Duru: Hatima ya Muungano na dalili za kuvunjika mapema

Nguruvi3

Platinum Member
Jun 21, 2010
15,419
31,439
HISIA ZAJITOKEZA, UTAIFA WATAWALA ''WATANGANYIKA WAKITOA YA MOYONI HAPAKALIKI' WAZANZIBAR WATAWANYIKA, HAWANA KAULI, SASA NGUMI MKONONI
SEHEMU YA I

Ndugu wanaduru Bunge la katiba la CCM au Samwel Sitta linaendelea kwa kuunga unga, likipoteza mvuto maana na thamani. Wajumbe wameacha kazi aliyodai wanaifanya, sasa wageuza ukumbi eneo la mipasho dhidi ya UKAWA

Jitihada za kutoa zawadi ili kuungwa mkono zinaendele. Mwenyekiti Sitta akiahidi kutumia pesa za umma kama mali yake, vifungu nyeti kama cha 1 na 6 vikiwekwa pembeni ili kujadili vile venye mvuto hasa wa kupendeza wazanzibar

Kila kifungu kimejadiliwa kkidhi haja za Wazanzibar ili mradi 2/3 ya nguvu ipatikane. Vifungu ambavyo ni moyo wa katiba vimewekwa kiporo kuchelea Unyeti ''sensitivity' kulivunja bunge la CCM bila UKAWA au jambo jingine.

SINTOFAHAMU ILIANZA SIKU NYINGI

Wazanzibar waliondoka kwao na msimamo wa S3, msimamo uliosimamia mambo mengi yakiwemo kuvunja katiba, kuondoa mambo ya muungano, kupunguza madaraka ya rais wa JMT visiwani n.k.

Ni haki kusema bila kujali CCM au CUF msimamo wa S3 ni wao. Hata kura za maoni ikiwemo maoni ya tume yanaeleza hivyo.

Hulka ya wazanzibar ni wamoja kwa baadhi ya nyakati, lakini huwa wamoja zaidi dhidi ya 'adui' yao Tanganyika. Wznz hukumbwa na kihoro wanapotoka znz. Waliofika Dodoma, umoja wa S3 ukatawanyika. Pandu kificho akisema hakuwemo, waziri wa sheria akilalamika 'tulikubaliana'

UMOJA KATIKA UNAFIKI

Umoja wa wazanzibar una aina za unafiki. Kama tulivyosema, kuvunjika kwa msimamo wa S3 ni dalili moja.

Kujitoa kwa mwanasheria mkuu katika kamati ya uandishi wa katiba ya Sitta, nao unawakilisha unafiki. Maana yake, wapo wanaoamini maafikiano yao kabla, wanaoamini S3 na mkataba bila kujali mrengo wa kisiasa,kwa pamoja hawawezi kusema. Wapo UKAWA wanaosema na CCM wanaotetea mfumo uliopo.

Unafiki una mizizi,ni wznz wanaosema Tanganyika imewageuza koloni, wananyonywa, wanaibiwa na wanateseka ndani ya muungano,waasisi wa muungano wakitukanwa hadharani. CUF wakimshambulia Karume kwa ukatili, CCM&CUF wakimzodoa Nyerere laana .

Ni Wazanzibar wanaodai muungano hauna faida, laiti ingekuwepo nchi za jirani zingeshajiunga Na ni wazanzibar wanaodai, muungano umefunga fursa zao za kukigeuza kisiwa chao kuwa 'pepo' ya Afrika. Madai hayo yakiwemo matusi yanapotolewa, hakuna kiongozi wa CCM au CUF anayesimama kukemea.

Tena wapo wanaorudia maneno kama Nyerere! ilimradi wanazi wao waitikie Laanatullah Hakujatokea kiongozi yoyote kusimama na kukemea dhihaka na kejeli hizo. Leo wanapotokea wazanzibar wakitetea muungano eti kumuenzi Nyerere, duru hatuelewi ni unafiki wa kiwango gani. Kutokana na kutoelewana au kuelewa wanachokizungumzia, hamkani si shwari tena kwa upande wao

Inaendelea sehemu ya II...
 
SEHEMU YA II

HAMKANI SI SHWARI
Wazanzibar walijisahau na kudhani ni wadau muhimu sana katika muungano.
Walidhani uwepo wao ndani ya muungano ni haki yao peke yao.
Walichokijua ni ukweli kuwa wao wana muda, mwenye saa ni Tanganyika.

Hasira za Watanganyika zinazofichwa chini ya kapeti la CCM zinazidi kupanda.
Lipo kundi kubwa linaloona muungano ni kumbebesha Mtanganyika mzigo na ipo haja ya kubadili muundo.

Lipo kundi linaloamini Zanzibr imeachiwa na sasa kutaka kutawala.
Lipo kundi linaloamini katika muungano wa uchumi na jinsi znz ilivyo tatizo

Mbunge wa Nkasi Mh Keissy anawakilisha sehemu kubwa ya wabunge na Watanganyika na jamii ya Watanganyika.

Alichokisema kama mwakilishi wa wananchi kinabeba sehemu kubwa ya jamii yetu na ni ujinga kumpuuza.
Mh Keissy alichosema kwa kujitoa mhanga ndani ya chama na kutolewa ngeu na wznz si cha kubeza.

Mh Keissy amejenga hoja zake kwa mantiki akisaidiwa na ushahidi.

Katika kamati yake, walimwita Gavana wa benki kuu ya Tanzania, katibu mkuu wa fedha muungano, na katibu mkuu wa wizara ya fedha Zanzibar.Hivyo mh Keissy alishapata ukweli na uhalali wa madai yake, ambayo bila shaka yanaungwa mkono na wabunge wengi.

Kilichoshangaza ulimwengu ni jinsi wajumbe kutoka Zanzibar walivyokosa ustaarabu, ustahamilivu na uvumilivu wa kumsikiliza mh Keissy.

Hawa wznz wakati wanatoa madai, matusi, kejeli na kama kero, hata pale watu walipofahamu hayana ukweli, hakuna aliyetishiwa kupigwa, si mtaani wala si bungeni.

Walipewa fursa ya kuutukana muungano kadri walivyoweza.
Leo wanapokosa uvumilivu wa kusikiliza hoja kinzani, ni ustaarabu wa hali ya chini sana, ulioonyesha kiwango duni, hafifu na dhalili cha ufahamu kwa wznz.

Walichopaswa kufanya ni kujibu hoja za Mh Keissy kwa hoja za maana.
Kwa bahati mbaya tulichosikia, si tu ni udhalili, bali moral decay ya hali ya juu ya wazanzibar.

Kumwita Keissy ni Mwarabu, hilo si tusi kwake, ni tusi kwa jamii nzima ya wazanzibar inayoundwa na sehemu kubwa sana ya Waarabu. Ni kiashirio kuwa wznz wana tatizo ingawa linafichwa kwa mwamvuli wa Tanzania.

Kwani kuwa Mwarabu kuna tatizo gani?
Nyerere na wenzake waliingia LEGCO katika jengo la mhindi.
Akahutubia bunge la kwanza la Tanganyika huru Karimjee.

Mjenzi wa wodi ya Sewa Haji ni Mwarabu.
Aliyeanzisha kitongoji cha Sinza ni mzungu Derek Bryson.

