Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,517
- 34,314
Kwa kipindi kirefu sana CCM imekuwa ikisiasisha usalama (Politicize national security) wa Taifa letu.
Mwanzoni wengine wenye umri mkubwa kidogo ingawa hatujafikia umri wa kina johnthebaptist tulielewa.
Huko tulikotoka kabla ya mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi uliporudishwa tena, mambo ya ulinzi na usalama wa nchi yetu yalisimamiwa moja kwa moja na CCM.
Mfumo wa ulinzi na usalama moja kwa moja ulifungamanishwa na uongozi wa CCM kupitia Umoja wa Vijana Tanzania (UVT).
Ilikuwa kama haiwezekani kabisa kuwa Askari Polisi, Askari Magereza, Afisa usalama wa Taifa au Askari Jeshi la wananchi bila ya kuwa mwana CCM na kuthibitishwa kama unafaa na viongozi wa UVT.
Kwa ivo kuwa na mabaki ya watu ndani ya mifumo ya ulinzi na usalama wanaoamini mhimili wa mifumo hiyo ni CCM haikusangaza sana.
Lakini Leo zaidi ya miaka 32 tangu Sheria ya kuvitenganisha vyombo vyetu vya ulinzi na usalama toka CCM ilipotungwa, kuona vyombo hivyo kama bado vinaendeshwa chini ya CCM, inasikitisha sana.
Ulinzi na usalama ni tasnia/fani ya jeshi/sanaa ambayo Taifa huwekwa mbele kuliko taasisi nyingine yoyote Ile.
Lakini Kwa Tanzania ni kama CCM ni vyombo vya ulinzi na usalama na Vyombo vya ulinzi na usalama ni CCM.
CCM kusiasisha vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kutoka kwenye misingi ya kazi zao na kuwa sehemu ya kuilinda CCM badala ya serikali, kumeua ufanyaji kazi kiweledi wa vyombo hivyo.
Jambo hili ni la hatari sana kwani inaweza kufika mahali vyombo hivyo vya ulinzi na usalama vikaanza kudhani maadui wa CCM ni maadui wa Taifa letu pia.
Vyombo vya ulinzi na usalama vinapoacha (Compromise) misingi ya kuwepo kwake, Taifa haliwi salama tena bali hujawa na hofu inayoleta utulivu bandia.
Mwanzoni wengine wenye umri mkubwa kidogo ingawa hatujafikia umri wa kina johnthebaptist tulielewa.
Huko tulikotoka kabla ya mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi uliporudishwa tena, mambo ya ulinzi na usalama wa nchi yetu yalisimamiwa moja kwa moja na CCM.
Mfumo wa ulinzi na usalama moja kwa moja ulifungamanishwa na uongozi wa CCM kupitia Umoja wa Vijana Tanzania (UVT).
Ilikuwa kama haiwezekani kabisa kuwa Askari Polisi, Askari Magereza, Afisa usalama wa Taifa au Askari Jeshi la wananchi bila ya kuwa mwana CCM na kuthibitishwa kama unafaa na viongozi wa UVT.
Kwa ivo kuwa na mabaki ya watu ndani ya mifumo ya ulinzi na usalama wanaoamini mhimili wa mifumo hiyo ni CCM haikusangaza sana.
Lakini Leo zaidi ya miaka 32 tangu Sheria ya kuvitenganisha vyombo vyetu vya ulinzi na usalama toka CCM ilipotungwa, kuona vyombo hivyo kama bado vinaendeshwa chini ya CCM, inasikitisha sana.
Ulinzi na usalama ni tasnia/fani ya jeshi/sanaa ambayo Taifa huwekwa mbele kuliko taasisi nyingine yoyote Ile.
Lakini Kwa Tanzania ni kama CCM ni vyombo vya ulinzi na usalama na Vyombo vya ulinzi na usalama ni CCM.
CCM kusiasisha vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kutoka kwenye misingi ya kazi zao na kuwa sehemu ya kuilinda CCM badala ya serikali, kumeua ufanyaji kazi kiweledi wa vyombo hivyo.
Jambo hili ni la hatari sana kwani inaweza kufika mahali vyombo hivyo vya ulinzi na usalama vikaanza kudhani maadui wa CCM ni maadui wa Taifa letu pia.
Vyombo vya ulinzi na usalama vinapoacha (Compromise) misingi ya kuwepo kwake, Taifa haliwi salama tena bali hujawa na hofu inayoleta utulivu bandia.