Dkt. Mpango, Watanzania wana haki ya kujua viongozi wao walipo na wanachofanya

Burkinabe

JF-Expert Member
Feb 12, 2023
1,926
3,237
Habari wanajamvi.

Moja kwa moja kwenye mada.

Hivi karibuni kumezuka taharuki ambayo haikuwa na sababu ya msingi, juu ya wapi alipo Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Philip Isdory Mpango. Makamu huyu alikuwa hajaonekana hadharani kwa takribani mwezi mzima kwa mujibu ya vyanzo vya habari ikiwamo mitandao ya kijamii.

Hali hii ilipelekea Watanzania waulize ni wapi alipo kiongozi wao huyo kwa muda upatao wiki 2 au zaidi. Kumekuwa na uvumi na habari mbalimbali za kukanganya Umma, huku wengine wakidai yuko nje ya nchi kwa kazi "maalum", wengine anaumwa na anafanyiwa upasuaji wa koo huko Korea Kusini, wengine wakienda mbali zaidi na kusema ameshafariki!

Serikali iliamua kukaa kimya, ukitoa tamko la waziri Mkuu ambalo pia lilikuwa linaacha maswali mengi kwa raia.

Sasa shida imekuja baada ya Makamu wa Rais kuibukia kanisani na baadaye Ikulu na kuanza kuwashutumu Watanzania waliokuwa wanataka kujua yuko wapi na anafanya nini!

Dkt. Mpango, sisi kama Watanzania tulikuwa tunakuulizia kwa sababu ya nafasi yako unayoishikilia kwa sasa na wala siyo vinginevyo.

Ndiyo maana hatujawaulizia Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Edward N. Lowasa, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Mzee Ali Hassan Mwinyi n.k. Hatuwezi kuwaulizia hao siyo kwa sababu hawana umuhimu kwetu, bali kwa sababu hawako kwenye ofisi zetu za Umma na kwa hiyo hawana msaada kwetu wa moja kwa moja kama ulivyo wewe pamoja na viongozi wengine mlioko madarakani kwa sasa.

Nimalizie kwa kukumbushia tu kile ambacho Wakili Mwabukusi aliwahi kusema, kwamba, "kama kuna kiongozi wa Umma ambaye hataki kufuatiliwa na Umma au hataki mambo yake yajulikane kwa Umma, basi ajiudhuru aone kama tutataka kujua chochote kumuhusu yeye au familia yake."
 
Daktari Philip Isdor Mpango, habari?

Prof Chachage Seithy Loth Chachage - alitumia neno ‘Collective Imbecilization’ kueleza uzuzu, ubwege, ufala wa pamoja unaoweza kufanywa na serikali

Hili jaribio la kuwapumbaza watu mamilioni kwa mpigo. Ni kama vile kuwakusanya watu milioni 50, ukawaweka ndani ya ukumbi mmoja kwa ukubwa huo

Ukafunga madirisha na milango, ukawanyunyizia dawa ya uzuzu, ubwege na ufala, ikawakolea, ukawaachia waende Duniani waendelee shughuli zao.

Haiwezekani, isipokuwa inawezekana watu wakapumbazwa kwa pamoja, wakafanywa mazuzu kwa pamoja, wakageuzwa mabwege kwa pamoja

Hata kama watu hao hawajioni ndani ya ukumbi huo na hawasikii harufu ya dawa ya ajabu wanayopuliziwa na kuwafanya kuwa mabwege na mazuzu.

Ipo mifumo imetumika, kutufanya sote tuwe mazuzu kama ambavyo alieleza Chachage alipokuwa akizungumzia “collective imbecilization”

Kwamba Makamu wa Rais ni special force au secret service? Kwamba Makamu wa Rais unatumwa kazi za siri za serikali? Ukajificha usijulikane ulipo?

Daktari Mpango, hivi ni kwanini unawaona watanzania wote ni mazuzu? Tunakubaliana kwamba, mazuzu yapo, lakini siyo wote ni mazuzu.

Dkt. Mpango, usilalamikie mitandao ya kijamii. Lawama peleka ofisi ya Makamu wa Rais. Watanzania wanayo haki ya kuhoji alipo Makamu wa Rais.

Dkt. Mpango, unashukuru kuombewa na watu gani? Wanakuombea wapi na vipi wakati unasema ulikuwa katika shughuli maalum na siyo ugonjwa?

Watanzania hawajui ulipokuwa ukipokea matibabu Korea Kusini. Ni wapekuzi wachache tulifahamu hadi jina la hospitali uliyofanyiwa upasuaji.