Waziri wetu wa fedha mwenye heshima kubwa Amir Jamal ni Mhindi.
Waziri wetu wa afya wa Tanganyika huru baada ya mkoloni kuondoka ni Leader Sterling

Hatuwezi kupima michango wa watu wenye unasaba au rangi nyingine katika taifa la Tanganyika.
Wote ni Watanganyika wala hatuwatambui kwa rangi au nywele zao. Hili la wazanzibar ni la kulaaniwa sana.

Na hapo kuna hoja kubwa, kwamba ubaguzi waliouanza dhidi ya Watanganyika kama kuwachoma moto hautaishia hapo.

Ubaguzi wa kudai vyeo kwa uzanzibar na si sifa hautaishia hapo.
Dhambi ya kuwatukana Waarabu kwa jina la Keissy ni kubwa, na sijui wale wznz wenye unasaba na waarabu leo damu zao zinachemkaje.

WAZANZIBAR WASHINDWA KUJITETEA

Hoja za Mheshimiwa Keissy zilijengwa katika mukatadha huu.
1. Kwavile kuna mambo wznz wameyaondoa katika muungano, uwepo wao Dodoma ni kitu gani kama si utalii
2. Gavana na makatibu wakuu wa fedha wamethibitisha znz kutochangia muungano, muungano upi wanajadili?
3. Kwanini watumie rasilimali za Tanganyika nyingi kwenda kutibiwa na mishahara kwa mambo yasiyowahusu?
4. Wazn wanachukua mishara ya SMZ kutoka Dar, je huo si unonyaji na wizi kwa Tanganyika?

MAJIBU YA WZANZIBAR

1. Wewe Mwarabu nenda kwenu
2. Zanzibar inachangia muungano kwa kupoteza kiti UN na kutojulikana Duniani
3. Toka nje tukuonyeshe ''***nzi we!
4. Matusi ya nguoni.

Katika majibu hayo ya kipuuz yaliyokosa stara, elimu na ustaarabu, ni moja tu tutalijibu hapa.

Zanzibar imepoeteza kiti chake UN na Kutojulikana duniani kama Tanganyika ilivyopteza kiti UN na kutoweka kabisa

Leo hakuna anayejua Tanganyika, ingawa znz ipo katika ramani.
Jibu hili ni la kitoto kutolewa na mtalii T. Kombo. Haya ndiyo maoke ya kubeba watoto wa wazee, na gharama za mtalii anazobeba Mtanganyika. Huyu ni mmoja wa wale wanaokula mishahara ya bilioni 126, watu 84 tu. Tunabeba gharama

Katika zama za leo muungano ni uchumi na si maneno au jina.
Hatuwezi kusema tumeungana kwa kiti cha UN tulichopoteza wote.

Kwa mantiki na hoja , mh Keissy ameongelea mambo ya maana kuliko watalii 84 waliojizatiti kutukana ndugu zao Waarabu huko pemba na Unguja.

Katika bandiko la I tumeeleza unafiki wa wazanzibar, na hili ni ushahidi.

Huwezi kujiita mtalii wa znz pale Dodoma ukiwa na inda kuhusu Waarabu unaopanga nao mipango ya kukabliana na muungano. Unafiki mkubwa.Leo wanasema wznz wanaonewa, swali ni kuwa wznz ni wapi kama kuna turufu ya Uarabu imeingia?

Inaendelea...
 
[MENTION]SEHEMU YA III[/MENTION]

MADAI YA WZNZ YALIVYOYEYUKA KAMA THELUJI

Miaka dahari, wznz wameanishwa kuwa nchi yao ni moja, raia wake ni wamoja na kwamba ni taifa tajiri sana

Madai hayo yalihusisha kunyonywa na Tanganyika, kunyimwa fursa ndani ya muungano, kubanwa katika fursa za kisiasa na kiuchumi zikiwemo za Utamaduni

Kwa hoja zinaotolewa na viongozi kama gavana wa benki kuu, ni dhahiri znz haina mchango katika muungano.
Hili halina mjadala na wznz walikubali kama lilivyo.

Kwamba wananyonywa, si kweli. Wao ni vinara wa kuchukua hadi mishahara ya serikali yao.

Kwamba, ni wamoja, si kweli, madai ya Uarabu yasingezuka wakiwa katika nchi ya kigeni tena wakitukana ndugu zao

Kwamba, wananyimwa fursa, si kweli, fursa wanazopata katika muungano ni kubwa na nyingi tena za wizi na dhulma

Kwamba wananyimwa nafasi ya utamaduni, pengine lina ukweli, wangekuwa BLW Uarabu n.k. ni utamaduni wao

Kwamba, kuna watalii 84 wanakomba pesa hadi za posa kwa wake zao, hilo halina mjadala tena

Kwamba, rasilimali za Tanganyika zinatumika znz kuliko Tanganyika, hilo halina mjadala

Kwamba, Watanganyika wanang'ang'ania muungano, hilo ni uongo mkubwa

Kwamba, Watanganyika wanawagawa, hilo si kweli, kauli za kulaani Uarabu zinatoka vinywani mwao.

Kwamba, nje ya muungano watakuwa Dubai, hilo si kweli, hawawezi kukwepa mkono wa Tanganyika kijiografia

Kwamba, SMZ inaendeshwa kwa fedha za hazina Dar, hilo halina mjadala

Orodha ni ndefu na inahitimisha madai ya hovyo ya kila siku ya wznz kuhusu Tanganyika.

WATIA KIDONDA CHUMVI

Kutokana na madai ya wzn kila mara, hilo limesaidia sana Watanganyika kujitambua.

Leo wanajua hasara kubwa anayopata kutokana na muungano wa sasa ambao znz inatumia jina kudai haki isiyowajibika kwake. Kwamba, kila wanapotaka mafao wao ni Watanzania , nje ya hapo hawana habari na hawaijui Tanzania.

Mwamko wa Watanganyika ni wa kiwango kikubwa tena ukija kama mvua ya gharika.

Wengi wametanabahi,znz ambayo ki ukubwa na idadi ni ndogo kuliko sehemu nyingine ya wailaya za Tanganyika, inachukua rasilimali kubwa kuliko wilaya hizo.

Kwamba, muungano unabebwa kwa gharama za Mtanganyika,Mtanganyika analipa gharama kubeba SMZ na taasisi zake.

Hayo yote yanakuja katika gharama kubwa ya kodi, ushuru n.k. kwa Mtanganyika huku wenzao wa znz wakiendelea kuburudika na mismaha ya kodi, wakipunga upepo kwa kutambua jomba Tanganyika atamwaga mapesa.

Hali inatia hasira na uchungu pale inapobainika Tanganyika imegeuzwa kituo cha ajira za Wazanzibar.

Kwa mfano, watalii 84 wanaoitwa wabunge wanakomba mishara tu zaidi ya bilioni 126.
Ukichanganya mambo mengine na pesa za majimbo, ni zaidi ya Bilioni 200.

Kiwango hicho ni kikubwa kuliko pesa za kuendesha taasisi kama chuo cha Walimu Changombe, kujenga zaidi ya vituo vya afya 20 katika wastani wa bilioni 10 kila kimoja, kumaliza tatizo la madawati la Tanganyika n.k.
Hawa ni watu 84 tu.

