatizo sio majengo bali tatizo ni mindset za wazazi na wanafunzi haziko sawa.

Mimi wakati nasoma sekondari fulani hapo nachinwea waalimu walikuwa hawazidi saba walioajiriwa.

Darasa lwtu moja tu kulikuwa na wanafunzi >100.

Lakini waliofaulu kwenda advance hawakuzidi 15.

Hii maana yake ni kuwa a level ingekuwepo kwa wakati huo watoto wa kusini wangekuwa wachache sana kinganisha na mikoa mingine.

Sijui kwa lwo hali ikoje lakini ukweli ni kuwa hakuna uhaba wa shule za A level kwa sababu hakuna ambae alifaulu akakosa kwenda A lwvel ukizingatia kuwa wanaofaulu ni wachache.

Ninao ndugu zangu waliomaliza miaka ya 2014 n.k wifaulu vizuri wakaenda A level shule mbalimbali.

Wanatatua matatizo ambayo hayapo.
 
Hapo nachingwea kuna shule ngapi za highschool, Ni chache sana. Hivyo hiyo ni hatua njema ya kujenga majengo. Kikwete alijenga maabara shule za sekondari,aliyefuatilia aliweka tools and lab equipments

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Ni hatua nzuri sana sio siri.

Lakini ukitazama idadi ya wale wanaofaulu kwenda advance katika wilaya ya nachingwea ina mahusiano gani na kujengwa kwa high school ?
 
"Yani kama bado wana nachingwea mnawaza kuwa elimu iko chini kwa sababu ya majengo basi poleni sana sana sana sana sana sana"

Wewe hamna tofauti na mfalme juha. Wamekwambia elimu iko chini? Bila shaka wanaongeza shule ili ziwe nyingi tena za bweni ambazo kwa sasa iwe ndo foccus. Shule za bweni huongeza ushirikiano baina ya watanzania kwa kuwa itachukua wanafunzi hadi nje ya mkoa. Lakni ufundishaji wake ni rahisi kwa kuwa mwanafunzi anakuwa controlled and monitored all the time during the school season.

Badala ya kuwakejeli yafaa uwaunge mkono. Ebo!
 
Baadhi ya wananchi wa Nachingwea ambao wapo ktk kundi sogozi la WhatsApp la NACHINGWEA YETU, wamekabidhi mifuko 300 ya saruji kuunga mkono ujenzi wa mradi mpya wa Nachingwea boys high school inayojengwa kwa kutumia mapato ya ndani ya halmashauri ya wilaya ya Nachingwea iliyopo mkoa wa Lindi

Shule hiyo inatarajiwa kukamilika kwake kuchukua wanafunzi 1600 kuanzia kidato Cha Kwanza Hadi Cha sita.

Aidha shule hiyo mpya ya wavulana inatarajiwa kuwa na jumla ya majengo 54 ikiwemo madarasa, mabweni, nyumba za walimu, duka, zahanati na sehemu ya kula chakula.

Shule hiyo inajengwa nje kidogo ya mji wa Nachingwea katika kijiji Cha chiumbati kata ya chiumbati tarafa ya Naipanga

Akizungumza wakati wa kupokea mchango huo, aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo ambaye kwa sasa Ni katibu tawala mkoa wa DSM Bwn Hassan Abasi Rugwa, amewashukuru wadau hao wa Nachingwea Yetu Whatsapp group kwa mchango wao na kuwasisitiza wananchi wa Nachingwea kuendelea kushikamana kwa pamoja ili kufanya Mambo makubwa zaidi.

Serikali imeonesha Nia ya kuunga mkono ujenzi wa shule hiyo baada ya kuona jitihada za dhati zinazofanywa na wananchi

View attachment 1809113

View attachment 1809115
Machinga mmestuka usingizini. Wenzenu Kilimanjaro walianza miaka mingi iliyopita. Wananchi walitoa mpaka mashamba yao Kujenga shule
 
Wewe hamna tofauti na mfalme juha.
Sawa mkuu acha niheshimu mawazo yako pengine uko sahihi zaidi.
Wamekwambia elimu iko chini?
Hata kama hawajasema hilo ndo kauli yao.kila siku mnalalamika kusini elimu iko chini.

Na hao wamechangia kwa sababu ya kukuza elimu ambayo wanaona iko chini na hichi ni kilio cha wana nachingwea wanalia kila siku bila kujua tatizo nini.

Kama wanabisha waje waseme hapa kwamba elimu nachingwea haipo chini na wamefanya hivyo kwa lengo gani.
Bila shaka wanaongeza shule ili ziwe nyingi tena za bweni ambazo kwa sasa iwe ndo foccus.
Ili iwe focus ya nini ?

Lengo zikiwa nyingi hizo shule kitokee nini ?
Shule za bweni huongeza ushirikiano baina ya watanzania kwa kuwa itachukua wanafunzi hadi nje ya mkoa
Ni kweli faida hii inapatikana katika shule za bweni kwa sababu hata pale nachingwea girls wanafunzi wengi wapo ambao ni wa mikoa mingine.

Lakini nakuambia tena,hili unalolitaja wewe sio lengo kuu la wana nachingwea ati waboreshe mahusiano ama mashirikiano ?

Hayo ni katika faida ndogondogo ambazo zonapatikana katika shule faida ambazo tunaweza kuzipata katika maingiliano mwngine ya kijamii,lakini wana ajenda yao kubwa ambayo ni kuinua elimu.


Lakni ufundishaji wake ni rahisi kwa kuwa mwanafunzi anakuwa controlled and monitored all the time during the school season.
Kama lengo ni hili maana yake ikiwa mwanafunzi atakuwa easy controlled maana yake ufaulu upande alafu unakataa kwamba lengo lao sio kupandisha elimu ambayo iko chini kwa sababu ya changamoto za kutokuwa na shule za bweni ?


Badala ya kuwakejeli yafaa uwaunge mkono. Ebo!
Mimi natoa maoni mkuu sina ulazima wa kuwaunga mkono katika kila jambo.

Tatizo la kusini sio majengo wala mazingira tatizo la kusini ni mindset za wazazi na watoto wao.

Mazingira ya kusoma yako mazuri kwa sababu nachingwea hapajawa mji wa anasa kama vile dar es salaam.

Nachingwea leo hii mazingira yake ni rafiki kwa kijana mwenye focus akafocus kwenye kusoma na asiharibiwe na changamoto za kijamii ambazo zipo katika miji kama dar es salaam.

Kwenye mji kama nachingwea shule ya mbweni haina umuhimu mkubwa kama ambavyo shule ya mbweni hiyo ina umuhimu mkubwa katika miji mikubwa kama dar es saalaam.

Ni mtu asiyeelewa tu ndo atasema kuwa mazingira ya nachingwea eti yanaweza kumharibu mwanafunzi hivyo mabweni yawe mengi,je mazingira ya dar na miji mingine mikubwa ?

Narudia Tatizo sio mazingira pale nachingwea tatizo ni mondset za wazazi na watoto wao.
 
Back
Top Bottom