Biblia inatabiri siku ya kurudi Yesu atakuta watu wengine wakiwa watumwa na watwana

Cashman

JF-Expert Member
Jun 8, 2018
2,401
4,144
Mwanzo nilipokuwa nasoma kitabu cha ufunuo,niliona mahali pakiandikwa kana kwamba ujio wa Yesu,utakuta baadhi ya watu ni watumwa na watwana na wengine mabwana.Nilijiuliza sana jambo hili linawezekanaje katika dunia hii ya sasa watu kuchezea mijeledi kama enzi za zamani!?

Hata hivyo sasa ninaona kila kitu kinawezekana.Historia hujirudia.Kama watu wako tayari kuandamana kufurahia kutawaliwa,hili ni jambo la kusikitisha sana.

Tumekiri kabisa kuwa akili zetu,na maarifa yetu yamefikia mwisho na suluhisho ni kuwakabidhi wanaoweza kufikiri kwa niaba yetu watusaidie kufanya hivyo.

Kwa sasa sioni sababu ya kuwekeza matrilioni ya pesa vyuo vikuu kwani kwa sehemu kubwa havina tija kabisa katika nchi hii.

Serikali iwekeze kwenye fani muhimu kama za udaktari Kilimo na Jeshi tu ambako fani mbali mbali hufundishwa.

Ninaamini kizazi kijacho kitatushangaa sana kwamba mtu anasoma hadi chuo kikuu halafu mshauri wake kwenye masuala nyeti kabisa ya nchi,ni machawa wengi wao darasa la saba.
 
Mwanzo nilipokuwa nasoma kitabu cha ufunuo,niliona mahali pakiandikwa kana kwamba ujio wa Yesu,utakuta baadhi ya
Umeongea kwa uchungu sana, yaani naumia sana sijui Hawa viongozi wamelishwa nini Hadi hata ufahamu mdogo kabisa umetoweka. Mbaya zaidi hata niliokuwa nawaamini sana kama PM Majaliwa naona nao wimbo ni ulele. Yaani saizi nikiwasha tu TV nikawaona Hawa viongozi nazima hapohapo
 
Mwanzo nilipokuwa nasoma kitabu cha ufunuo,niliona mahali pakiandikwa kana kwamba ujio wa Yesu,utakuta baadhi ya watu ni watumwa na watwana na wengine mabwana.Nilijiuliza sana jambo hili linawezekanaje katika dunia hii ya sasa watu kuchezea mijeledi kama enzi za zamani!?

Hata hivyo sasa ninaona kila kitu kinawezekana.Historia hujirudia.Kama watu wako tayari kuandamana kufurahia kutawaliwa,hili ni jambo la kusikitisha sana.

Tumekiri kabisa kuwa akili zetu,na maarifa yetu yamefikia mwisho na suluhisho ni kuwakabidhi wanaoweza kufikiri kwa niaba yetu watusaidie kufanya hivyo.

Kwa sasa sioni sababu ya kuwekeza matrilioni ya pesa vyuo vikuu kwani kwa sehemu kubwa havina tija kabisa katika nchi hii.

Serikali iwekeze kwenye fani muhimu kama za udaktari Kilimo na Jeshi tu ambako fani mbali mbali hufundishwa.

Ninaamini kizazi kijacho kitatushangaa sana kwamba mtu anasoma hadi chuo kikuu halafu mshauri wake kwenye masuala nyeti kabisa ya nchi,ni machawa wengi wao darasa la saba.
Dah, Mkuu! Kunani tena. Mbona tunabishana. Yaani turudi tena kwenye mijeledi. Yesu atarudi lini!
 
Ndio maana binafsi nimeamua niwekeze maisha yangu katika ulimwengu ule wa milele (wa rohoni). ulimwengu huu wa nyama na damu ni wa hovyo sana. ukiuzingatia utakuwa unaumia kila siku.


JESUS IS LORD&SAVIOR
 
Umeongea kwa uchungu sana, yaani naumia sana sijui Hawa viongozi wamelishwa nini Hadi hata ufahamu mdogo kabisa umetoweka. Mbaya zaidi hata niliokuwa nawaamini sana kama PM Majaliwa naona nao wimbo ni ulele. Yaani saizi nikiwasha tu TV nikawaona Hawa viongozi nazima hapohapo
Ukweli ni kwamba usitegemee lolote la maana kutoka kwa aina ya watawala tulio nao. Ni watu walioamua kuutumikia unafiki na hadaa.
 
Back
Top Bottom