Swali la kujiuliza, uwekezaji huu wa gharama, tena kwa kodi za Watanganyika una mafao gani mbele ya safari?

Lakini pia, Watanganyika wameelewa, kumbe kiburi na jeuri ya znz ya kuvunja katiba ya nchi, haina maana kwasababu katika muungano wao ni tegemezi ''parasite''. Sasa jeuri hiyo inatoka wapi.

Ni kwa mukatadha huo hali ya muungano kwasasa ni mbaya kuliko wakati mwingine.

Na hali ni mbaya hasa kwa wznz, kwasababu Watanganyika kwa mtazamo wapo tayari kwa lolote.

Inaendelea...
 
Sehemu ya IV

S3 zitawokoa wazanzibar
Inapotokea ndani ya CCM kuna minyukano hadi kuitana Waarabu na wa kipili pili, ni dhahiri CCM haina nguvu za kuzuia kuvunjika kwa muungano. Inaweza kuahirisha lakini si kuzuia anguko.

Kwa mtazamo huo, S3 ni muafaka kwa wazanzibar kwa wakati huu kuliko wakati mwingine.

S3 zitaamanisha uwepo wa Tanganyika, na hivyo znz inaweza kuja kuzungumza na mbia mwenza.

S2 zina maana moja, wazanzibar watakuwa daraja la pili, katika vyama na serikali kuu.

Hakutatokea tena mzanzibar kuangaliwa kwa jicho la hamasa kama ilivyokuwa huko nyuma.

Haiwezekani mznz aje kuongelea mambo ya Tanganyika ikiwa hana lolote la maana katika muungano anaoongelea

Kutokana na hilo, Mtanganyika atabaki superior na mznz sasa ameabaki kuwa omba omba na si mbabe tena.

Hivyo, wznz wana machaguo matatu

1. Kuvunja muungano tugawane mbao

2. Kuendelea na S2, wakiwa daraja la 2 kwa kukosa heshima.
Hawatakuwa na nguvu ya kujenga hoja wakiwa na mikono mitupu na kapu la malalamiko.

Na huu ndio utahitimisha malalamiko yao kwa vile hakuna atakayewasikiliza ikiwa hawawezi kujibu hoja za mtu mmoja, mh Keissy. Hivyo wao watabaki kuwa daraja la 2 kwa lolote.
Ndio, daraja la 2 kwasababu wanaomba uwepo wa muungano na si wabia wa muungano.

3. S3, ni muhimu kwao. Watapata japo nguvu ya kuwa na mbia mwenza kati kati akiwemo baba yao Tanzania.

Tanzania ataweza kuwanusuru kwa hadhi na heshima japo kidogo. Ndiye msuluhishi.

Hivyo S3 si muhimu kwa Tanganyika, ni muhimu kwao.

Kwa Tanganyika S3 ni kukamilisha azma ya kuwa na fiscal autonomy.
Kwao ni muhimu kuendelea kuwa katika kivuli cha Tanganyika, ambacho hawawezi kukikwepa kwa kanuni za asili tu

Kwa sasa Tanganyika itazinduka kwa gharika. Ujio wake kama hautaangaliwa na kuheshimiwa, tunaweza kujikuta katika wakati mgumu.

Ujio wa Tanganyika utaambatana na kutoa ya mayoni na hasira ambazo taratibu zinaanza.

Ni muhimu hilo lizingatiwe, na wala si CCM au CUF bali wazanzibar wenyewe.

HITIMISHO

Ingawa bunge linaendelea kwa matumaini ya kupata 2/3 ya wznz kwa kuwafurahisha, katiba itakosa uhalali wa kisiasa kama ilivyojitokeza.

Lakini pia kuna tatizo mbele ya safari, wznz hawaeleweki na lolote linaweza kutokea wakirudi znz kutoka Dodoma, na katika kura ya maoni.

Kwa hali yoyote bunge la sasa ni kupoteza muda.
Na pengine serikali ingechukua nafasi ya kutafakari kuhusu hatima ya muungano kwa siku zijazo badala ya kumsikiliza Sitta na vituko vinavyoendelea Dodoma.

Si rahisi kudhani serikali inaweza kuwaridhisha wznz na kuendelea kuwatukana Watanganyika.

Hali iliyopo ni mvinyo kutoka katika chupa. Kile kilichofichwa kwa Tanganyika miaka nenda rudi sasa kipo wazi.

Hivyo, lazima kwanza, iwepo katiba yenye maridhiano.
Tanganyika iundwe katika mkondo wa kisheria na si kusubiri iundwe kwa sheria za mitaani.

CCM wanaweza kuahirisha tatizo, lakini siku litakapofumuka, huo ndio utakuwa mwisho wa muungano.

Muungano utavunjika kama glass ya maziwa.

Haya ya Dodoma ya kuambizana bila haya au soni, ni dalili za tatizo kubwa lililojificha.

Kwa upande wa znz, ni wakati sasa waangalie mustakabali wao kabla mambo hayajaenda kombo.

Ni bora nusu ya shari kuliko shari kamili.
Muungano upo njia panda, ni ima uvunjike kama glass au ushikiliwe kwa kamba nzito za S3.

S2 imeshindwa kwa miaka 50. Badala ya kuwa wamoja tumezidi kutengana.

Wznz watambue mchawi wao ni wao wenyewe. Jibwa lililolala sasa limeamka.

Tembo yupo chumbani, wana nafasi moja tu ya kujinusuru, kuiachia Tanganyika irudi, kinyume chake ni majuto makubwa

Tusemezane
 
Nguruvi3,

Hakika Huko Ndio tuendako.
Nikianza na hoja yako juu ya moto unaozidi kuchochea ndani ya CCM, kwa kweli ni Vigumu kuelewa nini itakuwa ni hatima ya cheche hizo ndani ya chama. Kwa mfano Mdogo tu, Kabla ya kufunga kikao cha bunge usiku wa jumatatu iliyopita, Samuel Sitta aliwaeleza wajumbe Kwamba kila mmoja wao atapewa Cheti kilichosainiwa na rais Kikwete kuonyesha Kwamba mjumbe huyo amefanya "kazi muhimu na ya kihistoria ya kutunga katiba".

Ni Vigumu kuelewa iwapo mpango huo ulikuwepo tangia awali/Kabla ya mchakato kuingia nyongo, au ni mpango mpya ulioletwa na Sitta kwa ajili ya kuwalaghai wajumbe Kwamba watatambuliwa na rais. Wengi tunajiuliza, kwanini then rais Kikwete alifikia makubaliano na ukawa hivi karibuni Kwamba kwa muda na mazingira yaliyopo, katiba mpya haiwezi kupatikana; Kauli ya Sitta kuja baada ya kauli ya rais Kikwete iliyokiri Kwamba katiba Mpya haiwezekani Kabla ya uchaguzi 2015 maana yake ni nini? Je Ina maana Sitta Ana mamlaka makubwa zaidi ya Mwenyekiti wake na rais wa nchi juu ya suala Zima la katiba mpya?

