Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,770
- 10,660
Hivi huyu mchambuzi feki bado yupo jukwaani?Wakati Simba ikijitafuta kutatua changamoto zake yanga inaamini bado iko salama na huenda wako na hali nzuri zaidi. Niukweli usiofichika katika jicho la wanakabumbu kuwa yanga wana shida kwenye maeneo kadhaa na kuifanya timu hiyo kuwa na changamoto kadhaa.
Yafuatayo ni maeneo yenye walakini kwa Yanga.
1.Safu ya ushambuliaji-Bado yanga inashida kupata mshambuliaji wa aina ya mayele au anaemfikia walau hata nusu. Safu hii ilibebwa sana na Mayele ambae alikua na idadi kubwa kuwazidi washambuliajinwenzake kama msonda na mzize. Ingizo ka Konkoni bado halijaleta mwanga sababu bado hajapewa nafasi ni bora akapewa nafasi ili kupima uwezo wake na kufanya maamuzi kabka dirisha la usajili halijafungwa. Ikitokea likapuuziwa yanga atapata shida mapaja dirisha dogo na timu itakua imeanguka kwenye nafasi yake ha hata kutoka katika mashindano muhimu ya CAF champ.
2.Mbadala wa Bakari ndondo na Aucho. binafsi naona Hawa ni wachezaji muhimu kwenye nafasi zao lakini hakuna mbadala wao hivyo timu itakua kwenye shida endapo itatokea wana tumikia adhabu au majeruhi.
Simba ameamnza kujitibu taratibuu lakini uzuri anajua shida yake na ameanza kuchukua hatua
Mlimda mlango
Beki wa Kati mbadala wa Inonga
Kiungo mkabaji
Nawasilisha maoni yangu Yanga iamke.