Tetesi: Dili la Mayele kwenda Pyramid lina asilimia kubwa ya kubuma, huenda akaungana na Feitoto Azam

LIKUD

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
15,204
27,328
Kwa jinsi mambo yanavyokwenda inaonekana hao Pyramid hawana hata shida na Mayele kihivyo. Ni hivi za nyuma ya kapeti kutoka mitaa ya jangwani ni kwamba:

1. Mpaka sasa Pyramid bado hawajaingiza hata senti tano kwenye akaunti ya Yanga kwa ajili ya malipo ya kumnunua Mayele.

2. Yanga wamewapa Pyramid siku tatu kutoka jana wawe wamesha ingiza pesa or else Yanga watafanya maamuzi mengine.

3. Pamoja na Yanga kutoa hiyo ultimaltum lakini Pyramid bado wapo kimya wala hawajafanya movement yoyote (Wanasuasua).

4. Yanga wamesha mleta Dar striker wa mabao (Emmanuel Mahop kutoka Cameroon/ ambae ndio mfungaji bora wa ligi ya Cameroon msimu ulio pita akifunga magoli kumi na tano Kati ya mechi ishirini alizo cheza plus assist tatu)

5. Pamoja na kumleta Mahop ili awe mrithi wa Mayele lakini Yanga bado hawajamsainisha Mahop kwa sababu bado hawana uhakika na dili la Mayele. Wanahofia kwamba endapo watamsaini Mahop watakuwa wamekamilisha idadi ya wachezaji wa kigeni. Ikitokea Pyramid wasipo weka mkwanja kwa ajili ya kumnunua Mayele dili la Mayele litakufa na Mayele atakosa nafasi ya kucheza Yanga so Yanga ima watalazimika kumuuza Mayele kwenye timu ambayo itakuwa na nafasi ya mchezaji wa kigeni (Azam wanatajwa kuwa tayari kumnunua Mayele endapo dili lake litabuma) au kumtoa Azizi Ki kwa Mkopo kwenda Singida FG ili wamsaini Mahop ampe changamoto Mayele au wasitishe mpango wa kumsajili Mahop.

6. Inasemekana Wakili Jasmini ambae ni msimamizi wa Mayele anataka Mayele aende Azam kuungana na Fei Toto.

Let's wait and see hii sinema inaishia wapi.

Ushauri wangu kwa uongozi wa Yanga: Msainisheni Mahop, ni mtu na nusu. Dili la Mayele kwenda Pyramid hata likibuma muuzeni Azam akaungane na Fei Toto. Endeleeni na spirit yenu ya kutomnyenyekea mchezaji kwa sababu hata hivyo hachezi bure analipwa.

Muacheni Mayele akacheze na Fei Toto kama alivyopiga kijembe kwenye instagram live juzi kwamba amemiss sana kucheza na Fei na atatamani sana kucheza na Fei plus kijembe alichopiga wiki kadhaa zilizopita kwamba eti wacongo wanapenda sana hela (kwani watu wa nchi gani ndio hawapendi hela)

Mashabiki wa Yanga wamesha move on na tayari nafsi zao zimeshakubali kuishi bila Mayele.

Ushirikiano wake na Fei na taarifa kwamba alikuwa anaidengulia Yanga kusaini mkataba mpya vimewafanya mashabiki wa Yanga waanze kumtoa taratibu kwenye nafsi zao.

Wakili Jasmini hayupo tena loyal kwa Yanga, suala la Fei bado analichukulia personal dhidi ya Hersi. Anacho kitaka yeye ni kuona Hersi anafeli hivyo sio busara kuendelea kuwa na mchezaji ambae anasimamiwa na Jasmini.

Yanga will always be Yanga with or without Mayele.
 
Mpaka kesho Fergusion anaendelea kuwa kocha bora niliye mshuhudia,aliweka misingi ya kwamba hamna mkubwa zaidi ya club na yeye ndio boss. Ndio maana yule jamaa alikuwa anapata mafanikio makubwa, kwa wachezaji wa kawaida.

Mchezaji kama haitaki club maana yake hatacheza kwa moyo, Man Utd kulikuwa na Park,Mached,Fletcher, Brown, Oshea nk.Wachezaji walikuwa wakawaida ila walikuwa na nidhamu na kucheza kwa moyo na kwa maelekezo ya kocha.

Kama hataki aende cha msingi hela yetu na kama ikiwezekana kama wakala haeleweki, uza wachezaji wake wote na usichukue mchezaji anaye milikiwa nae.

Sasa hivi tena huyo Jasminie kawaambia Yanga,gharama za Msuva mil 700,anazani anaikomoa Yanga wakati ukiingia Kongo, Zambia, Uganda unapata winga kwa dola 100k sema basi bongo hatujawekeza sana kwenye Scout.Hata huyo Bacca nae kama huyo mama akimjaza upepo wa mwache nae.
 
Kwa jinsi mambo yanavyokwenda inaonekana hao Pyramid hawana hata shida na Mayele kihivyo. Ni hivi za nyuma ya kapeti kutoka mitaa ya jangwani ni kwamba:

1. Mpaka sasa Pyramid bado hawajaingiza hata senti tano kwenye akaunti ya Yanga kwa ajili ya malipo ya kumnunua Mayele.
Hamna tofauti na Kuku waliokatwa vichwa. Ukiamka tu mkeo akakwambia mboga ya Jana ilibaki basi unakuja kutusumbua na habari za kuungaunga.
 
Back
Top Bottom