Tayari watanganyika wengi wameanza kuona athari za mwenendo wa Sitta kwa Tanganyika, Zanzibar na muungano kwa ujumla, lakini sijui Kama wajumbe wa BLK wanaelewa nini kinafuatia kutokana na mwenendo wa Sitta na katiba mpya. Kwa mfano - Sitta ameingiza masuala ya ardhi, maji, viwanda, uvuvi, serikali za Mitaa, uwekezaji, na takukuru Kama masuala ya muungano. Tuangalie baadhi ya mambo haya kwa undani:

Tukianza na Ardhi - Kuchukua mambo ya Tanganyika Kama vile ardhi na kuyaingiza Katika katiba ya muungano, hii ni Kinyume na rasimu ya tume. Pia kufanya hivyo ni kurekebisha katiba iliyopo, huku sio kutunga katiba mpya. Kazi hii haipaswi kufanywa na BLK Bali bunge la JMT. Kwa mfano, katiba ya JMT (1977) inataja suala la umilikaji wa ardhi Katika ibara ya 24. Kila Raia wa JMT anayo Haki ya kumiliki Mali na ulinzi wa Mali yake, ingawaje Haki hii Ipo upande mmoja tu wa muungano.

Sheria ya ardhi ya mwaka 1999 Katika sura yake ya 113, kifungu cha 3(a) kinatoa Dira na Sheria kuhusu kanuni muhimu ya sera ya taifa ya ardhi. Kanuni hii imemkabidhi rais wa JMT usimamizi wa ardhi kwa niaba ya wananchi wa JMT. Pia Sheria ya ardhi ya kijiji sura namba 414 na Sheria ya kusajili ardhi Sura ya 334, hizi Ndio uongoza usimamizi wa matumizi ya ardhi kwa Mujibu wa Sheria na sera ya ardhi. Tatizo ni hili:

Pamoja na Kwamba Sheria hii Inahusu jamhuri ya muungano wa Tanzania, ni suala lililo wazi Kwamba Sheria hii haitumiki Zanzibar. Anachofanya Sitta kwa wazanzibari ni kuwaletea kitu kipya yani kuagiza Zanzibar kuruhusu ardhi Yao kutumiwa na Raia wa Tanganyika, suala ambalo wamelikataa Katika kipindi chote cha muungano, na kuliweka sasa itakuwa ni moja ya njiti za kibiriti zitazowasha moto na machafuko.

Masuala mengine Kama vile serikali za Mitaa, takukuru, vyama vya Ushirika, uwekezaji, viwanda, vijijini vya ujamaa, vitongoji, uvuvi, pembejeo, Kilimo etc, haya yote ni masuala yanayohusu Tanganyika moja kwa moja serikali ya Tanganyika. Ndio maana tume ya katiba ikayaweka haya Kando, nje ya muungano. Kama tunakumbuka vyema, haya ni sehemu ya malalamiko mengi ya wananchi Wakati wa ziara za tume ya katiba, ambapo wapo wananchi waliolalamika Kwamba haya mambo yanahusu Tanzania bara pekee (Tanganyika) lakini yanaendeshwa kwa kodi za wananchi wote wa Tanzania.

Tukichukulia mfano wa uwekezaji, kwanini TIC iwe ni ya muungano, huku taasisi hii kwa upande wa Zanzibar ibakie nje ya muungano? Wazanzibari ni mabingwa wa kusamehe kodi, kwa vile mjomba Tanganyika yupo kutoa fedha. Kitendo cha TIC kuwa Chombo cha muungano kitakuwa Kama uwepo wa TRA na ZRA Zanzibar, mzigo kwa Tanganyika.

Tukija kwenye suala la viwanda, sekta hii Ndio inayobeba matumaini ya Ajira kwa vijana wetu. Kufanya viwanda kuwa sehemu ya muungano, Wakati viwanda karibia vyote vitakuwa bara ni kujenga mazingira Kama yake ya 21% ya Ajira kwa wazanzibari; wazanzibari watadai vijana wao waajiriwe kwa quota Fulani Katika viwanda ambavyo haviwahusu, huku mtanganyika akiumia. Na kwa viwanda ambavyo vitashamiri znZ iwapo itatokea hivyo, watanganyika hawatopewa fursa kule.

Tukichukulia mfano TAKUKURU, Sitta na Kundi lake wanaigeuza kuwa ni ya muungano Wakati Chombo Hiki hakiruhusiwi kufanya kazi nchi Jirani ya Zanzibar. Nchi hii Jirani haitambui takukuru ni kiumbe gani, na Wala haimo Katika Orodha ya mambo ya muungano kwa Mujibu wa mkataba wa muungano (1964). Unga'ng'anizi huu wa Sitta na wenzake ni kuua muungano, sio kuboresha muungano.

Zanzibar wana Chombo kinachofanana na takukuru, kinaitwa - kamishen ya rushwa na uhujumu uchumi. Kitendo cha Sitta kuifanya takukuru kuwa ni suala la muungano ni kuzidi kuiminya Zanzibar, lakini pia kuongeza matumizi ya fedha za walipa kodi wa Tanganyika kwa nchi Jirani bila ya faida kwani gharama za kuendesha Chombo Hiki chini ya serikali Mbili, wazanzibari watasema Hilo ni la muungano (Tanganyika).

Nchi Mbili zinapoungana, hubadilika huwa nchi moja yenye mamlaka moja ya Kidola. Tofauti na hili, kupitia katiba yake ya 2010, chini ya uongozi wa Sitta na wenzake, Zanzibar imekuwa ni nchi huru. Ina bendera yake, Wimbo wake wa taifa, Ina serikali yake kamili inayoambatana na political autonomy, na Ina fiscal and policy autonomy.

Katiba yake inatambua Kwamba Zanzibar ni nchi, na Sitta na wenzake wanatambua Kwamba nchi hii Ipo ndani ya nchi nyingine ya Tanzania, lakini wanadhania Kwamba hatari hii watanganyika watapuuzia na suala hili litapita tu Kama upepo. Katiba ya Zanzibar imeruhusu nchi hii ya Jirani kuanzisha majeshi yake, ambayo yapo chini ya amiri jeshi mkuu wa nchi hiyo Jirani. Tuna uhakika gani Kwamba hatutaanza kutuniana misuli Kama Korea kusini na kaskazini kwa masuala ya rasilimali? Kitendo cha kuruhusu znZ kuwa ni nchi kamili, nchi hii itakuwa na Haki ya kutetea Kile inachoamini ni chake na hata Jumuiya ya kimataifa itaelewa hivyo.

Kitendo cha wajumbe wa BLK pale Dodoma kushabikia juhudi za Sitta kuzima serikali Tatu kitasababisha muungano kuingia Katika machafuko makubwa sana ndani ya kipindi kifupi. Kutaibua migogoro mipya ndani ya muungano, hasa baada ya watanganyika Kuamka na kujua nini kinaendelea. Hali hiyo itavunja muungano. The question that follows ni je, Nani atakuwa loser zaidi Kati ya Tanganyika na Zanzibar? Jibu ni dhahiri - ZANZIBAR.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi

Wengi hawapendi kutazama matatizo ya mufa mfupi na mrefu retrospectively

Suala la ardhi
Tume imeeleza resentment ya Watanganyika. Kwamba, hawana fursa kama wazanzibar.
Hapa kuna scenario nyingi

Scenario 1;
Kwa wznz hiyo ni advantage, hata hivyo ni ya muda mfupi wasababu ya Complications zitakazofuata

Scenario 2
Kwa Watanganyika ni disadavantage kwasababu hawatafaidika na uamuzi huo

Complication
Rais wa JMT ni mmiliki wa ardhi yote. Wazanzibar hawawezi kukwepa neno Tanzania. Ardhi itabaki mikononi mwa Rais, Jamhuri ya muungano.

