Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Mawazo ya serikali Tatu yalikuwa ni mawazo ya Nani?

Na ni Nani aliyefanya mawazo ya serikali Tatu yasivuke kibaha?
Kwa bahati mbaya sana Mchambuzi, wengi wetu tumekuwa kama watu waliofungwa vitambaa machoni na kuwekewa pamba masikioni; tunakaza macho lakini hatuoni, tunatega masikio lakini hatusikii. Nina wasi wasi kama Mtanganyika alikuwa anaufahamu msimamo wa awali wa Mh. Jaji Warioba kuhusu muundo wa Muungano wakati anateuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba. Ukweli, kama alivyotudokezea moja ya waliokuwa wajumbe wa Tume, Prof. Baregu, ni kwamba msimamo wa Jaji Warioba pamoja na wajumbe wengi kwenye Tume kuhusu muundo wa Muungano, ulikuwa ni wa serikali mbili. Lakini kadiri walivyozidi kuendelea na majadiliano huku wananchi wakizidi kutoa dukuduku zao, taswira iliyokuja kujengeka na kuonekana bora katika kukabiliana na kero za miaka nenda rudi iliegemea kwenye Muundo wa serikali tatu. Hivyo napata shida sana kwa watu wanaomkomalia Jaji Warioba kama vile mapendekezo ya muundo wa serikali yalitokana na utashi wake binafsi kama Mwenyekiti wa Tume na si wananchi. Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Katibu wa Tume wote walikuwa waumini wa muundo wa serikali mbili.

Nikiacha hilo naomba nitoe maoni kidogo kwa Mtanganyika kuhusu msimamo wake anaodai haufungamani na upande wowote; kwamba kwake yeye ufumbuzi wa kero upo katika muundo wa serikali moja. Kusema kweli huu ni msimamo wa kufikirika ambao hata yeye akitaka kuwa mkweli kwa nafsi yake anajua fika kwamba ni msimamo usioweza kutekelezeka...sio sasa, sio kesho na sio katika wakati wowote ulio karibu. Tofauti na mawazo ya wengi, mimi naamini muundo wa serikali tatu utatusogeza karibu kuliko muundo wa serikali mbili.

Kwa nini nasema hivyo? Baada ya miaka 50 kero zimeongezeka na zitazidi kuongezeka na safari hii kutoka kwa waliokuwa wamelala lakini sasa wameamka na wako macho na sasa nao wameanza kudai chao, Watanganyika! Ni bahati sana kwamba mpaka sasa wanaidai kwa amani lakini kwa mizengwe hii wanayowekewa si muda mrefu wataidai kwa shari.

Majirani wanaweza kuishi tu kwa amani na hata kushirikiana kwa mengi tu kama hakuna moja wao anaona ushirikiano unamletea karaha...ushirikiano wenye maelewano unaweza kukua, kukomaa na kadiri siku zinavyoendelea ukazaa muungano imara.
 
Mchambuzi na Mag3 Naomba nichangie hoja zenu kuhusu@Mtanganyika
@Mchambuzi , swali lako Mtanganyika hatalijibu, si kwakuwa hana jibu, anayo mengi.
Majibu yake yataharibu kazi aliyotumwa kuifanya.


Na nina ushahidi wa haya nisemayo.
1.Kilichomuondoa Jumbe Madarakani ni S3
2)Kundi la G55 lilitaka S3
3) Tume ya Nyalali ya chama kimoja ilitaka S3

4)Tume ya jaji kisanga ilitaka S3.

5)Tume ya awali ya Warioba, ilitaka S3.

6) Wazanzibar na wengine wakiwa ‘wamelawitiwa''madai yao ni S3
7) Seraza CUF ni S3

8)Sera za Chadema ni S3
9)Maoniya tume ya Warioba, pande zote ni S3.


Ndio maana Mag3 anasema wengeni wameamua kujitoa fahamu makusudi.
Niseme, hawajajitoa fahamu, wanazo, njaa inaweza kulazimisha mtu kusema asilotaka. Njaa haina adabu.


Mag3, S1 anayosema Mtanganyika ipo karibu sana na S2 kulikoS3.
Miaka50, S2 imekuwa mbali sana na S1 na anachokisema ni kujaribu kuficha rangi yake halisi kuwa ni muumini wa rasimu ya Chenge na Sitta.


Anafahamu ni madudu tu yametendeka, nafsi inamsuta hata akiwa kwenye keyboard peke yake.
Ili kuiosha nafsi anasema S1


Kuhusu Tanganyika, kwakweli mchakato mzima umewaamsha Watanganyikavizuri sana.
Leo wanatambua kitumbua chao kilichowekwa rehani.


Ni suala la muda mfupi sana, ima muungano utavunjika kabisana kama utakuwepo kuna mambo mawaili.
1)Wznz kuishi kwa mashaka Tanganyika, kwasababu Watanganyika wamejua wznz ni kupena mzigo kwao.


2)Wznz watabaki na rasimu au katiba ya Chenge wakiwa raia daraja la II, nawataendelea kudhalilika vizuri sana.


Hivi hata leo kuna mznz gani anaweza kuongelea muunganoWatanganyika wakamuona wa maana au kumsikiliza
Wznz hawatasikilizwa hata leo kwasababu siyo, narudia siyowashirika wa muungano. Wao ni kupe waliong'ang'ania mgongoni mwa ng'ombe.

Watanganyikawameng'amua haya
1)Kwamba, znz haina mchango wa aina yoyote kwa maendeleo ya Tanganyika.

2) Kwamba znz ni mzigo mzito sana kwa uchumiwa Tanganyika
3)Kwamba, bila znz hakuna athari za aina yoyote kwa Mtanganyika
4)Kwamba, znz inategemea uwepo wa Tanganyika imara


Kwa maana hiyo, znz ni eneo tegemezi na hawana sifa ya kuwawashirika, bali kupe wa muungano.
Wznz watakuwa wamepoteza fursa wenyewe.

Laiti wangekubali S3, leo wangekaa na mshirika mwenza kwaheshima.
Hali inavyoonekana wamekubali kubaki chini ya kivuli cha Tanganyika.


Ni kivuli hicho ndicho kitakachowapa hadhi ya Raia daraja la II nchini Tangayika
Hawawezikuwa raia daraja la I kwasababu imedhihirika pasi na shaka, wznz ni tatizo


Hatari kubwa Zaidi, ni pale Watanganyika watakapoamua kudaichao.
Njia ya mkato ni kuondoa udhia, na hilo ninasikitika kusema litakuja kwa gharama za wazanzibar.
Just a matter of time.
 
Nguruvi3, Mchambuzi na Mag3, msitarajie watawajibu maswali yenu maana wengi wao ni watumwa wa mawazo ya katiba pendekezwa, watakachojitetea kikubwa hapa ni kwamba wanakinda Muungano uliosisiwa na baba wa taifa na Karume. Lakini wanasahau Time effect na kwamba ni lazima wabadilike na muda maana aina ya Muungano tulionao haujatatua kero kwa miaka karibu 50, je hawaoni ni busara kusoma alama za nyakati na kukubaliana na mabadiliko ili kuulinda huu muungano kama kweli tunautaka??

Watu hawa unawashangaa wanajifanya wanaenzi muungano wa kale na hawataki kuubadilisha pamoja na kwamba nyakati zinawalazimisha, mfano nyumba za zamani za tembe na kuezekwa majani watu sasa wanaziacha na kuanza kujenga nymba zinazoendana na muda, wao bado wanasema nyumba za tembe tuzitumie hata kama zinavuja maana nikuenzi muungano.

