Undava King
JF-Expert Member
- Aug 11, 2017
- 3,253
- 5,411
Katika kitabu kilichoandikwa na Sir Ernest Alfred Wallis Budge "Legends of the Gods" tunapata simulizi nzuri ya miungu ya kimisri ambayo inatupatia mwangaza kidogo katika hili la chanzo cha Mungu kulingana na kwamba hadithi hizi zimekuwapo miaka maelfu kabla ya ujio wa maandiko ya dini za kileo.
Kitabu hiki kinazungumzia vyema chanzo na mwanzo wa dhana ya uwepo wa Mungu na kinatoa ufafanuzi mzuri ambao unakosekana katika maandiko matakatifu ya dini ambayo hayajaweza kuelezea kinaga ubaga juu ya kipi kilifanyika kuwa umungu kabla ya Mungu kufanya uumbaji wake.
Simulizi hii haiwezi kukamilika ikiwa hatutoweza kumzungumzia Neb-er tcher (the lord to the uttermost limit) yenye maana ya "Bwana asiye na ukomo" Neno "ukomo" uashiria muda na nafasi (time & space), na ndiye Mungu wa milele wa ulimwengu.
Ni jinsi gani aliweza kutokea huyu Neb-er tcher haijazungumzwa katika kitabu cha wahenga hawa, isipokuwa katika maandiko ya kikoptiki, anaongelewa kwa sifa zote za Kimungu waleo.
Neb-er tcher alikuwa na nguvu zisizoshindwa wala kuwa na kikomo ambazo zilitanda mahali pote katika nafasi yenye utupu. Pindi alipopata shauku ya kuumba dunia, hapo ndipo alipouvaa uhusika kama Mungu Khepera, ambaye ni mwanzo na mwisho;Muumba. Akitambulika kama Mungu muumba na wamisri.
Wakati Neb-er tcher akibadilika kuwa Khepera dunia ilikuwa bado haijaumbwa. Kwa hali iliyoonekana ni kuwa kwa wakati huo kulikuwa na maji mengi sana ambayo yalitanda juu ya uso wa ulimwengu au dunia nzima ya wakati huo iliyoitwa NU, na uwezekano ni kuwa ndani ya bahari hii ndipo mabadiliko yalikochukulia nafasi.
Ndani ya bahari hii kuu kulikuwamo na chembe chembe za uhai wa viumbe wote ambao nao baadae walikuja kuvaa uhusika wa viumbe mbingu na ardhi. Lakini kwa nyakati hizi waliishi katika hali ya utepetevu na kutojiweza.
Kutoka ndani ya bahari hii kubwa ndipo Khepera alikojiinua, hivyo akafahulu kupita hali ya utepetevu na ajizi (state of passiveness and inertness) mpaka katika kutenda.
Pindi Khepera alipokuwa katika hatua za kujiinua kutoka katika lindi kubwa la maji alikumbana na hali ya sintofahamu baada ya kujikuta katika sehemu ya utupu wa space pasipo hata na mahali pa kukanyaga/kujitegemezea.
Katika toleo la pili la mafunjo (papyrus) ya kimisri inaelezea kuwa Khepera alijipatia uwezo wa kuendelea kuwepo katika hali ya kujitegemeza pasipo mahali pa kutia unyayo au kushikilia chochote kupitia kulitamka jina lake mwenyewe. Tukirudi katika toleo la kwanza la maandiko ya mafunjo linatudokeza kuwa Khepera alitumia maneno ili kujitwalia mahali pake anapoweza kukanyaga.
Kwa maana nyingine ni kuwa wakati Khepera akiwa bado ni sehemu ya kiumbe Neb-er tcher, alitamka NENO "Khepera" na punde Khepera akatokea. Vivyo hivyo alipohitaji mahali pa kujitegemeza katika nafasi tupu (space) alitamka tu majina ya vitu na vikawa.
Toleo hilo hilo la kwanza linazungumzia pia juu ya Moyo, wakati toleo la pili likizungumzia uwepo wa Roho ya Nafsi (heart-soul) namna ilivyo mwezesha muumba katika kufikia ubunifu wa kutenda. Kwa namna hii aliweza kutambua kupitia moyo wake kipi akitaraji kukiumba na namna gani akipe jina na punde kiwe kama alivyotarajia kiwe.
