Dada yangu ukipata mtu mnayependana usimvuruge akaenda, utajutia baadae

Matongee

JF-Expert Member
Jun 17, 2023
630
1,527
Kabla ya yote tukae kimya dakika moja kuwaombea wale wote ambao wake zao wanaendeleza mawasiliano na waliokuwa wapenzi wao (ma-ex). Wanapitia magumu kwa kujua au bila kujua. Wanastahili sala zetu.

Mimi nikiwa kijana mwenye uzoefu mkubwa na haya mambo ya mapenzi kwa huu ukanda chini ya jangwa la Sahara nimeona leo nisemee hili suala la kina dada walio wengi kuendelea kuhangaika na waliokuwa wapenzi wao huku tayari wakiwa ndani ya ndoa. Ni tabia mbaya ambayo hata shetani anaweza kukataa kuhusishwa nayo. Binafsi ni mfuasi wa ule msemo wa "Ombea adui yako aishi siku nyingi ili unapobarikiwa ajionee kwa macho"... hii ni kumaanisha kuwa sina tabia ya kublock mtu tukiachana. Huwa ninakubaliana na hali na kuendelea na mishe zangu.

Nimeandika uzi kwasababu ninasikitishwa na tabia za waliokuwa wapenzi wangu kuendelea kunipigia simu mara kwa mara na kutuma msgs. Video calls nazo zimekuwa zikipigwa. Huwa hakuna cha maana wanachosema zaidi ya salamu na kukumbushia mambo yaliyopita. Kuna mmoja huwa anapatwa na hisia kali na kuanza kunilaumu mimi ndo chanzo tusioane.

Baada ya kutafakari kwa kina nimegundua mimi ni mtu mwema na mwaminifu sana nikiwa kwenye uhusiano. Pia ni mtu niliye na commitment 100% kwenye uhusiano. Watu kama mimi huwa wanapatikana kwa nadra sana. Ninashauri kina dada wanapopata mtu kama mimi wasituvuruge bali nao pia wawe committed ili kufanikisha suala la ndoa badala ya kuolewa na mtu hajampenda. Matokeo yake baadae ni kutusumbua na kutaka kututia kwenye matatizo ya kuwasiliana na wake za watu.
 
Back
Top Bottom