Kuhusu gharama za serikali tatu hawasemi tena maana wanajua madudu na utitiri wa viongozi waliowaweka, ni aibu tu kwa watetezi ya rasimu hii ya CCM na ni mzigo mzito kwa Watanganyika than ever before
 
King Suleiman, Mag3, Nguruvi3,

Ningependa kujadili hoja zenu kwa pamoja.

Kero za muungano ambazo rais Kikwete juzi Alitamka Kwamba sasa zimeondolewa, kero hizi zimekuwepo kwa miaka 50 sasa, yani tangia kuundwa kwa taifa letu la "Tanzania". Hakuna Ukweli wowote Kwamba rasimu ya Mafichoni ya CCM imezitatua. Mfumo wa serikali Mbili umetumika kwa miaka 50 sasa, lakini Tazama idadi ya manung'uniko, malalamiko na hata hujuma za kuvunja muungano.

Hata rais alikiri Katika hotuba yake bungeni Wakati wa kuzindua BLK Kwamba - kuna utata mwingi kwenye mjadala wa suala la "Zanzibar ni nchi kamili inayojitegemea au ni sehemu ya jamhuri ya muungano". Cha ajabu ni Kwamba, Wakati wa makabidhiano ya rasimu ya mafichoni juzi, rais wa Zanzibar dr shein akatamka Kwamba "Zanzibar ni sehemu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania", jamani, what's going on??? Ina maana hata shein hajui Kwamba katiba aliyoapa kuilinda Kule Zanzibar inatamka Kwamba Zanzibar ni "nchi"????

Kina Sitta, lukuvi, Wassira, Chenge, migiro, na hata marais Kikwete na shein, hawa wote ni wanachama wa CCM. Na wanajua Kwamba ibara ya (1) ya mkataba wa muungano (1964) Inasema kuwa - jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya Watu wa Zanzibar zinaungana na kuwa nchi moja yenye mamlaka ya Kidola. Ibara ya (1) ya katiba ya muungano Inasema Kwamba "jamhuri ya muungano wa Tanzania ni nchi moja", lakini mabadiliko ya katiba Zanzibar (2010) yanaitambua Zanzibar Kama nchi kamili ndani ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Lakini sio hivyo tu, ndani ya mabadiliko hayo, Zanzibar imekuwa nchi huru, imejiundia bendera yake, Wimbo wake wa taifa, Ina mihimili yake mitatu kamilifu - serikali, bunge, Mahakama, kwa Mujibu we katiba yake ili itambulike kuwa ni nchi kamili. Kwanini CCM wanataka kuchezea Watu akili?

Kuzima hoja ya serikali Tatu kwa namna wanavyofanya muda sio mrefu kutaufanya upande wa pili wa muungano Kuhoji nini kinaendelea. Tume ya jaji warioba ilifanya kazi nzuri sana ya kujaribu kutegua bomu hili. Katiba ya Zanzibar inaunda majeshi kwa Mwamvuli wa "idara maalum za serikali ya mapinduzi ya Zanzibar". Majeshi hayo yapo Katika ibara ya 12 ya katiba ya Zanzibar. Kitendo Hiki ni Kinyume cha katiba ya JMT ambayo inapiga marufuku mtu yoyote au shirika lolote au kikundi chochote kuunda na kuweka jeshi nchini/ndani ya JMT. Kwa maana hii, ni Wakati Rasmi sasa kwa CCM kuacha kutumia jina la mwalimu nyerere na mzee karume kutetea Mfumo wa muungano kwa Mujibu wa rasimu ya CCM ya mafichoni kwani Malengo ya serikali Mbili kwa nchi moja yalishakufa siku nyingi na kuzikwa pamoja na waasisi wa muungano. Ni taahira tu ndiye anayeweza kukubali Kwamba unaweZa kuwa na serikali Mbili Katika nchi Mbili. Ndani ya nchi Mbili AMA kuna serikali moja au serikali Tatu, basi!

Hoja Kwamba Kitendo cha Tanzania bara kuvaa koti la muungano hivyo kujinufaisha binafsi au kutumia rasimali za Zanzibar haiwezi kuzimwa kwa kuipa Zanzibar "uhuru wa bandia" wa kujiamulia masuala yake. Vile vile Mgawanyo wa Mapato ya muungano na uchangiaji wa gharama za muungano Kati ya serikali ya muungano na serikali ya Zanzibar hakuwezi patiwa ufumbuzi kwa kuwaambia Raia wa nchi Jirani ya Zanzibar Kwamba sasa mna uhuru wa kukopa nje, Kujiunga na Jumuiya za kimataifa, kuagiza bidhaa na kuendesha uchumi wenu bila ya kupitia Tanzania bara. CCM inatakiwa ijiulize - je, inapopinga serikali Tatu na kuleta serikali Mbili zile zile za miaka 50, je sasa Zanzibar wataridhika na Hali hiyo? Hawataibua Madai Mapya kuhusu Zanzibar kuwa nchi kamili? Je kuna mamlaka kamili Zanzibar bila ya uwepo wa Tanganyika?

Je tuseme Zanzibar wakanyamaza, je upande wa Tanzania bara, wao hawatadai Tanganyika Yao? Je, Hali ya hewa ya kisiasa ya 1984 haitajirudia, Tena Wakati huu kwa kuvunja Kabisa muungano?

CCM wanatakiwa kukaa chini na kutafakari haya:

Chama kijiulize, kwanini viongozi wa Zanzibar wamebadili msimamo ghafla kutoka serikali Tatu na sasa Wanaunga Mkono serikali Mbili Wakati kitovu cha malalamiko dhidi ya serikali Mbili kwa miaka 50 ni za zibT na sio Tanganyika? Kwa akili ndogo tu, CCM Inabidi iamke na kutambua Kwamba wake wote waliokuwa wanapigia chapuo katiba inayopendekezwa ni waumini wa serikali Tatu, sio serikali Mbili. Nitafafanua:

• iwapo wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, basi wasingesema Kwamba Zanzibar ni nchi kamili ndani ya muungano. Dr shein hawezi kutamka Kwamba Zanzibar ni sehemu ya muungano akiwa nchini Zanzibar, hayo anayatamka akiwa kwenye ziara nje ya nchi yake Yani nchini Tanganyika Kama alivyofanya juzi Wakati wa kupokea katiba inayopendekezwa.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, baraza la wawakilishi lisingepitisha azimio la kutaka Mfumo wa serikali Tatu.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, baraza la wawakilishi lisingeamuru Kwamba Sheria zote zinazotungwa na bunge la muungano ni lazima zipitiwe kwanza na baraza la wawakilishi Kabla ya Sheria hizi kutumika Zanzibar.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, wasingevimega vitu vya pamoja vya muungano.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, wasingetaka wapate bendera Yao, majeshi Yao, Wimbo wao wa taifa pamoja na uraia.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, wasingesema Kwamba umaskini wa wazanzibari umesababishwa na muungano.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, wasingedai wapi kuna fedha, wapi kuna rasilimali, Mafuta, gesi, na wasingepanga mikakati ya kutumia rasilimali hizi na pia sekta ya utalii kwa manufaa ya wazanzibari.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, wasingedai mipaka ya Utawala Kati ya SMZ na serikali ya muungano.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, wasingefanya mabadiliko ya katiba Yao 2010 kufanya serikali ya muungano kuwa Kama mbia wa Zanzibar huku katiba ya JMT 1977 ikitamka wazi Kabisa Kwamba rais wa muungano ni mtawala hadi Zanzibar.