Mfumo huu wa kifikra uelezewa na wamisri kama "Laying the foundation in the heart" yaani kujiwekea msingi wa kiroho moyoni. Ili kufanikisha yote haya Khepera pia alipata msaada toka kwa Mungu mke Maat, ambaye uchukuliwa kama Mungu wa sheria, Agizo na ukweli.
Na katika nyakati za zamani Maat alichukuliwa kuwa kama sehemu ya kike ya Mungu Thoth "the heart of the god Ra" yaani moyo wa Mungu Ra. Kwa mujibu wa wahenga inaonekana kama Maat alichukua uhusika zaidi wa kuwa Mungu wa Hekima "wisdom" kama ilivyoelezewa katika kitabu cha Mithali, "for it was by Maat that he "laid the foundation" ikimaanisha kuwa 'ni kwa kupitia Maat, "aliweza kusimika misingi.
Sasa kutokana na tukio lile la kusimama, ikatokea kitu ambacho wamisri walikipachika uhusika wa triad au trinity "UTATU" Khepera alipata kuunganika na kivuli chake na matokeo yake ni kupata kizazi ambacho kilitokana na mwili wake na kuunda miungu Shu na Tefnut.
Kulingana na maandiko ya kwenye mapiramidi tukio hili lilitokea katika eneo lijulikanalo kama ON (Heliopolis) tumezoea kupaita mbinguni. Na kwa namna ya kale ya hadithi za kihenga zinaelezea kwa kuhusisha uzalishaji wa Shu na Tefnut na kitendo cha kujichua.
Kiuhalisia miungu hii inavaa uhusika wa hewa na ukavu pamoja na vimiminika, kutokana na kuumbwa kwao ndipo vifaa (material) vya ujenzi wa anga na matabaka yake vikapatikana.
Shu na Tefnut walibarikiana, na vizazi vyao ni Keb;Mungu wa dunia, na Nut; Mungu mwana mke wa anga.
Mpaka hapo tunakuwa na miungu mitano jumla yaani:
Khepera- mwenye kanuni nzima ya ubunifu (the creative principle)
Shu- Tabaka la angahewa (the atmosphere)
Tefnut- Maji ya anga/mvua (the waters above the heavens)
Nut- Mungu mwanamke wa anga (the sky-goddess)
Keb- Mungu wa dunia (the earth-god)
Katika kipindi hiki jua lilikotokea na kuangaza kwa mara ya kwanza kutoka katika vilindi vya maji ya NU, nakuangazia dunia na ikatokea mchana.
Katika zama za kale mwanga wa jua ulichukuliwa kama muundo wa Shu. Miungu Keb na Nut waliunganishwa katika mwanga na kubarikiana na ujio wa mwanga ndiyo uliokuwa ukiwatenganisha; mfano inapotokea ikawa ni mchana, Nut; Mungu mke wa anga, alibakia katika eneo lake juu ya dunia, akipata support toka kwa Shu, lakini pindi jua linapozama uachilia anga na taratibu uteremka mpaka pale linapotua juu ya mwili wa Keb; Mungu wa dunia.
Sasa kubariki huku kukapelekea Keb na Nut kupata miungu wengine watano baada ya kuzaliwa; Osiris, Horus, Set, Isis na Nephthys.
Osiris na Isis walioana hata kabla ya kuzaliwa kitendo kilichopelekea kuzaliwa kwa mwanao wa kiume aliyeitwa Horus; Set na Nephthys nao vivyo hivyo wakamzaa Anpu (Anubis), japo huyu Anu ajaongelewa kiundani na wahenga katika simulizi zao.
Katika miungu wote hawa ni Osiris pekee ndiye aliyetajwa katika maandiko ya wahenga kwa kupewa umuhimu ambapo katika simulizi ya Khepera akiongea kama Neb-er tcher, anasema kuwa jina lake ni Ausares, yeye ambaye ni kiini cha jambo la kitambo kirefu ambalo yeye mwenyewe ameundwa/kutokana nalo. Hivyo Osiris alikuwa wa dutu ile ile kama Mungu mkuu aliyeumba ulimwengu.