Ardhi ndiyo ‘uhai' wa viumbe na mali. Zanzibar kwa mfano, ikipata rasilimali zilizomo katika ardhi, mmiliki wake ni Rais wa JMT.Mafuta na gesi walivyoondoa vitakuwa cosmetic,yapo katika ardhi ya muungano kwa mujibu wa katiba na si yao ya 2010

Rais wa Zanzibar ana uwezo wa kugawa ardhi kwa mujibu wa katiba yao.
Uwezo wake utakuwa limited kwasababu mmiliki wa ardhi ni Rais wa JMT
Hatua zozote atakazochukua Rais wa znz ni kuvunja katiba kama ilivyo sas

Bunge la JMT litakuwa limited kuzungumzia ardhi ya Zanzibar kutokana na
sheria na katiba ya znz ya 2010 iliyodhibiti ardhi isiwe ya muungano

TUNAELEKEA WAPI

Tunakoelekea ni kule tulikoshindwa kujifunza. Watanganyika wakienda znz kwa passport, hilo liliamsha hisia na siku moja wabunge wakapitisha azimio nao waje kwa passport, ilitishia muungano, thanks to busara za wazee wa enzihi

Wabunge hawakuumizwa na passport, ni manung'uniko mengine.
Mwanya wa passport ulipojitokeza ikawa wakatumia kama silaha.

Ukweli,walikuwa na manung'uniko mengine hiyo ikawa sababu tu yak u-justify.
Ndicho kilichozaa G55 na suala la OIC

Kwa hili la ardhi, nalo ni manung'uniko kwa pande zote.
Hivyo ikitokea fursa kidogo, suala litatumika si kama silaha bali kuhitimisha safari ya miaka.
Huko ndiko Samwel Sitta na bunge lake wasikokuona na ndiko tunakwenda. Tena safari ni fupi sana.

Watanganyika wameshakuwa ''sensitive' na hilo limewajengea curiosity katika kila jambo.

Mfano, watu wanahoji asilimia 21 ajira ilipatikana vipi.
Kuna uwezekano siku za nyuma walikuwa wanapata zaidi ya asilimia hiyo. Kutokana na curiosity and sensitivity ya muungano, sasa wanahoji asilimia 21 zimepatikanaje. Hili halina jibu na linabaki kuwa ni resentment katika mioyo yao.

Ukifikiria jinsi Watanganyika wanavyoumia katika kubeba muungano, kubeba SMZ na yatokanayo, hakuna shaka wana hasira na chuki mioyoni.Hilo linahitaji sababu ndogo sana kama njiti ya kibiriti kuwalipua.Mambo kama ardhi ni precusor nzuri sana ya kuwasha moto. Tunaona mapigano ya wakulima na wafugaji, sijui nini kitafuta, isipokuwa nina uhakika si kizuri.

Ikifika hapo muungano utakufa within a day or two. Utakufa kama glass inavyovunjika

Tusemezane
 
Katika hitimisho la ripoti ya Baraza La Mapinduzi Zanzibar juu ya muungano (2004), BLM linasema Kwamba:

"Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulianzishwa kwa kuzingatia msingi mkuu wa undugu na kuaminiana. Kwa tafsiri fasaha, muungano ni mashirikiano ya kijamii zilizo hai na hivyo hauna budi kuenziwa ili wananchi wasiuone muungano usioshuka kwenye vichwa vyao. Ni vyema kila mwananchi akajivunia muungano kwa kufaidika na matunda yake. Kwa hiyo, muungano ujitahidi kuzisaidia pande zote mbili katika kutekeleza majukumu yake kwa wananchi."

Angalau viongozi wa Zanzibar Mara nyingine huwa wanaweka wazi matarajio ambayo wananchi wake wanatakiwa kuyapata ndani ya muungano, na tumeona that in action kupitia katiba ya Zanzibar ya 2010. Kwa upande wa Tanganyika, juhudi hizi hazipo.

1. Mfumo wa serikali Mbili zilizoboreshwa utaleta Matunda gani kwa wananchi wa Tanganyika?

2. Mfumo wa serikali Mbili zilizoboreshwa utasaidiaje Tanganyika kutekeleza majukumu yake kwa wananchi?

3. Serikali Mbili zilizoboreshwa zitaweza vipi kujenga utanzania kwa njia ya kuruhusu ujenzi wa uzanzibari na kukandamiza utanganyika?

Kuna haja ya watanganyika na wazanzibari kuunganisha Nguvu zao Katika kuidai Tanganyika, kwani Tanganyika haikwepeki Tena. Hii ni kwa sababu, tukiangalia kwa upande wa Zanzibar kwa mfano,Serikali mbili zilizoboreshwa (bila ya serikali Tanganyika), ni sawa na kuipa Zanzibar uhuru wa bandia, na Hali hii itazidi kuchochea utaifa wa Zanzibar. Hauwezi kuipa Zanzibar mamlaka ya kujiamulia “mambo yake ya ndani” halafu ukaizuia kufanya hivyo kwa mambo yake ya nje - kwa mfano kuteua mabalozi wake na kuwa na kiti chake katika umoja wa mataifa. Pia hauwezi kuipa Zanzibar (mshirika mmoja wa muungano), mamlaka ya kujiamulia mambo yake “ya ndani”, halafu usifanye hivyo kwa mshirika mwingine (Tanganyika). Huku ni kuchochea utaifa kwa watanganyika. Chini ya mfumo wa serikali mbili zilizoboreshwa, hakuna kitakachokuwa cha “Zanzibar Peke Yake”. Ndani ya serikali mbili, badala yake kutakuwa na Zanzibar, na Tanganyika, lakini iliyovaa KOTI LA MUUNGANO. Koti liliwabana Zanzibar, na sasa limeanza kuwabana watanganyika. Chuki zitazidi kujengeka na kila upande utataka koti hili sasa livuliwe, pengine na kutupwa kabisa lisionekana tena.

Uhuru wa bandia wa kuipa Zanzibar mamlaka kamili bila ya kuwepo kwa Tanganyika sio suluhisho la kero za muungano. Zanzibar yenye mamlaka kamili itapatikana iwapo tu serikali ya Tanganyika itazinduliwa. Hakuna jinsi nyingine ya Zanzibar kupata “mamlaka kamili” kwani mamlaka kamili yamefunikwa na Koti la Muungano lililovaliwa na “Tanganyika”.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
WAZANZIBAR WASHINDWA KUJITETEA

Hoja za Mheshimiwa Keissy zilijengwa katika mukatadha huu.
1. Kwavile kuna mambo wznz wameyaondoa katika muungano, uwepo wao Dodoma ni kitu gani kama si utalii
2. Gavana na makatibu wakuu wa fedha wamethibitisha znz kutochangia muungano, muungano upi wanajadili?
3. Kwanini watumie rasilimali za Tanganyika nyingi kwenda kutibiwa na mishahara kwa mambo yasiyowahusu?
4. Wazn wanachukua mishara ya SMZ kutoka Dar, je huo si unonyaji na wizi kwa Tanganyika?