•iwapo viongozi wa Zanzibar wangekuwa kweli ni waumini wa serikali Mbili, wasingesema Kwamba Tanganyika imevaa koti la muungano, hivyo serikali inayotawala muungano ni serikali ya Tanganyika, huku serikali hii ikituhumiwa Kwamba inanufaika zaidi na rasilimali za pamoja.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Wakuu naomba mnisaidie maana nimechanganya kidogo, hivi kwa wananchi ili katiba ipite inahitaji 50% + au ni 2/3 (75%) kama ilivyokua bungeni??
Maana hata kama wananchi wengi hawana uelewa wa kutosha, kwa mchakato ulivyokwenda naona ugumu sana kupitishwa kwa katiba hii kihalali bila hila zozote

Kwa Mujibu wa rasimu ya Chenge ukiangalia ukurasa wake wa mwisho Inasema hivi:

"Mambo ambayo mabadiliko yake yanahitaji kuungwa Mkono kwa zaidi ya nusu ya kura halali zilizopigwa na wananchi wa Tanzania bara na zaidi ya nusu ya kura halali zilizopigwa na wananchi wa Tanzania Zanzibar Katika kura ya maoni":

1. Muundo wa muungano.
2. Uwepo wa serikali ya jamhuri ya muungano.
3. Kubadilisha masharti ya ibara ya 129(i)c ya katiba inayopendekezwa.

Kwahiyo mkuu Jibu umelipata, CCM imebadili formula iliyowekwa na tume ya jaji warioba, formula inayotumika duniani kote yani Robo Tatu, na kuweka formula Yao ya mafichoni ya 50.01%. CCM wanajua Kwamba Kupata two thirds ni Ngumu sio kwa Zanzibar tu, Bali hata kwa bara; uchakachuaji huu wa formula ukiachwa upite, rasimu ya CCM itapita. Wananchi wana haja ya kujua wanaenda kupigia nini kura, Kwamba wanapitisha pia formula ya kura ya maoni ambayo itakuja wanyonga Mbeleni.

Super majority (two thirds) ni muhimu sana Katika major issues Kama constitutional changes Vinginevyo simple majority (50.01%) italetwa matatizo makubwa sana muda sio mrefu;










Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kwa Mujibu wa rasimu ya Chenge ukiangalia ukurasa wake wa mwisho Inasema hivi:

"Mambo ambayo mabadiliko yake yanahitaji kuungwa Mkono kwa zaidi ya nusu ya kura halali zilizopigwa na wananchi wa Tanzania bara na zaidi ya nusu ya kura halali zilizopigwa na wananchi wa Tanzania Zanzibar Katika kura ya maoni":

1. Muundo wa muungano.
2. Uwepo wa serikali ya jamhuri ya muungano.
3. Kubadilisha masharti ya ibara ya 129(i)c ya katiba inayopendekezwa.

Kwahiyo mkuu Jibu umelipata, CCM imebadili formula iliyowekwa na tume ya jaji warioba, formula inayotumika duniani kote yani Robo Tatu, na kuweka formula Yao ya mafichoni ya 50.01%. CCM wanajua Kwamba Kupata two thirds ni Ngumu sio kwa Zanzibar tu, Bali hata kwa bara; uchakachuaji huu wa formula ukiachwa upite, rasimu ya CCM itapita. Wananchi wana haja ya kujua wanaenda kupigia nini kura, Kwamba wanapitisha pia formula ya kura ya maoni ambayo itakuja wanyonga Mbeleni.

Super majority (two thirds) ni muhimu sana Katika major issues Kama constitutional changes Vinginevyo simple majority (50.01%) italetwa matatizo makubwa sana muda sio mrefu;










Sent from my iPhone using JamiiForums



Thanks Mchambuzi,
nilikua nachanganyikiwa sana juu ya hilo maana from wht i knw nilikua najua ni 2/3 yaani majority na hata zanzibar katiba yao walipitisha kwa sheria hiyo ambayo umesema ndio standrds kwa nchinyi duniani, sasa kwa nn sisi iwe tofuti na kuna umuhimu gani wa 50%+ badala ya 2/3??

Sasa nimepata jibu kwa nn makada wa CCM na washirika wao wanasema kazi kubwa ilikua kupata akidi bungeni si kwa wananchi mtaani, kumbe kuna loophols za kuchakachua akidi wametengeza, kumbe wameshusha grades za kuipitisha hii katiba yao kijanja janja?? Maana kiuhalisia hata bara pamoja na mapungufu yetu 75% kuipata kwa namna mchakato ulivyokwennda. Ni kazi sana kuipata.

Maswali kwa nyie great thinkers sasa,
1. Sisi wanchi tusio na vyama (na basically ndio tutaumizwa zaidi kama kituko hiki kitapita) tunahitaji kufanya nini ili kuzuia huu uhuni usifanyike??

2. Kwa trend ya mahakama zetu kwa isu sensitive, je mahakama inaweza kuwa njia sahihi kupeleka shauri kutatua mzozo kuhusu kura halisi za kupitisha katiba??

3. Na je kuna haja ya kuvitegemea vyama vya siasa vitupiganie juu ya hili jambo ( maaana kiuhalisia strategies zao nyingi zimefeli na wamejikuta wakiuvaa mkenge kwa kucollude na serikali na kushindwa, Nguruvi 3 ameeleza sana kwenye nyuzi zake hasa za juice ya ikulu).

4. Generally mnashauri nini kifanyike ili kuokoa hali hii ambayo naamini hii katiba Imekosa uhalali kwa vitu vingi ambavyo mmevijadili kwa kina. kwa kweli wasicheze na akili zetu na kujua kuna watu wanaelewa wafanyao,
 
Mchambuzi na Mag3 Naomba nichangie hoja zenu kuhusu@Mtanganyika
@Mchambuzi , swali lako Mtanganyika hatalijibu, si kwakuwa hana jibu, anayo mengi.
Majibu yake yataharibu kazi aliyotumwa kuifanya.


Na nina ushahidi wa haya nisemayo.
1.Kilichomuondoa Jumbe Madarakani ni S3
2)Kundi la G55 lilitaka S3
3) Tume ya Nyalali ya chama kimoja ilitaka S3

4)Tume ya jaji kisanga ilitaka S3.

5)Tume ya awali ya Warioba, ilitaka S3.

6) Wazanzibar na wengine wakiwa ‘wamelawitiwa''madai yao ni S3
7) Seraza CUF ni S3

8)Sera za Chadema ni S3
9)Maoniya tume ya Warioba, pande zote ni S3.


Ndio maana Mag3 anasema wengeni wameamua kujitoa fahamu makusudi.
Niseme, hawajajitoa fahamu, wanazo, njaa inaweza kulazimisha mtu kusema asilotaka. Njaa haina adabu.


Mag3, S1 anayosema Mtanganyika ipo karibu sana na S2 kulikoS3.
Miaka50, S2 imekuwa mbali sana na S1 na anachokisema ni kujaribu kuficha rangi yake halisi kuwa ni muumini wa rasimu ya Chenge na Sitta.


Anafahamu ni madudu tu yametendeka, nafsi inamsuta hata akiwa kwenye keyboard peke yake.
Ili kuiosha nafsi anasema S1


Kuhusu Tanganyika, kwakweli mchakato mzima umewaamsha Watanganyikavizuri sana.
Leo wanatambua kitumbua chao kilichowekwa rehani.