Kulingana na maandiko haya ya wamisri yanatanabaisha kuwa kuzaliwa kwake duniani Osiris ilikuwa ni re-incarnation ya babu mkuu.
Kipande hiki cha maelezo ya wahenga kinatusaidia kupata majawabu juu ya mtizamo uliojengwa juu ya Osiris kwa miaka mingi kuhusiana na kuchukuliwa kama roho kuu ya mababu (the great ancentral spirit) ambaye kipindi alipokuwa duniani alileta faida kubwa kwa binadamu na alipokuwa mbinguni alikuwa ni mwokozi wa nafsi.
Wahenga wanalizungumzia jua kama jicho la Khepera au Neb-er tcher, ambalo upatwa na misukosuko mingi inayopelekea kufifisha mwanga wake na hivyo kabla ya anguko lake na kuzima kabisa, Mwezi uliyoundwa na Khepera utumike kama jicho la pili uangaza badala ya jua na kuupa furaha jicho hilo la kwanza.
Hivyo jua alilipatia kipaumbele maalumu kwa kulipachika katikati ya kipaji chake cha uso na kulipa mamlaka ya kutawala juu ya uso wa dunia na kuwezesha uhai huku mwezi wenyewe ukiusishwa na nguvu ya uzazi na mavuno.
Kulingana na simulizi za wahenga, Mwanaume na Mwanamke hawatokani na dunia, bali moja kwa moja kwenye mwili wa Mungu Khepera au Neb-er tcher, ambaye aliwaweka pamoja watu wake na kuwanyunyizia machozi yake, papo hapo wakawa viumbe hai, kutokana na machozi yaliyodondoka kutoka katika macho yake.
Hakuna mahali katika simulizi ambapo viumbe wengine (ukiachilia binadamu) wamepewa umuhimu katika uumbaji wao, isipokuwa aliumba kila kitu kwa namna yake, ikiwemo na viumbe wakubwa, wakiume kwa wakike,na viumbe vyote vilizaliana na kuongezeka kwa namna zao na kwa sababu hiyo dunia ikajazwa na uzazi wao mpaka waleo.
NB: Hii ni kwa kujibu wa maandiko kutoka katika papyrus of Nes-Menu.
Kitabu hiki kinazungumzia vyema chanzo na mwanzo wa dhana ya uwepo wa Mungu na kinatoa ufafanuzi mzuri ambao unakosekana katika maandiko matakatifu ya dini ambayo hayajaweza kuelezea kinaga ubaga juu ya kipi kilifanyika kuwa umungu kabla ya Mungu kufanya uumbaji wake.
Simulizi hii haiwezi kukamilika ikiwa hatutoweza kumzungumzia Neb-er tcher (the lord to the uttermost limit) yenye maana ya "Bwana asiye na ukomo" Neno "ukomo" uashiria muda na nafasi (time & space), na ndiye Mungu wa milele wa ulimwengu.
Ni jinsi gani aliweza kutokea huyu Neb-er tcher haijazungumzwa katika kitabu cha wahenga hawa, isipokuwa katika maandiko ya kikoptiki, anaongelewa kwa sifa zote za Kimungu waleo.
Neb-er tcher alikuwa na nguvu zisizoshindwa wala kuwa na kikomo ambazo zilitanda mahali pote katika nafasi yenye utupu. Pindi alipopata shauku ya kuumba dunia, hapo ndipo alipouvaa uhusika kama Mungu Khepera, ambaye ni mwanzo na mwisho;Muumba. Akitambulika kama Mungu muumba na wamisri.
Wakati Neb-er tcher akibadilika kuwa Khepera dunia ilikuwa bado haijaumbwa. Kwa hali iliyoonekana ni kuwa kwa wakati huo kulikuwa na maji mengi sana ambayo yalitanda juu ya uso wa ulimwengu au dunia nzima ya wakati huo iliyoitwa NU, na uwezekano ni kuwa ndani ya bahari hii ndipo mabadiliko yalikochukulia nafasi.