Ulikaa kimya umetumwa kazi ya kijasusi, mwezi mmoja baadae, uibukie kanisani halafu ukapokelewe Ikulu na Rais? Aah! Akili gani hii Daktari?

Ni mara ya pili hii, unazusha taharuki ukiwa katika matibabu, baadae unatoka kuzungumza na umma, unawasuta. Kuna kusema ulikuwa mgonjwa?

Na kwanini unawafokea watu waliokuwa wanauliza makamu wa Rais yupo wapi? Unasema ulikuwa unaona kila kitu ukiwa mafichoni, ukanyuti.

Sasa kwanini unawasuta leo watu wanaokupenda na walikuwa wanauliza ulipo? Kwamba hawakuwa na haki ya kuuliza Makamu wa Rais alipo?

Hii ni tabia mbaya na haitakiwi kuwa desturi kwa watawala kuwapumbaza watanzania. Tunakataa. Watanzania ndiyo mabosi wenu viongozi/watawala.

Unapotea, mwezi haujulikani ulipo. Waajiri wako tunaanza kukutafuta, umejificha sehemu (tunajua hospitali), unatuchora tu? Unaona upo sawa?

Ok! Baada ya mwezi mzima, unapatikana, unaibuka kanisani na Ikulu, kutufokea. Unatufokea watu tunakununulia kila kitu ambacho unakula na kuvaa?

Daktari Mpango, Rais ni bosi wako, sisi, watanzania ni waajiri wako, sisi ndiyo mabosi wako, pia mabosi wa Rais. Unawajibika kwa Rais, unatumikia wananchi.

Daktari, SIJAPENDA.

Brigedia Mtikila, MMM
 
Siku zote sie masikini kufurahia kifo cha watu walio tuzidi au kufanikiwa kimaisha. Sidhani kwamba wengi walio hoji mpango iko wapi ni kwa ajiri ya mapenzi laa wengi walitaka kusaka taarifa ya kuwafurahisha ya kifo. Watanzania tunaishi kiunafiki sanaaa.
 
Siku zote sie masikini kufurahia kifo cha watu walio tuzidi au kufanikiwa kimaisha.......sidhani kwamba wengi walio hoji mpango iko wapi ni kwa ajiri ya mapenzi laa wengi walitaka kusaka taarifa ya kuwafurahisha ya kifo.....watanzania tunaishi kiunafiki sanaaa
Huu ni uhalisia wa jamii ya kimasikini hasa Tanzania. Tunachukia watu waliotuzidi hata kama ni kidogo tu.

Kuna kipindi niliishi kijiji fulani, sikuwahi kuwa na mgogoro na mtu. Siku moja nikapata ajali ya pikipiki majira ya saa mbili usiku nikiwa kijiji cha nne kutoka pale nilipokuwa nikiishi na kukimbizwa hospitali nikiwa sijaumia ila nilipoteza fahamu kwa muda mfupi nikajitambua (nilikuwa na jamaa wa kijiji kingine ambaye alivunjika mkono).

Ajabu niliporuhusiwa asubuhi mapema narudi kijijini nawakuwa watu kibao (ambao wana utamaduni wa kuchelewa kuamka na kufungua biashara zao kwenye ile senta) wamefungua bar wanakunywa pombe kusherekea kuwa nimefariki! Siku hiyo ndo niliwaelewa wale wanaosema umasikini ni laana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ni uhalisia wa jamii ya kimasikini hasa Tanzania. Tunachukia watu waliotuzidi hata kama ni kidogo tu.

Kuna kipindi niliishi kijiji fulani, sikuwahi kuwa na mgogoro na mtu. Siku moja nikapata ajali ya pikipiki majira ya saa mbili usiku nikiwa kijiji cha nne kutoka pale nilipokuwa nikiishi na kukimbizwa hospitali nikiwa sijaumia ila nilipoteza fahamu kwa muda mfupi nikajitambua (nilikuwa na jamaa wa kijiji kingine ambaye alivunjika mkono).

Ajabu niliporuhusiwa asubuhi mapema narudi kijijini nawakuwa watu kibao (ambao wana utamaduni wa kuchelewa kuamka na kufungua biashara zao kwenye ile senta) wamefungua bar wanakunywa pombe kusherekea kuwa nimefariki! Siku hiyo ndo niliwaelewa wale wanaosema umasikini ni laana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio masikini wote tuko hivo hapana tuko masikini tunaojitambua kwanini ni sherekee kifo cha mwenzangu kisa kanizidi jambo fulani......ila watanzania wengi ndo tulivo ata makazini mimi staki rafiki tena nahitaji comrades tu
 
Daktari Philip Isdor Mpango, habari?