Ni suala la muda mfupi sana, ima muungano utavunjika kabisana kama utakuwepo kuna mambo mawaili.
1)Wznz kuishi kwa mashaka Tanganyika, kwasababu Watanganyika wamejua wznz ni kupena mzigo kwao.


2)Wznz watabaki na rasimu au katiba ya Chenge wakiwa raia daraja la II, nawataendelea kudhalilika vizuri sana.


Hivi hata leo kuna mznz gani anaweza kuongelea muunganoWatanganyika wakamuona wa maana au kumsikiliza
Wznz hawatasikilizwa hata leo kwasababu siyo, narudia siyowashirika wa muungano. Wao ni kupe waliong'ang'ania mgongoni mwa ng'ombe.

Watanganyikawameng'amua haya
1)Kwamba, znz haina mchango wa aina yoyote kwa maendeleo ya Tanganyika.

2) Kwamba znz ni mzigo mzito sana kwa uchumiwa Tanganyika
3)Kwamba, bila znz hakuna athari za aina yoyote kwa Mtanganyika
4)Kwamba, znz inategemea uwepo wa Tanganyika imara


Kwa maana hiyo, znz ni eneo tegemezi na hawana sifa ya kuwawashirika, bali kupe wa muungano.
Wznz watakuwa wamepoteza fursa wenyewe.

Laiti wangekubali S3, leo wangekaa na mshirika mwenza kwaheshima.
Hali inavyoonekana wamekubali kubaki chini ya kivuli cha Tanganyika.


Ni kivuli hicho ndicho kitakachowapa hadhi ya Raia daraja la II nchini Tangayika
Hawawezikuwa raia daraja la I kwasababu imedhihirika pasi na shaka, wznz ni tatizo


Hatari kubwa Zaidi, ni pale Watanganyika watakapoamua kudaichao.
Njia ya mkato ni kuondoa udhia, na hilo ninasikitika kusema litakuja kwa gharama za wazanzibar.
Just a matter of time.

Siku zote mtu ukiwa nje ya game utaongea meeeeeeeengi sana lakin ukiingia ndani ya game UNAUFYATA kama alivyoufyata Mh Keissy au ukuliona hiloooooo?

Mimi naamini hata wewe ungekuwa pale mjengoni Dodoma ungeipigia katika ile kura ya ndio kwa ibara zoooote kama alivyofanya mshirika wako Mh Keissy.

Ok all in all kama wa TGk wameyagundua hayo sasa zamu yao kufanya maamuzi katika kisanduku cha kura kuikataa KAMA watavyoinyonga kule Znz.

Siku zooote njia ya muongo ni fupi sana. Tuvute subra na kuomba umri na kheir tutayaona meeengi.

Pole sana

 
HISIA ZAJITOKEZA, UTAIFA WATAWALA ''WATANGANYIKA WAKITOA YA MOYONI HAPAKALIKI' WAZANZIBAR WATAWANYIKA, HAWANA KAULI, SASA NGUMI MKONONI
SEHEMU YA I

Ndugu wanaduru Bunge la katiba la CCM au Samwel Sitta linaendelea kwa kuunga unga, likipoteza mvuto maana na thamani. Wajumbe wameacha kazi aliyodai wanaifanya, sasa wageuza ukumbi eneo la mipasho dhidi ya UKAWA

Jitihada za kutoa zawadi ili kuungwa mkono zinaendele. Mwenyekiti Sitta akiahidi kutumia pesa za umma kama mali yake, vifungu nyeti kama cha 1 na 6 vikiwekwa pembeni ili kujadili vile venye mvuto hasa wa kupendeza wazanzibar

Kila kifungu kimejadiliwa kkidhi haja za Wazanzibar ili mradi 2/3 ya nguvu ipatikane. Vifungu ambavyo ni moyo wa katiba vimewekwa kiporo kuchelea Unyeti ''sensitivity' kulivunja bunge la CCM bila UKAWA au jambo jingine.

SINTOFAHAMU ILIANZA SIKU NYINGI

Wazanzibar waliondoka kwao na msimamo wa S3, msimamo uliosimamia mambo mengi yakiwemo kuvunja katiba, kuondoa mambo ya muungano, kupunguza madaraka ya rais wa JMT visiwani n.k.

Ni haki kusema bila kujali CCM au CUF msimamo wa S3 ni wao. Hata kura za maoni ikiwemo maoni ya tume yanaeleza hivyo.

Hulka ya wazanzibar ni wamoja kwa baadhi ya nyakati, lakini huwa wamoja zaidi dhidi ya 'adui' yao Tanganyika. Wznz hukumbwa na kihoro wanapotoka znz. Waliofika Dodoma, umoja wa S3 ukatawanyika. Pandu kificho akisema hakuwemo, waziri wa sheria akilalamika 'tulikubaliana'

UMOJA KATIKA UNAFIKI

Umoja wa wazanzibar una aina za unafiki. Kama tulivyosema, kuvunjika kwa msimamo wa S3 ni dalili moja.

Kujitoa kwa mwanasheria mkuu katika kamati ya uandishi wa katiba ya Sitta, nao unawakilisha unafiki. Maana yake, wapo wanaoamini maafikiano yao kabla, wanaoamini S3 na mkataba bila kujali mrengo wa kisiasa,kwa pamoja hawawezi kusema. Wapo UKAWA wanaosema na CCM wanaotetea mfumo uliopo.

Unafiki una mizizi,ni wznz wanaosema Tanganyika imewageuza koloni, wananyonywa, wanaibiwa na wanateseka ndani ya muungano,waasisi wa muungano wakitukanwa hadharani. CUF wakimshambulia Karume kwa ukatili, CCM&CUF wakimzodoa Nyerere laana .

Ni Wazanzibar wanaodai muungano hauna faida, laiti ingekuwepo nchi za jirani zingeshajiunga Na ni wazanzibar wanaodai, muungano umefunga fursa zao za kukigeuza kisiwa chao kuwa 'pepo' ya Afrika. Madai hayo yakiwemo matusi yanapotolewa, hakuna kiongozi wa CCM au CUF anayesimama kukemea.

Tena wapo wanaorudia maneno kama Nyerere! ilimradi wanazi wao waitikie Laanatullah Hakujatokea kiongozi yoyote kusimama na kukemea dhihaka na kejeli hizo. Leo wanapotokea wazanzibar wakitetea muungano eti kumuenzi Nyerere, duru hatuelewi ni unafiki wa kiwango gani. Kutokana na kutoelewana au kuelewa wanachokizungumzia, hamkani si shwari tena kwa upande wao

Inaendelea sehemu ya II...

Nguruvi3,

Acha kunung'unika mtoto wa kiume wewe. Mbona unatia aibu hivyo.

Siku zote njia ya muongo ni fupi sana NAWE NAFIKIRI UNAJIBARAGUZA HIVI SASA.

Mimi nilifikiri utamlaumu swahiba wako Mh Keissy aliposimama na kupiga kura yake ya wazi kwa kuzikubali ibara zooote kwa kura ya NDIO bila kufikiria matamko yake ya awali.

Na mara nyingi sana wewe hapa barzani ulikuwa ukimtumia kama mfano wa kuigwa JE UMEYAONA WATGK WENZAKO WALIVYO ...

