sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,407
- 19,047
Na mimi nililelewa kwa staili hii lakini nilipokuja kuona tunaishi tofauti na jamii nilimkaidi mzee na ndio ponea yangu, (nilishaweka uzi huu).
Ipo hivi yani, Mzee ni mtu ambae alikuwa anatulea katika mtindo ambao ulitufanya tuwaone watu nje ya familia kama vile hawahitajiki.
Basi kaka yangu alikolezwa sana na hayo malezi kiukweli kawa hawa mnaowaita ma introvert, ni mtu wa kupenda sana kukaa peke yake, Nyumbani kwake hakunaga wageni kabisa labda iwe ni wale wa upande wa mke wake tu.
Ugeni katika kuishi na watu kwa kukosa mwanya huo akiwa mtoto umemfanya apitie mengi mazito, katika kujaribu hivi ukichanganya na ugeni wa urafiki kajikuta mara kadhaa akigeuzwa kuwa ngazi bila kujua anatumika tu, mbaya zaidi alipopata hata rafiki alikuwa ni kunganganizi sana hata rafiki yake wakigombana yeye anatumia nguvu sana kumbembeleza na kuomba msamaha, hii ilifanya wahuni kumtumia kirahisi
vitu vinahitaji kiasi chake, ukizidisha unaharibu,
Maisha ni kama baiskeli, unapomfundisha mtoto kuiendesha kuna muda unamshika kuna muda unamwachia kidogo, akitaka kudondoka unamshika, ivo ivo mpaka huku ukubwani tayari anajua kuendesha baiskeli bila kushikiliwa,
Ipo hivi yani, Mzee ni mtu ambae alikuwa anatulea katika mtindo ambao ulitufanya tuwaone watu nje ya familia kama vile hawahitajiki.
- Kufungiwa ndani, yani geti kali hakuna kutoka.
- Hakuna kucheza na watoto wengine hata uwanja wa karibu ama nje ya geti
- Hakuna kuingiza marafiki ndani,
- Kila mara kutuasa kwamba watu ni wabaya hawaaminiki bila kutuelimisha ni vipi tunakabiliana na huo ubaya zaidi ya kufungiwa ndani tu.
Basi kaka yangu alikolezwa sana na hayo malezi kiukweli kawa hawa mnaowaita ma introvert, ni mtu wa kupenda sana kukaa peke yake, Nyumbani kwake hakunaga wageni kabisa labda iwe ni wale wa upande wa mke wake tu.
Ugeni katika kuishi na watu kwa kukosa mwanya huo akiwa mtoto umemfanya apitie mengi mazito, katika kujaribu hivi ukichanganya na ugeni wa urafiki kajikuta mara kadhaa akigeuzwa kuwa ngazi bila kujua anatumika tu, mbaya zaidi alipopata hata rafiki alikuwa ni kunganganizi sana hata rafiki yake wakigombana yeye anatumia nguvu sana kumbembeleza na kuomba msamaha, hii ilifanya wahuni kumtumia kirahisi
vitu vinahitaji kiasi chake, ukizidisha unaharibu,
Maisha ni kama baiskeli, unapomfundisha mtoto kuiendesha kuna muda unamshika kuna muda unamwachia kidogo, akitaka kudondoka unamshika, ivo ivo mpaka huku ukubwani tayari anajua kuendesha baiskeli bila kushikiliwa,