Ndani ya bahari hii kuu kulikuwamo na chembe chembe za uhai wa viumbe wote ambao nao baadae walikuja kuvaa uhusika wa viumbe mbingu na ardhi. Lakini kwa nyakati hizi waliishi katika hali ya utepetevu na kutojiweza.
Kutoka ndani ya bahari hii kubwa ndipo Khepera alikojiinua, hivyo akafahulu kupita hali ya utepetevu na ajizi (state of passiveness and inertness) mpaka katika kutenda.
Pindi Khepera alipokuwa katika hatua za kujiinua kutoka katika lindi kubwa la maji alikumbana na hali ya sintofahamu baada ya kujikuta katika sehemu ya utupu wa space pasipo hata na mahali pa kukanyaga/kujitegemezea.
Katika toleo la pili la mafunjo (papyrus) ya kimisri inaelezea kuwa Khepera alijipatia uwezo wa kuendelea kuwepo katika hali ya kujitegemeza pasipo mahali pa kutia unyayo au kushikilia chochote kupitia kulitamka jina lake mwenyewe. Tukirudi katika toleo la kwanza la maandiko ya mafunjo linatudokeza kuwa Khepera alitumia maneno ili kujitwalia mahali pake anapoweza kukanyaga.
Kwa maana nyingine ni kuwa wakati Khepera akiwa bado ni sehemu ya kiumbe Neb-er tcher, alitamka NENO "Khepera" na punde Khepera akatokea. Vivyo hivyo alipohitaji mahali pa kujitegemeza katika nafasi tupu (space) alitamka tu majina ya vitu na vikawa.
Toleo hilo hilo la kwanza linazungumzia pia juu ya Moyo, wakati toleo la pili likizungumzia uwepo wa Roho ya Nafsi (heart-soul) namna ilivyo mwezesha muumba katika kufikia ubunifu wa kutenda. Kwa namna hii aliweza kutambua kupitia moyo wake kipi akitaraji kukiumba na namna gani akipe jina na punde kiwe kama alivyotarajia kiwe.
Mfumo huu wa kifikra uelezewa na wamisri kama "Laying the foundation in the heart" yaani kujiwekea msingi wa kiroho moyoni. Ili kufanikisha yote haya Khepera pia alipata msaada toka kwa Mungu mke Maat, ambaye uchukuliwa kama Mungu wa sheria, Agizo na ukweli.
Na katika nyakati za zamani Maat alichukuliwa kuwa kama sehemu ya kike ya Mungu Thoth "the heart of the god Ra" yaani moyo wa Mungu Ra. Kwa mujibu wa wahenga inaonekana kama Maat alichukua uhusika zaidi wa kuwa Mungu wa Hekima "wisdom" kama ilivyoelezewa katika kitabu cha Mithali, "for it was by Maat that he "laid the foundation" ikimaanisha kuwa 'ni kwa kupitia Maat, "aliweza kusimika misingi.
Sasa kutokana na tukio lile la kusimama, ikatokea kitu ambacho wamisri walikipachika uhusika wa triad au trinity "UTATU" Khepera alipata kuunganika na kivuli chake na matokeo yake ni kupata kizazi ambacho kilitokana na mwili wake na kuunda miungu Shu na Tefnut.
Kulingana na maandiko ya kwenye mapiramidi tukio hili lilitokea katika eneo lijulikanalo kama ON (Heliopolis) tumezoea kupaita mbinguni. Na kwa namna ya kale ya hadithi za kihenga zinaelezea kwa kuhusisha uzalishaji wa Shu na Tefnut na kitendo cha kujichua.
Kiuhalisia miungu hii inavaa uhusika wa hewa na ukavu pamoja na vimiminika, kutokana na kuumbwa kwao ndipo vifaa (material) vya ujenzi wa anga na matabaka yake vikapatikana.
Shu na Tefnut walibarikiana, na vizazi vyao ni Keb;Mungu wa dunia, na Nut; Mungu mwana mke wa anga.