Prof Chachage Seithy Loth Chachage - alitumia neno ‘Collective Imbecilization’ kueleza uzuzu, ubwege, ufala wa pamoja unaoweza kufanywa na serikali

Hili jaribio la kuwapumbaza watu mamilioni kwa mpigo. Ni kama vile kuwakusanya watu milioni 50, ukawaweka ndani ya ukumbi mmoja kwa ukubwa huo

Ukafunga madirisha na milango, ukawanyunyizia dawa ya uzuzu, ubwege na ufala, ikawakolea, ukawaachia waende Duniani waendelee shughuli zao.

Haiwezekani, isipokuwa inawezekana watu wakapumbazwa kwa pamoja, wakafanywa mazuzu kwa pamoja, wakageuzwa mabwege kwa pamoja

Hata kama watu hao hawajioni ndani ya ukumbi huo na hawasikii harufu ya dawa ya ajabu wanayopuliziwa na kuwafanya kuwa mabwege na mazuzu.

Ipo mifumo imetumika, kutufanya sote tuwe mazuzu kama ambavyo alieleza Chachage alipokuwa akizungumzia “collective imbecilization”

Kwamba Makamu wa Rais ni special force au secret service? Kwamba Makamu wa Rais unatumwa kazi za siri za serikali? Ukajificha usijulikane ulipo?

Daktari Mpango, hivi ni kwanini unawaona watanzania wote ni mazuzu? Tunakubaliana kwamba, mazuzu yapo, lakini siyo wote ni mazuzu.

Dkt. Mpango, usilalamikie mitandao ya kijamii. Lawama peleka ofisi ya Makamu wa Rais. Watanzania wanayo haki ya kuhoji alipo Makamu wa Rais.

Dkt. Mpango, unashukuru kuombewa na watu gani? Wanakuombea wapi na vipi wakati unasema ulikuwa katika shughuli maalum na siyo ugonjwa?

Watanzania hawajui ulipokuwa ukipokea matibabu Korea Kusini. Ni wapekuzi wachache tulifahamu hadi jina la hospitali uliyofanyiwa upasuaji.

Ulikaa kimya umetumwa kazi ya kijasusi, mwezi mmoja baadae, uibukie kanisani halafu ukapokelewe Ikulu na Rais? Aah! Akili gani hii Daktari?

Ni mara ya pili hii, unazusha taharuki ukiwa katika matibabu, baadae unatoka kuzungumza na umma, unawasuta. Kuna kusema ulikuwa mgonjwa?

Na kwanini unawafokea watu waliokuwa wanauliza makamu wa Rais yupo wapi? Unasema ulikuwa unaona kila kitu ukiwa mafichoni, ukanyuti.

Sasa kwanini unawasuta leo watu wanaokupenda na walikuwa wanauliza ulipo? Kwamba hawakuwa na haki ya kuuliza Makamu wa Rais alipo?

Hii ni tabia mbaya na haitakiwi kuwa desturi kwa watawala kuwapumbaza watanzania. Tunakataa. Watanzania ndiyo mabosi wenu viongozi/watawala.

Unapotea, mwezi haujulikani ulipo. Waajiri wako tunaanza kukutafuta, umejificha sehemu (tunajua hospitali), unatuchora tu? Unaona upo sawa?

Ok! Baada ya mwezi mzima, unapatikana, unaibuka kanisani na Ikulu, kutufokea. Unatufokea watu tunakununulia kila kitu ambacho unakula na kuvaa?

Daktari Mpango, Rais ni bosi wako, sisi, watanzania ni waajiri wako, sisi ndiyo mabosi wako, pia mabosi wa Rais. Unawajibika kwa Rais, unatumikia wananchi.

Daktari, SIJAPENDA.

Brigedia Mtikila, MMM
Nafikiri kuhoji halikuwa tatizo, tatizo lilikuwa kwa wale waliohusisha swala hilo na kifo, hadi kupelekea kuweka picha yake na mishumaa kuashiria kuwa ameshafariki kitu ambacho hakikuwa kweli.

Kifo kipo na kila binadam atakufa. Lkn sasa kulikuwa na uharaka gani wa kukimbilia kulihusisha swala hilo na kifo indirect bila kutangaziwa kuwa tayari ameshafariki au la?

Ni kama vile kuna watu walijaribu kulitumia swala hili kisiasa kama walivyotumia kwa yule mlinzi wa Magufuli, matokeo yake alielitumia akaja kuumbuka baada ya mwenyewe kujitokeza na kusema alipokuwa.
 
Back
Top Bottom