BINAFSI NAPENDA KUKUPA POLE kwani yooote unayolalama upande wa Znz wameyaona na ndio maana ilikuwa kizaazaa pale mjengoni kupata 2/3 ya kura za ndio kutoka Znz. LAKIN KWA UPANDE WA BARA ilikuwa kama kumsukuma mlevi.

Mimi naamini hata wewe pamoja na kunung'unika kwako ungekuwa ni mmoja wa mbunge wa BLK hilo basi ungepiga kura ya wazi kama Mh Keissy mtu wa mfano kwako na kuvipitisha cifungu vyote kwa kura ya Ndio.

Acha kujibaraguza hapa barzani kwa kusema waZnz kwani wao ni mfano wa kuigwa kwa misimamo yao tena mchana kweupeeeeee na ugenini huko DODOMA.

Nakupa akiba ya maneno hapa. ITAKUWA KIZAAZAA KUPATA 2/3 YA KURA YA NDIO KWA ZNZ lakin KURA HIZO ZA KUPITISHA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA NA BLK la Mh Sitta itakuwa kama kumsikuma mlevi kwa upande BARA.

Sijui kama utaweza kubisha hilo.

WAACHWE ZNZ WAPU
MUEEEEE. ZNZ HURU ILEEEEEEEEEEEEEEEE.
 
Nguruvi3,

Acha kunung'unika mtoto wa kiume wewe. Mbona unatia aibu hivyo.

Siku zote njia ya muongo ni fupi sana NAWE NAFIKIRI UNAJIBARAGUZA HIVI SASA.

Mimi nilifikiri utamlaumu swahiba wako Mh Keissy aliposimama na kupiga kura yake ya wazi kwa kuzikubali ibara zooote kwa kura ya NDIO bila kufikiria matamko yake ya awali.

Na mara nyingi sana wewe hapa barzani ulikuwa ukimtumia kama mfano wa kuigwa JE UMEYAONA WATGK WENZAKO WALIVYO ...

BINAFSI NAPENDA KUKUPA POLE kwani yooote unayolalama upande wa Znz wameyaona na ndio maana ilikuwa kizaazaa pale mjengoni kupata 2/3 ya kura za ndio kutoka Znz. LAKIN KWA UPANDE WA BARA ilikuwa kama kumsukuma mlevi.

Mimi naamini hata wewe pamoja na kunung'unika kwako ungekuwa ni mmoja wa mbunge wa BLK hilo basi ungepiga kura ya wazi kama Mh Keissy mtu wa mfano kwako na kuvipitisha cifungu vyote kwa kura ya Ndio.

Acha kujibaraguza hapa barzani kwa kusema waZnz kwani wao ni mfano wa kuigwa kwa misimamo yao tena mchana kweupeeeeee na ugenini huko DODOMA.

Nakupa akiba ya maneno hapa. ITAKUWA KIZAAZAA KUPATA 2/3 YA KURA YA NDIO KWA ZNZ lakin KURA HIZO ZA KUPITISHA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA NA BLK la Mh Sitta itakuwa kama kumsikuma mlevi kwa upande BARA.

Sijui kama utaweza kubisha hilo.

WAACHWE ZNZ WAPU
MUEEEEE. ZNZ HURU ILEEEEEEEEEEEEEEEE.


barubaru, kwa mtazamo wangu wazanzibar ndio wenye tatizo hilo la unafiki kuliko wabara, wao wakiwa Zenji watakuambia ni nchi kamili na wengi wanataka NKataba, wakivuka maji tu kuja nchi jirani ya Tanganyika watakuambia Zanzibar sio nchi ni sehem ya JMT, mfano halisi hata raisi wao kauonyesha juzi wakati wa makbidhiano ya rasimu ya CCM pale Dodoma, katamka wazi Zanzibar ni sehem ya JMT na sio nchi, kiukweli Zanzibar inaihitaji zaidi Tanganyika than Tang. Needs Zanzibar.

Tatizo la Watanganyika ambalo basically ndio linawatesa ni uoga wao kulidai jina la Tanganyika kwa uhuru na kuongea wazi kwamba tunaotaka kupumua ni Watanganyika maana nchi jirani ya Zenji wanatutegemea na kutunyonya kwenye mengi kuanzia Kiuchumi, ulinzi, Elimu na mengi neyo.
 
barubaru, kwa mtazamo wangu wazanzibar ndio wenye tatizo hilo la unafiki kuliko wabara, wao wakiwa Zenji watakuambia ni nchi kamili na wengi wanataka NKataba, wakivuka maji tu kuja nchi jirani ya Tanganyika watakuambia Zanzibar sio nchi ni sehem ya JMT, mfano halisi hata raisi wao kauonyesha juzi wakati wa makbidhiano ya rasimu ya CCM pale Dodoma, katamka wazi Zanzibar ni sehem ya JMT na sio nchi, kiukweli Zanzibar inaihitaji zaidi Tanganyika than Tang. Needs Zanzibar.

Tatizo la Watanganyika ambalo basically ndio linawatesa ni uoga wao kulidai jina la Tanganyika kwa uhuru na kuongea wazi kwamba tunaotaka kupumua ni Watanganyika maana nchi jirani ya Zenji wanatutegemea na kutunyonya kwenye mengi kuanzia Kiuchumi, ulinzi, Elimu na mengi neyo.
Wanaotaka Tanganyika ni wachache zaidi ya ambao hawajali uwepo wake. Watanzania bara wengi hawajali haya mambo ya serikali tatu kama mnavyoaminishwa.
 
Mtaendelea kuyaita "uongo" Yale yote ambayo fahamu zikiwarudia huwa mnaona Kwamba kumbe hayafai.

Ni hivi - hoja ya kuwepo kwa baraza la wawakilishi la Tanzania bara litakaloshughulikia masuala ya Tanzania bara chini ya Mfumo wa muungano wa serikali Mbili, hata ziboreshwe vipi, ni Jambo ambalo lisingewezekana. Hatua yenu ya kujaribu kuja na mkakati wa kuzuia wabunge kutoka visiwani kushiriki mjadala usio husu mambo ya muungano ingekuwa ni kuchochea tu mgogoro. Hii ni kwa sababu mmepata ufahamu na Kugundua Kwamba hakuna "mambo ya Tanzania bara peke yake" yatakayopatikaba chini ya Mfumo wa serikali Mbili hata mkiziboresha vipi, mwisho wake kutakuwa na mambo ya Zanzibar na mambo ya muungano tu, kwisha.

Mlipopata fahamu mkagundua Kwamba ndani ya serikali Mbili, hauwezi kuwa na bunge la Tanzanka bara na bado Mkazunguka kwa wananchi na katiba mnayopendekeza Kwamba bunge Hilo litakuwa ni la wananchi. Ndani ya serikali Mbili hata mziboreshe namna gani hakuwezi kuwa na msimamizi wa mambo ya Tanzania bara kwa sababu serikali ya kufanya hivyo ni serikali ya Tanganyika ambayo hamuitaki licha ya wananchi kuzidi kuitaka. Fahamu zenu zikarudi na mnaona kuleta Bunge la Tatu ndani ya serikali Mbili - hakuna atakayewajibika pale aliyeagizwa atashindwa kutekeleza alichoagizwa.

Fahamu zilipowarudia, mmegundua Kwamba duniani kote, bunge ni moja ya mihimili mitatu ya dola, mingine ikiwa ni Mahakama na serikali. Mligundua Kwamba hakuwezi kuwepo mabunge mawili ndani ya bunge la muungano - bunge la TANZANIA bara bila ya kuwepo baraza la mawaziri la Tanzania bara, bila rais au waziri mkuu.