MAJIBU YA WZANZIBAR

1. Wewe Mwarabu nenda kwenu
2. Zanzibar inachangia muungano kwa kupoteza kiti UN na kutojulikana Duniani
3. Toka nje tukuonyeshe ''***nzi we!
4. Matusi ya nguoni.

Ukiuliza wengine wanaendeleza yale yale matusi. Nimefurahi kuwa hayo amesema Keissy angesema mbara ingekuwa tatizo sana. na majibu yao tumeyaona.
 
Huu ni Muungano Wa CCM bara na CCM Zanzibar. Lakini kama utapigiwa kura, nadhani sio Watanganyika wala Wanzinzibar Wanao taka Muungano.
Hata CCM wenyewe wameshindwa kuelewa ni muungano gani.

CCM znz wanasema wanaonewa na JMT. CCM bara wamechoka kubeba furushi la samadi.
Haya tunayoyaona ni sehemu tu, ipo CCM si CCM au serikali yao ngumi zaitatokea hadharani.

Ni muda mfupi sana tutasikia umevunjika kama glass. Zile zama za kudanganya watu zimekwisha.
 
Ukiuliza wengine wanaendeleza yale yale matusi. Nimefurahi kuwa hayo amesema Keissy angesema mbara ingekuwa tatizo sana. na majibu yao tumeyaona.
Mkuu, huyu Keissy ni wa Nkasi. Ni miongoni mwa wazalendo waliochoshwa na muungano. Hii ni mara ya pili wanawapa waznz 'makavu''.
Ni mara ya pili anakimbizwa kwa ngumi na watalii wa Dodoma.

Watalii kutoka znz hawana sababu za msingi za kujibu hoja za Keissy. Kazi yao kubwa ni ngumi.
Wameelezwa kuwa wao ni mzigo kwa Tanganyika, hawajibu wanamkimbiza Keissy hadi akatokea mlango wa uani.
 
Mazingaombwe yanaendelea Dodoma. Udanganyifu sasa hakuna hata haya.
Wanaotenda ni wazee, wanaoshangilia ni vijana.

Taifa lipo njia panda, ni jibu lililoiva linasubiri kutumbuka.

tutaendelea kwa wiki moja, kuangalia wapi tulipo na wapi taifa linaelekea..
 
JK APATA PA KUTOKEA

AWAGEUKA UKAWA KAMA KAWAIDA

SASA ATAMANI S3, BAADA YA KUZIKANA HADHARANI

Rais Kikiwete amekabidhiwa rasimu ya CCM. Ni ya CCM kwasababu ya kukosekana kwa muafaka na kuandikwa na CCM

Kitendo cha kuwaita UKAWA kilikuwa kupoteza muda wakati mipango inafanywa ili kukamilisha 2/3.
Hatudhani katiba inaandikwa kwa kupata watu 2 ambao haijulikani walipatikanaje.

Hakuna uhalali wa kikanuni au kimantiki watu hao ambao ni siri ya Samwel Sitta wamepigia kura rasimu ya CCM wakiwa nje kama UKAWA. JK na Sitta wanaamini kwa dhati kabisa kuwa katiba inaweza kupatikana kwa kura ''2'' za maruhani.

Ni kitendo cha kukosa uhalali licha ya kwamba uhalali ulishatoweka.
Mabalozi na wana diplomasia wameona uhuni huo ambao Rais ameamua kuuchukua.

Suala la muungano lilihitaji mjadala wa kina na ufumbuzi.
Wanachokifanya CCM ni kuwasha moto zaidi. Kibaya zaidi, kitendo cha kuwafukuza kazi waliopinga si kwamba ni kukosa demokrasia lakini pia kina harufu kali ya kutisha, kuogofya na kuwasokomeza CCM matambara ya mdomoni wasiseme.

Duru tumekuwa tukisema, CCM wamesokomezwa matambara kuziba sauti zao.
Hata hivyo wanadamu wana muda wa uvumilivu kama ilivyoanza kuonekana

Mwanasheria mkuu wa znz kufukuzwa kazi kumeamsha hisia za uonevu, na kwamba kuna jambo linafichwa

Mwanasheria alipiga kura kama mjumbe na si mwanasheria.
Hakukuwa na kitu kinachowafunga wabunge kuhusu upigaji kura.Na endapo kulikuwa na jambo hilo, iweje Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM aseme, katiba haikuwa agenda ya CCM?

Hili nalo linaonyesha jinsi rasimu ya CCM ilivyokosa uhalali wa kiroho, kikanuni na kisheria kwa mantiki zote

Tunawafahamu wazanzibar kwa jinsi wanavyogeuka.
Baada ya kumaliza kuandika rasimu ya CCM, watakaporejea visiwani hali itakuwa tofauti sana.

Kwanza, suala la kubadili katiba ya znz iwiane na ya CCM lina ugumu sana.
Pili, kitendo cha mwanasheria kufukuzwa kazi kinatoa ''sympathy'' na kuupa nguvu upinzani.

Tatu, haieleweki kama znz 2/3 watasema hapana kwa rasimu haramu na bara wakasema ndio nini kitafuata.

Nne, madai ya katiba mpya yapo pale pale kwasababu wananchi hawakusikilizwa


Sita, sasa ni wazi wizi wa kura ni utamaduni wa CCM na hilo linajulikana kimataifa si kwa hisia bali ushahidi.


Inaendelea...
 
Rais Kikwete ameonyesha udhaifu wa kubabaika katika mchakato mzima. Suala hili lilikosa maridhiano na alishauriwa aahirishe mchakato.
Wapo wanaojiuliza, je alikuwa na nia ya kukwamua mchakato?
Je, kubadilika kauli zake kila siku ni dalili ya nini? Kukosa maono, kushindwa uongozi au kitu gani.

Rais aliyekubaliana na Wapinzani kuhusu kuahirishwa mchakato, ni huyo huyo amekubali mchakato haramu uliojaa udanganyifu usiohotaji microscope kuubaini.

Anachokifanya JK ni kuhakikisha anapata katiba bila kujali ubora wake.
Hata hivyo, inampasa aelewe kuwa sasa ameuweka muungano katika nafasi mbaya kuliko ilivyowahi kutokea huko nyuma.


  1. Yale madai ya wznz kuhusu kupewa mamlaka zaidi yataendelea kwa nguvu kubwa ya wananchi ambao serikali haina ubavu wa kuwafukuza kazi
  2. Kwasasa, kuna madai mazito sana kutoka Tanganyika ambayo hayana majibu. Rasimu ya CCM imezidi kuonyesha jinsi donda llilivyokubwa na lisilo na dawa

Kinachofuata ni wananchi kudai haki si kwa kutumia njia za kisheria bali njia zozote. Kutakuwa na mtifuano mkubwa baina ya pande mbili.

Njia aliyotumia JK ya kubabaisha wapinzania ilikuwa kutafuta mlango wa kutokea.
Kwa bahati mbaya hakutoka, na sasa jumba litaanguka akiwa ndani na sehemu ya hisoria ya anguko la muungano.

Kikwete hakubabaisha umma tu, bali ndani ya chama chake kuna timbwili kubwa.
Ni kati ya wahafidhina na wanaotaka mabadiliko.