Mpaka hapo tunakuwa na miungu mitano jumla yaani:
Khepera- mwenye kanuni nzima ya ubunifu (the creative principle)
Shu- Tabaka la angahewa (the atmosphere)
Tefnut- Maji ya anga/mvua (the waters above the heavens)
Nut- Mungu mwanamke wa anga (the sky-goddess)
Keb- Mungu wa dunia (the earth-god)
Katika kipindi hiki jua lilikotokea na kuangaza kwa mara ya kwanza kutoka katika vilindi vya maji ya NU, nakuangazia dunia na ikatokea mchana.
Katika zama za kale mwanga wa jua ulichukuliwa kama muundo wa Shu. Miungu Keb na Nut waliunganishwa katika mwanga na kubarikiana na ujio wa mwanga ndiyo uliokuwa ukiwatenganisha; mfano inapotokea ikawa ni mchana, Nut; Mungu mke wa anga, alibakia katika eneo lake juu ya dunia, akipata support toka kwa Shu, lakini pindi jua linapozama uachilia anga na taratibu uteremka mpaka pale linapotua juu ya mwili wa Keb; Mungu wa dunia.
Sasa kubariki huku kukapelekea Keb na Nut kupata miungu wengine watano baada ya kuzaliwa; Osiris, Horus, Set, Isis na Nephthys.
Osiris na Isis walioana hata kabla ya kuzaliwa kitendo kilichopelekea kuzaliwa kwa mwanao wa kiume aliyeitwa Horus; Set na Nephthys nao vivyo hivyo wakamzaa Anpu (Anubis), japo huyu Anu ajaongelewa kiundani na wahenga katika simulizi zao.
Katika miungu wote hawa ni Osiris pekee ndiye aliyetajwa katika maandiko ya wahenga kwa kupewa umuhimu ambapo katika simulizi ya Khepera akiongea kama Neb-er tcher, anasema kuwa jina lake ni Ausares, yeye ambaye ni kiini cha jambo la kitambo kirefu ambalo yeye mwenyewe ameundwa/kutokana nalo. Hivyo Osiris alikuwa wa dutu ile ile kama Mungu mkuu aliyeumba ulimwengu.
Kulingana na maandiko haya ya wamisri yanatanabaisha kuwa kuzaliwa kwake duniani Osiris ilikuwa ni re-incarnation ya babu mkuu.
Kipande hiki cha maelezo ya wahenga kinatusaidia kupata majawabu juu ya mtizamo uliojengwa juu ya Osiris kwa miaka mingi kuhusiana na kuchukuliwa kama roho kuu ya mababu (the great ancentral spirit) ambaye kipindi alipokuwa duniani alileta faida kubwa kwa binadamu na alipokuwa mbinguni alikuwa ni mwokozi wa nafsi.
Wahenga wanalizungumzia jua kama jicho la Khepera au Neb-er tcher, ambalo upatwa na misukosuko mingi inayopelekea kufifisha mwanga wake na hivyo kabla ya anguko lake na kuzima kabisa, Mwezi uliyoundwa na Khepera utumike kama jicho la pili uangaza badala ya jua na kuupa furaha jicho hilo la kwanza.
Hivyo jua alilipatia kipaumbele maalumu kwa kulipachika katikati ya kipaji chake cha uso na kulipa mamlaka ya kutawala juu ya uso wa dunia na kuwezesha uhai huku mwezi wenyewe ukiusishwa na nguvu ya uzazi na mavuno.
Kulingana na simulizi za wahenga, Mwanaume na Mwanamke hawatokani na dunia, bali moja kwa moja kwenye mwili wa Mungu Khepera au Neb-er tcher, ambaye aliwaweka pamoja watu wake na kuwanyunyizia machozi yake, papo hapo wakawa viumbe hai, kutokana na machozi yaliyodondoka kutoka katika macho yake.
Hakuna mahali katika simulizi ambapo viumbe wengine (ukiachilia binadamu) wamepewa umuhimu katika uumbaji wao, isipokuwa aliumba kila kitu kwa namna yake, ikiwemo na viumbe wakubwa, wakiume kwa wakike,na viumbe vyote vilizaliana na kuongezeka kwa namna zao na kwa sababu hiyo dunia ikajazwa na uzazi wao mpaka waleo.
NB: Hii ni kwa kujibu wa maandiko kutoka katika papyrus of Nes-Menu.