Na kuhusu hoja yako nyingine hapo juu kuhusu uwepo wa marais Saba, hoja ambayo imezurura zurura bila
tija, hoja ya Kujibu ambayo mlikuwa mpo busy bungeni mkipotosha umma huku pia kina nape wakizunguka nchi nzima kuijenga ni Kwamba nanukuu:

"Serikali Tatu ni kuongeza gharama na kuifanya nchi kuwa na marais watatu, suala ambalo pia litaleta mgongano wa madaraka".

Je marais Saba ndani ya serikali Mbili ni nafuu zaidi kwa walipa kodi kuliko mapendekezo ndani ya rasimu ya tume? Je, marais Saba hakutaleta mgongano wa madaraka?



Sent from my iPhone using JamiiForums
Katiba ya uvunguni uliyoielezea wewe msingi wake ulikuwa ni mabunge matatu. Hilo ndiyo jambo pekee lililobeba mada yako, labda ungerudi ukasoma ule uzi.

Kuhusu gharama za muungano wa serikali 3 vis a vis serikali mbili, mimi nimekukaribisha mara nyingi sana twende kwenye numbers na matokeo yake ni wewe kukimbia na kutoa ahadi bila kuzitekeleza na bila kuona aibu kuwa uliwahi kuahidi.

Hilo jambo limekushushia heshima na ndiyo maana mara kwa mara nakuita muongo kwa sababu hii.

Gharama za serikali siyo idadi ya maraIsi bali uendeshaji mzima wa serikali tatu na bureaucracies zake. Hilo unalijuwa ila kwa sababu mind yako ishakuwa corrupted, basi inabidi ushikilie vistatements ambavyo havina ueledi.

Hao marais saba ni uongo na ni very shallow thinking kwa sababu walikuwepo tangu enzi za katiba ya '84 na ni madaraka tu ndiyo yaliyobadilika.

Hakuna marais saba ambao wote wana executive branches na mahakama zao. Kuna executive branches mbili na mahakama mbili na mabunge mawili. Hakuna marais saba, acha uongo na upotoshaji kwa sababu kiaina Fulani huo ni wizi na ufujaji wa hela za wananchi waliokusomesha.

STOP IT!
 
Ndugu Mchambuzi

Kama ni suala la porojo za kisiasa unaweza kushika namba moja kwenye jukwaa la siasa. Kwa watu wasiofahamu siasa za Tanzania, ninatumaini wanazinunua sana porojo zako za kisiasa.

Siyo muda mrefu ulidai una documents za Rasimu ya Katiba uliyokuwa unadai ya mfukoni ya CCM na pia una audio za wajumbe wa Kamati Kuu na NEC wakijadiliana kuhusu Rasimu ya Katiba uliyokuwa unaita ya mfukoni katika thread hii,

https://www.jamiiforums.com/katiba-...ili-zilizoboreshwa-na-hatima-ya-muungano.html

Tulikuomba utuwekee hapa hizo documents and audio ili kutimiza Jf Motto inayosema We Dare Talk Openly lakini ukaingia 'mitini'.

Uliibuka hapa Jf na maelezo haya,
Pamoja na Muungano sasa kuwa na Nchi MBILI, SERIKALI MBILI, CCM bado inasema kwamba serikali mbili hizi “zitaziboreshwa”, huku chama kikipendekeza kwamba – katika katiba ijayo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano (ambae leo hii ni Dr. Bilal), anyang’anywe mamlaka aliyokuwa nayo ya kuwa msaidizi mkuu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, na badala yake, mamlaka hayo yahamie kwa Rais wa nchi jirani ya “Zanzibar”. Kwa maana nyingine, chini ya serikali mbili “zilizoboreshwa” na CCM, Rais wa nchi jirani ya “Zanzibar” atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa Rais wa Muungano kwa masuala ya Zanzibar, lakini pia atakuwa ni mmoja wa viongozi wakuu wa nchi (Tanzania). CCM haisemi lolote kuhusu kiongozi atakayekuwa msaidizi wa Rais wa Muungano katika masuala ya Tanganyika (ukipenda, sema - Tanzania Bara).

Hukuishia hapo, ukaamua pia kuja na hoja hii,
Katika maboresho yake ya serikali mbili, CCM inapendekeza kuwepo Kwa MABUNGE MATATU (chini ya serikali mbili), kwa kuongeza Bunge la tatu litakaloitwa “Baraza La Wawakilishi la Tanzania Bara”. Jukumu la chombo hiki litakuwa ni kusimamia masuala ya Tanzania Bara pekee, tofauti na sasa ambapo masuala haya yanasimamiwa na Bunge la Muungano ambalo, wabunge kutoka nchini jirani ya Zanzibar pia ni sehemu ya bunge hili la Muungano. CCM inapendekeza kwamba – wakati Bunge la Muungano litakapo kuwa linajadili mambo ya muungano, wabunge wote – kutoka Tanzania Bara na nchi jirani ya Zanzibar, watashiriki katika majadiliano. Lakini pale mijadala juu ya masuala ya Tanzania bara pekee itakapoanza, wabunge kutoka Zanzibar hawataruhusiwa kushiriki katika mijadala hiyo. Kwa maana nyingine, mijadala juu ya “Tanzania Bara” itakapoanza ndnai ya Bunge, hii itawapa Wabunge kutoka nchi jirani ya Zanzibar, fursa ya - nikiazima maneno ya Nguruvi3, “KUTALII”.
Mtu ambaye ni Muungwana angeomba msamaha kwa kuwalisha wanaJf ''matango pori'' lakini badala yake, bado unakuja na porojo kama kawaida!.

You should apologise to Jf Members!
 
Thanks Mchambuzi,
nilikua nachanganyikiwa sana juu ya hilo maana from wht i knw nilikua najua ni 2/3 yaani majority na hata zanzibar katiba yao walipitisha kwa sheria hiyo ambayo umesema ndio standrds kwa nchinyi duniani, sasa kwa nn sisi iwe tofuti na kuna umuhimu gani wa 50%+ badala ya 2/3??

Sasa nimepata jibu kwa nn makada wa CCM na washirika wao wanasema kazi kubwa ilikua kupata akidi bungeni si kwa wananchi mtaani, kumbe kuna loophols za kuchakachua akidi wametengeza, kumbe wameshusha grades za kuipitisha hii katiba yao kijanja janja?? Maana kiuhalisia hata bara pamoja na mapungufu yetu 75% kuipata kwa namna mchakato ulivyokwennda. Ni kazi sana kuipata.

Maswali kwa nyie great thinkers sasa,
1. Sisi wanchi tusio na vyama (na basically ndio tutaumizwa zaidi kama kituko hiki kitapita) tunahitaji kufanya nini ili kuzuia huu uhuni usifanyike??

2. Kwa trend ya mahakama zetu kwa isu sensitive, je mahakama inaweza kuwa njia sahihi kupeleka shauri kutatua mzozo kuhusu kura halisi za kupitisha katiba??

3. Na je kuna haja ya kuvitegemea vyama vya siasa vitupiganie juu ya hili jambo ( maaana kiuhalisia strategies zao nyingi zimefeli na wamejikuta wakiuvaa mkenge kwa kucollude na serikali na kushindwa, Nguruvi 3 ameeleza sana kwenye nyuzi zake hasa za juice ya ikulu).