Kwa kitendo cha kukiri haikuwa agenda ya CCM, swali linazuka, ni wapi JK na CCM walipata uwezo wa kuziba wabunge wao midomo?
Kwanini isiwe agenda ya CCM lakini isimamiwe na CCM?

Mchakato mzima unaonyesha Rais hakuwa na mtazamo kuhusu katiba. Aliongozwa na makundi bila yeye kufahamu. Kwa mfano, CCM walimwambia S3 ni hatari sana zitapindua nchi. Leo anasema walikuwa na hofu isiyo na sababu.

Hapa ni baada ya kubaini kuwa hata ndani ya CCM bado S3 zimejitokeza na kwamba hilo haiepukiki. Rais hakuamini maoni ya wananchi, anayaamini wakati mambo yameshaharibika.

Rais amepokea rasimu iliyotengenezwa na CCM na kupatishwa kwa njia za kughushi. Haiwezekani ashauriwe kuwa rasimu ya katiba, nyaraka ya kwanza aliyoishika kabla ya kuingia Ikulu inaweza kupigiwa kura na ‘wabunge waliolala nyumbani ili kupata 2/3, kupigiwa kura kwa Whatsupp na face book!!!

Tukiangalia nyuma tunaona kauli za kushangaza sana za Rais

  1. Kwamba alijulishwa mchakato mzima na kukubali. Hivyo alijua rasimu ya Warioba ilikuwa na na nini. Hayo yalikuwa maoni ya wananchi. Wapi Rais anapata ushaujaa wa CCM kuteka nyara maoni hayo ikiwa anakiri haikuwa agenda ya CCM?
  2. Aliwahi kuongea na CCM na kuwaeleza wajiandae na mabadiliko. Je, mabadiliko ndiyo hayo ya akina Chenge?
  3. Alikutana na TCD kwa mara ya kwanza na kuwahahikishia maoni ya wananchi yaheshimiwe. Je, Rasimu ya CCM ndicho alichomaanisha?
  4. Akafungua bunge na kuvuruga mchakato kwa kuwatusi wajumbe hadharani
  5. Akakutana na wapinzania kupitia TCD na kukubaliana waahirishe mchakato, je Dodoma ndicho alichokabdihiwa
  6. Sasa anadai S3 zinawezekana suala ni kujengewa hoja. Hicho hakukuiona alipokuwa anakutana na tume

Inaendelea…
 
Asante mkuu Nguruvi3 kwa bandiko zuri sana,
ni kwa hakika sasa mambo yamewafika shingoni na kuanza kuwanyonga, wnatumia kila mbinu kuhakalisha Haramu. Nimemsikiliza jana Rais Kikwete hotuba yake pamoja na mwenzie Shein nikangamua mambo mengi sana yapo nyuma ya pazia kuhusiana na hii bora katiba ya CCM.

Hakika sasa even the magicians run out of tricks, kila wanakofanya kuhalalisha haramu ya hii katiba uhalisia unawaumbua, naamini ni suala la muda tu Watanganyika nao watafunguka akili zao na kuzinduka katika usingizi mzito wa kukandamizwa fikra zao na watawala na kuanza kufanya maamuzi sahihi juu ya nchi zao.

Tuendelee kuelimishana mkuu, na asanteni sana kwa michango yenu yenye tija kwa taifa na inayotufungua macho tuone mbele zaidI
 
RAIA WAKATA TAMAA

HALI NI TETE KWASABABU HAWANA WA KUMSIKILIZA

SHERIA ZA MWITUNI HUENDA ZIKIFANYA KAZI

Kutokana na kukosa mwelekeo kwa Rais ambaye kazi kubwa ilikuwa kuliongoza taifa, wananchi wamekosa imani.
Hawatamsikiliza mtu yoyote wakati wanadai haki zao.Wameondokewa na wasi wasi kuhusu udanganyifu

Muungano upo mashakani,mchakato mzima umeibua mambo yasiyojulikana na yanayohitaji majibu.
Kwa upande wa Tanganyika, kuna kutosikilizwa hoja zao,wataendelea kubeba mzigo mzito kwa miaka mingi ijayo.

Jambo hili ni la hatari, linajenga hali ya chuki badala ya maridhiano.
Mfano, madai mengi ya Watanganyika sasa inabainika muungano si wa kiuchumi au kisiasa bali kuwabeba wazanzibar.

Watanganyika wanatambua jinsi znz imekuwa kama sehemu tofauti ya taifa hili, ikipewa vipaumbele bila kuwa na mchango wa aina yoyote kwa Mtanganyika au Tanzania kwa ujumla.

Wakati znz ikipata ubwete huo, Watanganyika wanalazimika kuumia zaidi kwa kodi na madeni ya maeneo yasiyowahusu.

Zanzibar ni nchi yenye tawala na kila chombo kama nchi kamili.
Watanganyika wanajiuliza, kuna sababu gani waumie kwa kodi kuelekeza eneo hilo lisilo sehemu ya nchi hii?
Kuna return gani kwa investment ya juu kiasi hicho kwa wazanzibar? Ni faida yake

Zanzibar si sehemu ya Tanzania kwa mujibu wa katiba yao.
Kwa hali ilivyo sasa ni znz haitakuwa tayari kubadili katiba kukidhi matakwa ya wanaCCM

Ndani ya BLW hakuna uwezekano wa kuapata muafaka wa kuifanyia katiba hiyo marekebisho.
Sehemu kubwa ya wawakilishi ni hawa UKAWA ambao Rais Kikwete amechezea akili zao.
Hatuoni ni kwa muafaka upi katiba ya znz inaweza kupata 2/3 achilia mbali 2/3 ya wananchi.

Kwa maneno mengine, rasimu ya CCM itatumika na kuleta mgongano mkubwa wa kikatiba.
Itakapofika hapo, hoja ya Watanganyika kuumia ndani ya muungano itakuwa na nguvu zaidi ya inavyodhaniwa.

Wao hawana mtetezi, na itabidi wakubaliane na wznz kuhusu katiba yao kwa gharama za Watanganyika

Kwamba, znz haiwezi kubadili katiba hilo halina mjadala, ni ukweli.
Kwamba rasimu ya CCM ikipitishwa kwa wizi wa kura n.k. itakinzana na ile ya znz , pia halina mjadala.

Katika mgongano huo wa kikatiba hakutakuwa na nafasi ya majadiliano tena.

Ikumbukwe wapinzani watakuwa na chuki ya kuchezewa akili na Kikwete.
Hilo tu litakwamisha kila jambo na itafika mahali hata kura za siri hazitasaidia.

Ni kwa mwendo huo, suala la muungano ni la muda tu.
Hali inaweza kuonekana imetulia, lakini si njema hata kidogo.

Jipu litakapotumbuka Kikwete atakuwa na mambo mawili ya kufanya
1. Ima kusitisha mchakato wa CCM unaotarajia kuanza kwa kutumia CCM aliopokea jana. Na itakuwa ni aibu na fedheha kubwa
2. Kulazimisha mchakato uendelee kwa gharama kubwa ya damu.

Jibu rahisi zaidi litakuwa kuvunja muungano ili kila upande uishi kwa amani.

Kama Kikwete anadhani amechanga karata vizuri kwa udanganyifu, hakika atakuwa amedanganywa.

