Search results

  1. S

    Shairi: Nyoka mwenye makengeza amwaga sumu ghalani

    KIKAO CHA NYIKANI Sauti toka nyikani, naipaza kwa kulia. Mwenyekiti bwana Nyani, Kikao nawaitia. Sungura Swala Kongoni, na Sokwe muso mikia. Wanyama walao nyama, tuwatolee tamko. Wote mlao majani, wamatunda nanyi pia. Jongeeni kikaoni, na sasa nakifungua. Jengeni hoja makini, kikao...
  2. S

    SHAIRI: Mchakato wa katiba (tunatibu malaria kwa dawa ya usingizi).

    WAWATIBU MALARIA KWA DAWA YA USINGIZI. Mgonjwa wetu wa tanga, twamlilia nyikani. Na nduguye ni majanga, ni yule wa visiwani. Madokta wamewapanga, wawili wote wodini. Wawatibu malaria, kwa dawa ya usingizi. Hapa pana siri kali, kuwatibu watu hawa. Mara dozi ziwe mbili, wakasema wenye...
  3. S

    Shairi: Baby badili jina

    JINA LAKO LITANIPA TB. Mpango chupa za coka, umeleta sokomoko. mpenzi nawe wataka, chupa yenye jina lako. nimemaliza maduka, Kibaha mpaka Keko. Mpenzi badili jina, nisije pata TB. Nasasa nimeshafika, kiwandani Makondeko. Makreti napachika, godauni ndo niliko. Jinalako nalisaka, Nyaminzi mwana...
  4. S

    Shairi: Alokwenda kwa mjomba ameishia njiani

    ALOKWENDA KWA MJOMBA AMEISHIA NJIANI. Alitangaza safari, nduguze tukusanyike. Tukalipanga shauri, nauli tuchange kwake. Akatuaga kwaheri, kwa mjomba asifike! Alokwenda kwa mjomba, ameishia njiani. Alipofika mjini, wakamdaka wenzake. Wewe mjomba wa nini, muache apumzike. Walimu kwako ni nani...
  5. S

    Mwanamke zake sifa, usiache kumsifu

    MWANAMKE ZAKE SIFA. Kipindi wamtokea, ulimsifia kwanza. Ndipo kakukubalia, leo ndio wake mwenza. Upendo unafifia, kusifu ukipunguza. Mwanamke yake sifa, usiache kusifia. Sio mali kutumia, eti utamtuliza. Nyumbani ukiingia, kama bubu wanyamaza. Mkeo anaumia, au mume namkwaza? Mwanamke zake...
  6. S

    Shairi:Tunda la ajabu

    TUNDA LA AJABU. Nimetulia mtini, nala tunda liso kokwa. Laini shinda maini, ladha kuku wa kupakwa. Chumvi nitake ya nini, nala bivu si kidakwa. Naulinda mti wangu, unatunda la ajabu. Tunda sikukuta chini, liangani likadakwa. Ladha yake ulimini, akili zangu zarukwa. Ladha zazidi...
  7. S

    Sifa za mke nimtakae (Shairi)

    NATAKA KUOA: Naogopa majaribu, kuoa nimenuia. Kwa kukwepa maswahibu, yaliopo kwenye ndoa. Nimepanga taratibu, sifa za anae faa. Natafuta wa kuoa, mdada alo na sifa. Namtafuta bubu, awe na kiziwi pia. Huyu huwa hana gubu, hatosikiza umbea. Nitaziepuka tabu, tutadumu kwenye ndoa. Natafuta wa...
  8. S

    Shairi: Twaboronga Kiswahili

    TWABORONGA KISWAHILI. Twajua neno ONESHA, kwa chenye kuonekana. ONESHA kuwa ONYESHA, hapa ni lugha gongana. ONYESHA kunyumbulisha, ONYA, ONYO, ONYEANA. Twajiita waswahili, kiswahili twaboronga. TWASIKIA kwa SIKIO, lugha yenye burudani. SIKIO kuwa SHIKIO, tunalishikisha nini? SHIKIO kwa...
Back
Top Bottom