4. Generally mnashauri nini kifanyike ili kuokoa hali hii ambayo naamini hii katiba Imekosa uhalali kwa vitu vingi ambavyo mmevijadili kwa kina. kwa kweli wasicheze na akili zetu na kujua kuna watu wanaelewa wafanyao,

Refferrendums nyingi hupitishwa by simple majority. Kama wananchi wanapiga kura ya kumchagua rais, ni asilimia ngapi inahitajika?

Mabunge mengi hutumia super majority kwa sababu uwakilishi siyo njia direct ya kujua wananchi wanataka nini ila ni njia rahisi. Kwa mfano,wabunge wa Zanzibar waliopiga kura ya ndiyo, haimaanishi kuwa wakazi wa majimbo yao walitaka wapige kura ya ndiyo. Ndiyo maana it's safer kutumia supermajority.

Sababu nyingine ya wawakilishi kutakiwa super majority ni tofauti kati ya idadi ya watu, ndiyo maana utaona jimbo kama la Kawe na Ubungo ambayo wawakilishi wake wangepigia kura ya hapana na ni wengi kuliko jimbo la Kiembesamaki ambalo mwakilishi wake kapiga kura ya ndiyo watakuwa wameonewa.Hivyo super majority inasaidia ku-neutralize vitu kama hivyo.

Kwa United States kwa mfano, lower house ambayo representation yake per capita ni kubwa kuliko Senate, inatumia simple majority na Senate inatumia super majority au kwa maneno mengine, ni simple majority iliyo vulnerable to filibuster kwa hiyo ili isipigwe filibuster huwa wana-prefer super majority 60%.

Kama unata kufahamu niulize mimi, usimuulize mtu kama Mchambuzi kwa sababu watakupotosha kutokana na minds zao kuwa corrupted already. Yaani tushawapoteza.
 
Last edited by a moderator:
Wanaotaka Tanganyika ni wachache zaidi ya ambao hawajali uwepo wake. Watanzania bara wengi hawajali haya mambo ya serikali tatu kama mnavyoaminishwa.

Umerudi baada ya kukimbia hoja za asilimia 21 na 4.5 usizona majibu nazo. Watanganyika wengi sana wanajua sasa hivi jinsi muunganoulivyo mzigo kwao na jinsi znz inavyorumia jina la Tanzania kuongeza mzigowasopaswa kuubeba.

Sasa hivi unakimbilia trivial argument unaacha maswalimuhimu sana.

Pamoja na hayo mawili hapo juu, tumekuuliza uonyeshe punguzo lagharama kwa rasimu yenu wewe, Mkandara, Sitta na Chenge. Huna jibu.

Wewe kama Mkandara, hamtaki jina Tanganyika kwasababu litaondoaa utegemezi wa znz kwa Watanganyika.
Kwasasa ni too late, Tanganyikaiwepo iswepo wazanzibar ni raia wa daraja la II Tanzania. Mtanganyika ndiye Mtanzania.

Wewe na Mknadara mnachotetea si muungano, it is another primitivereasons ,mnazijua na kwa unafik ihamsemi.

Mkandara alisawahi kusema kwa bahati mbaya mara 2(nukuu zipo) siku akija vema tutavuta na kumwanika.
Umerudi baada ya kukimbia hoja za asilimia 21 na 4.5 usizona majibu nazo.

Watanganyika wengi sana wanajua sasa hivi jinsi muunganoulivyo mzigo kwao na jinsi znz inavyorumia jina la Tanzania kuongeza mzigowasopaswa kuubeba.

Sasa hivi unakimbilia trivial argument unaacha maswalimuhimu sana.
Pamoja na hayo mawili hapo juu, tumekuuliza uonyeshe punguzo lagharama kwa rasimu yenu wewe, Mkandara, Sitta na Chenge. Huna jibu.

Wewe kama Mkandara, hamtaki jina Tanganyika kwasababulitaondoaa utegemezi wa znz kwa Watanganyika.
Kwasasa ni too late, Tanganyikaiwepo iswepo wazanzibar ni raia wa daraja la II Tanzania. Mtanganyika ndiyeMtanzania

Tunaendelea na elimu, ipo siku ukweli utadhihiri hukomitaani! Hapo ndipo mtajua kumbe Watanganyika ni wengi.
 
Umerudi baada ya kukimbia hoja za asilimia 21 na 4.5 usizona majibu nazo.
Watanganyika wengi sana wanajua sasa hivi jinsi muunganoulivyo mzigo kwao na jinsi znz inavyorumia jina la Tanzania kuongeza mzigowasopaswa kuubeba.
Sasa hivi unakimbilia trivial argument unaacha maswalimuhimu sana. Pamoja na hayo mawili hapo juu, tumekuuliza uonyeshe punguzo lagharama kwa rasimu yenu wewe, Mkandara, Sitta na Chenge. Huna jibu.
Wewe kama Mkandara, hamtaki jina Tanganyika kwasababulitaondoaa utegemezi wa znz kwa Watanganyika. Kwasasa ni too late, Tanganyikaiwepo iswepo wazanzibar ni raia wa daraja la II Tanzania. Mtanganyika ndiyeMtanzania.


Wewe na Mknadara mnachotetea si muungano, it is another primitivereasons ,mazijua na kwa unafik ihamsemi. Mkandara alisawahi kusema kwa bahati mbaya mara 2(nukuu zipo) siku akija vema tutavuta na kumwanika.
Umerudi baada ya kukimbia hoja za asilimia 21 na 4.5 usizona majibu nazo.


Watanganyika wengi sana wanajua sasa hivi jinsi muunganoulivyo mzigo kwao na jinsi znz inavyorumia jina la Tanzania kuongeza mzigowasopaswa kuubeba.


Sasa hivi unakimbilia trivial argument unaacha maswalimuhimu sana. Pamoja na hayo mawili hapo juu, tumekuuliza uonyeshe punguzo lagharama kwa rasimu yenu wewe, Mkandara, Sitta na Chenge. Huna jibu.


Wewe kama Mkandara, hamtaki jina Tanganyika kwasababulitaondoaa utegemezi wa znz kwa Watanganyika. Kwasasa ni too late, Tanganyikaiwepo iswepo wazanzibar ni raia wa daraja la II Tanzania. Mtanganyika ndiyeMtanzania.


Wewe na Mknadara mnachotetea si muungano, it is another primitivereasons .


Kwasasa hamna majibu, mume umbuka. Suala la gharama out,hamjui 21 ya ajira inapatikanaje, 4.5 ya mapato ya Tanganyika kwanini ipewe znzn.k.


Tunaendelea na elimu, ipo siku ukweli utadhihiri hukomitaani! Hapo ndipo mtajua kumbe Watanganyika ni wengi.




Kwasasa hamna majibu, mume umbuka. Suala la gharama out,hamjui 21 ya ajira inapatikanaje, 4.5 ya mapato ya Tanganyika kwanini ipewe znzn.k.
Tunaendelea na elimu, ipo siku ukweli utadhihiri hukomitaani! Hapo ndipo mtajua kumbe Watanganyika ni wengi.
Siku zote huwa unazusha kuwa mimi nakukimbia, mimi siwezi kumkimbia mtu pointless kama wewe. Na nimeshakujibu kuhusu 4.5% mara nyingi tu.

It's based on population i.e wazanzibari ni 4.5% ya watanzania. Na kimadaraka ni 20% ya Tanzania i.e 5 regions out of 25 regions. Ndiyo maana Warioba alipendekeza bunge la Muungano liwe hivyohivyo ... GOT IT NOW?
 
