mchawi wa kusini
JF-Expert Member
- Apr 18, 2018
- 809
- 817
Habari Ya Futari Wana JF
AZAM HAWAJAPENDA CRDB KUDHAMINI FA.
Wanashindwa kutoka hadharani na kuliongelea hili lakini Moyoni wanaumia sana.
-Jana shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) na Bank ya CRDB waliingia mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya billion 3.759 na mkataba ambao ulianza jana hatua ya 16 bora ya kombe la shirikisho na Rais wa TFF alitangaza sasa shindano hilo litajulikana kama "CRDB Bank Federation Cup" badala ya "AZAM Sports Federation Cup".
-Pamoja na mabadiliko ya jina hilo AZAM Media bado inaendelea kutambua shindano hilo kama zamani lakini kwenye page za TFF tayari walishaanza kuyatangaza kama CRDB Bank Federation Cup. Swali langu kwa nini AZAM wenye haki ya mataganzo ya shindano hilo hawatangazi mabadiliko ya jina la shindano? Kuna shida gani au na wao walikuwa tayari kuendelea na mkataba?
-Nimejaribu kuangalia tangu mwanzo tangazo la kuingia mkataba AZAM Media hawawapi haki yao wadhamini wapya wa shindano hata tu picha ya mchezaji bora mchezo ambaye anapewa laki tano na Bank ya CRDB, AZAM Media hawatangazi wala kupost kwenye page zao akiwa kwenye bango la CRDB shida nini? Basi kama kuna shida nyuma ya pazia tuambieni na sisi tujue.
-Kwenye pita pita zangu nimeona kuwa, September 2019, Azam Media na TFF walisaini mkataba wa miaka minne wenye thamani ya bilioni 4.5 kwa ajili ya shindano la kombe la shirikisho maana hiyo mkataba huo uliisha September 2023, kwa maana hiyo TFF wako sahihi kusaini mkataba mpya na CRDB na kama kuna shida au tatizo lipo basi tuambiwe tujue.
-Haiwezekani mkataba ulishaanza jana kutumika ila AZAM Media hawataki kutambua mabadiliko hayo hata waandishi wao wanapohoji bado wamaendelea kuyatambua mashindano haya kama zamani "Azam Sports Federation Cup" hii sio haki kwa mdhamini mpya (CRDB Bank) hapati haki yake kama wadhamini mpya wa shindano wadhamini wanahitajika sana na wanatakiwa kulindwa kwa gharama yoyote.
Asantee..
AZAM HAWAJAPENDA CRDB KUDHAMINI FA.
Wanashindwa kutoka hadharani na kuliongelea hili lakini Moyoni wanaumia sana.
-Jana shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) na Bank ya CRDB waliingia mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya billion 3.759 na mkataba ambao ulianza jana hatua ya 16 bora ya kombe la shirikisho na Rais wa TFF alitangaza sasa shindano hilo litajulikana kama "CRDB Bank Federation Cup" badala ya "AZAM Sports Federation Cup".
-Pamoja na mabadiliko ya jina hilo AZAM Media bado inaendelea kutambua shindano hilo kama zamani lakini kwenye page za TFF tayari walishaanza kuyatangaza kama CRDB Bank Federation Cup. Swali langu kwa nini AZAM wenye haki ya mataganzo ya shindano hilo hawatangazi mabadiliko ya jina la shindano? Kuna shida gani au na wao walikuwa tayari kuendelea na mkataba?
-Nimejaribu kuangalia tangu mwanzo tangazo la kuingia mkataba AZAM Media hawawapi haki yao wadhamini wapya wa shindano hata tu picha ya mchezaji bora mchezo ambaye anapewa laki tano na Bank ya CRDB, AZAM Media hawatangazi wala kupost kwenye page zao akiwa kwenye bango la CRDB shida nini? Basi kama kuna shida nyuma ya pazia tuambieni na sisi tujue.
-Kwenye pita pita zangu nimeona kuwa, September 2019, Azam Media na TFF walisaini mkataba wa miaka minne wenye thamani ya bilioni 4.5 kwa ajili ya shindano la kombe la shirikisho maana hiyo mkataba huo uliisha September 2023, kwa maana hiyo TFF wako sahihi kusaini mkataba mpya na CRDB na kama kuna shida au tatizo lipo basi tuambiwe tujue.
-Haiwezekani mkataba ulishaanza jana kutumika ila AZAM Media hawataki kutambua mabadiliko hayo hata waandishi wao wanapohoji bado wamaendelea kuyatambua mashindano haya kama zamani "Azam Sports Federation Cup" hii sio haki kwa mdhamini mpya (CRDB Bank) hapati haki yake kama wadhamini mpya wa shindano wadhamini wanahitajika sana na wanatakiwa kulindwa kwa gharama yoyote.
Asantee..