Si zaidi ya mwezi mmoja ujao kutakuwa na vurugu. Narudia kutakuwa na vurugu ambazo zinaweza kupelekea umwagikaji wa damu.

Tunasema hivi kwa kuzingatia ukweli kuwa rasimu ya CCM imejenga mazingira nyevu 'fertile environment' ya vurugu.

Hasira zinazjijenga taratibu, zitakapofikia kiwango cha kutosha zitajitokeza.

Muungano sasa upo katika hali mbaya kuliko wakati mwingine wa historia ya miaka 50.

Tusemezane
 
KWANINI TUNAONA HATARI MBELE YA SAFARI NA TAIFA KWA UJUMLA?

Hatari inayolikabili taifa ni hii ya kudanganya watu na si kutafuta suluhu.
Kwa muda kumekuwa na madai ya wazanzibar wakaitaka nafasi zaidi za kujiendeleza kiuchumi.

Hali imebadilika , yapo madai muhimu sana ya Watanganyika ambayo yameibuiliwa na mchakato mzima.
Watanganyika hawakujua mambo mazito yanayowakabili.

Swali linakuja, je, baada ya wapinzani kuondoka na kubaki CCM, maswali muhimu yamejibiwa na rasimu ya CCM?


  1. Tanganyika imevaa koti la muungano.
  2. Je, rasimu haramu ya CCM ime address tatizo hilo? Kama haikuwa na jibu nini kinafuata kama si jipu kuendelea kujaza usaha
  3. Mambo mengi yameingizwa kinyemela kautoka mkataba wa muungano. Je, CCM wenyewe wameweza kujibu swali hilo kwa kuongeza na si kupunguza?


  1. S3 itakuwa ni mzigo kwa mlipa kodi. Je, CCM yenyewe bungeni wameweza kueleza upungufu wa gharama kwa muundo wa rasimu yao?
  2. Tanganyika imebeba mzigo mzito wa muungano. Je, CCM wenyewe wameweza kujibu hoja hiyo kwa kutumia rasimu yao?
  3. Kuna mgongano wa katiba ya JMT na ile ya SMZ. Je, CCM wenyewe wameweza kujibu swali hilo leo na siku za baadaye?

Maswali hayo ni muhimu kwa mustakabali wa muungano.
Kama hayana majibu, na ndivyo ilivyo, basi mazingira ya kuvunjika kwa muungano hayana utata tena bali suala la muda.

Utaweza kuona jambo kuhusu rasimu ya CCM. Tangu imetolewa hakuna msisimmko wa kujiadili kinyume na ile ya Warioba.

Hili linaeleza jambo moja, kwamba wananchi hawakuridhishwa na mchakato uliotupa maoni yao porini na kuchukua maoni ya wahafidhina wengine wakiwa hawana uadilifu.

Mkakati wa CCM si kwenda vijijini, huko wanajua kama kawaida yao wataungwa mkono na wananchi wasio na weledi.

Huko vijijini hawana tatizo la kuiba kura. Endapo wameweza kuiba kura ndani ya bunge nje ya bunge ni jambo rahisi sana.
Ni wazoefu wa hilo.

Kwa sasa wanaelekeza nguvu zao katika maeneo mawili makuu

  1. Kupata kuungwa mkono na kundi la wasomi. Mkakati ni kujadili rasimu katika TV na midahalo ili kuupa uhalali wa kitaifa hata kama inajulikana ni rasimu ya chama cha mapinduzi.
  2. Kutisha viongozi watakaokinzana na maoni ya viongozi hao. Mkakati umeanza na mwanasheria mkuu wa znz.
  3. Kupata kuungwa mkono na viongozi wa makundi ya dini walionunuliwa.

Katika makundi hayo matatu, mawili ni ‘vulnerable''

  1. a)Kutumia vyombo vya habari. Hapa watanunuliwa waandishi ili kuanza vipindi vya promotion ya rasimu ya CCM kama rasimu ya taifa. Kundi hili lina uteta sana kwasababu masilahi hukinzana sana na maadili ya kazi zzo. Bahasha zitafanya kazi
b)Wasomi, nao kama waandishi taratibu tutaanza kuwasikia wakizungumzia rasimu hii na wala si uharamu uliotokana na rasimu
yenyewe

2.Kutisha viongozi. Hili limeanza na litaendelea, ni katika harakati za kuchomeka matambara zaidi midomoni mwa CCM

3.Kuwanunu viongozi wa dini. Hili kundi lina matatizo sana. Ni kundi linalofanya kazi kama wanyama wa porini. Ni kundi lenye
utata, lisilo na mwelekeo na linalonunulika kirahisi sana.

Sehemu inayofuata tutaliangalia kundi la viongozi wa dini kwa undani ili kubainisha utata na matatizo yanayolikumba katika mchakato huu.

Itaendelea……
 
Endelea kutuelimisha mkuu, tunakushukuru kwa elimu hii njema,

nina mchango kidogo kuhusu viongozi wa dini,
Hawa watu ni watu wenye influence kubwa sana katika jamii yetu na basically ni watu ambao walitakiwa kuwa kama dira na viongozi wa haki kwenye jamii, tatizo lao kubwa wengi wao ni viongozi wa dini ambao wapo kimaslahi zaidi badala ya malengo halisi ya utumishi wao, hawa ukipenyeza rupia kidogo tu umeshawayumbisha na kuvuruga umoja wao, na hapa CCM wanajua kucheza nao vizuri sana.

Mfano dhahiri utaona mathalani makanisa kwa umoja wao walitoa tamko kuupinga uharamia wa katiba na ubabe wa mwenye kiti na walikua na standing zao toka mwanzo, kwa akili ya kawaida nilitegemea huo ndio msimamo wa viongozi wote wa dini hiyo, loooh, lahaula, wakajitokeza wengine tena wapo bungeni kushabikia ule upuuzi kinyume cha viongozi wao walio nje kuupinga, na nikashangaa wengine eti wakienda kusalisha siku ya makabishiano pale Dodoma, nikabaki kujiuliza umoja wao uko wapi, kumbe hawa sio wamoja maslahi yanaweza kuwagawanya kirahisi na kuchanganya waumini wao.

Lakini bado nawapa credit viongozi kadhaa wa kadha wa dini wana msimamo mwanzo mwisho, hawakubaliani na kila upuuzi unaopndekezwa na watawala, wakati wote hukosoa na kuonya pale wanapoona mapungufu, mentioning few ni Shura ya Maimam, Ask. kakobe, Padr. Mapunda,Ask. Ngalalekumtwa na wengineo, hawa japo hawajawa na misimamo ya 100% lakini anagalau wameonyesha guts za kuikosoa serikali kwenye huu mchakato wa bora katiba iliyoandaliwa na ccm na washirika wake.

Ninaamini viongozi wa dini wana impact kubwa sana na watatumika sana kujaribu kuhalalisha haramu hii ya bora katiba ya CCM na washirika wake, na kwa nchi yetu ambapo uelewa wa wa wanchi wake wengi upo chini, udanganyifu mkubwa sana utafanywa na hawa watu, ambao bila aibu watashabikia hii katiba ambayo mwenyekiti wake Sitta aliwatukana viongozi wao na kuwadharau
 
Back
Top Bottom