Refferrendums nyingi hupitishwa by simple majority. Kama wananchi wanapiga kura ya kumchagua rais, ni asilimia ngapi inahitajika?
Mabunge mengi hutumia super majority kwa sababu uwakilishi siyo njia direct ya kujua wananchi wanataka nini ila ni njia rahisi. Kwa mfano,wabunge wa Zanzibar waliopiga kura ya ndiyo, haimaanishi kuwa wakazi wa majimbo yao walitaka wapige kura ya ndiyo. Ndiyo maana it's safer kutumia supermajority.
Sababu nyingine ya wawakilishi kutakiwa super majority ni tofauti kati ya idadi ya watu, ndiyo maana utaona jimbo kama la Kawe na Ubungo ambayo wawakilishi wake wangepigia kura ya hapana na ni wengi kuliko jimbo la Kiembesamaki ambalo mwakilishi wake kapiga kura ya ndiyo watakuwa wameonewa.Hivyo super majority inasaidia ku-neutralize vitu kama hivyo.
Kwa United States kwa mfano, lower house ambayo representation yake per capita ni kubwa kuliko Senate, inatumia simple majority na Senate inatumia super majority au kwa maneno mengine, ni simple majority iliyo vulnerable to filibuster kwa hiyo ili isipigwe filibuster huwa wana-prefer super majority 60%.
Kama unata kufahamu niulize mimi, usimuulize mtu kama Mchambuzi kwa sababu watakupotosha kutokana na minds zao kuwa corrupted already. Yaani tushawapoteza.

Yeye hakuataka kujua ya Marekani. Alichotaka kujua sheria yamchakato wa Tanzania inasema nini kuhusu hilo. Wala hakutaka ufafanunuzi.Unatakiwa uelewe swali, ni sehemu muhimu sana ya mtihani. Na wengi wanafelikwasabau hiyo.

Halafu unasema watu wakuulize, mbona wamekuuliza umekimbiamara 3. Hebu tuambie 21% ya ajira za Tanganyika wanazopewa wznz ni kutokana navigezo gani. Pili, 4.5% ni kutokana na vigezo na formula gani na Tatu, je hiirasimu yenu na Chenge imejibu suala la gharama za S3?
 
Siku zote huwa unazusha kuwa mimi nakukimbia, mimi siwezi kumkimbia mtu pointless kama wewe. Na nimeshakujibu kuhusu 4.5% mara nyingi tu. It's based on population i.e wazanzibari ni 4.5% ya watanzania. Na kimadaraka ni 20% ya Tanzania i.e 5 regions out of 25 regions. Ndiyo maana Warioba alipendekeza bunge la Muungano liwe hivyohivyo ... GOT IT NOW????

Anachronism, hakuna kitunkama population. Hakuna mtu awewaziri au katibu mkuu anayejua hasa kwanini 4.5. Hili si jibu na inaonyeshaulivyo out of touch. Hapo ndipo tulisubiri uingie na sasa subiri utaumbuliwa.

Kwa ufupi wznz hawajui kwanini 21% na wala 4.5%. AliulizwaAboud, Duni na wengine akiwemo Alli. Hakuna aliyekuja na jibu. Mwigulu Nchembaanajua hakuna jibu na kama lipo nimemwalika aje hapa.

Kuna kitu kinaitwa Bernett formula kule England. Kipo wazi
hakina population wala ubabaishaji. Huwezi kutumia population kufikia hatima hiyo kwasababu Dar isingepata inachopata.

Ni hivi 21 na 4.5 huna jibu. Mkandara alijisema hana jibupamoja na Happy Feet. Nawewe umesema huna jibu kwa majibu ya kitoto kutokaMarekani ! yee uwwwih, tatenanee !

Haya onyesha rasimu yenu na Chenge ina unafuu gani wa gharama ukilinganisha na S3. Mkuu huko US unafanya shughuli gani, naona upo out of touch na Tazania/Marekani, upo Atlantic ocean, ha ha ha haha completely lost but in denial state. Hebu rudi usome unayanika siku moja ujiridhishe kama exposureilkusaidia siku moja
 
Yeye hakuataka kujua ya Marekani. Alichotaka kujua sheria yamchakato wa Tanzania inasema nini kuhusu hilo. Wala hakutaka ufafanunuzi.Unatakiwa uelewe swali, ni sehemu muhimu sana ya mtihani. Na wengi wanafelikwasabau hiyo.

Halafu unasema watu wakuulize, mbona wamekuuliza umekimbiamara 3. Hebu tuambie 21% ya ajira za Tanganyika wanazopewa wznz ni kutokana navigezo gani. Pili, 4.5% ni kutokana na vigezo na formula gani na Tatu, je hiirasimu yenu na Chenge imejibu suala la gharama za S3?
Amependa kuonyesha shukran kwangu. Yeye ndiye angeandika hayo uliyoyaandika hapo juu. Huoni aibu?

Halafu mbona hukuzungumzia mfano wangu wa Ubungo na Kiembesamaki? Na kuna ubaya gani nikiongezea Marekani? Usiwe na kijiba na mimi, YOU WILL BE WASTING YOUR TIME!
 

Anachronism, hakuna kitunkama population. Hakuna mtu awewaziri au katibu mkuu anayejua hasa kwanini 4.5. Hili si jibu na inaonyeshaulivyo out of touch. Hapo ndipo tulisubiri uingie na sasa subiri utaumbuliwa.
Kwa ufupi wznz hawajui kwanini 21% na wala 4.5%. AliulizwaAboud, Duni na wengine akiwemo Alli. Hakuna aliyekuja na jibu. Mwigulu Nchembaanajua hakuna jibu na kama lipo nimemwalika aje hapa.
Kuna kitu kinaitwa Bernett formula kule England. Kipo wazihakina population wala ubabaishaji. Huwezi kutumia population kufikia hatimahiyo kwasababu Dar isingepata inachopata.
Ni hivi 21 na 4.5 huna jibu. Mkandara alijisema hana jibupamoja na Happy Feet. Nawewe umesema huna jibu kwa majibu ya kitoto kutokaMarekani ! yee uwwwih, tatenanee !

Haya onyesha rasimu yenu na Chenge ina unafuu gani wa gharamaulilinganisha na S3. Mkuu huko US unafanya shughuli gani, naon upo out of touch na Tazania na Marekani, upo Atlantic ocean, ha ha ha haha


Nimekupa jibu murua kabisa!! .... hizo numbers hazijatoka from the air bali zime-base kwenye kitu Fulani. Now, wether it makes sense to you or not, that's another issue. Halafu kukaa Marekani ni uchaguzi tu wa mtu kuendesha maisha yake, haimaanishi kuwa ninatakiwa niwe juu kuliko let say anaekaa bongo. UNACHEMSHA!
 
Last edited by a moderator:
Amependa kuonyesha shukran kwangu. Yeye ndiye angeandika hayo uliyoyaandika hapo juu. Huoni aibu??
Halafu mbona hukuzungumzia mfano wangu wa Ubungo na Kiembesamaki? Na kuna ubaya gani nikiongezea Marekani? Usiwe na kijiba na mimi, YOU WILL BE WASTING YOUR TIME!
Nimeogopa kuongelea Ubungo na Kiembe Samaki kwasababu itabidi John Mnyika apewe ving'ora kama Rais wa Unguja! teeh tehe tehe . Mkuu znz unayodhani ni Tembo, ni panya mkuu. Huko US mkuu unashuguulika na nini.
 
Back
Top Bottom